Bagamoyo: Mwanamke ashindwa kuzika mwili wa mumewe. Mgogoro wasababisha afunge geti marehemu alikopaswa kuzikwa na kutokomea kusikojulikana

Bagamoyo: Mwanamke ashindwa kuzika mwili wa mumewe. Mgogoro wasababisha afunge geti marehemu alikopaswa kuzikwa na kutokomea kusikojulikana

Mtu akishakuwa ni mume/mke wa mtu halali mwenzie akitangulia all alobaki ndio wa kupanga ni wapi mume/mke wangu atazikwa! Sio ndugu......ndugu kuingilia kupanga flani azikiwe wapi ndio wana jambo lao
Huo utaratibu ni kwa mujibu wa kabila gani hapa duniani? Au ni kwa mujibu wa dhehebu lipi? Au ni kwa mujibu wa sheria ipi ya nchi hii?
 
Tunaomba picha zake huyu mdada mtata hadi kwa marehemu, mwenzie kafumba macho jenezani yeye anawaza hela.

Nadhan hata alipokuwa hospital alikuwa anauliza kila mara hajafa??

Ila na sisi wanaume tupo wa ajabu sana, unaishije na mtu wa aina hii usione dalili na tabia zote hizi mbaya.

Au madawa ya limbwata????????
Jamaa alikuwa mpole sana na mstaarabu
 
Tukubaliane tu huyo mwanamke ndo kamwondoa mume ili auze nyumba.

Namsikia chumvi hapa akisema mke na ndugu wa mke walifunga geiti la nje na la ndani wakatulia ndani kimya.

Kilichofanyika ni kuvunja kuingiza mwili ndani na kuzika.

Si mama wala mtoto wala wakwe walizika.

Hapa niseme tu, wanawake ziiii
 
Mi yalinikuta kwa hao Wachaga nilibaki kimbaumbau kidogo nidanje, sijui nilitoka vipi ktk lile dimbwi la mauti [emoji849]

Asante sana Mungu kuniokoa [emoji2960]
Huyu ni Mchaga ila kaoa Msukuma, sijui alikosa washauri, wanawake wazuri wapo Moshi, sijui kwa nini alienda kuoa kwa hao washamba na wachawi
 
WOSIA batili.

Wosia ni utashi na maamuzi ya marehemu juu ya mambo aliyo na mamlaka nayo 100% na yanayokubalika kisheria.

Ukifa nyumba inakuwa ya mjane, na mjane hataki kaburi mlangoni. Huna haki ya wosia kutaka kuzikwa hapo.

Na huwezi kusema nikifa mke asiuze nyumba wala asipake rangi ya kijivu wala asiingize ndani ki ben 10. Nyumba si yako tena!

Mjane kata rufaa.
Bush lawyer.
 
Ni UPUMBAVU wa UKRISTO. Uislam hauna huo muda wa sijui tusubiri nini mara vile, ni tunazika na chap mtu anastirika, kuna vitu mnataka kuendekeza havina maana. Ushawahi sikia ujinga kama huo kwa waislam??

Ila kwenye Ukristo utasikia kila sehemu, wala sio wachaga peke yao, Mnawaonea tu ishu hapo ni ujinga wa Dini yenu.

Wekeni misingi imara na sheria imara, MFALME WA OMAN anakufa saa 1 asubuhi na saa 7 mchana anazikwa iwe huyo boya asiyekuwa hata na uhakika wa kuwa na boxer 100??
Waislam ni maarufu wa kugombea maiti!
 
Nisichoelewa ndugu wanaweza kumpangia mjane halali namna ya matumizi ya nyumba yake au wapi amzike mme wake?

Sio ndugu tu, hata yeye marehemu hana haki na nyumba ambayo imechukuliwa na mjane baada ya kufariki.

Umiliki wa joint tenancy wa mke au mme unakoma punde mwanandoa mmoja anapokufa. Aliyebaki anachukua umiliki. Na ndo maana sheria haikubali uandike wosia wa kurithisha mali ya joint tenancy. Hata chumba kimoja huwezi kusema abakiziwe mtoto wangu Athumani aishi na mkewe.

Hii ni kwa sababu nyumba ya joint tenancy haki yake haigawanyiki na haimilikiwi kwa vipande, bali mnaimiliki mazima nyote wawili kwa pamoja. Ukifa haki zote zinahamia kwa aliyebaki.

Kwa hiyo huwezi kujitengea eneo la garden eti kwa ajili ya kaburi lako, pale si kwako tena!

KUZUIA mali ardhi kuuzwa, restraint on alienation, pia kunatajwa kama nia, motive, ya wosia wa marehemu. Hicho kitu kinapingwa vikali na misingi ya common law ya Mwingereza ambayo tuliirithi. Free Market Economy ya Mwingereza na baadae Mmarekani inasemwa ilishamiri baada ya kuruhusu watu kuuziana mali kwa uhuru. Kwa hiyo, kwa taratibu zenye manufaa kwa umma public policy, vipengele vya wosia na mikataba vinavyosema mali isiuzwe vilikuja futwa karne iliyopita.

Mjane yuko sahihi kukataa makaburi mlango wa mbele nyumbani kwake. Hakimu amepotoka.
 
Ni UPUMBAVU wa UKRISTO. Uislam hauna huo muda wa sijui tusubiri nini mara vile, ni tunazika na chap mtu anastirika, kuna vitu mnataka kuendekeza havina maana. Ushawahi sikia ujinga kama huo kwa waislam??

