Baba yetu amefariki lakini hakuacha wosia wowote

Baba yetu amefariki lakini hakuacha wosia wowote

Ila hatua ya kwanza, ni kujua mahitaji ya watoto hao, ni hela kiasi gani inahitajika, na mambo ya kuuza ni baadaye tena Muuze Kwa Bei ya FAIDA na sio ya hasara.
Yaani ungeelewa point yangu ni kwamba mahitaji ya watoto tupo tayari kuhangaika nao , kwa sababu sisi wakubwa tuna uwezo wakuwalea , ila nilichotamani kusikia asiwepo wakusema kiwanja kiuzwe haswa watoto aliowaacha mama mdogo .
 
Una umri mzuri tu kuwasaidia vizuri. Kumbuka penye hela mikono mingi itawekwa.. Pia Nenda Mahakama na ww upewe Haki za kusimamia Mali. Na USIOGOPE KUWA MKALI UKIONA MTU ANALETA UROHO KWENYE MALI NA HELA ZISIZOMHUSU.
Nami hapo ndo nataka nisimamie kabisa ,
 
Ushauri Msiuze Kitu Chochote Kwanza. Muwe na mpango mzuri kabisa wa kuwasaidia. Kama ww ni kaka mkubwa, tafuta ndg wa karibu mwenye hekima, haki, na mwaminifu sana akusaidie.
Asante sana ndugu yangu.
 
Kwenye hili suala ninavyoona mimi
Kama kutakua hakuna kugombea mali kila mtu akae kwenye mji wake
Hao watoto wadogo mali ya baba yao iwe chini ya uangalizi wa mtu wakifikisha umri wakujitambua wakambiziwe
 
Hilo linawezekana lkn wao bado wadogo sana na siku zote kikao chetu kiliazimia shina la watoto wote wa marehemu ni hapa kijijini . Je mtoto akifa azikwe tofauti na kwenye shina la baba yake ?
KUZIKWA ni jambo lingine na mali ni kitu kingine...maiti aiwezi kutupangia sehemu ya kumzika...ila mtu awezi kupangiwa pia jinsi ya kutumia mali zake...kama mlikuwa familia 2....kila familia imejengewa na imewekewa aset zake...nyie bakini na zakwenu na madogo nao waachieni mali zao wakikuwa wataziendeleza...kisiuzwe kitu chochote....naongea kwa niaba ya marehemu mzazi wenu
 
Kwenye hili suala ninavyoona mimi
Kama kutakua hakuna kugombea mali kila mtu akae kwenye mji wake
Hao watoto wadogo mali ya baba yao iwe chini ya uangalizi wa mtu wakifikisha umri wakujitambua wakambiziwe
Hili ndiyo jibu sahihi.

Mimi huwa nasema mara zote, kama unataka kuoa mke zaidi ya mmoja, basi kila mama na watoto wawe na mji wao.

Kama una wanawake wawili hakikisha una nyumba mbili za kila familia, ili hata baba akiondoka duniani, familia zinatabaki kwenye nyumba zao bila ugomvi.

Unless otherwise labda mzee alikuwa na nyumba mbili na sehemu nyingine amejenga nyumba ya biashara, hapo watoto wanaweza kugawana hiyo nyumba ya biashara.
 
Hilo kwanza siyo suala la kisheria ni suala la kumaliza kwenye familia tu.

Suala dogo kama hilo unahitaji ushauri wa kisheria ?

Kwanini hakuenda kwenye ofisi ya wakili akapata ushauri mdogo tu ambao hauhitaji kuanika family affairs kwenye mitandao japokuwa anatumia fake identity ?
Sasa mkuu unataka aende kulimaliza kujadili kifamilia bila kujua chochote atachangia nini? Hata akienda kwa mwanasheria ataenda bila A,B,C na ushauri wa kwenda kwa mwanasheria anaweza upata hapahapa. Umeitwa kwenye interview, umeenda kama mbumbumbu hujui lolote kuhusu hiyo organization na hints zake utajibu nini sasa

Ili uweze kuchangia kwenye mjadala lazima uwe na msimamo unaojengwa na facts. Unawaambia tusiuze mali kwa sababu ya sheria hii, ukitaka kuuza tushirikishe kwa sababu hii. Bila kujua sheria watafanya maamuzi blindly ambayo hayana LAWFUL CONSIDERATION

Hajakosea kuomba ushauri. Hizi tabia za kutaka watu wafyatuke tu bila kuuliza utaratibu hazifaidishi lolote
 
Ushauri wangu.
Km kuna watoto wadogo kwenda shule ndo wa kuwazingatia na pili km wapo wadogo ni vema ndugu wote wakahusika ikiwemo wa upande wa wadogo zako wa mama mdogo.
Mkajadili kwa hekima na busara.
Mkiandika mihutasari na lipatikane msimamiz wa mirathi.

