Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 15,835
- 23,776
Kipindi tukiwa watoto, baba unakuta amesafiri, kaenda zake shamba wiki mbili au tatu, akirudi unaona mama kapika ugali-kuku na maziwa ya mgando ,mchicha pembeni na pilipili kichaa vijana wa mjini wanaita mwendokasi.
Asubuhi tunatumwa sokoni kuandaa karanga mbichi na mbata, alafu mama anasema baba yenu anakuja leo.
Basi wote tunafuraaahi kweli kweli ,baba anarudi, khee, akija anatusalimia, anaenda zake kuoga, tunamrukia rukia anatupa zawadi ya maembe sindano/kunyonya, dodo ,lawa-lawa na mapera alafu unasikia mama anasema "msimsumbue baba yenu anaumwa kichwa, anaenda kulala , msimsumbue, leo nawapa rukhsa mkacheze kwa mama Mwakitobo ila msiumizane"
SWALI : Hii mbinu wazazi wa kisasa mnaitumia?
Asubuhi tunatumwa sokoni kuandaa karanga mbichi na mbata, alafu mama anasema baba yenu anakuja leo.
Basi wote tunafuraaahi kweli kweli ,baba anarudi, khee, akija anatusalimia, anaenda zake kuoga, tunamrukia rukia anatupa zawadi ya maembe sindano/kunyonya, dodo ,lawa-lawa na mapera alafu unasikia mama anasema "msimsumbue baba yenu anaumwa kichwa, anaenda kulala , msimsumbue, leo nawapa rukhsa mkacheze kwa mama Mwakitobo ila msiumizane"
SWALI : Hii mbinu wazazi wa kisasa mnaitumia?