Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Baba wa Taifa na tatizo la Udini

Belo,
Tunaweza tukafanya mjadala wa adabu na heshima bila ya kejeli na kebehi.

Mathalan ukishanisoma na ukaona kuna jambo una fikra tofauti na zangu ukaeleza.

Sasa hii "kulia," na maneno ya kukashifiana yanatoa ladha ya mjadala.
Shikamoo Mzee Said. Hongera kwa uandishi wako kwa njia ya vitabu na makala.

Hongera pia kwa kutetea usawa katika jamii.

Mzee Said nimekuwa mfanyakazi wa umma sehemu mbalimbali, kiukweli sijawahi ona sehemu ambayo ilifanyika makusudi na viongozi au sekretariati ya ajira kutoajiri mtu kwa sababu ya dini yake. Kikubwa ni sifa ya mtu wala sio dini. Ungesema kabila na ukanda hapo tungekuelewa kidogo maana kuna baadhi ya taasisi huko nyuma (sio enzi hizi za sekretariati ya ajira) zilijaa watu wa kabila au kanda fulani.

Udini kidogo umeanza kurise kuanzia 2000s tena kwa baadhi ya taasisi.

Huko nyuma ni kweli kulikuwa na gap kubwa kati ya mkristo na muislamu (sababu kubwa ilikuwa elimu, kuna upande uliwekeza zaidi elimu ya dini kuliko elimu dunia), ila kwa sasa wengi wa vijana na watoto wa kitanzania wamesoma bila kujali dini wala kabila....hata jamii za waokota matunda na mizizi pamoja na wafugaji wako wengi kwenye mfumo wa elimu na ajira.

Hivyo, Mzee wangu tambua hilo gap la elimu lilivyokuwa huko nyuma ukizingatia taasisi nyingi za elimu zilikuwa chini ya dini fulani.
 
Mkoloni hakuona kuwa muislamu au mwarabu hakuona huyu mkristu aliona wote waafrika weusi .
Sisi ndio tumechanganyikiwa tunaangalia kwa dini. Hamna sehemu walienda kugombea uhuru kuwa uhuru wapewe waislamu au uhuru wapewe wakristu . Uhuru uliombwa wapewe waafrika watanganyika.

Mtu mzima kuingiza dini katika mazungumzo ya waafrika kuhusu kuendesha nchi ni kuchanganyikiwa

nampongeza sana baba wataifa kuliona hili na kulizuia ila bado majinga yanachochea dini ukabila.

tuache ujinga ndugu zangu watanzania
 
Kong...

Uadilifu II

Serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani Mwaka (2015), Rais alifanya uteuzi wa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi mbalimbali. Uteuzi wake ulikuwa kama ifuatavyo:

Mawaziri na Manaibu: 30.

Waislamu 10, sawa na asilimia 33%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 67%.

Makatibu Wakuu na Manaibu: 50.

Waislamu 10, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 40, sawa na asilimia 80%.

Wakuu wa Mikoa na Wilaya: 166.

Waislamu 41, sawa na asilimia 25%.

Wakristo 125, sawa na asilimia 75%.

Makatibu Tawala wa Mikoa na Wilaya: 163.

Waislamu 24, sawa na asilimia 15%.

Wakristo 139, sawa na asilimia 85%.

Wakurugenzi mbalimbali: 249.

Waislamu 45, sawa na asilimia 18%.

Wakristo 204, sawa na asilimia 82%.

Manaibu Kamishna wa Polisi: 25.

Waislamu 5, sawa na asilimia 20%.

Wakristo 20, sawa na asilimia 80%.

Makamishna Wasaidizi Waandamizi wa Polisi: 33

Waislamu 7, sawa na asilimia 21%.

Wakristo 26, sawa na asilimia 79%.

Jumla Kuu ya Uteuzi:

Waislamu asilimia 20%.

Wakristo asilimia 80%.


Uteuzi huo umekuwa kama Sera kwa teuzi zinazoendelea ndani ya miaka yote mitano. Vilevile kama Mwongozo kwa wateule wenye mamlaka ya kuteuwa. Mwelekeo huo unakinzana na Katiba ya nchi ibara ya 13(4)(5), inayokataza ubaguzi wa aina zote. Kwa hakika Taifa halihitaji kiongozi wa nchi akiwa Muislamu basi ateuwe idadi kubwa ya Waislamu wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi wa nchi au akiwa Mkristo atumie uongozi wake kuteua idadi kubwa ya Wakristo wenzake katika uongozi nchini. Au akiwa Mzanaki ateuwe idadi kubwa ya Wazanaki wenzake katika nafasi mbalimbali za uongozi na mfano wa hayo.

