Baharia; (Ujasusi, Mapenzi na Upelelezi wa kutisha)

Baharia; (Ujasusi, Mapenzi na Upelelezi wa kutisha)

RIWAYA; BAHARIA


NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660


SEHEMU YA KUMI NA MOJA


“Sikia bwana mdogo,hii kitu tunakupa kwa garama ndogo tu, nayo ni siri kuhusu yanayoendelea, lakini pia tunataka uhakikishe demu wako hakutani na askari yeyote bila sisi kujua na pia hakikisha kila akitoka hapa unajua anakoenda na sisi kila jioni tutakuletea hii kitu” Cholo alimwambia Jay huku akipunga fundo dogo la karatasi hewani.

“Hiyo uliopata inatosha kwa sasa, ukizidisha tutakupeleka mochwari” Cholo alisema tena huku akisimama na kisha akawapa ishara wenzie na wakaanza kutoka ndani ya ile nyumba na kumwacha Jay akianguka chini kwa mauzauza yanayoukumba mwili wake.

Chozi lilitoka kwa uchungu, ila hakuwa na la kufanya zaidi ya kutulia chini na kuacha mwili usisimke kwa furaha ya kununua.

Jay rasimi alikuwa ameingia kwenye uraibu wa madawa ya kulevya bila kupenda.

Lakini kwa nini hawa jamaa wanayafanya haya yote?

Hakuna aliejua chanzo cha yote ni nini, je ni baharia au ni kitabu cha baharia?

Bado hakuna aliejua na Baharia aliona nini; alijua nini hadi kifo kikamkuta? Bado lilikuwa ni swali bila jibu.

Bado Cholo;Panga na Gomba walikuwa washindi kwenye mchezo ule usio na jina la kueleweka, walitumia nguvu nyingi bila sababu ya msingi kueleweka.

Lakini siku zote waswahili wanasema; “Mwenda kombo kwa hisani, hurudi kwa aibu ya huzuni” mchezo uliingiliwa na wababe wa fitina wakiongozwa na Zedi Wimba.


Vedi alifika nyumbani kwa Jay na kukuta nyumba ikiwa kimya licha ya taa za ndani kuwaka.

Alisukuma mlango na kuingia kwa tahadhari.

Macho yake yaliona mwili wa Jay ukiwa umelala chini, haraka akakimbia na kwenda kumuinua huku akimuita.

Jay alipofumbua macho alikutana na sura ya Vedi ikiwa inamtazama huku mwili wake ukiwa umepakatwa na Vedi.

Jay alijitahidi kusema kitu ila alishindwa na kuishia kukohoa na kutoa udenda kama teja aliezidisha dozi.

Vedi aligundua mpenzi wake anataka kusema kitu; akainama na kumsikiliza na kwa mbali alipata kusikia alichokisema Jay.

“Tafadhali ondoka hapa kwangu!” Jay alisema kwa tabu kubwa.

Vedi alitikisa kichwa kukataa huku akilia; alilia kwa sababu asingeweza kutoka na kumwacha akiwa katika hali ile.

Uso ulimvimba na alionekana kuwa ni dhoofu wa mwili.

Vedi alisimama na kumkokota Jay hadi kwenye sofa na kumkaliza.

Alihitaji kumpa msaada lau wa kumkanda na maji ya moto baada ya kuona namna alivyoumizwa na uso kumvimba.

Muda wote huo bado Jay alionesha ishara ya kumtaka Vedi atoke.

Vedi hakukubali kirahisi, aliendelea kushugulika na jiko ili yapatikane maji ya moto kwa ajili ya huduma ya kwanza kwa Jay.

Licha ya maswali mengi kichwani mwake kuhusu yaliompata Jay hadi kufikia vile; ila hakuwa na uwezo wa kumuuliza mana alionekana yupo kwenye hali mbaya sana, hivyo alihitaji kupata huduma ya kwanza kisha aone uwezekano wa kumuuliza yaliompata na pia alikuwa na shauku ya kujua msibani kumeendelea nini na kisha amwambie yale yanayoendelea katika maisha yake kwa sasa.

Maji hayakuchukua dakika nyingi kuchemka, akayachukua na kutafuta kitambaa safi kisha akaelekea sebuleni kumpa huduma mchumba wake aliempenda kuliko kitu chochote.

Jay hakuwa na namna zaidi ya kubaki akimtizama tu Vedi.

Vedi alimkanda na kumsafisha hapa na pale kisha akataka kumvua shati na hapo ndipo Vedi alikumbuka kitu.

Wakati anapitisha kitambaa usawa wa pua za Jay ni kama aliona ungaunga mweupe ukiwa umesalia kwenye tundu za pua.

Vedi alimtizama Jay machoni; Jay akakwepesha macho yake na kutazama pembeni.

Vedi kuna hisia fulani zilimpitia, ila akazipuza na badala yake akaendelea kumvua shati Jay.

Alipomaliza alimtaka waelekee bafuni kuoga; Jay alikataa na alisema.

“Naomba uniache tu msaada wako umetosha kwa hapa tafadhali” Jay alikataa na kumfukuza Vedi.

Vedi alitazama pembeni kwa muda kisha akamuuliza.

“Jay ulikuwa na mimi kwa sababu gani labda!”.
Jay alizubaa kwa swali lile mana hakutegemea kulipata kwa muda ule.

“Nilikuwa na wewe kwa sababu nilikupenda sana” Jay alijibu.

“Kwa hiyo sasa hivi hunipendi sio!” Vedi alihoji.

