Baharia; (Ujasusi, Mapenzi na Upelelezi wa kutisha)

Baharia; (Ujasusi, Mapenzi na Upelelezi wa kutisha)

RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA.

SEHEMU YA SABA


Aligwaya mwanamke yule ambae taratibu uzito wa mwili wake ulianza kupungua.

“Nadhani umeona mlichokubaliana na huyo bae wako, sina mwanamke anaeitwa Vedi ila nina mwanamke anaeitwa marehemu Vedi. Si ndivyo ulitaka?” Alimaliza kwa kuhoji bwana Juma.

“Tafadhali Jay naomba unisikilize mpenzi wangu” Alisema Vedi kwa kusihi.

“Huna cha kunambia, nawahi msibani nikamzike mpenzi wangu” Jay alisema na kuendea mlango.

“Nooo!! Ja….” Hakumalizia kauli yake alijikuta peke yake ndani ya chumba huku akisikia mlango ukifungwa kwa nguvu na kutoa kelele za malalamiko huku mfungaji akiufunga kwa hasira.

Vedi alijikuta peke yake chumbani na badala ya kujadili kilichomleta na kusaidiwa mawazo ila amejikuta akikutana na jambo jipya kabisa.

Hakujua habari zile za uongo ni nani aliempa mchumba wake na aliempa alilenga nini.

Hakika ulikuwa ni mtihani usiojibika.

***

Vedi alitumia zaidi ya nusu saa akiwa amekaa chini huku akilia na alishindwa kabisa kuelewa ni kitu gani hasa kilikuwa kinaendelea katika siku mbili zile.

Alichoka kulia na alinyanyuka chini kisha akachukua maji ya kuoga na kuelekea bafuni kuoga na alipomaliza alibadili nguo na kuvaa nguo zake ambazo huwa anaziacha nyumbani kwa mchumba wake kama dharura tu.

Alivaa gauni refu na kwa ndani aliamua kuvaa suruali na kisha akajifunga mtandio na aliporidhika akataka kutoka na hapo akakumbuka kitu, akaamua kufungua droo ya kitanda na kutoa simu ndogo.

Alijua simu ile huwa inakuwa pale siku zote na ni baada ya kukosa matumizi kwa wahusika wake.

Akatoa laini mpya aliokuwa ameisajili na kuiweka, kisha akawasha simu na ikafanya kazi, akaweka vocha na kupiga namba alizochukua kwenye kitabu cha Banzi.

Alipiga simu na simu ikabaki ikiita bila kupokelewa na hatimae ikakata.

Akapiga tena!

Ikaita muda mrefu na hatimae ilipokelewa na mpokeaji alikaa kimya.

Vedi nae akakaa kimya kwanza.

Kutegeana kwao kuongea, hatimae aliepigiwa akauliza.

“Nani!?”

Vedi akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha akajibu.

“Naitwa binti Mashimo”

“Ndio nikusaidie nini” Alihoji mpokeaji.

“Bila shaka naongea na Mamu?” Alihoji Vedi.

Upande wa pili ukaguna kisha kwa jaziba akasema.

“Wewe ni askari; mgambo ama bado mnanifuatilia?”

Zilikuwa ni sentesi mbili zenye maana mbili tofauti.

Aliuliza kama ni askari aliepiga, lakini pia aliuliza kama ni wanaomfuatilia.

Kina nani?

Vedi alikosa jibu katika maswali aliojiuliza.

“Mimi si yeyote kati yao Dada” Alijibu Vedi.

“Ila ni nani na wataka nini!?” Alifoka tena.

“Samahani dada naomba kukuona tafadhali!” Vedi alisema kwa kusihi.

Upande wa pili ukakaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha ukasikika.

“Shida gani hadi tuonane na unahisi ni lazima kuonana?”

“Ni kuhusu Banzi Kela!” Vedi aliamua kutupa jiwe gizani na kweli lilimpata mtu.

Vedi alisikia mtu yule akipandisha na kushusha pumzi kwa haraka yani ni kama mtu alietoka usingizini na kubanwa na kichomi cha gafla.

“Unasema nini wewe!” Alihoji Mamu.

“Simu si salama dada naomba tuonane tafadhali” Alisihi Vedi.

Mamu aliongea kama ambae hataki watu wengine wasikie anachomwambia binti Mashimo.

“Sasa sikia, jitahidi ufike Hard Rock Café saa moja jioni, ukichelewa hautonikuta” Alisema Mamu na kukata simu.

Vedi akabaki akiiangalia ile simu kama vile haamini kama ni simu au ni mdoli.

Hard Rock Café!
Akalitamka tena lile jina.
Kama aliegutushwa na kitu akaudaka mkoba wake na kutoa kitabu cha kumbukumbu alichokichukua ndani ya meli.

Akakifunua kurasa kadhaa na hatimae akapata kile alichokitaka.

Ulikuwa ni ukurasa uliokuwa na jina lile la Hard Rock Café lakini pia kulikuwa kuna jina la mtu au jina la kitu chenye uhai; Jezebeli.

Vedi hajawahi kukutana na jina hilo la Jezebeli wala hakuwahi kusikia mtu akiitwa hilo jina na halikufanania kuwa la mtu, ila litakuwa linatumika kwa kiumbe kilichohai au kumaanisha jambo.

