mtzmweusi
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 8,658
- 8,994
Mkuu hii nikilipia naipata?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
omba mola nzi asidondokee kwenye hii mboga iloanza kunoga!Mboga imeanza kunoga sasa
omba mola nzi asidondokee kwenye hii mboga iloanza kunoga!
Santee afadhali tumepata mkomboziRIWAYA; BAHARIA
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Muda wote Jay alikuwa akimtizama bila kusema kitu.
Ajabu simu iliita.
Vedi alishangaa, kisha akahesabu siku za ndoa na kugundua zilipita siku nne tu tangu walipokuwa kwenye sherehe za ndoa sasa vije tena simu iwe hewani wakati ilitakiwa wawe Nairobi.
Lakini hata yeye alijishangaa, kwanini alipiga wakati anajua kabisa wapo Nairobi?”
.
Simu ikapokelewa.
“Hallow!!” ikaitika upande wa pili.
Vedi alijua ni sauti ya Nyamizi.
“Vedi hapa naongea!” .
Vedi akasikia upande wa pili ukipumua kwa nguvu.
“Vedi yupi anaeongea?” Nyamizi alihoji.
“Usitake kusema hata sauti yangu hujaijua shoga angu” Vedi alilalama.
“Sauti yako haiwezi nipotea hata nikiwa katikati ya koma, ila imetokea nini tena nasikia sauti yako wakati tumeambiwa umekufa?” Nyamizi alihoji.
Vedi aliguna.
“Wewe upo wapi kwani” Vedi alihoji.
“Huwezi amini nimetokea msibani, nilichanganyikiwa kusikia ni wewe uliejitupa kwenye maji, raha ya fungate ilikata, tafadhali nambie kumetokea nini mpenzi” Nyamizi aliongea kwa hisia.
“Ngoja kukuchwe nadhani tutaonana” Vedi alisema.
“No! Nadhani tuonane hata sasa ili nijiridhishe ni wewe mpenzi” Nyamizi aliongea.
Vedi na Nyamizi walikubaliana kuonana usiku ule na ilikuwa ni mishale ya saa tano za usiku.
Vedi akatoka na kama kawaida.
Jay nae akaandika ujumbe kwenda kwa watesi wake kuwajulisha Vedi anakoelekea.
-------------
Mwendo wa nusu saa ulitosha kuwakutanisha Nyamizi na Vedi. Walikutana sehemu walioona ni sahihi kwao kukutana.
Jambo la kwanza walilofanya marafiki wale ni kukumbatiana kwa hisia huku kila mmoja akilia kwa hisia.
Moyo wa Vedi ulifarijika kuona lau sasa amefanikiwa kupata mtu anaeweza kusimama nae wakati mgumu kama huu wakati ambao hata ndugu yake wa damu alimkataa na kumuita jini, wakati ambao watu wamemkimbia na kumwacha akipitia kipindi ambacho hakujua mwanzo wake wala mwisho wake ila alijikuta tu akiingia kwenye kipindi kama hicho, kipindi cha mateso ya akili na hisia bila watesaji kujitokeza mbele yake.
Walikaa sehemu iliokuwa inautulivu katika mgahawa mmoja ambao waliona unafaa.
“Mbona uko peke yako shemeji yuko wapi?” Vedi aliuliza.
“Ndie kanisindikiza hapa ila amepaki kule na kabaki ndani ya gari” Nyamizi alisema huku akielekeza kidole upande wa pili wa mgahawa ule. Vedi aligeuka na kuona gari zuri la kisasa likiwa limepaki.
“Kwanza nambie imekuwaje huko msibani?” Vedi alihoji kwa shauku kubwa.
Nyamizi aliguna kidogo.
“Mchana kuna tukio lilitokea ambalo lilizuia kila kitu na hapa navyokwambia maiti imerudishwa mochwari kwa uchunguzi zaidi” Nyamizi alimwambia Vedi na Vedi alikaa vizuri kwenye kiti.
“Wakati tunasubiri taratibu za mazishi; Jay alikuja ndani akiwa na mtu mwingine na alipofika dada ako akampeleka ndani alikokuwa mama na punde wakarejea huku mama akionekana dhahiri kuna kitu alitaka kumwonesha kwenye ule mwili pale mara tukashangaa Mama anapiga kelele kama mwehu na kujikuna hovyo na kabla hatujafanya lolote Jay nae akaanguka na kuzimia, hazikuzidi hata dakika kumi gari la wagonjwa likafika na kuwapeleka muhimbili”
Vedi alijifuta machozi kwa uchungu.