“Kwa ulioyafanya, hakika sikupendi tena na ni bora ukaniacha na maisha yangu tu” Jay alisema huku akitazama pembeni.

Vedi alimtazama kwa muda wa dakika moja nzima bila kusema kitu.

“Kwa hiyo uminizika?” hatimae Vedi alipata kauli.

Jay alistuka kwa swali lile na hapo akakumbuka yaliotokea kwa Mama msangu; Mama yake Vedi na hakujua hadi muda huo ni wapi atakuwa alipelekwa mwanamke yule.

Kitu kama kaa la moto likapita moyoni mwa Jay.

Alitamani kusema kitu ila akajikuta nafsi inakataa, aliwakumbuka Gomba na wenzake hapo nafsi ikajaa woga.

“Nimekwambia sitaki kukusikia mana Vedi ameshafariki na wewe ni kama kivuli chake tu,tafadhali nisingependa uendelee kuwepo hapa” Jay ilibidi afoke huku akikwepa kujibu swali la Vedi.

“Ok! Na nini kilichokukuta hapa ndani hadi kuwe hivi, nimekukuta upo hoi na dhahiri umepigwa na pia unaoekana hapa ndani kumefanyika rabsha za hapa na pale.” Vedi aliuliza huku akiwa amemkazia macho.

Lilikuwa ni swali lingine gumu kujibika kirahisi na hata akijibu Atajibu kwa aina gani ya ushawishi ili aeleweke?

Ikawa ni ngumu kwa Jay.

“Nadhani hupaswi kuniuliza lolote wakati huu, zaidi ningekuona wa maana kama ungeondoka hapa ndani Vedi” Jay alikwepa kujibu swali kwa mara nyingine.

Vedi alisimama kisha akamsogelea Jay.

“Nitazame machoni Jay kisha unambie hutaki kuniona hapa kwako!” Vedi alisema huku akimtizama Jay usoni.

Jay alishindwa kusema lolote.

“afu kuna kitu unakificha mpenzi wangu, na yawezekana una matatizo zaidi yangu” Vedi alimwambia Jay huku akianza kuondoka pale sebuleni.

Jay alikumbuka kitu.

Ili asalimike kwenye mikono ya wale wababe ni lazima awe karibu na Vedi,hivyo kumfukuza ni kumweka mbali nae na pia atakosa tiba ya ugonjwa alioambukizwa.

Mwili wake alihisi unaanza kurudi kwenye hali yake ya kawaida, hivyo akataka kusimama ili aelekee chumbani ila wakati akitaka kusimama ni wakati huo ambao Vedi alifika pale akiwa na kikombe cha chai.

“Nadhani unapaswa kunywa hii ili upashe tumbo joto, hapa sitoki na ukiona nakukera nifukuze kwa kunivuta hapo nitaamini hutaki uwepo wangu hapa.” Vedi alimwambia Jay huku akikaa karibu yake na kikombe cha chai.

Jay alipata kusikia ya kuwa; mtu yeyote ambae anatumia madawa ya kulevya chai kwake ni sumu na endapo akiitumia muda mchache baada ya kuvuta, basi athari kubwa zaidi atakayoipata ni kifo.

Jay aliogopa na hakutaka kuinywa ile chai.

Akaipokea na kisha akamtazama Vedi na akaamua kukwepa kisomi.

“naomba unipikie ugali tafadhali” Jay alisema kiyonge na muda huohuo alimuona Vedi akisimama na kuelekea upande kulipokuwa na jiko na yeye akasimama na kuelekea nje na akiwa na kikombe cha chai mkononi.

Huko nje wala hakunywa chai ile, isipokuwa aliishia kuimwaga tu kisha akabaki na kikombe mkononi huku mambo mengi yakipita kichwani mwake.

Mara akagutuka, alimuona Vedi akiwa ameshika simu na aliambiwa ajitahidi kujua mienendo ya Vedi.

Akatoa simu yake mfukoni na kutafuta namba zilizokuwa zimehifadhiwa kwa jina la “Mtesi” akaandika ujumbe mfupi na alipohakikisha umeenda akaianama na kufuta chozi kwa uchungu.

Nafsi yake ilikataa kabisa kukubaliana na kile alichokuwa anakifanya.

Roho ilimuuma ila hakuwa na la kufanya kuepuka hali ile.

Alikaa nje hadi wakati alipoitwa kula.

Muda mwingi kulitawala ukimya wa kutisha baina yao na hakuna aliemsemesha mwenzie.

Walipomaliza kula; Vedi aliSimu yake na kujaribu kupiga namba za Nyamizi rafiki yake, japo aliamini si rahisi kupatikana kwa sababu fungate walipanga lifanyikie Nairobi baada ya ndoa yao.

Vedi alijikuta akiwaza tu na kupiga.

Muda wote Jay alikuwa akimtizama bila kusema kitu.

Ajabu simu iliita.

Vedi alishangaa, kisha akahesabu siku za ndoa na kugundua zilipita siku nne tu tangu walipokuwa kwenye sherehe za ndoa sasa vije tena simu iwe hewani wakati ilitakiwa wawe Nairobi.
Lakini hata yeye alijishangaa, kwanini alipiga wakati anajua kabisa wapo Nairobi?”
.
Simu ikapokelewa.

“Hallow!!” ikaitika upande wa pili.

Vedi alijua ni sauti ya Nyamizi.

“Vedi hapa naongea!” .

Vedi akasikia upande wa pili ukipumua kwa nguvu.