Jambo gani; Vedi hakujua kabisa bali akaamua kupitisha tu ya kuwa linatumika kwa kiumbe hai.

Sasa kwa nini limeandikwa kwenye kitabu hiki na lina husishwa na mgahawa ule maarufu ndani ya jiji la Dar?

Hakukuwa na wa kumjibu.

Vedi akatazama saa ukutani.

“Ooh my God!!” Vedi alilalama.

Ilikuwa ni saa tisa na nusu mchana na alijua ni huo muda ambao kulikuwa kuna mazishi ya mtu kama yeye.

“Inamaana kweli watu wote wanaamini nimekufa kweli? Lakini mbona…mh…

Vedi alimalizia kwa kuguna, kuna kitu kilipita kichwani mwake.

Alipoenda kwa dada yake Msangu alikutana na taharuki na mwishowe dada yake akamkimbia na halikadhalika alipofika nyumbani kwao watu walimkimbia, lakini kwa nini Juma yeye hakustuka wala kushangaa alipoingia ndani.

Inaweza kuwa ni kwa zile jumbe na picha? Hapana kuna kitu mimeona machoni mwa Jay; Jay namjua vyema kuna kitu…aah..kitu gani sasa?

Vedi alijiuliza bila kupata majibu.

Vedi aliwaza tena kwenda nyumbani kwao, ila aliogopa kuzua mtafaruku mkubwa zaidi, akachukua tena simu yake na kupiga simu ya baba yake baada ya kunakili namba alizokariri.

Simu iliita bila kupokelewa.

Akanakili namba za Mama yake; nazo alipiga hazikupokelewa.

Akaweka simu kwenye mkoba wake na kujilaza kitandani huku akikadiria muda wa kuamka ili asichelewe miadi yake na Mamu.

****

Juma ama Jay kama alivyoitwa na mchumba wake Vedi; baada ya kutoka ndani na kupigiza mlango, alielekea barabarani moja kwa moja kwa lengo la kupanda daladala awahi mazishini. Alikuwa akitembea huku akilia kiume, alilia bila kutoa machozi.

Kuna kitu kilikuwa kinamsumbua rohoni mwake na kitu kile kilizidi hasa baada ya kumuona Vedi.

Alisimama njiani huku akijishauri ni kama arudi nyumbani kwake azungumze na Vedi ama aende msibani atoe taarifa za kuwepo Vedi ama afanye nini!

Alikumbuka sauti ya Dr Masimba.

Alitamani siku zirudi nyuma na aone kama ni ndoto tu ya mambo yale mabaya anayoyashiriki bila ridhaa yake.

Akajiuliza ni kwanini alienda kupima kwenye hospitali binafsi ya Dr Masimba ilioko hapo mbagala?

Jay alilaani kitendo alichofanyiwa ndani ya hospitali ile.

Usiku wa ndoa ya rafiki yao Nyamizi yeye hakuhudhuria sababu alikuwa anajihisi ni mgonjwa na aliona bora aende Vedi peke yake,na kulipokuchwa akaamkia kwenye hospitali binafsi ya Dr Masimba iliokuwa Mbagala rangi tatu karibu na kituo cha mabasi; hospitali ambayo ilikuwa ni maarufu sana kwa huduma zake za uhakika na kujali wateja.

Akapanda bodaboda na ilimfikisha hadi hapo hospitali na baada ya taratibu zote kukamilika alielelekea chumba cha maabara ili akachukuliwe vipimo.

Akiwa kule maabara, taratibu zote zilifuatwa na akachukuliwa vipimo na kijana mmoja ambae baada ya kumchukua kiasi kidogo cha damu alielekea chumba maalumu kwa ajili ya upimaji wa sampo ile ya damu.

Kijana yule hakukawia sana, akarejea na kumuomba Jay aelekee chumba namba kumi kilichokua kushoto mwa maabara ile.

Alijua anaenda kupata majibu yake ila alienda kikutana na zaidi ya majibu ambayo yanamwendesha katika maisha yake! Majibu ambayo yalibadili maisha yake kabisa.

Akiwa hana wasiwasi aliingia hadi kwenye chumba kile na alikutana na Dr Masimba mwenyewe na akiwa na watu wengine watatu ambao nyuso zao hazikuonekana kuwa na usalama.

Alipoingia mmoja wa watu wale akaruka na kuukomea mlango kwa ndani.

Jambo lile lilimpa wasiwasi Jay; akataka kufungua ili atoke, ila kasi yake haikuwa sawa na kasi ya mtu yule aliekuwa ameufunga mlango.

Akawa kumzuia!

“Vipi bwana mdogo, haujitaji majibu ya vipimo vyako?” Alihoji mtu mwingine ambae alikuwa amevaa miwani na kofia ya Pama huku akiwa amevaa na koti licha ya hali ya hewa kuonekana ni joto na jua kali.

“Sasa majibu ya vipimo ndo hutolewa hivi?” Alihoji Jay.

“Relax bwana mdogo, taratibu kwanza!!” Alisema Dr Masimba ambae Jay alimfahamu kwa kuwa alikuwa akifika pale mara kwa mara kuangalia afya yake.

