Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Najua data unazotunza ni zile zinazokubaliana na hoja zako tu,zinazopinga hoja zako huwezi kuzitunza ,kwa tunaokufahamu hapa JF hatushangai baada ya wiki utaanzisha mada kama hii na hoja zako ni hizi hizi
Pole mkuu.hata hili hawezi kujibu.upepo haupo upande wake kwa sasa

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
 
Ndugu zanguni kwa kawaida hivi ndivyo tunavyomaliza mara zote mijadala hii.
Jaribu kuanzia hapa rudi nyuma soma michango.
Lakini kunakuwa na faida inapatikana kwa wale ambao hawakuwa wanaijua historia ya uhuru wa Tanganyika kujifunza historia ya kweli.
Hivi wewe huchoki na huu upuuzi wako, historia ya kweli my foot! Bahati nzuri wale uliowazoea wakimeza hizi ngano zako idadi yao imekuwa ikipungua kila siku. Amka Mohamed Said, dunia haikusimama kama unavyoelekea kuamini na kwa sasa hadi wajukuu wako watakuwa wanakushangaa wakijiuliza huyu babu vipi. Naomba nikupe ushauri mdogo, umeshahangaika vya kutosha heri sasa ung'atuke upumzike.
 
Hivi wewe huchoki na huu upuuzi wako, historia ya kweli my foot! Bahati nzuri wale uliowazoea wakimeza hizi ngano zako idadi yao imekuwa ikipungua kila siku. Amka Mohamed Said, dunia haikusimama kama unavyoelekea kuamini na kwa sasa hadi wajukuu wako watakuwa wanakushangaa wakijiuliza huyu babu vipi. Naomba nikupe ushauri mdogo, umeshahangaika vya kutosha heri sasa ung'atuke upumzike.
Mag3,
Unaandika umechukia na mimi sioni kipi kinakupandisha hasira.

Hapa tunafanya mazungumzo kama vile tuko barzani jioni tumekaa.

Haya matusi ya ''upuuzi,'' ya nini ndugu yangu.
Wala mimi sihangaiki kama unavyodhani.

Inawezekana wewe hujui vipi nimeamsha hamu kwa watu kusikia historia ya uhuru na hasa historia ya Abdul Sykes na wazalendo wengine.

Nyumbani kwangu vyombo vya habari havipungui.

Ingia You Tube angalia nimefanya mahojiano na vyombo vingapi hadi documentary ambazo nimeshiriki kama mtaalamu wa historia ya Tanganyika - AZAM TV, TBC, DW, Clouds, Mlimani TV, Hamza, Kassongo, Masudi Kipanya.

Niko kila mahali.
Sijapata kuhangaika.

Vyombo vya haari ndivyo vinavyohangaika kunitafuta.

Mimi nitakushauri kitu kidogo sana.
Ikiwa wewe hupendezewi nami acha kunisoma.

Kwa hili ni jambo kubwa ambalo huwezi kufanya?
Kwa nini uitaabishe nafsi yako ndugu yangu?

Angalia hiyo picha hapo chini.

Mwaka wa 2007 niko Tanga Hamza Kassongo ananiunga na simu nishiriki katika kipindi chake ''Hamza Kassongo Hour.''

1643603065473.png


1643603488299.png

Hawa ni TBC
 
Najua data unazotunza ni zile zinazokubaliana na hoja zako tu,zinazopinga hoja zako huwezi kuzitunza ,kwa tunaokufahamu hapa JF hatushangai baada ya wiki utaanzisha mada kama hii na hoja zako ni hizi hizi
Belo,
Mdomo haumkatai bwana wake.
Unaweza kusema chochote upendacho huu uwanja huru.
 
Ni upumbavu 21 century mtu kulia lia mambo ya dini yangu nimebaguliwa,dini yangu naowa sizai watoto nikizaa hawathaminiwi dini yangu tupo wengi sijui tulipigania uhuru blah blah blahs tunaonewa usichokijua sisi ambao tumo humu tunaopata wasaa wakubishana huu ujinga ni vile tunajikuta tuna viji-channel vya kuingiza shiling mbili tatu yupo muislam pale Tandale muda huu hana hata mia mbovu ameenda kwa mangi Mkristo kukopa unga watoto wake wa kiislam wale walale yeye humkuti humu akijadili wala he don't give a sh*t about it!!!