“Ulifanikiwa kujua kilichoendelea huko Muhimbili lakini shoga angu?” Vedi aliuliza.
“ Shemeji yako alifuatilia na badae akaja na taarifa ambazo hazikumpendeza kila mtu, alisema mumeo hakuonekana hospitali ila Mama amewekwa wodi ya uangalizi wa matatizo ya akili, mana kawa kama kichaa kiukweli” Nyamizi aliongea huku machozi yakimlenga.
“Ahsante sana kwa upendo huo mnaoonesha kwangu, hakika u rafiki mwema sana Nyamizi; kwanza mlikatisha fungate lenu ili mje kuhudhuria msiba wangu na sasa upo hapa na mimi wakati watu wote wakiniona wananikimbia kwa sababu ya kuhofia mimi ni jini” Vedi alijifuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake.
“Tuko pamoja mpenzi; kwani Jay anasemaje au umefanikiwa kuonana nae?”
Vedi alibabaika kidogo kwa swali lile.
“Kiukweli Jay nimeonana nae ila amekuwa sio Jay unaemfahamu, amekuwa ni mtu wa ajabu sana hivi karibuni, haeleweki na hapa nimetoka kwake ila hajanambia hata kuhusu mama angu……masikini Mama jamani!” Vedi alianza kulia kwa sauti ya chini.
“basi hupaswi kulia sasa, kikubwa labda unishirikishe kimetokea nini hadi kutangazwa umekufa?” Nyamizi alihoji na alionekana kuwa na uchu wa kujua hilo jambo.
Vedi alivuta pumzi nyingi na kuzishusha, hakuwa na sababu ya kuficha kwa rafiki makini kama yule.
Akamweleza yaliomkuta ndani ya meli na hadi kufikia hapo alipo.
Wakati Nyamizi na Vedi wakisimuliana; Boneka mume wa Nyamizi alikuwa ametulia ndani ya gari huku mawazo yakimpita kwa kasi. Mbali ya ubilionea aliokuwa nao ambao alilirithi kwa wazazi wake ila hakuna mtu ambae alijua ni nini kinaendelea nyuma yake.
Boneka alikuwa ni ofisa wa kitengo maalumu na kazi maalumu na aliwekwa kwenye kitengo kile na Kamishina wa jeshi la polisi Zenge wa Zenge. Kamishina Zenge wa Zenge aliamini akili ya Boneka tangu akiwa kiongozi wake ndani ya jeshi la polisi na walifanya kazi Dodoma na kufanikiwa kuzima mtandao wa mbwa mwitu katika kisa kilichoandikwa vyema na mwandishi Bahati Mwamba na kukipa jina la “DAKIKA ZA MWISHO with Wolf rules” na Boneka alifanya makubwa licha ya kuja kusaidiwa na Zedi Wimba jasusi hatari.
Na sasa Boneka ni mfanyabiashara mkubwa ila bado anatumikia taifa akiwa kwenye kitengo cha “Special operations” kilicho chini ya Kamishina Zenge wa Zenge. Kitengo hiki kimesheheni watu makini akiwemo Zedi Wimba; Honda Makubi; Haji Makame; Elias Ziga na Mwinyi Kisoda. Watu hawa wote wametokea jeshini ila Boneka pekee ndie ametoka jeshi la polisi pamoja na Kamishina mwenyewe. Mbali na Kamishina ambae alikuwa kazini siku zote ila vijana wake wote walikuwa nje ya kazi na kila mtu anafanya kazi zake na hukutana wakati wa kazi maalumu tu na wakimaliza kila mmoja huchukua hamsini zake.
Boneka tangu mwanzo aliposikia kuhusu kifo cha Vedi akili yake haikukubali mapema, mana hata wakati watu wanakimbia ndani ya meli kwenda kuona mtu aliejitupa ndani ya maji, yeye alitoka pia na kwa mbali alimuona Vedi akiwa miongoni mwa watu waliotaka kushuhuidia tukio lile.