“Majibu yaonenesha unaumwa maralia kali sana” Alisema Dr.

Jay baada ya kusikia vile akasimama na kuaga.

“Mbona unaharaka sana komredi, hatujamaliza bado” Alisema yule mtu ambae alikuwa amevaa kofia na miwani usoni.

“Mbali na majibu yako, ila na sisi tuna letu jambo” Alisema jamaa alievaa miwani na kofia ya pama kisha akaendelea.

“Mkeo Vedi; ametuibia, ila kabla hatujamfikia inabidi uwe daraja kwanza”

“Kawaibia nini na mmejuaje mi ndo mumewe?” Aliuliza Jay huku akitetemeka.

“Kwa sasa hatutakwambia alichotuibia, ila unachotakiwa kufanya ni kuwa upande wetu tu, endapo alivhokiiba kikiwa na madhara kwetu” Alisema yule bwana.

“Sasa nitakubali vipi kuwa nanyi ikiwa sijui kimemtokea nini na nyinyi ni kina nani?” Alisema Jay.

Na hapo yule mtu alicheka kidogo huku wengine wakiwa kimya muda wote kama hawamo mle ndani.

“Kwa sasa hupaswi kujua ila hadi tujiridhishe upo upande wetu, na ili uwe upande watu inabidi tukuongezee ugonjwa mwingine” Alisema yule bwana.

Baada ya kusema vile Jay alishangaa akishikwa kwa nguvu na zile njemba mbili ziliokuwa mle chumbani kisha yule aliekuwa amevaa miwani alimfunga na karatasi yenye gundi mdomoni ili asipige kelele,kisha Dr Masimba alisimama na kuchukua sindano iliokuwa kenywe mkebe na ilikuwa na dawa kwenye bomba lake.

Akamfuata Jay ambae alikuwa ameshikwa vyema licha ya kujitikisa kwa uoga bila mafanikio.

Sindano ilizama kwenye nyama na kisha ikasukumwa dawa yote iliokuwa mle na Jay alibaki akiona kizunguzungu huku macho yake yakishindwa kuona vyema, alitamani kuongea ila alishindwa, alitamani kulia napo alishindwa, akajibweteka kwenye kiti baada ya kuachiwa
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA NANE



Baada ya kusema vile Jay alishangaa akishikwa kwa nguvu na zile njemba mbili ziliokuwa mle chumbani kisha yule aliekuwa amevaa miwani alimfunga na karatasi yenye gundi mdomoni ili asipige kelele,kisha Dr Masimba alisimama na kuchukua sindano iliokuwa kenywe mkebe na ilikuwa na dawa kwenye bomba lake.

Akamfuata Jay ambae alikuwa ameshikwa vyema licha ya kujitikisa kwa uoga bila mafanikio.

Sindano ilizama kwenye nyama na kisha ikasukumwa dawa yote iliokuwa mle na Jay alibaki akiona kizunguzungu huku macho yake yakishindwa kuona vyema, alitamani kuongea ila alishindwa, alitamani kulia napo alishindwa, akajibweteka kwenye kiti baada ya kuachiwa.

Alihisi kichwa kikiwa kizito na mwili mzima ukipitiwa na ubaridi wa ajabu huku maungio ya mifupa yake ikizizima kwa ubaridi ule, ni kama akili yake iliganda mana hakusikia kitu wala kuona kitu,alikaa kama sanamu la ibada.

Hakujua amekaa koma muda gani, ila alikuja kupata fahamu na kujikuta akiwa amelala kwenye kitanda cha wagonjwa na mwili wake ukiwa imara ni kama hakujatokea kitu muda mfupi uliopita.

Akainuka kitandani na kukutana na sura za watu wawili wakiwa wamemsimamia.

Walikuwa ni wale wawili wenye kuvaa nguo za kufanana na Dr Masimba pamoja na yule bwana anaevaa miwani hawakuwemo.

Akabaki akiwatizama.

“Umeamka na unajisikia vizuri bila shaka” Alihoji jamaa mmoja.

Jay hakujibu.

“Sasa sikiliza,sindano uliochomwa imekuondolea maralia yako ila imekupa ugonjwa wa kansa ya mifupa” Alisema bwana mwingine tena.

Jay alisimama kwa jaziba na kumvaa jamaa yule, ila alitulizwa chini kwa jebu moja na akabaki akilia kwa uchungu na kujibweteka kitandani kama zoba.

“Aliekuponza ni Vedi; ila usijali, kuna tiba yake na tutakupatia hadi ukifanikisha yale tunayoyataka na kikubwa zaidi uoneshe kufunga mdomo na ukijaribu kusema lolote, tumekuwekea kifaa kitakachokuwa kinatupa taarifa ya mazungumzo yako popote” Alisema jamaa mwingine aliempiga jebu Juma.

Jay aliiunua uso na kuwatazama watu wale na alipojaribu kusema kitu,alijikuta anashindwa kusema na kubaki akilia kwa uchungu.

“Umepandikwa kirusi Flora na kinakula chembe hai nyekundu na ndani ya siku kumi usipopata tiba unakufa, hivyo ni muhimu ufanye tunachokuagiza ili uokoe maisha yako” Alisema tena yule jamaa.

