BrownRange
JF-Expert Member
- Dec 25, 2020
- 927
- 1,191
Dah
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Makaveli...Nahitaji hiki kitabu mzee wanguS
Shukrani mzee wangu.Makaveli...
Kinauzwa Ibn Hazm Media Centre Msikti wa Manyama, Mtoro na Mtambani.
Pia unaweza kukipata Soma Bookshop na Elite Bookshop Mbezi Samaki shs. 10,000.00.
Kipo kwa Kiswahili na Kiingereza.
Unajua tofauti ya mada na maada!?..na hapo ulipata one o& a level!!Maada karibu 50 zote unalialia
Nafikiri sababu kubwa ni Geography na ukoloni, maeneo ambayo mkoloni alikuwa analima au kupata malighafi alijenga shule nyingi na aliwafanya wengi wa eneo hilo kwa wakristu, kwa hiyo wasomi wengi walikuwa wakristu hata baada ya uhuru na ndio hao walikuja kushika nchi, waislam nafikiri hawakupata Elimu kama wenzao kwa hiyo ikawa ngumu kushindana kupata hizo nafasi za utawala, lakini sasa naamini hatuna hilo tatizo ni juhudi yako tuu na hata maraisi wetu ni waislam na wakristu bila matatizoPep,
Mwalimu angeacha misingi mizuri leo tusingejikuta kwanza tunaandika upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Pili tusingekuwa na mjadala huu uliotukutanisha hapa.
Kong...Nafikiri sababu kubwa ni Geography na ukoloni, maeneo ambayo mkoloni alikuwa analima au kupata malighafi alijenga shule nyingi na aliwafanya wengi wa eneo hilo kwa wakristu, kwa hiyo wasomi wengi walikuwa wakristu hata baada ya uhuru na ndio hao walikuja kushika nchi, waislam nafikiri hawakupata Elimu kama wenzao kwa hiyo ikawa ngumu kushindana kupata hizo nafasi za utawala, lakini sasa naamini hatuna hilo tatizo ni juhudi yako tuu na hata maraisi wetu ni waislam na wakristu bila matatizo
Ukishasikiliza mazungumzo ya Mwalimu Nyerere katika hiyo video hapo juu sasa soma Hotuba yake aliyotoa Bungeni tarehe 10 Desemba, wakati Tanganyika inakua jamuhuri mwaka wa 1962.
Hotuba ya Nyerere ilijikita kwenye matatizo ya upogo kati ya Waislam na Wakristo.
Kwa nini ilikuwa lazima Mwalimu awataje Waislam katika hotuba ile?
Sababu ni jinsi Waislam walivyokuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukoloni na namna walivyounda TANU wakamchagua kama kiongozi na kuumuunga mkono toka siku alipochukua uongozi wa TAA katika uchaguzi wa tarehe 17 April, 1953 Ukumbi wa Arnautoglo alipogombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes aliyekuwa Act. President na Secretary wa TAA.
Kwa bahati mbaya sana hii ni historia ambayo ilifunikwa na hakuna yeyote aliyekuwa anaijua hadi nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na kuchapwa mwaka wa 1998.
Mwalimu anasema katika hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika:
''Hakuna njia nyepesi ya kuondoa tafauti baina ya raia wetu Waafrika na wasio Waafrika; hakuna njia nyepesi ya kuondoa tofauti za elimu kati ya Wakristo na Waislam, au baina ya wachache wenye elimu na wengi wa watu wetu wasio kuwa na elimu; hakuna njia nyepesi ambayo Wamasai na Wagogo wanaweza wakalingana na Wahaya na Wachagga na Wanyakyusa.''
Hii ilikuwa kauli ya serikali ya kudhihirisha nia yake njema ya kupigania haki na usawa kwa raia wote wa Tanganyika.
Kauli hii ilikuwa ya kuwapa matumaini na kuwahakikishia Waislam na wale wote walioathirika na dhulma ya wakoloni, kuwa serikali ilikuwa inatambua shida zao na itachukua hatua zifaazo kurekebisha hali hiyo.
Tarehe 5 Novemba, 1985 wakati Mwalimu anastaafu urais, Mwalimu aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam.