Walipofika Nairobi ndipo walipokea taarifa za kifo cha Vedi na hima wakarejea na kazi kubwa alioifanya ni kumtuliza mkewe Nyamizi ambae alikuwa analia wakati wote na hapo wakawasiliana na mwenyekiti wa kamati ya mapokezi ambae alitakiwa kuhakikisha watu wanaingia na kutoka salama na mwenyekiti akatoa majina ya watu wote waliosaini kitabu cha watu waliotoka salama ndani ya meli.
Jina la Vedi aliliona na alimuonesha mkewe sahihi ya Vedi na Nyamizi akakubali ya kuwa ule ni mwandiko wa Vedi.
Kuna nini hapa nyuma? Alijiuliza akiwa peke yake na alichukua kitabu kile akapitia tena majina ya watu walioingia na kutoka.
Jina moja liliingia ila halikutoka.
Lilikuwa ni jina la Masumula Hussein.
Ni nani huyu binti?
Akamuuliza mkewe na jibu lilikuwa ni mtoto wa shangazi yake na Nyamizi na yeye ndie alimpa kadi.
Ikabidi wapige simu nyumbani kwa kina Masumula na jibu lilikuwa ni tangu aage kwenda harusini, hakurejea tena nyumbani.
Boneka akajenga picha ya kuhusanisha mambo yale.
Na akajiuliza kwanini Vedi sasa ndie awe muhanga wa shida ile badala ya Masumula? Na Masumula kwa nini auwawe au Vedi aliona mauaji yake? Na wauaji walitaka kumziba mdomo?
Ikabidi waelekee msibani na hata wakati yale yanatokea msibani; Boneka aliyashuhudia ila alikuwa na mashaka na mwonekano wa Jay mana alimfahamu lakini pia alikuwa na mashaka na rafiki alieongozana na Jay; Macho yake ya kijasusi yalimwambia yule hakuwa mtu mwema kabisa.
Wakati Boneka akiwaza hayo ndani ya gari kuna kitu aliona.
Aliona mtu ambae alikuwa makini na nyendo za mkewe na shemeji yake Vedi ambao walikuwa wamekaa ndani ya mgahawa wakihabarishana mambo yao ambayo hakutaka kuyaingilia.
Alipomtazama vizuri mtu yule alimtambua.
Alikuwa ni yule aliekuwa ameongozana na Jay msibani.
Alimuona Gomba.
safi mkuu ila daa mnatuacha alosto sanaRIWAYA; BAHARIA
NA; BAHATI MWAMBA
SIMU; 0758573660
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Muda wote Jay alikuwa akimtizama bila kusema kitu.
Ajabu simu iliita.
Vedi alishangaa, kisha akahesabu siku za ndoa na kugundua zilipita siku nne tu tangu walipokuwa kwenye sherehe za ndoa sasa vije tena simu iwe hewani wakati ilitakiwa wawe Nairobi.
Lakini hata yeye alijishangaa, kwanini alipiga wakati anajua kabisa wapo Nairobi?”
.
Simu ikapokelewa.
“Hallow!!” ikaitika upande wa pili.
Vedi alijua ni sauti ya Nyamizi.
“Vedi hapa naongea!” .
Vedi akasikia upande wa pili ukipumua kwa nguvu.
“Vedi yupi anaeongea?” Nyamizi alihoji.
“Usitake kusema hata sauti yangu hujaijua shoga angu” Vedi alilalama.
“Sauti yako haiwezi nipotea hata nikiwa katikati ya koma, ila imetokea nini tena nasikia sauti yako wakati tumeambiwa umekufa?” Nyamizi alihoji.
Vedi aliguna.
“Wewe upo wapi kwani” Vedi alihoji.
“Huwezi amini nimetokea msibani, nilichanganyikiwa kusikia ni wewe uliejitupa kwenye maji, raha ya fungate ilikata, tafadhali nambie kumetokea nini mpenzi” Nyamizi aliongea kwa hisia.
“Ngoja kukuchwe nadhani tutaonana” Vedi alisema.
“No! Nadhani tuonane hata sasa ili nijiridhishe ni wewe mpenzi” Nyamizi aliongea.
Vedi na Nyamizi walikubaliana kuonana usiku ule na ilikuwa ni mishale ya saa tano za usiku.
Vedi akatoka na kama kawaida.
Jay nae akaandika ujumbe kwenda kwa watesi wake kuwajulisha Vedi anakoelekea.
