Baba niruhusu nizae

Baba niruhusu nizae

Hayo ni maombi ya mdada mmoja ambae,nilimlea toka akiwa na miaka 3 hadi kumfikisha chuo kikuu,kwa ngazi ya shahada ya uzamili,sasa ana miaka 34,hajazaa,hajaolewa.

Kila akipata mwanaume hafiki nae mbali,japo ni mdada ambae hanywi pombe,havuti sigara,sio mtu wa kutoka out na nimemlea kwa dini ya kikatoliki japo mie ni muislamu,kwani ndio dini ya wazazi wake ambao kwa sasa hawako duniani

Ana kazi yake na kipato japo sio kikubwa.Kasubiri sana kupata mchumba hapati,tunaongea nae sana,nilimuomba padri wake anakosali amuombee,lakini hakuna kitu,alipata wanaume kama 3 hivi na kumbe walikuwa wanamtapeli maana wote wana wake.

Sasa jana kanipigia simu,baba niruhusu tu ni zae bila ndoa, umri unapita,aisee bila kuficha nililia sana,mwishowe nimemwambia sawa,fanya roho yako itakavyokuongoza
'Njia ya MUNGU inaweza isiwe rahisi, lakini ndio njia Bora KULIKO zote'
 
Anamuomba baba yake amruhusu kuzaa mbona ni ushetani au wewe baba unam....., anapaswa kumuomba Mungu.
Wadada wengi hasa graduates na employees wana choices sana ila umri ukiwapiga teke wanasahau choices wanaanza kukimbilia maombi na waganga🤣🤣🤣
 
Nimesoma bandiko lako na Majibu yako, hapa, Nimefurahishwa na vitu 2.

1. Kumlea huyo binti kwa dini ya wazazi wake ambayo ni tofauti na wewe.
2. Kumruhusu afanye kama roho yake itakayo muongoza kwa sababu huwezi kumtua huo msalaba anao upitia.

Itoshe kusema you are amongest the Wise man i have known in this platform
 
Anamuomba baba yake amruhusu kuzaa mbona ni ushetani au wewe baba unam....., anapaswa kumuomba Mungu.
Wadada wengi hasa graduates na employees wana choices sana ila umri ukiwapiga teke wanasahau choices wanaanza kukimbilia maombi na waganga🤣🤣🤣
Ndoa ni majariwa mkuu, Tumewaona wengi pia ambao hawakua na choices lkn waliishia kutumika na kuachwa au kuzalishwa bila kuolewa
 
Mkuu, unajua wazazi kuna upande wa watoto wao huwa hawauju kabisa. Mfano mimi mwenyewe wazazi wangu wanaamini kabisa kijana wao nimenyooka vibaya mno. Hii ni kwa sababu kuna upande wangu wa pili huwa siwaoneshi wao. Ila siku wakiujua ndio watajua mm nipoje.

Sasa mkuu kwa maelezo yako inaonekana hakuna shida upande wako wala hakuna shida upande wa binti, basi tuseme ni dunia imeamua kumfanyia hivyo na si kingine. Kwa maana nyingine yanayomkuta yapo nje ya uwezo wa binadamu, hivyo hatuna cha kurekebisha bali ni kuacha iwe hivyo.

Kila la heri mkuu
Sometimes mazingira hayakukutanishi na watu wanao weza kua partener wako, unaishia kua na very limited choices.

Watu wajifunze kubadiri mazingira
 
Kumbe tupo wengi.story yake inafanana na yangu kwa asilimia kubwa. mimi nilipofikisha umri huo nikaamua kuzaa bila ndoa. sasa hivi ni 36 na katoto kangu kana miaka miwili. nina mfurahia sana mtoto wangu sasa napambana kwa ajili yake. na nina amani mambo ya ndoa nilishayaweka kwenye dampo la taka sasa ni kupambana tu na maisha. unaweza subiri ndoa mwisho wa siku umri ukakuacha kabisa ndoa ukakosa na mtoto ukakosa vilevile.
Hao mnaozaa nao, kwanini hawawaoi?
 
Nimesoma bandiko lako na Majibu yako, hapa, Nimefurahishwa na vitu 2.

1. Kumlea huyo binti kwa dini ya wazazi wake ambayo ni tofauti na wewe.
2. Kumruhusu afanye kama roho yake itakayo muongoza kwa sababu huwezi kumtua huo msalaba anao upitia.

Itoshe kusema you are amongest the Wise man i have known in this platform
Asante
 
Kumbe tupo wengi.story yake inafanana na yangu kwa asilimia kubwa. mimi nilipofikisha umri huo nikaamua kuzaa bila ndoa. sasa hivi ni 36 na katoto kangu kana miaka miwili. nina mfurahia sana mtoto wangu sasa napambana kwa ajili yake. na nina amani mambo ya ndoa nilishayaweka kwenye dampo la taka sasa ni kupambana tu na maisha. unaweza subiri ndoa mwisho wa siku umri ukakuacha kabisa ndoa ukakosa na mtoto ukakosa vilevile.
Mimi pia.tutaenda kuolewa mbinguni
 
Mtoto wa kike akiwa chuo anatakiwa atulie. Wakati wa chuo ndio umri sahihi wa kuolewa. Sasa wengi wao wakati huo ndio wanakuwa na mambo mengi.

Wanaume huwa wanaoa wanawake waliotulia.
Hata mavazi yake pia mtu aangalie. Kuna watu wanavaa kama wako uchi hakuna mwanaume ataoa mwanamke wa hivyo.
Lakini kama alitulia na ikatokea bahati mbaya hakupata wa kumuoa basi hapo huo ni mtihani kutoka kwa Mungu. Asikate tamaa nimeshuhudia wanawake kadhaa wakiolewa na miaka 40-42 ikiwa ni ndoa zao za kwanza
 
Mtoto wa kike akiwa chuo anatakiwa atulie. Wakati wa chuo ndio umri sahihi wa kuolewa. Sasa wengi wao wakati huo ndio wanakuwa na mambo mengi.

Wanaume huwa wanaoa wanawake waliotulia.
Hata mavazi yake pia mtu aangalie. Kuna watu wanavaa kama wako uchi hakuna mwanaume ataoa mwanamke wa hivyo.
Lakini kama alitulia na ikatokea bahati mbaya hakupata wa kumuoa basi hapo huo ni mtihani kutoka kwa Mungu. Asikate tamaa nimeshuhudia wanawake kadhaa wakiolewa na miaka 40-42 ikiwa ni ndoa zao za kwanza
huyo binti yangu ni mtulivu sana,hanywi oombe,haendi disco na wala hatoki out hata siku moja,na haya sasa kaajiriwa mahali,yuko so decent,na wala havai nguo ambazo hazina stara,ni mwanamke ambae hana makuu,bado hajapata bahati tu
 
Back
Top Bottom