“Vedi yupi anaeongea?” Nyamizi alihoji.

“Usitake kusema hata sauti yangu hujaijua shoga angu” Vedi alilalama.

“Sauti yako haiwezi nipotea hata nikiwa katikati ya koma, ila imetokea nini tena nasikia sauti yako wakati tumeambiwa umekufa?” Nyamizi alihoji.

Vedi aliguna.

“Wewe upo wapi kwani” Vedi alihoji.

“Huwezi amini nimetokea msibani, nilichanganyikiwa kusikia ni wewe uliejitupa kwenye maji, raha ya fungate ilikata, tafadhali nambie kumetokea nini mpenzi” Nyamizi aliongea kwa hisia.

“Ngoja kukuchwe nadhani tutaonana” Vedi alisema.

“No! Nadhani tuonane hata sasa ili nijiridhishe ni wewe mpenzi” Nyamizi aliongea.

Vedi na Nyamizi walikubaliana kuonana usiku ule na ilikuwa ni mishale ya saa tano za usiku.
Vedi akatoka na kama kawaida.


Jay nae akaandika ujumbe kwenda kwa watesi wake kuwajulisha Vedi anakoelekea.

***

Toa maoni yako
 
Hii mara ya tano nachungulia Kama umeongeza sehemu ya kumi na mbili
Ukishusha nitag mkuu Kudo
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA MBILI




Muda wote Jay alikuwa akimtizama bila kusema kitu.

Ajabu simu iliita.

Vedi alishangaa, kisha akahesabu siku za ndoa na kugundua zilipita siku nne tu tangu walipokuwa kwenye sherehe za ndoa sasa vije tena simu iwe hewani wakati ilitakiwa wawe Nairobi.
Lakini hata yeye alijishangaa, kwanini alipiga wakati anajua kabisa wapo Nairobi?”
.
Simu ikapokelewa.

“Hallow!!” ikaitika upande wa pili.

Vedi alijua ni sauti ya Nyamizi.

“Vedi hapa naongea!” .

Vedi akasikia upande wa pili ukipumua kwa nguvu.

“Vedi yupi anaeongea?” Nyamizi alihoji.

“Usitake kusema hata sauti yangu hujaijua shoga angu” Vedi alilalama.

“Sauti yako haiwezi nipotea hata nikiwa katikati ya koma, ila imetokea nini tena nasikia sauti yako wakati tumeambiwa umekufa?” Nyamizi alihoji.

Vedi aliguna.

“Wewe upo wapi kwani” Vedi alihoji.

“Huwezi amini nimetokea msibani, nilichanganyikiwa kusikia ni wewe uliejitupa kwenye maji, raha ya fungate ilikata, tafadhali nambie kumetokea nini mpenzi” Nyamizi aliongea kwa hisia.

“Ngoja kukuchwe nadhani tutaonana” Vedi alisema.

“No! Nadhani tuonane hata sasa ili nijiridhishe ni wewe mpenzi” Nyamizi aliongea.

Vedi na Nyamizi walikubaliana kuonana usiku ule na ilikuwa ni mishale ya saa tano za usiku.
Vedi akatoka na kama kawaida.


Jay nae akaandika ujumbe kwenda kwa watesi wake kuwajulisha Vedi anakoelekea.

-------------

Mwendo wa nusu saa ulitosha kuwakutanisha Nyamizi na Vedi. Walikutana sehemu walioona ni sahihi kwao kukutana.

Jambo la kwanza walilofanya marafiki wale ni kukumbatiana kwa hisia huku kila mmoja akilia kwa hisia.

Moyo wa Vedi ulifarijika kuona lau sasa amefanikiwa kupata mtu anaeweza kusimama nae wakati mgumu kama huu wakati ambao hata ndugu yake wa damu alimkataa na kumuita jini, wakati ambao watu wamemkimbia na kumwacha akipitia kipindi ambacho hakujua mwanzo wake wala mwisho wake ila alijikuta tu akiingia kwenye kipindi kama hicho, kipindi cha mateso ya akili na hisia bila watesaji kujitokeza mbele yake.

Walikaa sehemu iliokuwa inautulivu katika mgahawa mmoja ambao waliona unafaa.

“Mbona uko peke yako shemeji yuko wapi?” Vedi aliuliza.

“Ndie kanisindikiza hapa ila amepaki kule na kabaki ndani ya gari” Nyamizi alisema huku akielekeza kidole upande wa pili wa mgahawa ule. Vedi aligeuka na kuona gari zuri la kisasa likiwa limepaki.

“Kwanza nambie imekuwaje huko msibani?” Vedi alihoji kwa shauku kubwa.

Nyamizi aliguna kidogo.

“Mchana kuna tukio lilitokea ambalo lilizuia kila kitu na hapa navyokwambia maiti imerudishwa mochwari kwa uchunguzi zaidi” Nyamizi alimwambia Vedi na Vedi alikaa vizuri kwenye kiti.

“Wakati tunasubiri taratibu za mazishi; Jay alikuja ndani akiwa na mtu mwingine na alipofika dada ako akampeleka ndani alikokuwa mama na punde wakarejea huku mama akionekana dhahiri kuna kitu alitaka kumwonesha kwenye ule mwili pale mara tukashangaa Mama anapiga kelele kama mwehu na kujikuna hovyo na kabla hatujafanya lolote Jay nae akaanguka na kuzimia, hazikuzidi hata dakika kumi gari la wagonjwa likafika na kuwapeleka muhimbili”

Vedi alijifuta machozi kwa uchungu.