Maamuzi yasipokuwa shirikishi wanaweza kupiga mahakamani ikiwa hoja zitaibuka.
Hujazungumzia mama yenu yupo has au and hayupo.

Baada ya kua na amani katika familia ndipo Marathi ifanyike kisheria na hapo kila upande utakuwa maana yake na ukitapanya ni wao.
Maahakma unatoa /unaridhia mapendekezo ya mwongozo wa kusimama mali za wtt km wapo chini ya miaka 18.
 
Pole kwa kufiwa. Lakini nashindwa kujizuia kusema hili. Something wrong here! Yaani mwenza wako akiugua sana, unamwacha? Wakati ambao mweza wako anakuhutaji sana, unamwacha! Halafu unaoa mwingine? Mambo mengine ni magumu kuelewa.
Baada ya hapo waliaachana na mama yangu mzazi kwa sababu mama yangu aliugua sana akamtibisha bila kupata auhueni.
 
Pole kwa kufiwa. Lakini nashindwa kujizuia kusema hili. Something wrong here! Yaani mwenza wako akiugua sana, unamwacha? Wakati ambao mweza wako anakuhutaji sana, unamwacha! Halafu unaoa mwingine? Mambo mengine ni magumu kuelewa.

hmm mm mwenyewe nimeona hilo tatizo then baada ya hapo kuwapenda wadogo zako wa kule unconditionally inakuwa taabu kidogo maana mama yako ameachwa anaugua peke ake because of them, i am just saying sema kama ulivyosema baadhi ya mambo ni magumu kuyaelewa especially yakiwa ya kifamilia.
 
Bila kupepesa macho nyie hapo hamna chenu maana mama yenu hakufunga ndoa na Baba yenu,hivyo kisheria hatambuliki anayetambulika na huyo Mama yenu mwingine kama mkiamua kufuata mkondo wa kisheria,
Lakini cha kufanya haya mambo muyamalize kifamilia tu bila kuoneana wivu maana miyapeleka kisheria yatawagawa sana na kuwa acha na ugomvi mkubwa sana.!
 
Mimi ni mtoto kwa upande wa mke wa kwanza , mama yangu yupo hai lakini ni mgonjwa mpaka sasa. Ila kama nilivyoeleza hapo juu kwenye Uzi upande wa wadogo zetu na mama yao nae katangulia mbele za haki.
Mkuu nahisi wamjini wabaki mjini na mali zao na nyie wakijijini bakini na mali zenu.

Kama mna uwezo wa kifedha wasaidieni wadogo zenu bila kuuza chochote
 
Bila kupepesa macho nyie hapo hamna chenu maana mama yenu hakufunga ndoa na Baba yenu,hivyo kisheria hatambuliki anayetambulika na huyo Mama yenu mwingine kama mkiamua kufuata mkondo wa kisheria,
Lakini cha kufanya haya mambo muyamalize kifamilia tu bila kuoneana wivu maana miyapeleka kisheria yatawagawa sana na kuwa acha na ugomvi mkubwa sana.!
Mkuu naomba nikusahihishe hapa kidogo, kisheria watoto wote wa marehemu wana haki ya kurithi mali za baba yao. Hili swala kuna kesi zinazoliongelea na sababu ni ule msemo maarufu wa 'kitanda hakizai haramu' plus sheria ya mtoto ya 2009 plus mambo ya haki za binadamu.

Kuna mkanganyiko kwenye kuitumia hiyo sheria ya mtoto ya 2009 hasa watoto wanapokuwa na miaka 18+ sababu kule mtoto ni chini ya miaka 18 lakini bado hilo si kikwazo sababu zipo kesi zinasema kuwanyima haki yao ni kukiuka haki za binadamu.

Nadhani utakuwa umepata jambo hapa Mkuu.
 
Tatizo la mitoto ya sikuhizi imekalia kusubiria urithi tu na hapo ndio chanzo cha migogoro, ushauri mdogo tu achaneni na masuala sijui ya kuuza sijui kugawana sijui nini kama eneo ni prime kaeni wote hakuna cha mke sijui mdogo wala mkubwa wote watoto, fanyeni kitu cha maana kwa maendeleo yenu wote kinachofanya hii migogoro iendelee ni ubinafsi, mtu akishaanza kusema sijui mke mdogo sijui mkubwa hapo ndio shida inaanzia , nyie kama watoto wote baba yenu alikua mmoja , pambaneni muelewane muishi kwa amani hizo mali kwanza hazikuwa zenu hilo mosi, pili ulishawahi kusikia msiba wa masikini watu wanagombania mali? tafakari, wosia sio ishu sikuhizi
 
Hatujaelewana nadhani , maana yangu ni kwamba wale watoto wa mke wapili wakishawishiwa kuuzwa kiwanja chao je , sisi kama watoto wa wakubwa wa marehemu tuna pingamizi? Binafsi nilitamani tupaendeleze mjini ikiwezekana tuwe wamoja mwenye pesa apaendeleze kwa kujenga nyumba lkn iwe asset yakuwasaidia ambao bado ni watoto wadnaona
 
mi naona wote mnahaki ya kurithi ,Kwa upande wa Baba .

