Baba anayepata Mtoto Njiti kupata Likizo ya Siku 7

Baba anayepata Mtoto Njiti kupata Likizo ya Siku 7

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766

Bunge la Tanzania limepitisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Kazi (NA.13) wa Mwaka 2024 ambao umeongeza likizo ya uzazi kwa wanaojifungua Watoto njiti ambapo itaanza kuhesabiwa wiki 40 baada ya Mama kujifungua huku Baba wa Mtoto njiti akipewa likizo ya siku saba badala ya likizo ya siku tatu.

Akiwasilisha maelezo ya muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Kazi wa Mwaka 2024 (The Labour Laws (Amendments) Bill, 2024)kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete Waziri wa Madini Anthony Mavunde amesema hayo jijini Dodoma Januari 31, 2025

Aidha, marekebisho ya muswada huu ni utekelezaji wa maombi yaliyotolewa na Chama cha Wafanyakazi katika Sherehe za Wafanyakazi (Mei Mosi) zilizofanyika May 01 Mei 2024 Mkoani Arusha baaya kutangaza kuongezeka kwa Siku za Likizo kwa Wanawake wanaojifungua Watoto Njiti (Kabla ya Wiki 36 za Ujauzito)
 
mh! wangefanya mwezi kabisa 15 zakumliwaza mtoto na 15 zakumliwaza mama mtoto kwanza na wababa tupewe maternity leave kabisa tukafue vinguo vya akina junior!.
 
Mtaona wanaume watakavyosingizia kuwa wamepata watoto njiti ilikusudi wapate kupumzika.
 
Kuna wale wachepukaji watazitumia hizi siku ndivyo sivyo na michepuko yao huko hanimuni
 
Back
Top Bottom