Baba Chaula: Polisi niambieni mwanangu kama yu hai tu basi inatosha, nahisi roho yangu inashindwa kuvumilia haya maumivu

Baba Chaula: Polisi niambieni mwanangu kama yu hai tu basi inatosha, nahisi roho yangu inashindwa kuvumilia haya maumivu

Mkazi wa Kijiji cha Ntokela wilayani Rungwe, Mkoa wa Mbeya, Yusuph Chaula (56) amemwomba Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati suala la mwanawe Shadrack Chaula kutekwa na watu wasiojulikana.

Shadrack anadaiwa kutekwa na watu hao Agosti 2, 2024 ikiwa ni takribani siku 20 kupita tangu alipotoka Gereza la Ruanda Mkoa lililoko mkoani Mbeya, alipokuwa amehukumiwa kifungo cha miaka miwili au kulipa faini ya Sh5 milioni.

Kijana huyo mwenye miaka 24 alitiwa hatiani na Mahakama ya Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya na kuhukumiwa kifungo hicho baada ya kukiri kosa la kuchoma picha ya Rais. Baadaye alichangiwa faini na watumiaji wa mitandao ya kijamii kisha kuachiwa huru.

Leo Jumatano, Agosti 7, 2024, baba mzazi wa Shadrack amezungumza na Mwananchi iliyotaka kujua nini kinaendelea au kama kuna taarifa zozote amezipata juu ya mwanawe.
Baba
View attachment 3063745
Safi mzee..
Kazia hapohapo
Haisaidii kitu.

We need an extremely tough and difficult decisions against the brutal regime in order to stop these barbaric actions within this country.
 
Ukamataji wahalifu wa jeshi la polisi ungeshirikisha uongozi wa serikali ya mtaa

Polisi waambatane na mjumbe wa mtaa wako ndiyo ukubali.tofauti na hapo ni kuwaitia mwizi ndiyo itakomesha huu utekaji.

Wanakuja bila uniforms,bila vitambulisho na gari lolote hata IST wanachobeba ni bunduki mkubwa tu ndiyo ID
 
Waweza kuta Bibie hana habari naye machawa sasa
inabidi watanzania muweke akilini kuwa kuna hadhi/ cheo cha raisi katika nchi ambacho kuna vyombo na mamlaka zinakilinda kwa machozi na damu dhidi ya shambulio lolote liwe la ana kwa ana ama la mbali.

Na pia kuna mama samia hassan suluhu ambaye amepewa hadhi hiyo na nchi hivyo kwa issue kama hyo mama anaweza samehe kwa moyo mmoja lakini vyombo au mamlaka zikaona hapana kuna hatua inabidi zichukuliwe na hatua zinaweza chukuliwa bila hata rais mwenyewe kujua hii ni endapo issue hii inahusu serikali.

Kwa mtu ambae angeamua kufatilia gharama za kila siku za kumtunza rais yoyote wa nchi na gharama za kumpata kuanzia, malazi,mavazi na shughuli zake kila siku basi hakika yasingefanywa kama yaliyofanywa na huyu kijana mwenzetu.

Mwisho Niwahusie vijana wenzangu tuendelee kufata sheria za nchi kwa usalama wetu na familia zetu na nchi yetu kwa ujumla kwani sisi ndio wa kuijenga na kuibomoa nchi yetu.
 
inabidi watanzania muweke akilini kuwa kuna hadhi/ cheo cha raisi katika nchi ambacho kuna vyombo na mamlaka zinakilinda kwa machozi na damu dhidi ya shambulio lolote liwe la ana kwa ana ama la mbali.

Na pia kuna mama samia hassan suluhu ambaye amepewa hadhi hiyo na nchi hivyo kwa issue kama hyo mama anaweza samehe kwa moyo mmoja lakini vyombo au mamlaka zikaona hapana kuna hatua inabidi zichukuliwe na hatua zinaweza chukuliwa bila hata rais mwenyewe kujua hii ni endapo issue hii inahusu serikali.

Kwa mtu ambae angeamua kufatilia gharama za kila siku za kumtunza rais yoyote wa nchi na gharama za kumpata kuanzia, malazi,mavazi na shughuli zake kila siku basi hakika yasingefanywa kama yaliyofanywa na huyu kijana mwenzetu.

Mwisho Niwahusie vijana wenzangu tuendelee kufata sheria za nchi kwa usalama wetu na familia zetu na nchi yetu kwa ujumla kwani sisi ndio wa kuijenga na kuibomoa nchi yetu.
Kwa hiyo kumteka mwananchi kijinai ndiyo kufuata sheria huko?

Kosa lolote la jinai hufikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria.

