Bagamoyo: Mwanamke ashindwa kuzika mwili wa mumewe. Mgogoro wasababisha afunge geti marehemu alikopaswa kuzikwa na kutokomea kusikojulikana

Du mbona tunatishana...
Ila shida nyingine nikuoa mwanamke ambaye ambitions zenu zinalingana..
Bora uchukue pisi ya kijijini au uswazini ambayo ukiionga elfu 30 anaiona nyingi na kuithamini kama umempa milioni..Hadi akija kujanjaruka muda unakuwa umeenda sana..
Hawa wapenda mambo makubwa tuwaachie wakurugenzi, wabunge, mapedeshee, wastaafu n.k
 
Hayana formula,, tutarudi kule kule pa mke mwema hutoka kwa Mungu,, ni maombi tu ndo yatakupa kilicho bora hivi hivi ni ngumu kinoma

Ni kupeana tahadhari tu wala hatutishani, wanaumr mnatuua kwa unyanyasaji wa kimwili km kupiga nk ila sie tunatumia mbinu chafu za kimafia, tutendeane mema tu sio wanawake wote wanaweza kusamehe kwa dhati kabisa
 
Usikariri, Bruce Lee Alifia Hong Kong akazikwa Marekani.
 
Hapana mtu akiamua azikwe kwakwe na mazingira ya kuzika yapo nini shida? Unajua nauli yako kutoka hapo Iringa mpaka unyakyusani ukiwa mzima haizidi 30,000, hapo na chenji unapata lakini ukienda ukiwa maiti million haikuachi salama, na kama unavyojua kifo hakina taarifa kama harusi kwamba utajianda, kuepusha nongwa zote zikwa ulipo
 

Mkuu siwezi kumsingizia dada kama ingekuwa ni mimi maana sijaona tatizo kuwa mfuasi wa mange hata JPM alikuwa anamfatilia,Mama Samia alipiga naye picha ,mange nimemfollow kwenye instagram tu ,app yake naijua ila sijawai kuingia zaidi ya dada kuja kwangu kutaka kumsaidia kujiunga maana aliniambia ni ngumu mno na mimi nikafollow maelekezo nikamsaidia kujiunga,kwangu JF ni zaidi ya Mange App.
 
Mimi nawashangaa watu ambao husema mtu akifa anatakiwa kuzikwa alikozaliwa

Kwa hiyo ukizaliwa hospitali ya Muhimbili unatakiwa kuzikwa wodini Mihimili ulikozaliwa ukifa?
Wee nawee acha kujitoaa ufahamuuu...! Mtu hazikwi alipozaliwaa anazikwaa Kwao kwenye asilii yakee... Kama mchaga utasafirishwa kupelekwa kijijini kweny kwenye asili yenuu..Mbena iringaa kwenu hukoo hata kama ulizaliwaa Marekani.
 
Kufa tutakuzika popote sio unaacha maagizo kibao bila hata nauli
 
Mimi nawashangaa watu ambao husema mtu akifa anatakiwa kuzikwa alikozaliwa

Kwa hiyo ukizaliwa hospitali ya Muhimbili unatakiwa kuzikwa wodini Mihimili ulikozaliwa ukifa?
... kamuulize huyo mwanamke aliyetaka kumpeleka marehemu Moshi badala ya kumzika hapo nyumbani kwao hadi ndugu walipoingilia.
 
Marehemu alishaacha wosia azikwe Bagamoyo. Mke ndo amegoma kwa sababu za kibiashara. Mahakama imetoa amri mke ametoroka hajazika mumewe. Na hapo awali mke alishafumaniwa na picha zake zilichafua hali ya hewa kwa mange
Aiseeee [emoji15] [emoji15] sasa imekula kwake mazima...
 
Hujaelewa story ww.

Mwanamke kama hana roho mbaya asingehamia kwa huyo jamaa hata wiki tu haijaisha, na inasemekana mwanamke alichangia kumfilisi mmewe akaenda kuwekeza kwa huyo fala
UGONI sio kesi kwa sheria za Tanzania. Mwanamke ku chiti hakufuti haki miliki yake ya nyumba ya wanandoa iitwayo Joint Tenancy with Right of Survivorship.

Joint Tenancy with Right of Survivorship inahamisha haki zote za umiliki kwenda kwa mjane au mgane. Haigawanyi umiliki kama hisa, na hata kama ni jengo la apartment la uniit 20 huwezi kusema unit 10 au hata moja ni yangu nampa mwanangu nikiwa hai au nimekufa.

Na wote tunafahamu mkataba wa mauzo ya nyumba ya wanandoa bila idhini na saini ya mwenzio ni mkataba batili. Na wosia pia ni batili.

Uko hai huna maamuzi, ukifa ndio unao? Ukifa huna chako! Huwezi kuandika wosia juu ya kitu ambacho sio chako peke yako. Utazikwaje kwenye ki garden mlangoni kwa nyumba ya mwenzio?

Ukisikia maneno "nyumba ya wanandoa" shtuka! Ile ni dhana nzito yenye jina kisheria, inaitwa Joint Tenancy with the Right of Survivorship. Usibweteke na itifaki nzito ya kuitwa " baba mwenye nyumba," there is no such thing.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…