Hotuba hii ilijaa simanzi, Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo.
Katika hotuba hii Nyerere kwa mar ya kwanza hadharani alimtaja Abdul Sykes.
Mwalimu alimtaja na mdogo wake Abdul, Abbas Sykes na Dossa Aziz.
Wazee hawa aliokuwa anawahutubia wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono wakati wa kudai uhuru.
Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru.
Nyerere alisema neno zito sana kuwa upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake:
''Waislam wametupa nafasi kupitia sera yetu ya elimu, kurekebisha upogo.
Sasa nipo katika hali ya kufarahisha kwa kuwa wakati mwingine sielewi kama Mbunge mpya, Waziri, au Katibu Mkuu katika wizara zetu za serikali, ni Muislam au Mkristo au hana dini labda pale jina lake la kwanza linapotoa utambulisho.
Na hata hivyo hiyo siyo njia ya kuaminika kutoa utambulisho wa dini kwa kuwa tuna Wakristo wenye majina ya Kiislam, na Waislam wenye majina ya Kikristo.
Kuvumiliana huku nyie ndiyo sababu; nilichofanya mimi ni kuzungumzia maadili haya kwa niaba yenu.''
Swali linalokuja hapa ni kuwa ikiwa Mwalimu alisharekebisha upogo huu baina ya Waislam na Wakristo haya malalamiko ya leo kutoka kwa Waislam kuwa wanabaguliwa tunauelezaje?
Waislam hawasemi kweli?
Mgawano wa madaraka ndani ya serikali ya Tanzania baina ya Waislam na Wakristo ni 20:80.
Tumefikaje katika hali hii?
Ni muhimu sana mtu anapotaka kujadili tatizo hili la udini muhimu akaangalia historia hii kwanza kama nilivyoieleza hapo juu kwa kusikiliza mazungumza ya Mwalimu kuhusu udini na kusoma Hotuba yake ya Jamhuri ndani ya Bunge la Tanganyika mwaka wa 1962.
Tatizo hili la udini nimelijadili kwa kirefu sana katika kitabu cha Abdul Sykes.
Tatizo hili si tatizo la kupuuzwa na wala si la leo.
Tatizo hili lilianza mwaka wa 1958 na likasababisha ugomvi mkubwa baina ya Sheikh Suleiman Takadir na Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir akafukuzwa TANU.
View attachment 2096477
View attachment 2096478
Tangawizi,Shida yako kubwa ni kutaka waislamu wapewe special status Tanzania, kwa sababu ambazo kusema kweli hazina mashiko kabisa. Kila unapomuongelea baba wa Taifa, unaona kama hakufanya haki kuwapa waliokuwa waislamu katika kudai uhuru special favors.
Unalopigania kusema kweli hutalipata duniani na wala mbinguni maana lina lengo la kutugawa watanzania bila sababu
Boss hii 20:80 ni nini? fafanua kidogoTangawizi,
Soma kwa utulivu utaelewa kuwa ninachozungumza ni kuwa kuna tatizo serikali wanalikwepa toka enzi ya Mwalimu.
Hakuna popote nilipozungumza kuhusu, "special status," kwa Waislam.
Unadhani hii 20:80 ni sawa?
Ukishakuwa na hali hii tayari serikali yenyewe ishawagawa raia wake katika matabaka makubwa mawili.
Kwani mkuu si kazi zinatangazwa watu wanaomba na wanafanyiwa usahili ama ni hizi za kuteuliwa.Tangawizi,
Soma kwa utulivu utaelewa kuwa ninachozungumza ni kuwa kuna tatizo serikali wanalikwepa toka enzi ya Mwalimu.
Hakuna popote nilipozungumza kuhusu, "special status," kwa Waislam.
Unadhani hii 20:80 ni sawa?
Ukishakuwa na hali hii tayari serikali yenyewe ishawagawa raia wake katika matabaka makubwa mawili.
Boss hii 20:80 ni nini? fafanua kidogo
Kei...Kwani mkuu si kazi zinatangazwa watu wanaomba na wanafanyiwa usahili ama ni hizi za kuteuliwa.
