Babati town na Dodoma ipi sehemu nzuri ya kufanya biashara ndogo ndogo na penye unafuu wa maisha?

MoSantu

Senior Member
Joined
Feb 26, 2022
Posts
173
Reaction score
167
Habari za majukumu wadau?

Natumai mpo shwari.

Kama title inavyoonekana, jamani naombeni muongozo kati ya Babati town na Dodoma ipi sehemu nzuri ya kufanya biashara ndogo ndogo na penye unafuu wa maisha?

Kuhusu biashara ni yoyote ile naangalia fursa kwenye eneo.

Karibuni kwa maoni, ushauri.
 
Nenda babati kakamate fursa.
 

Kama unaangalia unafuu wa maisha dodoma hapakufai..aisee dodoma ni mji ghali haswa..nenda babati ufanye hizo biashara zako ndogo ndogo..ila kama unataka kukua njoo dodoma ila ujibane haswa..
 
Kibiashara Dodoma kwa sasa imechangamka na ina watu wengi sana huwezi kuilinganisha na Babati. Lakini kwa gharama za maisha Dodoma inaongoza, hivyo basi.. Fanya uchangamfu wa biashara VS gharama za maisha utajua uchague wapi.
 
Kama unaangalia unafuu wa maisha dodoma hapakufai..aisee dodoma ni mji ghali haswa..nenda babati ufanye hizo biashara zako ndogo ndogo..ila kama unataka kukua njoo dodoma ila ujibane haswa..
ASANTE nimekupata.
 
Kibiashara Dodoma kwa sasa imechangamka na ina watu wengi sana huwezi kuilinganisha na Babati. Lakini kwa gharama za maisha Dodoma inaongoza, hivyo basi.. Fanya uchangamfu wa biashara VS gharama za maisha utajua uchague wapi.
Gharama za maisha dom zinalingana na za Arusha ?
 
Arusha nadhani ziko juu zaidi. (Sina hakika na gharama za chakula) maana Dom ziko juu sana.
Maana Arusha maisha ni ghali ila gharama za chakula zipo chini. Sasa kama dom chakula + Maisha ni juu aisee inabidi ujipange kisawa sawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…