Wote mnahaki sawa na ni warithi halali wote.

Huyo mama yenu ambaye ni mgonjwa naye ataingia kama mrithi halali kwenye ile nyumba aliyojenga akiwa na mumewe.

Yeye hatahusika kwenye mgao wa nyumba aliyojenga mumewe akiwa na mke mdogo.

Ila nyie watoto wote kwa pamoja mnahaki ya kuzirithi mali zote za baba yenu kwa upande wote

Mimi siyo mwanasheria ila kwa uelewa wangu nafikiri ni hivyo.
 
Dini gani, kama muislam.. Sheria ziko wazi juu ya mirathi,

Dini nyingine sijui wamezungumziaje mirathi, ama la ukiona haki haipo panda mahakamani
 
Pole kwa kufiwa. Lakini nashindwa kujizuia kusema hili. Something wrong here! Yaani mwenza wako akiugua sana, unamwacha? Wakati ambao mweza wako anakuhutaji sana, unamwacha! Halafu unaoa mwingine? Mambo mengine ni magumu kuelewa.
Ahsante , lakini hakuna namna mkuu maamuzi ya mzee aliona kwake ni sahihi .
 
Pole sana Mkuu, maswali yako nitajitahidi kukujibu kwa mfumo wa maswali pia:

1. Baba yenu alikuwa anafuata mfumo gani wa maisha?, Nakuuliza hivi kwa sababu kwenye murathi kuna aina tatu za mfumo wa maisha ambayo ni:-

A. Mfumo wa kimila
B. Kikristu
C. Kiislamu

Sasa kama alifuata mfumo wa kimila mali zake zitagawanywa kwa mfumo au taratibu za kabila lenu, ila hapa kuna swala la ndia, sasa je alioa kimila?, na je ndoa zilisajiliwa?, na je alimtalaki mama yako?
Haya maswali muhimu kuyajibu ili tuelewe uelekeo wa kimfumo utaegemea bado hapa

Kama alifuata mfumo wa maisha ya kikristu, hapa ni kama alibatizwa/aliokoka na kuishi kwenye misingi ya dini za kikristu, huu mfumo utaleta utata kwenye hizi ndoa mbili endapo ta awali haikuwa na talaka. Ikumbukwe pia mfumo wa kikristu ndio mfumo unaoangaliana zaidi na sheria za kiserikali, sasa hapa ndoa ni ya mke mmoja, na hazifuatani mbili labda pawepo talaka, je talaka ipo?

Kama alifuata mfumo wa kiislamu, hapa utafuatwa ule utaratibu wa mgawanyo ulioelekezwa kwenye quorani, hapa ndoa zinaruhusiwa hadi nne hivyo kama hamna talaka na alioa kidini haitasumbua sana.

SASA, tuendelee hapo kwenye swala la mali kama wanaweza kuuza na kuja kuishi hapo kijijini.

Ipo hivi jambo muhimu kwanza ni kufanya vikao vya ukoo/familia ili mteue msimamizi wa mirathi hapo mtayajadili yote kwa maslahi ya watoto, hakikisheni mnajua nani atakuwa na jukumu la kuwalea hao watoto hii itategemea taratibu zenu inawezekana nyie wakubwa mkawaangalia wadogo zenu.

Msimamizi wa mirathi atafanya maombi mahakama ya mwanzo, kusipokuwa na mgogoro ni ahueni, ila hakikisheni mnajali maslahi ya watoto kwenye kikao maoema kabisa.

Swala la kuuza mali haliwezi kuamuliwa juu juu bila kuwepo msimamizi wa mirathi aliyeizinishwa na mahakama, mkiuza kiholela baadae mtapata migogoro ndugu.

Pia kila mtoto anayo haki ya kurithi mali za baba yake, swala ni kuzitambua mali za marehemu baba yenu ni zipi na hivyo kuzigawanya kwa taratibu sahihi.

Kila la kheri Mkuu. Ukiwa na swali usisite kuniuliza.
Karibu.
Wanaongelewa ni watoto. Suala la ndoa halina athari kwenye urithi wa watoto
 
Back
Top Bottom