“Ulifanikiwa kujua kilichoendelea huko Muhimbili lakini shoga angu?” Vedi aliuliza.

“ Shemeji yako alifuatilia na badae akaja na taarifa ambazo hazikumpendeza kila mtu, alisema mumeo hakuonekana hospitali ila Mama amewekwa wodi ya uangalizi wa matatizo ya akili, mana kawa kama kichaa kiukweli” Nyamizi aliongea huku machozi yakimlenga.

“Ahsante sana kwa upendo huo mnaoonesha kwangu, hakika u rafiki mwema sana Nyamizi; kwanza mlikatisha fungate lenu ili mje kuhudhuria msiba wangu na sasa upo hapa na mimi wakati watu wote wakiniona wananikimbia kwa sababu ya kuhofia mimi ni jini” Vedi alijifuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake.

“Tuko pamoja mpenzi; kwani Jay anasemaje au umefanikiwa kuonana nae?”

Vedi alibabaika kidogo kwa swali lile.

“Kiukweli Jay nimeonana nae ila amekuwa sio Jay unaemfahamu, amekuwa ni mtu wa ajabu sana hivi karibuni, haeleweki na hapa nimetoka kwake ila hajanambia hata kuhusu mama angu……masikini Mama jamani!” Vedi alianza kulia kwa sauti ya chini.

“basi hupaswi kulia sasa, kikubwa labda unishirikishe kimetokea nini hadi kutangazwa umekufa?” Nyamizi alihoji na alionekana kuwa na uchu wa kujua hilo jambo.

Vedi alivuta pumzi nyingi na kuzishusha, hakuwa na sababu ya kuficha kwa rafiki makini kama yule.

Akamweleza yaliomkuta ndani ya meli na hadi kufikia hapo alipo.


Wakati Nyamizi na Vedi wakisimuliana; Boneka mume wa Nyamizi alikuwa ametulia ndani ya gari huku mawazo yakimpita kwa kasi. Mbali ya ubilionea aliokuwa nao ambao alilirithi kwa wazazi wake ila hakuna mtu ambae alijua ni nini kinaendelea nyuma yake.

Boneka alikuwa ni ofisa wa kitengo maalumu na kazi maalumu na aliwekwa kwenye kitengo kile na Kamishina wa jeshi la polisi Zenge wa Zenge. Kamishina Zenge wa Zenge aliamini akili ya Boneka tangu akiwa kiongozi wake ndani ya jeshi la polisi na walifanya kazi Dodoma na kufanikiwa kuzima mtandao wa mbwa mwitu katika kisa kilichoandikwa vyema na mwandishi Bahati Mwamba na kukipa jina la “DAKIKA ZA MWISHO with Wolf rules” na Boneka alifanya makubwa licha ya kuja kusaidiwa na Zedi Wimba jasusi hatari.
Na sasa Boneka ni mfanyabiashara mkubwa ila bado anatumikia taifa akiwa kwenye kitengo cha “Special operations” kilicho chini ya Kamishina Zenge wa Zenge. Kitengo hiki kimesheheni watu makini akiwemo Zedi Wimba; Honda Makubi; Haji Makame; Elias Ziga na Mwinyi Kisoda. Watu hawa wote wametokea jeshini ila Boneka pekee ndie ametoka jeshi la polisi pamoja na Kamishina mwenyewe. Mbali na Kamishina ambae alikuwa kazini siku zote ila vijana wake wote walikuwa nje ya kazi na kila mtu anafanya kazi zake na hukutana wakati wa kazi maalumu tu na wakimaliza kila mmoja huchukua hamsini zake.

Boneka tangu mwanzo aliposikia kuhusu kifo cha Vedi akili yake haikukubali mapema, mana hata wakati watu wanakimbia ndani ya meli kwenda kuona mtu aliejitupa ndani ya maji, yeye alitoka pia na kwa mbali alimuona Vedi akiwa miongoni mwa watu waliotaka kushuhuidia tukio lile.

Walipofika Nairobi ndipo walipokea taarifa za kifo cha Vedi na hima wakarejea na kazi kubwa alioifanya ni kumtuliza mkewe Nyamizi ambae alikuwa analia wakati wote na hapo wakawasiliana na mwenyekiti wa kamati ya mapokezi ambae alitakiwa kuhakikisha watu wanaingia na kutoka salama na mwenyekiti akatoa majina ya watu wote waliosaini kitabu cha watu waliotoka salama ndani ya meli.

Jina la Vedi aliliona na alimuonesha mkewe sahihi ya Vedi na Nyamizi akakubali ya kuwa ule ni mwandiko wa Vedi.

Kuna nini hapa nyuma? Alijiuliza akiwa peke yake na alichukua kitabu kile akapitia tena majina ya watu walioingia na kutoka.

Jina moja liliingia ila halikutoka.

Lilikuwa ni jina la Masumula Hussein.

Ni nani huyu binti?

Akamuuliza mkewe na jibu lilikuwa ni mtoto wa shangazi yake na Nyamizi na yeye ndie alimpa kadi.

Ikabidi wapige simu nyumbani kwa kina Masumula na jibu lilikuwa ni tangu aage kwenda harusini, hakurejea tena nyumbani.

Boneka akajenga picha ya kuhusanisha mambo yale.

Na akajiuliza kwanini Vedi sasa ndie awe muhanga wa shida ile badala ya Masumula? Na Masumula kwa nini auwawe au Vedi aliona mauaji yake? Na wauaji walitaka kumziba mdomo?

