mwasipenjele
JF-Expert Member
- Jun 2, 2012
- 771
- 450
Ngoja aanze kutembea uchi tu karibuni ataanza,baba anaumwa we unaendekufanya anasa na mwanamke wa uzinifu tu,nakusihi diamond msikilize baba yako.
So sad! Kuelekea Zari show. Baba yake Diamond ambae anaumwa sana miguu ameshindwa hata kutembea ameomba mwanaeamsamehe kama baba na pia ameomba aje kumtembelea ampeleke hospitali asisubiri kufa.
Sisemi kwa ubaya, mi ni mmoja kati ya watu wanaojua maisha ya baba na mama waliotengena. Ukweli haijalishi uko level gani ugomvi wa mama yako na baba yako usiingilie hata siku moja tafadhalini...
Narudia tena, Diamond akifa leo baba yako hutopata Baba wa kukodi.
Kila la kheri..
==============
DIAMOND MWANANGU USISUBIRI NIFE!
Maskini! Wakati leo akiangusha pati ya nguvu na mpenzi wake, Zarinah Hassan Zari The Boss Lady inayokwenda kwa jina la Zari All White Party kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar, baba mzazi wa mwanamuziki Nasibu Abdul Diamond Platnumz, Abdul Jumaa yu hoi kitandani huku akimtaka mwanaye huyo kuonesha msamaha wa kweli aliotangaza kwenye vyombo vya habari na kwamba asisubiri hadi afe.
View attachment 248376
Baba mzazi wa Diamond Platnumz
TUJIUNGE NA CHANZO
Habari kutoka kwa chanzo makini kilicho karibu na baba Diamond kilidai kwamba kutokana na hali tete ya mzazi huyo ambapo kwa sasa anasumbuliwa na miguu kwa mara nyingine huku ikitoka magamba na kushindwa kutembea kwa muda mrefu, amekuwa akimlaumu mwanaye huyo kupita kiasi.
Chanzo hicho kilisema kuwa mzazi huyo amekuwa akisema kama alimkosea Diamond, alishamuomba msamaha na akasema amemsamehe lakini hakuonesha mabadiliko yoyote kwake wakati alikiri hadharani kupitia vyombo vya habari.
Kiliendelea kueleza kwamba kutokana na jambo hilo baba Diamond amekuwa akiumia kwani mwanaye huyo baada ya kutangaza amemsamehe hajaonesha mabadiliko yoyote ya kumjali.
MALALAMIKO
Chanzo hicho kilidai kwamba, baba Diamond amekuwa akilalamika kuwa ameugua kwa muda mrefu lakini Diamond hajawahi kwenda kumjulia hali hata siku moja.
Ukweli baba Diamond anaumia sana. Sasa hivi anaumwa, ameshindwa hata kutoka nje, miguu imevimba na ina muonekano wa ajabu, amekuwa akisema hajui ni kwa nini mwanaye anashindwa kulegeza moyo wake na kumsamehe wakati alishakiri kwenye vyombo vya habari.Anasema bora akaenda sasa hivi wakasameheane kuliko asubiri hadi siku akifa ndipo aende, kiliongeza chanzo hicho.
BOFYA HAPA KUMSIKIA BABA DIAMOND
Baada ya kupata habari hizo, gazeti hili lilitinga nyumbani kwa baba Diamond au Dangote maeneo ya Magomeni-Kagera, Dar na kumkuta akiwa katika hali mbaya kwani miguu imevimba huku ikiwa imepoteza muonekano wa kawaida na kuwa na ngozi ya ajabu.
Baada ya salamu, wanahabari wetu walimuuliza kulikoni yupo katika hali hiyo na kama Diamond alikuwa amekwenda kumjulia hali ambapo alikuwa na haya ya kusema:Ukweli nimeugua kwa muda mrefu lakini mwanangu Diamond hajawahi kuja kuniona.