Wakiwa bado wanazungumza mara akaingia yule mtu anaependa kuvaa koti na miwani wakati wote.

“Nadhani mwacheni aende, na maelekezo tutampa kwenye simu” Yule bwana alizungumza na kisha akamgeukia Jay.

“Bwana mdogo;ili usaidike inahitajika utimize tunayoyahitaji na hivi sasa maisha yako yapo kwetu, usiripoti kituo chochote cha polisi na usifanye ujinga wowote ule, nenda kapumzike ujumbe wako utaukuta kwenye simu na endapo Vedi akitokea fanya kile tutakachoakuagiza” Alisema tena bwana yule na punde akaingia mtu mwingine na kumwamuru Jay asimame waondoke pale ndani.

Jay hakuwa mbishi baada ya kugundua yupo kwenye mikono isio salama.

Lakini alijiuliza swali moja!

Kwanini wamtumie yeye kwenye matatizo yao na Vedi?; Vedi kachukua nini muhimu kwa watu hawa?.
Hakupata jibu hata kidogo na alitoka akiwa hana amani ya mwili wake na alihitaji kukaa na kutafakari kuhusu jambo lile.

Hakika alipagawa.

Baada ya kutoka kwenye kile chumba, walibaki watu watatu, ambao ni yule bwana mvaa kofia; koti na miwani pamoja na wale vijana ambao walipenda kuvaa nguo za kufanana wakati wote.

“Sasa Cholo unaamini hii itasaidia?” Alihoji kijana mmoja huku akimtizama yule jamaa anaependa kuvaa kofia na miwani ambae ndie Cholo.

“Panga; tukisema tumuue yule binti hivi sasa kiukwelii, itatupa shida, hatujui hadi hapo kawasiliana na nani baada yakuiona ile maiti, kikubwa ni kufunga mianya yote kisha tutajua cha kumfanya tukiwa na uhakika wa zilipo taarifa za yale alioyaona,kama isingekuwa kadi ya harusi aliodondosha mule na kisha kuchukua kile kitabu nilichokisahau pale, tusingejua lolote kuhusu mtu alieona ile maiti ya Baharia” Cholo alimweleza Panga.

Panga alitikisa mabega na kumwangalia mwenzie.

“Gomba unaonaje hizi mbinu”Cholo alimhoji Muki ambae alikuwa amekaa kimya muda wote.

“Tutazame mienendo yake, akileta utata ile mbinu yetu ya siku zote itamfaa bila shaka” Gomba alijibu na wote wakatabasamu mule ndani na kutoka nje wakikiacha chumba kikiwa kipweke kabisa.

**

Jay alijipiga kichwani baada mawazo yale kumpitia kwa kasi na kubaki akiwa amesimama barabarani bila kujua ametumia muda gani kuwaza yaliompata hadi kupelekea kumkana mpenzi wake wakati huu aliohitaji msaada wake.

Akajitazama na kuona alivyopendeza.

“Eti naenda kumzika Vedi niliemwacha ndani kwangu” Alijiwazia kwa uchungu huku akipiga hatua na kuelekea barabara kuu ili apate uber.

Lakini wale jamaa ni kina nani hasa na Vedi kawafanya nini?

Alijuliza tena huku akishindwa kuyazuia machozi yalioanza kumtoka.

Hakufika barabarani, mara mbele yake ikasimama gari nyeusi na vioo vikashushwa.

Walikuwa ni Gomba aliekuwa dereva na Panga aliekuwa nyuma amekaa.

“Bila shaka unahitaji msaada wa usafiri kwenda msibani!” Alisema Panga.

Jay alibaki akitetemeka baada ya kuwaona wale jamaa ambao ndani ya siku mbili waligeuka kuwa waongoza maisha yake.

“Njoo twende na tafadhali kuwa mtu wa majonzi, wewe ni mfiwa ujue” Alisema Gomba.

Jay hakuwa na namna akafungua mlango na kuingia, na hapo akagundua kulikuwa kuna mtu wa tatu na alikuwa ni Cholo.

“Tunaenda msibani; ila jitahidi sana usioneshe tofauti kama unavyofanya hivi hapo njiani bwana mdogo” Cholo aliasa.

“Lakini kwa nini mnatufanyia yote haya?” Alihoji Jay.

“Kwa sasa wewe bado mdogo ila ukikuwa utajua ndevu za wazee hazichezewi na nzi” Alisema Cholo kwa fumbo ambalo linahitaji akili kulifumbua.

Safari yao ilikuwa ni ya kimya kingi kuliko maneno na baada ya foleni za hapa na pale, hatimae walifika.

“Gomba utaongozana na huyu bwana mdogo” Aliagiza Cholo.

“Kwanini msiniache peke yangu aisee” Jay alisema huku akianza kushuka.

Cholo alicheka kidogo.

“Hadi hapo tushakuona una roho ndogo, hivyo hatuwezi kukuamini hata kidogo.” Cholo alisema huku akijiweka sawa bila kuonesha dalili ya kushuka.

Gomba alishuka na waliongozana na Jay kuelekea kwenye nyumba ya Mzee Mashimo.