Acha kubariki uzandiki, kwa mawazo, kwa maneno ama kwa vitendo.
 
inabidi watanzania muweke akilini kuwa kuna hadhi/ cheo cha raisi katika nchi ambacho kuna vyombo na mamlaka zinakilinda kwa machozi na damu dhidi ya shambulio lolote liwe la ana kwa ana ama la mbali.

Na pia kuna mama samia hassan suluhu ambaye amepewa hadhi hiyo na nchi hivyo kwa issue kama hyo mama anaweza samehe kwa moyo mmoja lakini vyombo au mamlaka zikaona hapana kuna hatua inabidi zichukuliwe na hatua zinaweza chukuliwa bila hata rais mwenyewe kujua hii ni endapo issue hii inahusu serikali.

Kwa mtu ambae angeamua kufatilia gharama za kila siku za kumtunza rais yoyote wa nchi na gharama za kumpata kuanzia, malazi,mavazi na shughuli zake kila siku basi hakika yasingefanywa kama yaliyofanywa na huyu kijana mwenzetu.

Mwisho Niwahusie vijana wenzangu tuendelee kufata sheria za nchi kwa usalama wetu na familia zetu na nchi yetu kwa ujumla kwani sisi ndio wa kuijenga na kuibomoa nchi yetu.
Ni upuuzi tupu.

Mnataka kujivika utukufu ili muonekane kuwa ni Watu wa maana zaidi kuliko watu wengine.

Hadhi au Jina la mtu halilindwi kwa kuwafanyia Uhalifu Watu wengine.

"Chema chajiuza chenyewe na kibaya chajitembeza."
 
Waweza kuta Bibie hana habari naye machawa sasa


Ni ngumu kuamini hayo.
Utakuwa mwenye Nyumba usijue yanayoendelea ndani ya Nyumba yako ?
Na ikifika hatua hiyo ujue shida ni kubwa zaidi somewhere
 
Kufuatia taarifa za kupotea katika mazingira yanayodaiwa ā€˜kutekwa’ kwa Shadrack Chaula ambaye ni Msanii wa Sanaa ya Uchoraji, baba mzazi wa kijana huyo, mzee Yusuph Sisala Chaula amesema anaomba ajulishwe tu mwanaye kama yu hai au la ili moyo wake uwe na amani.

Amesema ā€œUnajua inaweza kufa roho moja lakini hiyo moja ikafa na nyingine kadhaa kutokana na mawazo. Siku ya nne sasa sijui mwanangu yuko wapi.

ā€œPolisi wamesema wanaendelea na uchunguzi lakini mpaka sasa wapo kimya na sina taarifa zozote, kama yupo hai waniambie tu ili nafsi yangu itulie, kama ameshikiliwa na Vyombo vya Usalama waniambie tu pia nijue yupo hai tutaenda kumuona.

ā€œHata kama yupo gerezani waniambie tu nitajua yupo hai na ipo siku nitaenda kumuona, naongea kwa uchungu sana, najiona nashindwa kuvumilia haya maumivu, sijui nini kitatokea, lakini naomba Serikali iniambie tu mwanangu yuko hai hata kama wanaendelea kumshikilia kuliko huu ukimya uliopo sasa.

ā€œMara ya mwisho tumewasiliana na Mpelekezi tuliyepewa asimamie suala hilo jana (Agosti 5, 2024) baada ya hapo hatujapata taarifa nyingine ya ziada.ā€

JamiiForums ilimtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, jana Agosti 5, 2024, alipoulizwa kuhusiana na suala hilo alisema ā€œNipo msibani tutawasiliana baadaye.ā€ Baada ya hapo simu yake haikupokelewa.

Alipotafutwa leo Agosti 6, 2024, simu haikupokelewa, akatuma ujumbe ā€œNitakupigia baadaye.ā€

Ikumbukwe Julai 8, 2024, Shadrack Chaula aliachiwa huru kutoka gerezani baada ya kulipa faini ya Tsh. Milioni 5 ikiwa ni siku chache tangu kuhukumiwa kifungo cha Miaka Miwili jela au kulipa Faini hiyo kwa kosa la kutoa taarifa za uongo Mtandaoni.
Baba Chaula kuna ofisi inaitwa TLS kuna mwamba pale anaitwa Mwabukusi. Nenda pale utapata msaada
 
Ingekuwa ni Amdul kufanyiwa hivyo ingekuwaje?
Angejisikiaje ?
Wakati alishakuhumiwa na kulipa fine yote ?
Kinachozidi hapo nini kama sio dhuruma na udhalimu ?
 
Baba mzazi wa Shedrack mzee Chaula amesema anamtaka mwanae akiwa Hai au Mfu

Source: Mwananchi
 
Back
Top Bottom