AMTUMIA MESEJI
Hali hiyo ilinifanya juzikati kumwandikia meseji ya kukata tamaa na kumwambia kwamba anaona ameshanizika kutokana na kunisahau kwake lakini Diamond hakunijibu.
Namshukuru Mungu kwa sababu nina kibanda changu cha kulala, silipi kodi kuna watu walishanishauri eti niwatume watu wakaongee naye lakini nilikataa kwa sababu haoni thamani yangu.
ANASUBIRI NIFE?
Kama ni tofauti na mama yake (Sanura Kassim), tulishamaliza na kabla hajaugua alikuwa anakuja kuniona, nikimuuliza kuhusu Diamond alikuwa akiniambia alishaongea naye lakini kila siku alikuwa akisema atakuja tu kuniona mpaka leo sijamuona labda anasubiri hadi nife ndiyo aje.
Mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni kipindi kile alivyomvisha pete ya uchumba Wema Sepetu ndiyo alimleta kwangu kumtambulisha, tangu hapo huwa namsikia tu kwenye vyombo vya habari. Inauma sana; Yote kwa yote haya ni maisha tu.
DIAMOND YUPO BIZE
Ijumaa lilimtafuta Diamond ili kumfikishia habari juu ya baba yake ambapo hakupatikana hewani lakini watu wake wakaribu (Wasafi Classic Baby) walidai kwamba bosi wao huyo alikuwa yupo bize na Zari kwa ajili ya pati yao leo.
Chanzo: GPL
Leo naona. pichazake anahesabu Dollar kunamanufa!gan babayako hoi unahela makalioni aijalishi alikutendeanini. wapo waliokanwanababazao. leo. wanasimama kamakaka wWATOTO tufanyesehemu yamaishayetu jua. kuna. mbingu baadayahapo
Niwe open kabisa ningelikuwa Nasib Abdul hakyamungu baba huyu nisengeli msaidia hata kiduchi wacha mungu anihukumu
Niwe open kabisa ningelikuwa Nasib Abdul hakyamungu baba huyu nisengeli msaidia hata kiduchi wacha mungu anihukumu
Aijalishi lakipesa. nimerudiatena usiguseugomvi wawazazi waje...kamauamini. angalia. mkeulienae nini. mbali. muulize machungu yawanawake. Aliopata DIAMOND. kufikia. hapo. utajua siriyawazazi HUMONDANI
Kirohosafi DIAMOND. msaidiebabayako. India ufahamu. Weka baraka zawatotowako
Leo naona. pichazake anahesabu Dollar kunamanufa!gan babayako hoi unahela makalioni aijalishi alikutendeanini. wapo waliokanwanababazao. leo. wanasimama kamakaka wWATOTO tufanyesehemu yamaishayetu jua. kuna. mbingu baadayahapo
Baba aliweza kupanda mbegu kisha akakausha huyo sio baba ni mvulana, mtu mwenye busara uhakikisha anatoa huduma au hata kumwona mwanae haijalishi kuna ugomvi kiasi gani baina yake na mwenzie. naomba diamond amache tu yeye aangalie maisha ya aliyemwangaikia.
SI ndio wanajisifu wavulana kuwa hata nikimtelekeza mtoto akikua atanitafuta sasa wajue dunia imebadilika watoto wa siku hizi wanajitambua, yeye afe tu.
Wewe ni bandidu! Sio mchezo mama!
Hahahahaha!!!!!!! kama unaacha acha watoto jua ipo siku kitanuka., leeni watoto wenu hata kama mama humpendi toa matumizi ya mtoto tu.
Hawa baba wakati mwingine ni watu kusamehe tu. ila makosa wanayo. Akikuacha anazira na watoto. Ngoja iwe fundisho na kwa wengine.
Unahangaika na watoto weeee. Lleo yuko chuo ndo wa kwanza kumtafutia field.
Wanaume kosana na mke ila hii ya kusema na watoto wako chukua acheni. Sikio tu ndilo halikui. Watoto wanakua.