“Hakikisha mimi na wewe tunakuwa marafiki na mtu asijue tofauti zetu” Gomba alimuonya Jay huku wakidi kusonga.

Walifika hadi getini kulipokuwa na watu wawili kwa ajili ya kuongoza wageni wanaofika na mmoja kati yao alimfahamu Jay na hivyo alimsindikiza hadi ndani na kisha yeye kurudi.

“Kwa hiyo hadi ndani unataka kuingia?” Jay alimgeukia Gomba.

“Ulipo nipo bwana mdogo na usisahau mimi ni rafiki yako” Gomba alijibu huku akitabasamu kama kwamba ni jambo la kawaida tu analozungumzia.

Waliingia ndani na kuona jeneza likiwa limewekwa sebuleni huku wamama wakiwa wamelizunguka na nyuso za majonzi.

Msangu ambae ni dada yake Vedi alisimama baada ya kumuona shemeji yake akiwa ameongozana na mtu mwingine ambae hakumfahamu kabisa.

Msangu aliangusha chozi baada ya kumuona shemeji yake.

Jay nae aliangusha chozi, ila chozi lake lilikuwa lina mengi ndani yake.

Gomba alikuwa akiangaza na alimuona mwanamke mmoja akiwa amekaa sambamba na waombolezaji, mwanamke yule alimpa ishara fulani na Gomba alielewa mambo hayako sawa pale.

Msangu alimshika mkono Jay na akamwongoza kuelekea chumbani kwa wazazi wake na Gomba nae akafuata.

“Tafadhali, kuna muda inabidi utumie akili kuliko nguvu” Jay alimkoromea Gomba kwa sauti ya chini ila iliojaa jaziba. Gomba akasimama na kutafuta sehemu na kukaa pamoja na waombolezaji wengine.

Jay aliingizwa kule chumbani na kumkuta mama yake Vedi akiwa mkavu usoni huku akiwa hana hata chembe ya chozi.

Mama msangu alisimama baada ya kumuona Jay.

“Na wewe unaamini mkeo kafa kweli?” Mama msangu alihoji na Jay alishindwa cha kujibu.

Mama Msangu alianza kuongea kwa sauti huku akionekana dhahiri kutokukubaliana na suala lile la kifo cha Vedi hata pale ambapo Jay alitaka kutetea hoja ya kifo kile Mama yule alikataa kata kata na hatimae alimshika mkono Jay.

“Mwanangu twende nikuoneshe kitu; Mkeo hakuwa na mwanya kabisa licha ya kujitahidi kufanana ila nimemgusa midomo yake japo watu wamenizuia” Alisema Mama msangu huku akimshika akitembea kuelekea sebuleni.

Na walipotoka watu wakawatazama, Mama yule hakujali na akaelekea lilipo jeneza.

Gomba aliona kitendo kile na tayari alishaambiwa na yule mwanamke aliekuwa pale msibani kinachoendelea, haraka akasimama na kushika mfukoni na akapiga hatua ndefu hadi akawafikia na kwa kuwa Mama msangu alikuwa ameshika mfuniko wa jeneza;wamama wengine nao wakaanza kusogea kumkataza mana alishavuruga huko nyuma na hawakutaka kabisa aliguse jeneza lile,lakini kasi ya Gomba ilikuwa ni kubwa na kwa wepesi akamshika mkono Mama Msangu na Mama Msangu hakutaka kuzuiwa hivyo akautoa mkono ule na kutaka kuufuangua mfuniko wa jeneza.

Mara akasita na kujishika kichwa na kuanguka chini.

Haikupita dakika moja akainuka, ila aliinuka kwa mtindo wa ajabu, aliinuka kwa kujikuna huku akicheka na kuunguruma kama simba na kuongea maneno yasiyoeleweka.

Watu walijawa na taharuki na vilio vilianza upya.

Jay aliona tukio lile ila hakujua Gomba kwa nini alimshika mkono mama yake huyo.

“Wewe bwege umemfanya nini huyu mama?” Jay alifoka kwa jaziba licha ya kujizuia sauti isitoke.

Gomba akainua mabega kukataa.

Jay akamshika ukosi wa shati.

Ukaanza mvutano na mparanganyiko ndani ya nyumba ya mzee mashimo.

Mama Msangu anajikuna na kuunguruma hovyo huku Jay akiwa anavutana na rafiki yake wa bandia,watu nao wamebaha kwa yanayoendelea.

Jay alikuwa amegeuka mbogo alijua kabisa kuna kitu kimefanywa na Gomba kwa Mama msangu.

Yule mwanamke aliekuwa miongoni mwa waombolezaji akasogea hadi nyuma ya Jay na kama anaetaka kujifunia kanga aliojitanda akampiga pigo moja la kisogo bila mtu kugundua kilichotokea na akajitandua kanga na kujitanda tena.

Jay akalegea na kwenda chini kama gunia la chawa wa jaani.

Gomba akapaza sauti ya hamaniko huku akiwa amemshika Jay na watu walizidi kuchanganyikiwa zaidi.

Gomba akaomba kupiga simu ya dharura ili watu wale wawahishwe hospitali; Wazo lake liliungwa na wengi waliokuwapo pale ndani na akapiga simu.