-------------
Mwendo wa nusu saa ulitosha kuwakutanisha Nyamizi na Vedi. Walikutana sehemu walioona ni sahihi kwao kukutana.
Jambo la kwanza walilofanya marafiki wale ni kukumbatiana kwa hisia huku kila mmoja akilia kwa hisia.
Moyo wa Vedi ulifarijika kuona lau sasa amefanikiwa kupata mtu anaeweza kusimama nae wakati mgumu kama huu wakati ambao hata ndugu yake wa damu alimkataa na kumuita jini, wakati ambao watu wamemkimbia na kumwacha akipitia kipindi ambacho hakujua mwanzo wake wala mwisho wake ila alijikuta tu akiingia kwenye kipindi kama hicho, kipindi cha mateso ya akili na hisia bila watesaji kujitokeza mbele yake.
Walikaa sehemu iliokuwa inautulivu katika mgahawa mmoja ambao waliona unafaa.
“Mbona uko peke yako shemeji yuko wapi?” Vedi aliuliza.
“Ndie kanisindikiza hapa ila amepaki kule na kabaki ndani ya gari” Nyamizi alisema huku akielekeza kidole upande wa pili wa mgahawa ule. Vedi aligeuka na kuona gari zuri la kisasa likiwa limepaki.
“Kwanza nambie imekuwaje huko msibani?” Vedi alihoji kwa shauku kubwa.
Nyamizi aliguna kidogo.
“Mchana kuna tukio lilitokea ambalo lilizuia kila kitu na hapa navyokwambia maiti imerudishwa mochwari kwa uchunguzi zaidi” Nyamizi alimwambia Vedi na Vedi alikaa vizuri kwenye kiti.
“Wakati tunasubiri taratibu za mazishi; Jay alikuja ndani akiwa na mtu mwingine na alipofika dada ako akampeleka ndani alikokuwa mama na punde wakarejea huku mama akionekana dhahiri kuna kitu alitaka kumwonesha kwenye ule mwili pale mara tukashangaa Mama anapiga kelele kama mwehu na kujikuna hovyo na kabla hatujafanya lolote Jay nae akaanguka na kuzimia, hazikuzidi hata dakika kumi gari la wagonjwa likafika na kuwapeleka muhimbili”
Vedi alijifuta machozi kwa uchungu.
“Ulifanikiwa kujua kilichoendelea huko Muhimbili lakini shoga angu?” Vedi aliuliza.
“ Shemeji yako alifuatilia na badae akaja na taarifa ambazo hazikumpendeza kila mtu, alisema mumeo hakuonekana hospitali ila Mama amewekwa wodi ya uangalizi wa matatizo ya akili, mana kawa kama kichaa kiukweli” Nyamizi aliongea huku machozi yakimlenga.
“Ahsante sana kwa upendo huo mnaoonesha kwangu, hakika u rafiki mwema sana Nyamizi; kwanza mlikatisha fungate lenu ili mje kuhudhuria msiba wangu na sasa upo hapa na mimi wakati watu wote wakiniona wananikimbia kwa sababu ya kuhofia mimi ni jini” Vedi alijifuta machozi kwa mgongo wa kiganja chake.
“Tuko pamoja mpenzi; kwani Jay anasemaje au umefanikiwa kuonana nae?”
Vedi alibabaika kidogo kwa swali lile.
“Kiukweli Jay nimeonana nae ila amekuwa sio Jay unaemfahamu, amekuwa ni mtu wa ajabu sana hivi karibuni, haeleweki na hapa nimetoka kwake ila hajanambia hata kuhusu mama angu……masikini Mama jamani!” Vedi alianza kulia kwa sauti ya chini.
“basi hupaswi kulia sasa, kikubwa labda unishirikishe kimetokea nini hadi kutangazwa umekufa?” Nyamizi alihoji na alionekana kuwa na uchu wa kujua hilo jambo.
Vedi alivuta pumzi nyingi na kuzishusha, hakuwa na sababu ya kuficha kwa rafiki makini kama yule.
Akamweleza yaliomkuta ndani ya meli na hadi kufikia hapo alipo.
Wakati Nyamizi na Vedi wakisimuliana; Boneka mume wa Nyamizi alikuwa ametulia ndani ya gari huku mawazo yakimpita kwa kasi. Mbali ya ubilionea aliokuwa nao ambao alilirithi kwa wazazi wake ila hakuna mtu ambae alijua ni nini kinaendelea nyuma yake.