Ikabidi waelekee msibani na hata wakati yale yanatokea msibani; Boneka aliyashuhudia ila alikuwa na mashaka na mwonekano wa Jay mana alimfahamu lakini pia alikuwa na mashaka na rafiki alieongozana na Jay; Macho yake ya kijasusi yalimwambia yule hakuwa mtu mwema kabisa.

Wakati Boneka akiwaza hayo ndani ya gari kuna kitu aliona.

Aliona mtu ambae alikuwa makini na nyendo za mkewe na shemeji yake Vedi ambao walikuwa wamekaa ndani ya mgahawa wakihabarishana mambo yao ambayo hakutaka kuyaingilia.

Alipomtazama vizuri mtu yule alimtambua.

Alikuwa ni yule aliekuwa ameongozana na Jay msibani.

Alimuona Gomba.
 
Akina Gomba washaanza kukutana na mjanja mwenzao
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA MBILI




Muda wote Jay alikuwa akimtizama bila kusema kitu.

Ajabu simu iliita.

Vedi alishangaa, kisha akahesabu siku za ndoa na kugundua zilipita siku nne tu tangu walipokuwa kwenye sherehe za ndoa sasa vije tena simu iwe hewani wakati ilitakiwa wawe Nairobi.
Lakini hata yeye alijishangaa, kwanini alipiga wakati anajua kabisa wapo Nairobi?”
.
Simu ikapokelewa.

“Hallow!!” ikaitika upande wa pili.

Vedi alijua ni sauti ya Nyamizi.

“Vedi hapa naongea!” .

Vedi akasikia upande wa pili ukipumua kwa nguvu.

“Vedi yupi anaeongea?” Nyamizi alihoji.

“Usitake kusema hata sauti yangu hujaijua shoga angu” Vedi alilalama.

“Sauti yako haiwezi nipotea hata nikiwa katikati ya koma, ila imetokea nini tena nasikia sauti yako wakati tumeambiwa umekufa?” Nyamizi alihoji.

Vedi aliguna.

“Wewe upo wapi kwani” Vedi alihoji.

“Huwezi amini nimetokea msibani, nilichanganyikiwa kusikia ni wewe uliejitupa kwenye maji, raha ya fungate ilikata, tafadhali nambie kumetokea nini mpenzi” Nyamizi aliongea kwa hisia.

“Ngoja kukuchwe nadhani tutaonana” Vedi alisema.

“No! Nadhani tuonane hata sasa ili nijiridhishe ni wewe mpenzi” Nyamizi aliongea.

Vedi na Nyamizi walikubaliana kuonana usiku ule na ilikuwa ni mishale ya saa tano za usiku.
Vedi akatoka na kama kawaida.


Jay nae akaandika ujumbe kwenda kwa watesi wake kuwajulisha Vedi anakoelekea.

-------------

Mwendo wa nusu saa ulitosha kuwakutanisha Nyamizi na Vedi. Walikutana sehemu walioona ni sahihi kwao kukutana.

Jambo la kwanza walilofanya marafiki wale ni kukumbatiana kwa hisia huku kila mmoja akilia kwa hisia.

Moyo wa Vedi ulifarijika kuona lau sasa amefanikiwa kupata mtu anaeweza kusimama nae wakati mgumu kama huu wakati ambao hata ndugu yake wa damu alimkataa na kumuita jini, wakati ambao watu wamemkimbia na kumwacha akipitia kipindi ambacho hakujua mwanzo wake wala mwisho wake ila alijikuta tu akiingia kwenye kipindi kama hicho, kipindi cha mateso ya akili na hisia bila watesaji kujitokeza mbele yake.

Walikaa sehemu iliokuwa inautulivu katika mgahawa mmoja ambao waliona unafaa.

“Mbona uko peke yako shemeji yuko wapi?” Vedi aliuliza.

“Ndie kanisindikiza hapa ila amepaki kule na kabaki ndani ya gari” Nyamizi alisema huku akielekeza kidole upande wa pili wa mgahawa ule. Vedi aligeuka na kuona gari zuri la kisasa likiwa limepaki.

“Kwanza nambie imekuwaje huko msibani?” Vedi alihoji kwa shauku kubwa.

Nyamizi aliguna kidogo.

“Mchana kuna tukio lilitokea ambalo lilizuia kila kitu na hapa navyokwambia maiti imerudishwa mochwari kwa uchunguzi zaidi” Nyamizi alimwambia Vedi na Vedi alikaa vizuri kwenye kiti.

“Wakati tunasubiri taratibu za mazishi; Jay alikuja ndani akiwa na mtu mwingine na alipofika dada ako akampeleka ndani alikokuwa mama na punde wakarejea huku mama akionekana dhahiri kuna kitu alitaka kumwonesha kwenye ule mwili pale mara tukashangaa Mama anapiga kelele kama mwehu na kujikuna hovyo na kabla hatujafanya lolote Jay nae akaanguka na kuzimia, hazikuzidi hata dakika kumi gari la wagonjwa likafika na kuwapeleka muhimbili”

Vedi alijifuta machozi kwa uchungu.

“Ulifanikiwa kujua kilichoendelea huko Muhimbili lakini shoga angu?” Vedi aliuliza.

“ Shemeji yako alifuatilia na badae akaja na taarifa ambazo hazikumpendeza kila mtu, alisema mumeo hakuonekana hospitali ila Mama amewekwa wodi ya uangalizi wa matatizo ya akili, mana kawa kama kichaa kiukweli” Nyamizi aliongea huku machozi yakimlenga.