***

Dakika thelathini zilipita na gari la wagonjwa lilifika pale na haraka haraka wauguzi wa huduma ya kwanza walishuka na kuwabeba Jay na Mama Msangu na Msangu na Baba yake walikataliwa kuingia ndani ya gari lile kwa kisingizio ni dogo halitoshi msindikizaji.

Mazishi yaliingiliwa na taharuki, ratiba ikabadiliswa hadi ijulikane mstakabali wa afya za walengwa wa marehemu.

Ajabu nyingine ni kuwa; taharuki ilibeba mawazo ya watu kiasi hakuna aliekumbuka kufuatilia gari lile linaelekea hospitali gani.

Watu waliendelea na malumbano yasioyo na tija.

Lakini wangejua yanayoenda kuwapata ndugu zao, hakika wasingebishania ratiba ya mazishi ya maiti bandia.

**

Weka komenti yako ili iwafikie watu wengi zaidi.
 
Kazi nzuri mkuu kikubwa imeandikwa katika ustadi mkubwa sana japo naona hii vipande vyake ni vifupi kidogo ukiringanisha na ile ya Somalia nk
 
RIWAYA; BAHARIA
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660
SEHEMU YA NANE
Baada ya kusema vile Jay alishangaa akishikwa kwa nguvu na zile njemba mbili ziliokuwa mle chumbani kisha yule aliekuwa amevaa miwani alimfunga na karatasi yenye gundi mdomoni ili asipige kelele,kisha Dr Masimba alisimama na kuchukua sindano iliokuwa kenywe mkebe na ilikuwa na dawa kwenye bomba lake.
Akamfuata Jay ambae alikuwa ameshikwa vyema licha ya kujitikisa kwa uoga bila mafanikio.
Sindano ilizama kwenye nyama na kisha ikasukumwa dawa yote iliokuwa mle na Jay alibaki akiona kizunguzungu huku macho yake yakishindwa kuona vyema, alitamani kuongea ila alishindwa, alitamani kulia napo alishindwa, akajibweteka kwenye kiti baada ya kuachiwa.
Alihisi kichwa kikiwa kizito na mwili mzima ukipitiwa na ubaridi wa ajabu huku maungio ya mifupa yake ikizizima kwa ubaridi ule, ni kama akili yake iliganda mana hakusikia kitu wala kuona kitu,alikaa kama sanamu la ibada. Hakujua amekaa koma muda gani, ila alikuja kupata fahamu na kujikuta akiwa amelala kwenye kitanda cha wagonjwa na mwili wake ukiwa imara ni kama hakujatokea kitu muda mfupi uliopita.
Akainuka kitandani na kukutana na sura za watu wawili wakiwa wamemsimamia.
Walikuwa ni wale wawili wenye kuvaa nguo za kufanana na Dr Masimba pamoja na yule bwana anaevaa miwani hawakuwemo. Akabaki akiwatizama.
“Umeamka na unajisikia vizuri bila shaka” Alihoji jamaa mmoja.
Jay hakujibu.
“Sasa sikiliza,sindano uliochomwa imekuondolea maralia yako ila imekupa ugonjwa wa kansa ya mifupa” Alisema bwana mwingine tena.
Jay alisimama kwa jaziba na kumvaa jamaa yule, ila alitulizwa chini kwa jebu moja na akabaki akilia kwa uchungu na kujibweteka kitandani kama zoba. “Aliekuponza ni Vedi; ila usijali, kuna tiba yake na tutakupatia hadi ukifanikisha yale tunayoyataka na kikubwa zaidi uoneshe kufunga mdomo na ukijaribu kusema lolote, tumekuwekea kifaa kitakachokuwa kinatupa taarifa ya mazungumzo yako popote” Alisema jamaa mwingine aliempiga jebu Juma. Jay aliiunua uso na kuwatazama watu wale na alipojaribu kusema kitu,alijikuta anashindwa kusema na kubaki akilia kwa uchungu.
“Umepandikwa kirusi Flora na kinakula chembe hai nyekundu na ndani ya siku kumi usipopata tiba unakufa, hivyo ni muhimu ufanye tunachokuagiza ili uokoe maisha yako” Alisema tena yule jamaa.
Wakiwa bado wanazungumza mara akaingia yule mtu anaependa kuvaa koti na miwani wakati wote.
“Nadhani mwacheni aende, na maelekezo tutampa kwenye simu” Yule bwana alizungumza na kisha akamgeukia Jay.
“Bwana mdogo;ili usaidike inahitajika utimize tunayoyahitaji na hivi sasa maisha yako yapo kwetu, usiripoti kituo chochote cha polisi na usifanye ujinga wowote ule, nenda kapumzike ujumbe wako utaukuta kwenye simu na endapo Vedi akitokea fanya kile tutakachoakuagiza” Alisema tena bwana yule na punde akaingia mtu mwingine na kumwamuru Jay asimame waondoke pale ndani.
Jay hakuwa mbishi baada ya kugundua yupo kwenye mikono isio salama.
Lakini alijiuliza swali moja!