Ila kwenye Ukristo utasikia kila sehemu, wala sio wachaga peke yao, Mnawaonea tu ishu hapo ni ujinga wa Dini yenu.

Wekeni misingi imara na sheria imara, MFALME WA OMAN anakufa saa 1 asubuhi na saa 7 mchana anazikwa iwe huyo boya asiyekuwa hata na uhakika wa kuwa na boxer 100??
Wewe vipi bana acha kutuzingua. Tunachelewa kuzika kwa kuwa bado tuna hakiki cross check huenda marehemu hakufa.
 
tukienda nje ya mada kidogo WACHAGGA wanaushamba wa kijinga mno kuhusu suala la kuzikia manyumbani, serikali inatenga maeneo ya pamoja lakin wao uwa wauchu na mali hawataki kuzikwa mbali na nyumba zao, awa jamaa ni wasomi ila kwenye ili la kuzika manyumbani ni failure,

imagine miaka50 mbeleni uko moshi patakuawaje, kila kona makaburi tupu. ustaharabu wa ovyo kabisa huu
Uzuri makaburi yanahamishika tu. Watu wanasawazisha maisha yanaendelea.
 
Baadhi ya Waombolezaji kwenye msiba wa Kijana Henry Massawe aliyekuwa Mkazi wa Kiaraka Magengeni, Bagamoyo Mkoani Pwani, wamelazimika kuvunja geti la nyumbani kwa Marehemu ili kuingia kumzika baada ya kukuta geti hilo limefungwa huku Mke wake akiwa hajulikani alipo ikiwa ni muda mfupi tu baada ya Mahakama ya Bagamoyo kuamuru Marehemu azikwe Bagamoyo na sio Kilimanjaro kama alivyotaka Mkewe.

Kabla ya kuvunjwa kwa geti hilo Waombolezaji walikuwa wamekaa nje wakati wote na baada ya hapo wakaingia na kuuvunja pia mlango wa nyumba ya Marehemu ili mwili uingizwe sebuleni kama ilivyo taratibu za misiba ya kikristo.

Henry Massawe alifariki January 16, 2023 na mwili wake ulisubiri kuzikwa kwa wakati wote huo kutokana na mgogoro uliokuwepo baina ya Ndugu wa Marehemu waliotaka azikwe nyumbani kwake Bagamoyo huku Mke wa Marehemu akitaka azikwe Kilimanjaro kabla ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Bagamoyo Vedatus Mwalia kuamua kuwa Marehemu azikwe Bagamoyo.

Mahakama ya Bagamoyo mkoani Pwani leo January 24 2023 kuamuru mwili wa Henry Massawe kuzikwa nyumbani kwake Kiaraka, Bagamoyo kama watakavyo Ndugu zake na kutupilia mbali hoja za Mke wake aliyetaka akazikwe Mkoani Kilimanjaro.

Ndugu Jamaa na Marafiki waliojitokeza kwa ajili ya maziko ya Marehemu Henry wamekuta geti la nyumbani kwake limefungwa huku ikielezwa kuwa Mkewe hajulikani alipo.
Akazikwe huko alikozaliwa kama hakutaka kufuata dini ya mke. Nadhani ndio sababu huyo mke kaona aende kwao.
 
Hahaa pole mimi kuna dada alikuja nimsaidie kumuunga app ya mange.

Ni simple sana! VPN/M-pesa na ku install app yake tu basi.

Kwa urahisi jiunge M-pesa Visa card ila usiwe mbahili tu ,kwa huku utakatwa 2400 kwa Mwezi na sio 1000.
Kwa nini umsingizie Dada wakati ni wewe ndio umejiunga ili update umbea wa Mange?

Kwa maelezo haya wewe ni mfuasi nguli wa hiyo app ya Mange.

By the way sioni tatizo lolote, watu kama Mange ni muhimu kwenye jamii yetu, nimesoma post zote mpaka mwisho lakini reference za Mange zimefunga mjadala huu jamaa aliowa shangingi tu.

Mwanamke low profile hawezi kuwepo kwenye page za Mange eti kachafuwq hali ya hewa.

Na ninaposema low profile maana yake unaweza kuwa na maisha makubwa lakini siyo mtu wa spotlight, wengi sura halisi na Picha pamoja na video za Billionaire Bakhressa wa Azzam wameanza kuziona juzi tu, kwa miaka mingi Bakhressa anajurikana kwa jina tu, hata wewe unaweza kuwa ushahidi, hii ndio maana ya low profile ingawa mwenyewe ni high profile.
 
Mambo mengine ni upuuzi tu, huyo alitaka kujimilikisha msiba Ili akapate michango Kwa ndugu zake huko. Ndugu wa Mume wapo sahihi na wasibabaishwe na huyo mke wao.
Nadhani hujaelewa,nadhani angekubali kuzika hapo nyumbani kwake ndio angekua amijimilikisha msiba vizuri kuliko kwenda kuzikwa huko kijijini kwa mumewe,hapo nintamaa ya hilo eneo hakutaka liwe na kaburi ili iwe rahisi hata kuliuza
 
Hii BOMA maana yake nini? Weka kiswahili chake hapa ueleweke, sio wote tunaweza elewa matumizi ya neno hilo.

Nitokako mimi BOMA ni nyumba kubwa isiyoisha. Hapo umemaanisha nini?
Walivyokuwa wanatangaza walitumia neno boma kama sikosei wakimaanisha eneo lililojengwa nyumba yake kama kuna tafsiri nyingine sijajua boss.
 
Back
Top Bottom