“Ahsante sana kwa upendo huo mnaoonesha kwangu, hakika u rafiki mwema sana Nyamizi; kwanza mlikatisha fungate lenu ili mje kuhudhuria msiba wangu na sasa upo hapa na mimi wakati watu wote wakiniona wananikimbia kwa sababu ya kuhofia mimi ni jini” Vedi alijifuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake.

“Tuko pamoja mpenzi; kwani Jay anasemaje au umefanikiwa kuonana nae?”

Vedi alibabaika kidogo kwa swali lile.

“Kiukweli Jay nimeonana nae ila amekuwa sio Jay unaemfahamu, amekuwa ni mtu wa ajabu sana hivi karibuni, haeleweki na hapa nimetoka kwake ila hajanambia hata kuhusu mama angu……masikini Mama jamani!” Vedi alianza kulia kwa sauti ya chini.

“basi hupaswi kulia sasa, kikubwa labda unishirikishe kimetokea nini hadi kutangazwa umekufa?” Nyamizi alihoji na alionekana kuwa na uchu wa kujua hilo jambo.

Vedi alivuta pumzi nyingi na kuzishusha, hakuwa na sababu ya kuficha kwa rafiki makini kama yule.

Akamweleza yaliomkuta ndani ya meli na hadi kufikia hapo alipo.


Wakati Nyamizi na Vedi wakisimuliana; Boneka mume wa Nyamizi alikuwa ametulia ndani ya gari huku mawazo yakimpita kwa kasi. Mbali ya ubilionea aliokuwa nao ambao alilirithi kwa wazazi wake ila hakuna mtu ambae alijua ni nini kinaendelea nyuma yake.

Boneka alikuwa ni ofisa wa kitengo maalumu na kazi maalumu na aliwekwa kwenye kitengo kile na Kamishina wa jeshi la polisi Zenge wa Zenge. Kamishina Zenge wa Zenge aliamini akili ya Boneka tangu akiwa kiongozi wake ndani ya jeshi la polisi na walifanya kazi Dodoma na kufanikiwa kuzima mtandao wa mbwa mwitu katika kisa kilichoandikwa vyema na mwandishi Bahati Mwamba na kukipa jina la “DAKIKA ZA MWISHO with Wolf rules” na Boneka alifanya makubwa licha ya kuja kusaidiwa na Zedi Wimba jasusi hatari.
Na sasa Boneka ni mfanyabiashara mkubwa ila bado anatumikia taifa akiwa kwenye kitengo cha “Special operations” kilicho chini ya Kamishina Zenge wa Zenge. Kitengo hiki kimesheheni watu makini akiwemo Zedi Wimba; Honda Makubi; Haji Makame; Elias Ziga na Mwinyi Kisoda. Watu hawa wote wametokea jeshini ila Boneka pekee ndie ametoka jeshi la polisi pamoja na Kamishina mwenyewe. Mbali na Kamishina ambae alikuwa kazini siku zote ila vijana wake wote walikuwa nje ya kazi na kila mtu anafanya kazi zake na hukutana wakati wa kazi maalumu tu na wakimaliza kila mmoja huchukua hamsini zake.

Boneka tangu mwanzo aliposikia kuhusu kifo cha Vedi akili yake haikukubali mapema, mana hata wakati watu wanakimbia ndani ya meli kwenda kuona mtu aliejitupa ndani ya maji, yeye alitoka pia na kwa mbali alimuona Vedi akiwa miongoni mwa watu waliotaka kushuhuidia tukio lile.

Walipofika Nairobi ndipo walipokea taarifa za kifo cha Vedi na hima wakarejea na kazi kubwa alioifanya ni kumtuliza mkewe Nyamizi ambae alikuwa analia wakati wote na hapo wakawasiliana na mwenyekiti wa kamati ya mapokezi ambae alitakiwa kuhakikisha watu wanaingia na kutoka salama na mwenyekiti akatoa majina ya watu wote waliosaini kitabu cha watu waliotoka salama ndani ya meli.

Jina la Vedi aliliona na alimuonesha mkewe sahihi ya Vedi na Nyamizi akakubali ya kuwa ule ni mwandiko wa Vedi.

Kuna nini hapa nyuma? Alijiuliza akiwa peke yake na alichukua kitabu kile akapitia tena majina ya watu walioingia na kutoka.

Jina moja liliingia ila halikutoka.

Lilikuwa ni jina la Masumula Hussein.

Ni nani huyu binti?

Akamuuliza mkewe na jibu lilikuwa ni mtoto wa shangazi yake na Nyamizi na yeye ndie alimpa kadi.

Ikabidi wapige simu nyumbani kwa kina Masumula na jibu lilikuwa ni tangu aage kwenda harusini, hakurejea tena nyumbani.

Boneka akajenga picha ya kuhusanisha mambo yale.

Na akajiuliza kwanini Vedi sasa ndie awe muhanga wa shida ile badala ya Masumula? Na Masumula kwa nini auwawe au Vedi aliona mauaji yake? Na wauaji walitaka kumziba mdomo?

Ikabidi waelekee msibani na hata wakati yale yanatokea msibani; Boneka aliyashuhudia ila alikuwa na mashaka na mwonekano wa Jay mana alimfahamu lakini pia alikuwa na mashaka na rafiki alieongozana na Jay; Macho yake ya kijasusi yalimwambia yule hakuwa mtu mwema kabisa.

Wakati Boneka akiwaza hayo ndani ya gari kuna kitu aliona.