Kwanini wamtumie yeye kwenye matatizo yao na Vedi?; Vedi kachukua nini muhimu kwa watu hawa?.
Hakupata jibu hata kidogo na alitoka akiwa hana amani ya mwili wake na alihitaji kukaa na kutafakari kuhusu jambo lile.
Hakika alipagawa.
Baada ya kutoka kwenye kile chumba, walibaki watu watatu, ambao ni yule bwana mvaa kofia; koti na miwani pamoja na wale vijana ambao walipenda kuvaa nguo za kufanana wakati wote.
“Sasa Cholo unaamini hii itasaidia?” Alihoji kijana mmoja huku akimtizama yule jamaa anaependa kuvaa kofia na miwani ambae ndie Cholo.
“Panga; tukisema tumuue yule binti hivi sasa kiukwelii, itatupa shida, hatujui hadi hapo kawasiliana na nani baada yakuiona ile maiti, kikubwa ni kufunga mianya yote kisha tutajua cha kumfanya tukiwa na uhakika wa zilipo taarifa za yale alioyaona,kama isingekuwa kadi ya harusi aliodondosha mule na kisha kuchukua kile kitabu nilichokisahau pale, tusingejua lolote kuhusu mtu alieona ile maiti ya Baharia” Cholo alimweleza Panga.
Panga alitikisa mabega na kumwangalia mwenzie.
“Gomba unaonaje hizi mbinu”Cholo alimhoji Muki ambae alikuwa amekaa kimya muda wote.
“Tutazame mienendo yake, akileta utata ile mbinu yetu ya siku zote itamfaa bila shaka” Gomba alijibu na wote wakatabasamu mule ndani na kutoka nje wakikiacha chumba kikiwa kipweke kabisa. **
Jay alijipiga kichwani baada mawazo yale kumpitia kwa kasi na kubaki akiwa amesimama barabarani bila kujua ametumia muda gani kuwaza yaliompata hadi kupelekea kumkana mpenzi wake wakati huu aliohitaji msaada wake.
Akajitazama na kuona alivyopendeza.
“Eti naenda kumzika Vedi niliemwacha ndani kwangu” Alijiwazia kwa uchungu huku akipiga hatua na kuelekea barabara kuu ili apate uber.
Lakini wale jamaa ni kina nani hasa na Vedi kawafanya nini?
Alijuliza tena huku akishindwa kuyazuia machozi yalioanza kumtoka.
Hakufika barabarani, mara mbele yake ikasimama gari nyeusi na vioo vikashushwa.
Walikuwa ni Gomba aliekuwa dereva na Panga aliekuwa nyuma amekaa.
“Bila shaka unahitaji msaada wa usafiri kwenda msibani!” Alisema Panga.
Jay alibaki akitetemeka baada ya kuwaona wale jamaa ambao ndani ya siku mbili waligeuka kuwa waongoza maisha yake.
“Njoo twende na tafadhali kuwa mtu wa majonzi, wewe ni mfiwa ujue” Alisema Gomba.
Jay hakuwa na namna akafungua mlango na kuingia, na hapo akagundua kulikuwa kuna mtu wa tatu na alikuwa ni Cholo.
“Tunaenda msibani; ila jitahidi sana usioneshe tofauti kama unavyofanya hivi hapo njiani bwana mdogo” Cholo aliasa.
“Lakini kwa nini mnatufanyia yote haya?” Alihoji Jay.
“Kwa sasa wewe bado mdogo ila ukikuwa utajua ndevu za wazee hazichezewi na nzi” Alisema Cholo kwa fumbo ambalo linahitaji akili kulifumbua.
Safari yao ilikuwa ni ya kimya kingi kuliko maneno na baada ya foleni za hapa na pale, hatimae walifika.
“Gomba utaongozana na huyu bwana mdogo” Aliagiza Cholo.
“Kwanini msiniache peke yangu aisee” Jay alisema huku akianza kushuka.
Cholo alicheka kidogo.
“Hadi hapo tushakuona una roho ndogo, hivyo hatuwezi kukuamini hata kidogo.” Cholo alisema huku akijiweka sawa bila kuonesha dalili ya kushuka.
Gomba alishuka na waliongozana na Jay kuelekea kwenye nyumba ya Mzee Mashimo.
“Hakikisha mimi na wewe tunakuwa marafiki na mtu asijue tofauti zetu” Gomba alimuonya Jay huku wakidi kusonga.
Walifika hadi getini kulipokuwa na watu wawili kwa ajili ya kuongoza wageni wanaofika na mmoja kati yao alimfahamu Jay na hivyo alimsindikiza hadi ndani na kisha yeye kurudi.
“Kwa hiyo hadi ndani unataka kuingia?” Jay alimgeukia Gomba.
“Ulipo nipo bwana mdogo na usisahau mimi ni rafiki yako” Gomba alijibu huku akitabasamu kama kwamba ni jambo la kawaida tu analozungumzia.
Waliingia ndani na kuona jeneza likiwa limewekwa sebuleni huku wamama wakiwa wamelizunguka na nyuso za majonzi.
Msangu ambae ni dada yake Vedi alisimama baada ya kumuona shemeji yake akiwa ameongozana na mtu mwingine ambae hakumfahamu kabisa.
Msangu aliangusha chozi baada ya kumuona shemeji yake.