Boneka alikuwa ni ofisa wa kitengo maalumu na kazi maalumu na aliwekwa kwenye kitengo kile na Kamishina wa jeshi la polisi Zenge wa Zenge. Kamishina Zenge wa Zenge aliamini akili ya Boneka tangu akiwa kiongozi wake ndani ya jeshi la polisi na walifanya kazi Dodoma na kufanikiwa kuzima mtandao wa mbwa mwitu katika kisa kilichoandikwa vyema na mwandishi Bahati Mwamba na kukipa jina la “DAKIKA ZA MWISHO with Wolf rules” na Boneka alifanya makubwa licha ya kuja kusaidiwa na Zedi Wimba jasusi hatari.
Na sasa Boneka ni mfanyabiashara mkubwa ila bado anatumikia taifa akiwa kwenye kitengo cha “Special operations” kilicho chini ya Kamishina Zenge wa Zenge. Kitengo hiki kimesheheni watu makini akiwemo Zedi Wimba; Honda Makubi; Haji Makame; Elias Ziga na Mwinyi Kisoda. Watu hawa wote wametokea jeshini ila Boneka pekee ndie ametoka jeshi la polisi pamoja na Kamishina mwenyewe. Mbali na Kamishina ambae alikuwa kazini siku zote ila vijana wake wote walikuwa nje ya kazi na kila mtu anafanya kazi zake na hukutana wakati wa kazi maalumu tu na wakimaliza kila mmoja huchukua hamsini zake.
Boneka tangu mwanzo aliposikia kuhusu kifo cha Vedi akili yake haikukubali mapema, mana hata wakati watu wanakimbia ndani ya meli kwenda kuona mtu aliejitupa ndani ya maji, yeye alitoka pia na kwa mbali alimuona Vedi akiwa miongoni mwa watu waliotaka kushuhuidia tukio lile.
Walipofika Nairobi ndipo walipokea taarifa za kifo cha Vedi na hima wakarejea na kazi kubwa alioifanya ni kumtuliza mkewe Nyamizi ambae alikuwa analia wakati wote na hapo wakawasiliana na mwenyekiti wa kamati ya mapokezi ambae alitakiwa kuhakikisha watu wanaingia na kutoka salama na mwenyekiti akatoa majina ya watu wote waliosaini kitabu cha watu waliotoka salama ndani ya meli.
Jina la Vedi aliliona na alimuonesha mkewe sahihi ya Vedi na Nyamizi akakubali ya kuwa ule ni mwandiko wa Vedi.
Kuna nini hapa nyuma? Alijiuliza akiwa peke yake na alichukua kitabu kile akapitia tena majina ya watu walioingia na kutoka.
Jina moja liliingia ila halikutoka.
Lilikuwa ni jina la Masumula Hussein.
Ni nani huyu binti?
Akamuuliza mkewe na jibu lilikuwa ni mtoto wa shangazi yake na Nyamizi na yeye ndie alimpa kadi.
Ikabidi wapige simu nyumbani kwa kina Masumula na jibu lilikuwa ni tangu aage kwenda harusini, hakurejea tena nyumbani.
Boneka akajenga picha ya kuhusanisha mambo yale.
Na akajiuliza kwanini Vedi sasa ndie awe muhanga wa shida ile badala ya Masumula? Na Masumula kwa nini auwawe au Vedi aliona mauaji yake? Na wauaji walitaka kumziba mdomo?
Ikabidi waelekee msibani na hata wakati yale yanatokea msibani; Boneka aliyashuhudia ila alikuwa na mashaka na mwonekano wa Jay mana alimfahamu lakini pia alikuwa na mashaka na rafiki alieongozana na Jay; Macho yake ya kijasusi yalimwambia yule hakuwa mtu mwema kabisa.
Wakati Boneka akiwaza hayo ndani ya gari kuna kitu aliona.
Aliona mtu ambae alikuwa makini na nyendo za mkewe na shemeji yake Vedi ambao walikuwa wamekaa ndani ya mgahawa wakihabarishana mambo yao ambayo hakutaka kuyaingilia.
Alipomtazama vizuri mtu yule alimtambua.
Alikuwa ni yule aliekuwa ameongozana na Jay msibani.
Alimuona Gomba.