Mada yako hadi muda huu 20:47 usiku ina siku mbili ina likes 11 tu unadhani humu waislam wakukupa likes hawapo?wapo ila wanajua unaandika na unawajaza ujinga wao wanachojua maisha ya Tanzania mwisho wa siku bila kujali wewe ni muislam,Mkristo sijui Buddha yanataka uweke mkate mezani yenyewe maisha hayazijui hizo dini zenu miaka na miaka unaandika hizi pumba punguza elimisha jamii kwa ujumla umuhimu wa kujitambua na kuondokana na mdudu CCM,hizo ajira unazolilia hapa kwa waislam wenzako hawa ndo wanagawana wao wame-advance hawaangalii tena dini wanachoangalia ni ujamaa!
Saint...
Hili si suala la dini kama ''doctronaire,'' hapa tunaangalia iweje fursa za serikali zikahodhiwa na watu wa dini moja kw akiwango hiki cha 20:80?

Wanaostahili kuwajibu Waislam wako kimya.

Wewe ndiye unaetoa majibu.

Nakuhakikishia kuwa serikali haiwezi kutoka jibu jepesi kama lako.

Hii ndiyo sababu ya ukimya wake.
 
Nanren,
Nacheka peke yangu.

Klu Klux Klan kamkamata kijana wa Kinegro anamuuliza, "Unawapenda wanawake Wazungu?"

Kijana akadhani akisema ndiyo anawapenda atasalimika.
Akajibu, ''Ndiyo nawapenda.''

Jamaa akamwambia, "Aha kumbe unawatamani wanawake wetu ukiwapatia nafasi utawabaka."

Kajuta kaona bora angesema anawachukia.
Unazungumza na Mohamed Said.
Acha janja janja.
Jibu swali. Umepimaje au umejuaje kuwa hao ni wakristo au waislam?
 
Smart...
Ni hatari kuliko hatari yenyewe.

Ukiwa na watu wa dini moja wamehodhi fursa zote wakati wenzao wako nje ya hizo fursa unajenga chuki katika jamii.

Lazima hali hii iondoshwe.
Mzee Mo, mbona matajiri wengi hapa nchini, wanamichezo maarufu, wasanii mahiri wenye viwanda vikubwa nk wengi ni waislamu!?
Na hatujasikia wakristo wakilalamikia hilo.
Huu uchimbuaji wako wa historia uwe wa kuelimisha..unapoingia kwenye uhamasishaji wa chuki kati ya hizi dini mbili, utaacha dhahama kubwa kwa kizazi kijacho.

Wewe hutaathirika na hizi chuki unazopanda kwa vile hutakuwepo, ila jiulize..ni vizuri ukaange mbuyu na kuwaachia wengine watafune??
 
Kwa bahati mbaya sana hii ni historia ambayo ilifunikwa na hakuna yeyote aliyekuwa anaijua hadi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kuchapwa mwaka wa 1998.
Mkuu,
Ili kuweka mizania sawa kwenye huu uzi wako, Una maoni gani juu ya uchomaji Moto uliopelekea uteketezaji wa maelfu ya makanisa Bara na Znz wakati wa awamu ya 2 na ya 4 ?
 
Sis tunaijuwa, Nyerere/TANU ilileta uhuru. Abdul Sykes hakuwa Mtanganyika bali mtu wa Afrika Kusini. Hili wewe hutuambii. Kama ulikuwa hujui pata hiii ilmu toka kwangu. Picha hazielezi lolote zaidi na unavyozitafsiri. Piacha siyo prpoof kuwa hao walileta uhuru. Kama walikuwa serious kwa nini wakamwachia Nyerere. Kumbuka kudai uhuru ni siasa na siasa ni ushindani. Nyere alishindani nao aklawatolea mbali. Alikuwa na uwezo unaotakiwa na ndiyo maana ndiye alieonekana anafaa. Abdul Sykes aache kupigania uhuru wa kwao South Africa aje kupigania wa TZ. Kwanza wakoloni wangemtolea uvivu na ndiyo kwanza miaka ya kupata uhuru ingesogea mbele.
ksk,
Unasema mimi sijui.
Hapana asiyejua ni wewe.

Abdul Sykes kazaliwa Dar es Salaam 1924 akiwa kizazi cha pili cha Wazulu kutoka Imhambane, Mozambique.

Baba yake Kleist Sykes ni kizazi cha kwanza cha Wazulu kazaliwa Pangani 1894.
Picha inazungumza maneno 1000.

Ikiwa umeangalia picha hizi nilizoweka na hukuona kitu...

Mimi siwezi kusema kuwa (kuna neno ningeweza kuliweka hapa lakini nahofia lisitafsiriwe kama tusi kwako).

Lakini kwa ufupi tu picha hizo kila niliyemuonyesha zilimstua.
Wamepigwa na mshangao kwa kuwa hawakuwa wanayajua haya.

Umesema kweli kuwa Nyerere ndiye aliyeonekana kuwa anafaa zaidi kuongoza harakati za uhuru.

Uamuzi huu ulifanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio mwaka wa 1953 miezi ya mwanzo kabla ya mwezi April uchaguzi wa TAA ulipofanyika.