Hii inaleta mantiki na inaonesha kweli unafuatilia kwa karibu. Kuna sababu ya kulalamika...lakini bado pia acknowledge some of the factors kwa baadhi ya positions
 
Hii inaleta mantiki na inaonesha kweli unafuatilia kwa karibu. Kuna sababu ya kulalamika...lakini bado pia acknowledge some of the factors kwa baadhi ya positions
Hii ndio maana wazee kama hawa nyerere aliwapiga chini na nina furahi mtu kama huyu anapima watanzania kwa jicho la dini hafai katika jamii
 
Nauliza swali moja tu. Nyerere alipokewa na wazee wa dar au waislamu.?
Ada...
Hilo swali jibu lake lipo katika hotuba ya Mwalimu aliyotoa Ukumbi wa Diamond.

Itafute hotuba hiyo uisikilize kasema ni nani walimpokea Dar es Salaam.
 
Hii ndio maana wazee kama hawa nyerere aliwapiga chini na nina furahi mtu kama huyu anapima watanzania kwa jicho la dini hafai katika jamii
Ed...
Unaona sawa kuwa na 20:80?
 
Shikamoo Mzee Said. Hongera kwa uandishi wako kwa njia ya vitabu na makala.

Hongera pia kwa kutetea usawa katika jamii.

Mzee Said nimekuwa mfanyakazi wa umma sehemu mbalimbali, kiukweli sijawahi ona sehemu ambayo ilifanyika makusudi na viongozi au sekretariati ya ajira kutoajiri mtu kwa sababu ya dini yake. Kikubwa ni sifa ya mtu wala sio dini. Ungesema kabila na ukanda hapo tungekuelewa kidogo maana kuna baadhi ya taasisi huko nyuma (sio enzi hizi za sekretariati ya ajira) zilijaa watu wa kabila au kanda fulani.

Udini kidogo umeanza kurise kuanzia 2000s tena kwa baadhi ya taasisi.

Huko nyuma ni kweli kulikuwa na gap kubwa kati ya mkristo na muislamu (sababu kubwa ilikuwa elimu, kuna upande uliwekeza zaidi elimu ya dini kuliko elimu dunia), ila kwa sasa wengi wa vijana na watoto wa kitanzania wamesoma bila kujali dini wala kabila....hata jamii za waokota matunda na mizizi pamoja na wafugaji wako wengi kwenye mfumo wa elimu na ajira.

Hivyo, Mzee wangu tambua hilo gap la elimu lilivyokuwa huko nyuma ukizingatia taasisi nyingi za elimu zilikuwa chini ya dini fulani.
Soine,
Hujui.

Na kama hujui ndiyo hujui.
Utasema kile ukijuacho.

Mimi najua na naeleza nikijuacho.
Hakuna tatizo.
 
Kinyungu,
Sikupenda niliseme hili lakini nitalisema kukutoa shaka.

Mwaka wa 2011 nilialikwa University of Iowa, Marekani.

Likaja swali kama hili lako katika mhadhara niliofanya pale.

Wao wakaja na takwimu za CIA kuhusu "religious distribution," Tanzania na kueleza kuwa madaraka yamehodhiwa kwa wingi uliokuwapo.

Jibu langu lilikuwa swali kwa hadhira yangu ambayo yote ni hao watupu ukumbi mzima na wote ni maprofesa wa historia.

Nikawaomba wanipe mfano wa nchi moja duniani ambayo imevamiwa na wakoloni kutoka nje na waliosimama kunyanyua silaha na kupigana na wavamizi wakawa ni wale wachache.

Hapa nikatoa mfano wa Vita Vya Maji Maji.

Kwa bahati katika hadhira ile alikuwapo Prof. James Giblin ambae ameandika kitabu cha Maji Maji.

Nikatoa mfano mwengine nikauliza harakati za Waafrika kujitambua na kudai uhuru zilipoanza Tanganyika nani waliokuwa mstari wa mbele kudai nchi yao?

Nikawafanyia rejea katika kitabu cha Abdul Sykes ambacho wao wanakifahamu na wanakisomesha kama rejea katika historia ya Afrika.

Nikauliza historia yote ya kupigania uhuru wa Tanganyika nani waliokuwa mstari wa mbele?