Aliona mtu ambae alikuwa makini na nyendo za mkewe na shemeji yake Vedi ambao walikuwa wamekaa ndani ya mgahawa wakihabarishana mambo yao ambayo hakutaka kuyaingilia.

Alipomtazama vizuri mtu yule alimtambua.

Alikuwa ni yule aliekuwa ameongozana na Jay msibani.

Alimuona Gomba.
Santee afadhali tumepata mkombozi
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA KUMI NA MBILI




Muda wote Jay alikuwa akimtizama bila kusema kitu.

Ajabu simu iliita.

Vedi alishangaa, kisha akahesabu siku za ndoa na kugundua zilipita siku nne tu tangu walipokuwa kwenye sherehe za ndoa sasa vije tena simu iwe hewani wakati ilitakiwa wawe Nairobi.
Lakini hata yeye alijishangaa, kwanini alipiga wakati anajua kabisa wapo Nairobi?”
.
Simu ikapokelewa.

“Hallow!!” ikaitika upande wa pili.

Vedi alijua ni sauti ya Nyamizi.

“Vedi hapa naongea!” .

Vedi akasikia upande wa pili ukipumua kwa nguvu.

“Vedi yupi anaeongea?” Nyamizi alihoji.

“Usitake kusema hata sauti yangu hujaijua shoga angu” Vedi alilalama.

“Sauti yako haiwezi nipotea hata nikiwa katikati ya koma, ila imetokea nini tena nasikia sauti yako wakati tumeambiwa umekufa?” Nyamizi alihoji.

Vedi aliguna.

“Wewe upo wapi kwani” Vedi alihoji.

“Huwezi amini nimetokea msibani, nilichanganyikiwa kusikia ni wewe uliejitupa kwenye maji, raha ya fungate ilikata, tafadhali nambie kumetokea nini mpenzi” Nyamizi aliongea kwa hisia.

“Ngoja kukuchwe nadhani tutaonana” Vedi alisema.

“No! Nadhani tuonane hata sasa ili nijiridhishe ni wewe mpenzi” Nyamizi aliongea.

Vedi na Nyamizi walikubaliana kuonana usiku ule na ilikuwa ni mishale ya saa tano za usiku.
Vedi akatoka na kama kawaida.


Jay nae akaandika ujumbe kwenda kwa watesi wake kuwajulisha Vedi anakoelekea.

-------------

Mwendo wa nusu saa ulitosha kuwakutanisha Nyamizi na Vedi. Walikutana sehemu walioona ni sahihi kwao kukutana.

Jambo la kwanza walilofanya marafiki wale ni kukumbatiana kwa hisia huku kila mmoja akilia kwa hisia.

Moyo wa Vedi ulifarijika kuona lau sasa amefanikiwa kupata mtu anaeweza kusimama nae wakati mgumu kama huu wakati ambao hata ndugu yake wa damu alimkataa na kumuita jini, wakati ambao watu wamemkimbia na kumwacha akipitia kipindi ambacho hakujua mwanzo wake wala mwisho wake ila alijikuta tu akiingia kwenye kipindi kama hicho, kipindi cha mateso ya akili na hisia bila watesaji kujitokeza mbele yake.

Walikaa sehemu iliokuwa inautulivu katika mgahawa mmoja ambao waliona unafaa.

“Mbona uko peke yako shemeji yuko wapi?” Vedi aliuliza.

“Ndie kanisindikiza hapa ila amepaki kule na kabaki ndani ya gari” Nyamizi alisema huku akielekeza kidole upande wa pili wa mgahawa ule. Vedi aligeuka na kuona gari zuri la kisasa likiwa limepaki.

“Kwanza nambie imekuwaje huko msibani?” Vedi alihoji kwa shauku kubwa.

Nyamizi aliguna kidogo.

“Mchana kuna tukio lilitokea ambalo lilizuia kila kitu na hapa navyokwambia maiti imerudishwa mochwari kwa uchunguzi zaidi” Nyamizi alimwambia Vedi na Vedi alikaa vizuri kwenye kiti.

“Wakati tunasubiri taratibu za mazishi; Jay alikuja ndani akiwa na mtu mwingine na alipofika dada ako akampeleka ndani alikokuwa mama na punde wakarejea huku mama akionekana dhahiri kuna kitu alitaka kumwonesha kwenye ule mwili pale mara tukashangaa Mama anapiga kelele kama mwehu na kujikuna hovyo na kabla hatujafanya lolote Jay nae akaanguka na kuzimia, hazikuzidi hata dakika kumi gari la wagonjwa likafika na kuwapeleka muhimbili”

Vedi alijifuta machozi kwa uchungu.

“Ulifanikiwa kujua kilichoendelea huko Muhimbili lakini shoga angu?” Vedi aliuliza.

“ Shemeji yako alifuatilia na badae akaja na taarifa ambazo hazikumpendeza kila mtu, alisema mumeo hakuonekana hospitali ila Mama amewekwa wodi ya uangalizi wa matatizo ya akili, mana kawa kama kichaa kiukweli” Nyamizi aliongea huku machozi yakimlenga.

“Ahsante sana kwa upendo huo mnaoonesha kwangu, hakika u rafiki mwema sana Nyamizi; kwanza mlikatisha fungate lenu ili mje kuhudhuria msiba wangu na sasa upo hapa na mimi wakati watu wote wakiniona wananikimbia kwa sababu ya kuhofia mimi ni jini” Vedi alijifuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake.

“Tuko pamoja mpenzi; kwani Jay anasemaje au umefanikiwa kuonana nae?”