Kikao hiki kilikuwa kati ya Hamza Mwapachu, Abdul Sykes aliyekuwa Secretary na Act. President wa TAA na Ali Mwinyi Tambwe Secretary wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Abdul alimfahamisha Hamza kuwa amefika kwake ili apate kauli yake ya mwisho kuhusu Julius Nyerere kuongoza TAA kisha mwaka wa 1954 waunde TANU.

Historia hii nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Nasikitika kuwa unaandika umeghadhibika kwa kuwa tu hupendezewi na historia ya kweli ya Mwalimu Nyerere mwenyewe na historia nzima ya TANU.

1643606135980.png

Kulia Abdul Sykes na Hamza Mwapachu
 
Mzee Mo, mbona matajiri wengi hapa nchini, wanamichezo maarufu, wasanii mahiri wenye viwanda vikubwa nk wengi ni waislamu!?
Na hatujasikia wakristo wakilalamikia hilo.
Huu uchimbuaji wako wa historia uwe wa kuelimisha..unapoingia kwenye uhamasishaji wa chuki kati ya hizi dini mbili, utaacha dhahama kubwa kwa kizazi kijacho.

Wewe hutaathirika na hizi chuki unazopanda kwa vile hutakuwepo, ila jiulize..ni vizuri ukaange mbuyu na kuwaachia wengine watafune??
Ngorunde,
Kugombea haki si kuleta chuki.
Tanganyika haikudai uhuru wake kwa kuwa wanawachukia Waingereza.
 
Mkuu,
Ili kuweka mizania sawa kwenye huu uzi wako, Una maoni gani juu ya uchomaji Moto uliopelekea uteketezaji wa maelfu ya makanisa Bara na Znz wakati wa awamu ya 2 na ya 4 ?
Anti...
Fungua uzi mwinngine kwa hili watu wajadili.
 
Mbaya zaidi anayekuambia hivyo Ni mtoto mdogo na anatambua fika wewe ni sawa na baba yake
Belo,
Tunaweza tukafanya mjadala wa adabu na heshima bila ya kejeli na kebehi.

Mathalan ukishanisoma na ukaona kuna jambo una fikra tofauti na zangu ukaeleza.

Sasa hii "kulia," na maneno ya kukashifiana yanatoa ladha ya mjadala.
 
Ma
Unaandika umechukia na mimi sioni kipi kinakupandisha hasira.
Unaona? Wala sijachukia wala kupandisha hasira, nakuonea huruma tu kwa namna unavyohangaika. Ni bahati mbaya tu kuwa aliyetota hajui kutota.Je unasoma kweli na kufuatilia majibu unayoyapata humu pamoja na maswali ambayo huthubutu kuyajibu. Nilikushauri tu, kwaheri!
Mbaya zaidi anayekuambia hivyo Ni mtoto mdogo na anatambua fika wewe ni sawa na baba yake
Je unajua Mohamed Said kazaliwa lini? Yeye mwenyewe anajua kuna kaka zake humu. Alipojiunga na JF forum mwaka 2008 alitukuta humu na toka siku ya kwanza hoja zake ni hizo hizo mashujaa wake wa uhuru wa Tanganyika, wakiwa ni walowezi wa kutoka Afrika Kusini na Congo. Kisa? Waliishi pamoja mitaa ya Gerezani na wakaoleana.
 
Ni lazima ujibiwe, Uislamu wako ni bora kuliko utanzania wako? Kama babu zako walikua na aina hii ya fikra sintoshangaa ni kwanini haw Abdulakuandikwa katika historia ya Tanganyika, Inaonekana wazi walipanga kujinufaisha wao binafsi na kuleta u dini hapa nchini.
Masta...
Hujui historia ya uandishi wa historia ya uhuru wa Tanganyika na nini ilikuwa sababu ya wazee wangu kufutwa.

Nitakusomesha kidogo ili ujue usiwe unajadili jambo hulijui.

Matatizo ya kuandika histori hii yalianza mwaka wa 1962 TANU yenyewe ilipoamua kuandika historia yake na waandishi wa mradi huu wa historia walikuwa Abdul Sykes na Dr. Wilbard Kleruu.

Historia hii ilianza na Kleist Sykes 1929 na ilikuwa imeshaandikwa na Kleist kabla hajafa mwaka wa 1949.

Mswada huu alikuwanao Abdul Sykes na sasa uko katika kitabu na nakala halisi Maktaba ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (Daisy Sykes Buruku, ''The Townsman: Kleist Sykesí, katika Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, uk. 95-114. Angalia A.D. Sykes ''The Life of Kleist Sykes,'' University of Dar es Salaam Ref. No. JAN/HIST/143/15).