Je ni hawa wachache?

Nikawaomba watoe mfano wa nchi moja tu duniani ambako wachache walisimama kuikomboa nchi yao.

Ukumbi ulikuwa kimya.
Hapakuwa na jibu.

Ukweli ni kuwa siku zote wale wengi ndiyo wanaokuwa na nguvu ya kupambana na adui na wengine huwa nyuma kuongeza nguvu.

Picha hiyo niko darasani nasomesha University of Iowa kushoto ni Prof. James Giblin.

View attachment 2098290
Hongera sana.
 
Soine,
Sasa nakufahamisha.

Hali ilivyo katika serikali ni hii:

Wakristo wamehodhi 80%
Waislam 20%

Ukitaka maelezo zaidi nifahamishe nikuwekee mchanganuo.

Hili ndilo tatizo linalotukabili ulilokuwa hujui.
 
Unajuaje kama mimi sipo kwenye 0% ya representation..., Unajua Watanzania wote sio Wakristu au Waislamu..., kuna Traditional African Religions na wengine ni Unaffiliated...

Kwahio na mimi nianze kudai representation sababu ya Imani yangu na sio Weledi wangu ? Nadhani hii vita tungeipigana wote kuondoa uduni wa kila Mtanzania / Mtanganyika na sio kugawana umasikini (as I see it watanzania wengi ni duni no matter their beliefs)
Key...
Majibu si mepesi kama unavyodhania.
Wazee wetu wamepigania uhuru wa nchi hii kuondoa udhalili.

Soma historia ya Waislam katika Maji Maji hadi siasa za TANU unakuja na habari za Wapagani.

Kuna Wapagani waliokuwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika?

Au una picha hata kipande ya wachungaji wamepiga na Nyerere wakati wa ukombozi wa nchi hii?

Huna unachokijua katika tatizo hili.
Wanaostahili kujibu wako kimya.

Jitulize soma historia hii kwanza uielewe.
 
Key...
Majibu si mepesi kama unavyodhania.
Wazee wetu wamepigania uhuru wa nchi hii kuondoa udhalili.

Soma historia ya Waislam katika Maji Maji hadi siasa za TANU unakuja na habari za Wapagani.

Kuna Wapagani waliokuwa katika kupigania uhuru wa Tanganyika?

Au una picha hata kipande ya wachungaji wamepiga na Nyerere wakati wa ukombozi wa nchi hii?

Huna unachokijua katika tatizo hili.
Wanaostahili kujibu wako kimya.

Jitulize soma historia hii kwanza uielewe.
Historia yako unataka ianzie lini na wapi ? Nikikwambia kwamba wazee wetu waliteseka na hata huo udhalimu kuja baada ya hizi dini kuja na Merikebu takuwa ninakosea ?

Au ni mangapi yamefanywa kwa jina la hizi Imani ambazo kwa pande hizi za dunia ni Alien ?, Au ndio yale yale kwamba utamaduni wa mababu zetu ulikuwa ni wa kipumbavu na hizi Imani zilizokuja ndio ustaarabu ? Ni ajabu sana watu wanaoamini Binadamu wote ni sawa kuanza kudai kwamba wao wana Hati Miliki zaidi ya wengine...

Na ni nani alikwambia kwamba kujua Historia ndio kujua Mema na Mabaya ? Yaani sababu Waarabu waliwachukua Mababu zangu utumwani ndio leo niwachukie wajukuu zao ? Au unamaanishi nini nisome historia ili nielewe....

Samahani kama sielewi ila sijawahi kuona watu wanajenga kwa kubomoa na kutenga; Kwangu Umoja ni Nguvu na Umoja huo utapatikana kwa kushikilia umoja wetu na sio kutofautiana kwetu (Hizo Imani zibakie kwenye Mahekalu na Makanisa huku Kitaa Binadamu wote ni Sawa)
 
Key...
Ikiwa unataka tujadili historia ya utumwa vyema niko tayari.

Tuanze na Transatlantic Slave Trade.

Kisha tuingie Belgian Congo Slave Trade.

Karibu.
 
Key...
Ikiwa unataka tujadili historia ya utumwa vyema niko tayari.

Tuanze na Transatlantic Slave Trade.

Kisha tuingie Belgian Congo Slave Trade.

Karibu.
Belgian Congo slave trade ni tofauti na Transatlantic slave trade?
 
Naona unanadi kitabu chako kwa gia ya uislam
 
Back
Top Bottom