Bado natafuta mantiki ya kujenga hili Daraja la Kigongo - Busisi kwa Tshs. Bilioni 700

Bado natafuta mantiki ya kujenga hili Daraja la Kigongo - Busisi kwa Tshs. Bilioni 700

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Hapa ndipo daraja la Tshs bilioni 700, fedha ambazo hata hazikujadiliwa na bunge zinatumika. Eneo ni Kigongo-Busisi. Kwakweli Bunge la Ndugai litajibu haya mbele za Mungu!

Screenshot_20200915-062934_Maps.jpg

Nawaza tu bilioni 700 Tshs ambazo ni hela nyingi sana yani hata Richmond haioni nusu yake. Kama zingetumika kwa mtu kuona mbali. Kuliko kujenga hilo daraja litakalopitisha Hiace na mbaya zaidi kama tozo zitakuwa kubwa maana hili eneo lina watu wa kipato cha chini sana basi wakaamua kuachana na kulitumia wakaendelea na usafiri wao wa feri.

Embu tuangalie kama tungewaza vyema kwa hii bilioni 700
1. Tungechukua tu hapo kidogo tukawanunulia feri za kisasa.
2. Tukatumia hapo fedha nyingine kuboresha maisha ya watu wa eneo hilo kama kuwapa mikopo yenye riba nafuu kisha mzunguko wao wa hela ukawa mkubwa. Yani kiufupi tungefanya mambo mengine mengi sana na hii hela! Ila kwa kuzitumia kwenye huu mradi ni HAPANA!

Yani Magufuli alifanya tu ziara hapo akakumbuka kuwa alikuwa anachunga ng'ombe eneo hilo basi hapo hapo akaamua lijengwe daraja na tena akatamka kuwa wajenge chap chap maana kama atakuja Rais mwingine ataufuta huo mradi! Kumbe hata yeye akilini mwake anajua kuwa ni mradi wa hovyo kupindukia!

Naumia maana gharama za mradi huu unazidi ule wa Kigamboni ambao walau ulikuwa na maana ingawa nao ulishavurugwa vurugwa na kweli fedha zinatumika isivyo kabisa!
 
Lissu alipita hapo kigongo ferry akaubeza huo mradi lakini mhe Magufuli aliusifia na kueleza umuhimu wake. Ngoja tuone tar 28 wananchi watatuambia.

Mimi ninavyofahamu hilo eneo kwa siku linapitisha magari na watu wengi sana. Kuvuka kwa kivuko inakula kama dk 30 mpaka 45.
 
Si kila daraja lipo kwa ajili ya kupata faida. Mwanza kuna hospitali kubwa ya kanda, unapotumia feri wagonjwa wanachelewa kuvuka na kuhatarisha uhai/afya wao/zao.

Pia kivuko cha feri hakiaminiki si tu kwa usalama lakini pia hata utengemano si muda wote kitakuwa kizima.

Na inawezekana hata kwa mwaka hujawahi kupita katika njia hii ndio maana unabeza.

NOTE: NIMEKUJIBU LAKINI NATAMBUA WAZI UPO MLENGO WA KUPINGA.
 
Si kila daraja lipo kwa ajili ya kupata faida. Mwanza kuna hospitali kubwa ya kanda, unapotumia feri wagonjwa wanachelewa kuvuka na kuhatarisha uhai/afya wao/zao.

Pia kivuko cha feri hakiaminiki si tu kwa usalama lakini pia hata utengemano si muda wote kitakuwa kizima.

Na inawezekana hata hata kwa mwaka usiwahi kupita kwenye njia hii.

NOTE: NIMEKUJIBU LAKINI NATAMBUA WAZI UPO MLENGO WA KUPINGA.
Wajengee hospitality pale walipo, wawe stabilized then ndio wapelekwe bugando. Kusafirisha wagonjwa mahututi ni ushamba. Lisu alipelekwa ubelgiji, je kuna daraja kati ya tz na Ubelgiji.
 
Wajengee hospitality pale walipo, wawe stabilized then ndio wapelekwe bugando. Kusafirisha wagonjwa mahututi ni ushamba. Lisu alipelekwa ubelgiji, je kuna daraja kati ya tz na ubelgiji
Sawa
 
Si kila daraja lipo kwa ajili ya kupata faida. Mwanza kuna hospitali kubwa ya kanda, unapotumia feri wagonjwa wanachelewa kuvuka na kuhatarisha uhai/afya wao/zao.

Pia kivuko cha feri hakiaminiki si tu kwa usalama lakini pia hata utengemano si muda wote kitakuwa kizima.

Na inawezekana hata hata kwa mwaka usiwahi kupita kwenye njia hii.

NOTE: NIMEKUJIBU LAKINI NATAMBUA WAZI UPO MLENGO WA KUPINGA.
Kwa hiyo hela ungeweza kununua feri zaidi ya mbili kama zile za kivukoni na kujenga hospitali kubwa kama Muhimbili kule kule Kigongo. Yani haiingii akilini hata kidogo.
 
Hivi wewe hujui humuimu wa daraja linalounganisha mkoa mmoja na mkoa mwingine, kwanini lakini Chadema mnakuwa hivyo, kabla ya swali lako ungejiuliza umuhimu wa madaraja yafuatayo: Nyerere la Kigamboni, Kikwete la Malagarasi, Mkapa la Rufiji, Wami la mto wami na maeneo hayo yote yalikuwa na vivuko kabla ya ujenzi wa madaraja hayo.
 
Si kila daraja lipo kwa ajili ya kupata faida. Mwanza kuna hospitali kubwa ya kanda, unapotumia feri wagonjwa wanachelewa kuvuka na kuhatarisha uhai/afya wao/zao.

Pia kivuko cha feri hakiaminiki si tu kwa usalama lakini pia hata utengemano si muda wote kitakuwa kizima.

Na inawezekana hata hata kwa mwaka usiwahi kupita kwenye njia hii.

NOTE: NIMEKUJIBU LAKINI NATAMBUA WAZI UPO MLENGO WA KUPINGA.

Suala siyo DARAJA,

je, KIPAUMBELE KWA ENEO LA KANDA YA ZIWA NI DARAJA?
 
Back
Top Bottom