Kuna watu hawakupenda historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ianze na ukoo wa Sykes.
Abdul Sykes akajitoa katika ule mradi.

Mwaka wa 1963 Judith Listowel alikuja Dar es Salaam kuafanya utafiti wa historia ya Tanganyika na mwenyeji wake alikuwa Ally Sykes.

Listowel aliandika kitabu, ''The Making of Tanganyika,'' (1965).
Kitabu hiki kimeeleza mengi kwa ukweli wake.

Mwalimu amelalamika kuhusu hiki kitabu na alimwandikia Listowel kumfahamisha hisia zake.

Yako mengi sana lakini nadhani haya yanatosha kwa kukufahamisha tatizo la uandishi wa historia ya uhuru wa Tanganyika na wazee wangu hawahusiki na lolote katika matatizo haya ya kuandika historia ya TANU.

1643607683783.png
 
Mzee wangu, Mo

Naishi Tanzania sasa kwa zaidi ya miaka 30.

Katika kipindi hiki nimekua, nimesoma, nimetafuta kazi na nimefanya kazi na WATANZANIA.

Katika watanzania hawa, walikuwepo makabila tofauti na ya kwangu, dini tofauti na yangu.

Mpaka sasa hivi naandika, sijawahi kubaguliwa ama kumbagua mtu kwa dini yake.

Sijawahi kubaguliwa, wala mimi sijawahi kumbagua mtu kwa kabila lake.

Ni tofauti sana na hapo Kenya tu kwa mfano ambapo watu wanabaguliwa kwa makabila hadi leo.

Au ni tofauti sana na pale Nigeria (moja kati ya taifa elite kabisa Africa) ambapo wakristo na waislam wanabaguana kila leo.

Wanachomeana makanisa na misikiti.

Kwa hili, Baba wa taifa Mwl J.K Nyerere abarikiwe sana.

Mungu aendelee kumpa pumziko la milele.

He was one in a million
Well said brother; suala la UDINI Tanzania linakuzwa tu, najaribu ku imagine kwa mfano Mwalimu kwa dini yake halafu angeamua kunyang'anya shule za Waislam tu halafu aziache za Wakristo ili Watanzania wote wasome hali ingekuaje? NAhisi angesomewa hadi Albadiri. Eti analaumiwa mwalimu kwa kuweka udini?? Watu hata aibu hawana, watu wamezoea kutangaza dini zao kwa kutumia UONGO, lazima wamtangazie mtu wa dini nyingine UONGO ili tu ionekane kwamba walionewa. Huyu mzee alitaifisha shule zote za kanisa lake ili hata Waislamu na wapagani wasome, hadi shule iliomfanya yeye aje mjini nayo aliitaifisha ili wapagani, waislamu wasome halafu unasemaje huyu mtu aliwatenga Waislamu? Najaribu pia kujiuliza, hivi ni nchi gani duniani yenye waislamu wengi na HAWALALAMIKI!? Nitajieni moja.
 
Unaona? Wala sijachukia wala kupandisha hasira, nakuonea huruma tu kwa namna unavyohangaika. Ni bahati mbaya tu kuwa aliyetota hajui kutota.Je unasoma kweli na kufuatilia majibu unayoyapata humu pamoja na maswali ambayo huthubutu kuyajibu. Nilikushauri tu, kwaheri!

Je unajua Mohamed Said kazaliwa lini? Yeye mwenyewe anajua kuna kaka zake humu. Alipojiunga na JF forum mwaka 2008 alitukuta humu na toka siku ya kwanza hoja zake ni hizo hizo mashujaa wake wa uhuru wa Tanganyika, wakiwa ni walowezi wa kutoka Afrika Kusini na Congo. Kisa? Waliishi pamoja mitaa ya Gerezani na wakaoleana.
Mag,
Nasema umeghadhibika kwa kuona lugha yako inavyokuwa kali.
Hakika hoja zangu zote ni hizo hizo kwa kuwa historia ya wazee wangu ni moja hiyo hiyo.

Hapana neno kaka mimi ni kitukuu cha walowezi hili vipi nitalikana na ndiyo ukweli wenyewe?
Angalia hii picha kuna kitu:

1643608061149.png

Kulia waliosimama: Mohamed Said (Mmnanyema kitukuu cha mlowezi), wa tatu Kleist Sykes (Mzulu kitukuu cha mlowezi. Waliochutama wa kwanza kulia Abdul Mtemvu (Mluguru mtoto wa Mmanga Mtemvu) na anaefuatia ni Wendo Mwapachu (Mdigo mtoto wa Hamza Mwapachu) sisi wazee wetu walikuwa katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika. Huu ulikuwa mwaka wa 1968.
 
Back
Top Bottom