Vedi alibabaika kidogo kwa swali lile.

“Kiukweli Jay nimeonana nae ila amekuwa sio Jay unaemfahamu, amekuwa ni mtu wa ajabu sana hivi karibuni, haeleweki na hapa nimetoka kwake ila hajanambia hata kuhusu mama angu……masikini Mama jamani!” Vedi alianza kulia kwa sauti ya chini.

“basi hupaswi kulia sasa, kikubwa labda unishirikishe kimetokea nini hadi kutangazwa umekufa?” Nyamizi alihoji na alionekana kuwa na uchu wa kujua hilo jambo.

Vedi alivuta pumzi nyingi na kuzishusha, hakuwa na sababu ya kuficha kwa rafiki makini kama yule.

Akamweleza yaliomkuta ndani ya meli na hadi kufikia hapo alipo.


Wakati Nyamizi na Vedi wakisimuliana; Boneka mume wa Nyamizi alikuwa ametulia ndani ya gari huku mawazo yakimpita kwa kasi. Mbali ya ubilionea aliokuwa nao ambao alilirithi kwa wazazi wake ila hakuna mtu ambae alijua ni nini kinaendelea nyuma yake.

Boneka alikuwa ni ofisa wa kitengo maalumu na kazi maalumu na aliwekwa kwenye kitengo kile na Kamishina wa jeshi la polisi Zenge wa Zenge. Kamishina Zenge wa Zenge aliamini akili ya Boneka tangu akiwa kiongozi wake ndani ya jeshi la polisi na walifanya kazi Dodoma na kufanikiwa kuzima mtandao wa mbwa mwitu katika kisa kilichoandikwa vyema na mwandishi Bahati Mwamba na kukipa jina la “DAKIKA ZA MWISHO with Wolf rules” na Boneka alifanya makubwa licha ya kuja kusaidiwa na Zedi Wimba jasusi hatari.
Na sasa Boneka ni mfanyabiashara mkubwa ila bado anatumikia taifa akiwa kwenye kitengo cha “Special operations” kilicho chini ya Kamishina Zenge wa Zenge. Kitengo hiki kimesheheni watu makini akiwemo Zedi Wimba; Honda Makubi; Haji Makame; Elias Ziga na Mwinyi Kisoda. Watu hawa wote wametokea jeshini ila Boneka pekee ndie ametoka jeshi la polisi pamoja na Kamishina mwenyewe. Mbali na Kamishina ambae alikuwa kazini siku zote ila vijana wake wote walikuwa nje ya kazi na kila mtu anafanya kazi zake na hukutana wakati wa kazi maalumu tu na wakimaliza kila mmoja huchukua hamsini zake.

Boneka tangu mwanzo aliposikia kuhusu kifo cha Vedi akili yake haikukubali mapema, mana hata wakati watu wanakimbia ndani ya meli kwenda kuona mtu aliejitupa ndani ya maji, yeye alitoka pia na kwa mbali alimuona Vedi akiwa miongoni mwa watu waliotaka kushuhuidia tukio lile.

Walipofika Nairobi ndipo walipokea taarifa za kifo cha Vedi na hima wakarejea na kazi kubwa alioifanya ni kumtuliza mkewe Nyamizi ambae alikuwa analia wakati wote na hapo wakawasiliana na mwenyekiti wa kamati ya mapokezi ambae alitakiwa kuhakikisha watu wanaingia na kutoka salama na mwenyekiti akatoa majina ya watu wote waliosaini kitabu cha watu waliotoka salama ndani ya meli.

Jina la Vedi aliliona na alimuonesha mkewe sahihi ya Vedi na Nyamizi akakubali ya kuwa ule ni mwandiko wa Vedi.

Kuna nini hapa nyuma? Alijiuliza akiwa peke yake na alichukua kitabu kile akapitia tena majina ya watu walioingia na kutoka.

Jina moja liliingia ila halikutoka.

Lilikuwa ni jina la Masumula Hussein.

Ni nani huyu binti?

Akamuuliza mkewe na jibu lilikuwa ni mtoto wa shangazi yake na Nyamizi na yeye ndie alimpa kadi.

Ikabidi wapige simu nyumbani kwa kina Masumula na jibu lilikuwa ni tangu aage kwenda harusini, hakurejea tena nyumbani.

Boneka akajenga picha ya kuhusanisha mambo yale.

Na akajiuliza kwanini Vedi sasa ndie awe muhanga wa shida ile badala ya Masumula? Na Masumula kwa nini auwawe au Vedi aliona mauaji yake? Na wauaji walitaka kumziba mdomo?

Ikabidi waelekee msibani na hata wakati yale yanatokea msibani; Boneka aliyashuhudia ila alikuwa na mashaka na mwonekano wa Jay mana alimfahamu lakini pia alikuwa na mashaka na rafiki alieongozana na Jay; Macho yake ya kijasusi yalimwambia yule hakuwa mtu mwema kabisa.

Wakati Boneka akiwaza hayo ndani ya gari kuna kitu aliona.

Aliona mtu ambae alikuwa makini na nyendo za mkewe na shemeji yake Vedi ambao walikuwa wamekaa ndani ya mgahawa wakihabarishana mambo yao ambayo hakutaka kuyaingilia.

Alipomtazama vizuri mtu yule alimtambua.

Alikuwa ni yule aliekuwa ameongozana na Jay msibani.

Alimuona Gomba.
safi mkuu ila daa mnatuacha alosto sana
 
Back
Top Bottom