Yaani hata Kama wamefaulu wote waislamu wachukuliwe ,mana kigezo sio dini kukaa pale.
Mwishowe tutakuja mpaka darasani tutaanza kuona ratio ni ndogo so itabidi wawe wanabebwa kisa wao wapo wachache.
Kama vipi tuanze kucheki kila kabila liwe katika kila ofisi mkuu.
Tukikuta watu wame qualify hata watano Kati ya 20 position afu wote ni wamwera watolewe wawekwe wamang'ati ama wabarbaig
Kong...Boss hii 20:80 ni nini? fafanua kidogo
Wewe upo bize na mwelekeo wa udini sana ktk mada zako nyingi nilizowahi kufuatilia.Eti una mengi sana ktk historia ya waislam.Kama umeamua kuchukua upande wa dini moja endelea na akili zako za kijahazi.Kwaiyo wewe badala ya kujielekeza kwenye weledi kwemye teuzi wewe upo bize na teuzi ktk misingi ya dini.Umewahi kujiuliza Misri ni wangapi wasio wa dini ..waliopo madarakani?Pep,
Usikae mbali na mimi.
Nina mengi sana katika historia ya Waislam wa Tanganyika.
Nimekuwa nikitafiti na kuandika toka niko kijana mdogo sana labda wa 20s.
Mi pia nakihitaji na nipo Tabora.Makaveli...
Kinauzwa Ibn Hazm Media Centre Msikti wa Manyama, Mtoro na Mtambani.
Pia unaweza kukipata Soma Bookshop na Elite Bookshop Mbezi Samaki shs. 10,000.00.
Kipo kwa Kiswahili na Kiingereza.
Boss hii 20:80 ni nini? fafanua kidogo
Mount...Wewe upo bize na mwelekeo wa udini sana ktk mada zako nyingi nilizowahi kufuatilia.Eti una mengi sana ktk historia ya waislam.Kama umeamua kuchukua upande wa dini moja endelea na akili zako za kijahazi.Kwaiyo wewe badala ya kujielekeza kwenye weledi kwemye teuzi wewe upo bize na teuzi ktk misingi ya dini.Umewahi kujiuliza Misri ni wangapi wasio wa dini ..waliopo madarakani?
Huyu mzee mi namwona wakala wa Ibilisi kabisa!! Kazi kubwa ya Ibilisi ni kupinduapindua maneno, giza lionekane mwanga na mwanga eti tuseme ni giza. Narudia huyu ni mhalifu!Shida yako kubwa ni kutaka waislamu wapewe special status Tanzania, kwa sababu ambazo kusema kweli hazina mashiko kabisa. Kila unapomuongelea baba wa Taifa, unaona kama hakufanya haki kuwapa waliokuwa waislamu katika kudai uhuru special favors.
Unalopigania kusema kweli hutalipata duniani na wala mbinguni maana lina lengo la kutugawa watanzania bila sababu
Aamin mkuu.Tuendelee kuelimishana.Mount...
Umeanza kuandika na "Wewe..." dalili ya ghadhabu.
Naam umri wangu wote nimetafiti historia ya Waislam wa Tanganyika
Sababu ni kuwa hapakuwa na msomi aliyetaka kuandika historia yao.
Kimambo na Temu (1969) wameandika historia ya uhuru Waislam ambao ndiyo walikuwa mstari wa mbele hawamo.
Leo mimi nimeandika upya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Huijui historia ya Misri.
Zungumza unachokijua.
Nchi zenye Waislam wengi hakuna wapagani.
Jifunze utafahamu.
Soma "In Search of Identity," tawasifu ya Anwar Sadat utajua nani wanaongoza serikali ya Misri.
Soma "The Road to Ramadan," cha Mohamed Heykal utaijua Misri na walioko madarakani.
Dini ni muhimu kupita kiasi katika kutawala nchi yenye dini kubwa mbili.
Ukiachia serikali itawaliwe na watu wa imani moja utasababisha farka na fitna katika jamii.
Hutoweza kujenga umoja na amani nchini.
View attachment 2097635
Niko Alexandria, Egypt 1988.
Smart...Mambo ya wewe dini gani? Au wewe kabila gani ni mabaya sana...