Jay nae aliangusha chozi, ila chozi lake lilikuwa lina mengi ndani yake.
Gomba alikuwa akiangaza na alimuona mwanamke mmoja akiwa amekaa sambamba na waombolezaji, mwanamke yule alimpa ishara fulani na Gomba alielewa mambo hayako sawa pale.
Msangu alimshika mkono Jay na akamwongoza kuelekea chumbani kwa wazazi wake na Gomba nae akafuata.
“Tafadhali, kuna muda inabidi utumie akili kuliko nguvu” Jay alimkoromea Gomba kwa sauti ya chini ila iliojaa jaziba. Gomba akasimama na kutafuta sehemu na kukaa pamoja na waombolezaji wengine.
Jay aliingizwa kule chumbani na kumkuta mama yake Vedi akiwa mkavu usoni huku akiwa hana hata chembe ya chozi.
Mama msangu alisimama baada ya kumuona Jay.
“Na wewe unaamini mkeo kafa kweli?” Mama msangu alihoji na Jay alishindwa cha kujibu.
Mama Msangu alianza kuongea kwa sauti huku akionekana dhahiri kutokukubaliana na suala lile la kifo cha Vedi hata pale ambapo Jay alitaka kutetea hoja ya kifo kile Mama yule alikataa kata kata na hatimae alimshika mkono Jay.
“Mwanangu twende nikuoneshe kitu; Mkeo hakuwa na mwanya kabisa licha ya kujitahidi kufanana ila nimemgusa midomo yake japo watu wamenizuia” Alisema Mama msangu huku akimshika akitembea kuelekea sebuleni.
Na walipotoka watu wakawatazama, Mama yule hakujali na akaelekea lilipo jeneza.
Gomba aliona kitendo kile na tayari alishaambiwa na yule mwanamke aliekuwa pale msibani kinachoendelea, haraka akasimama na kushika mfukoni na akapiga hatua ndefu hadi akawafikia na kwa kuwa Mama msangu alikuwa ameshika mfuniko wa jeneza;wamama wengine nao wakaanza kusogea kumkataza mana alishavuruga huko nyuma na hawakutaka kabisa aliguse jeneza lile,lakini kasi ya Gomba ilikuwa ni kubwa na kwa wepesi akamshika mkono Mama Msangu na Mama Msangu hakutaka kuzuiwa hivyo akautoa mkono ule na kutaka kuufuangua mfuniko wa jeneza.
Mara akasita na kujishika kichwa na kuanguka chini.
Haikupita dakika moja akainuka, ila aliinuka kwa mtindo wa ajabu, aliinuka kwa kujikuna huku akicheka na kuunguruma kama simba na kuongea maneno yasiyoeleweka.
Watu walijawa na taharuki na vilio vilianza upya.
Jay aliona tukio lile ila hakujua Gomba kwa nini alimshika mkono mama yake huyo.
“Wewe bwege umemfanya nini huyu mama?” Jay alifoka kwa jaziba licha ya kujizuia sauti isitoke.
Gomba akainua mabega kukataa.
Jay akamshika ukosi wa shati.
Ukaanza mvutano na mparanganyiko ndani ya nyumba ya mzee mashimo.
Mama Msangu anajikuna na kuunguruma hovyo huku Jay akiwa anavutana na rafiki yake wa bandia,watu nao wamebaha kwa yanayoendelea.
Jay alikuwa amegeuka mbogo alijua kabisa kuna kitu kimefanywa na Gomba kwa Mama msangu.
Yule mwanamke aliekuwa miongoni mwa waombolezaji akasogea hadi nyuma ya Jay na kama anaetaka kujifunia kanga aliojitanda akampiga pigo moja la kisogo bila mtu kugundua kilichotokea na akajitandua kanga na kujitanda tena.
Jay akalegea na kwenda chini kama gunia la chawa wa jaani.
Gomba akapaza sauti ya hamaniko huku akiwa amemshika Jay na watu walizidi kuchanganyikiwa zaidi.
Gomba akaomba kupiga simu ya dharura ili watu wale wawahishwe hospitali; Wazo lake liliungwa na wengi waliokuwapo pale ndani na akapiga simu.
***
Dakika thelathini zilipita na gari la wagonjwa lilifika pale na haraka haraka wauguzi wa huduma ya kwanza walishuka na kuwabeba Jay na Mama Msangu na Msangu na Baba yake walikataliwa kuingia ndani ya gari lile kwa kisingizio ni dogo halitoshi msindikizaji.
Mazishi yaliingiliwa na taharuki, ratiba ikabadiliswa hadi ijulikane mstakabali wa afya za walengwa wa marehemu.
Ajabu nyingine ni kuwa; taharuki ilibeba mawazo ya watu kiasi hakuna aliekumbuka kufuatilia gari lile linaelekea hospitali gani.
Watu waliendelea na malumbano yasioyo na tija.
Lakini wangejua yanayoenda kuwapata ndugu zao, hakika wasingebishania ratiba ya mazishi ya maiti bandia.
**
Weka komenti yako ili iwafikie watu wengi zaidi.
sokoni inaingia lini hii kitu
 
Back
Top Bottom