Baba agoma kumuozesha mwane kwa mahari ya laki tatu kisa ana degree

Kifulu

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2021
Posts
557
Reaction score
2,064
Wakuu zengwe hili limetokea Leo hapa mtaani

Binti kamaliza chuo anataka kuoelewa na mwanaachuo mwenzie Ambae ndio kwanza ananijitafuta.

Baba amekataa kuoneshašŸ˜‚akidai ni dharau binti ameahidi kutoroka sijui itakuwaje

Wazazi mahari ni sawa na kumuuza binti badilikeni
 
Baba anaelewa anachokifanya nakupa kisa kilitokea .....
Binti mmoja aliolewa kwetu miaka mingi iliyopita!!! sasa yeye alisema hakuna haja ya mahari kwani si lazima na kwao hawajali hayo mambo.. alivishwa Pete ya uchumba na ndoa ilifungwa maisha yakaendelea baada ya miaka kumi maisha fresh na mume alifanikiwa kupata teuzi sasa ni muheshimiwa...
Sasa sisi tunatoka kabila ambalo mahari tunatolewwa ni kubwa huku binti kutolewa hata ng'ombe kumi ni kawaida sasa baada ya hiyo miaka kumi mama muheshimiwa na familia yake wakaanza kudai mahari ya million 20 wakithaminisha na degree yake .
Wazee walichukia sana nusu ndoa ivunjwe ilitokea sintofahamu kubwa sana na ndugu yetu ilifikia hatuna akachukua jiko la kabila letu na kutoa mahari stahili yenye vigezo.. maana inaonekana bidada alitaka ndoa huku akiwa amempimia future mwanaume.
Kutokana na lile zogo mama muheshimiwa alipata mke mwenza.
Baba wa mwanamke ana akili.
 
Mzee mpuuzi huyo, siku hizi watu wana degree hawana ishu kabisa kitaa wapo wapo tu , hakuna matumaini, wachache wamejiongeza ndo boda boda, mama ntilie n.k
 
Kweli ujinga ni mzigo mzito. Hivi kuna uhusiano gani wowote wa kiwango cha mahari na elimu ya anayetakiwa kutolewa mahari? Kiuhalisia suala la mahari ni la kitamaduni/kimila, sidhani kama lina uhusiano na elimu ya wahusika wanaotarajia kuingia katika ndoa.
 
aisee hii inatesa ndio changamoto ninayo pitia mimi. niliwambia wazazi wanitafutie binti wa kuoa huko kijijini kwetu baada ya kuona jitihada zangu zakupata mke zimegonga mwamba hapa mujini, binti alipatikana tena mzuri nika unganishwa nae tukayajenga na kukubaliana kabisa. shida imekuja kwenye mahali walikubaliana m1.6, wazazi wakasema sawa lakini sisi tutatoa m1 then kiasi kilicho baki kitamaliziwa siku za usoni maana kijana bado anajitafuta tunaomba na ndoa kabisa, wakakubaliana na siku ya kwenda kutoa. chaajabu baada ya siku kadhaa mzee wangu alipokea ujumbe kutoka kwa baba mkwe mtalajiwa ya kwamba mke wake kagoma ETI mpaka pesa ienee, nilishangaa sana mwisho nikawambia Kama hawataki basi wanitumie hala yangu nifanye mambo mengine. nime ambiwa nivute subira wanaweka mambo sawa, lakini kiukweli kama mambo nihaya naona kama kuoa itakua changamoto kwangu
 
Kwanza kijana anavyojitafuta ameshakuwa mzigo, halafu anajiongezea mzigo mwingine. Kama sio kujitafutia ugomvi ni nini?

Kama hawezi kumtolea mahari huyo binti ataweza kumtunza?
Mzee afukuze io mtu ikalete hela.
Huyo binti anaka awe anaishi kwa jamaa halafu kula awe anaomba hela nyumbani. Shenzi kabisa.
 
Niuze ng'ombe afu nipeleke ng'ombe ingine shule. Halafu hiyo ng'ombe ije iondoke bure; sasa, nitarudishaje ng'ombe zangu nilizouza?

Yaani maisha yangu kama mzazi yawe taabu tu?

Kwakweli hapana...
Kwaiyo mtoto wako unamshusha thamani mpaka unamfananisha na ng'ombe?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…