Baharia; (Ujasusi, Mapenzi na Upelelezi wa kutisha)

Baharia; (Ujasusi, Mapenzi na Upelelezi wa kutisha)

RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA TISA



Mazishi yaliingiliwa na taharuki, ratiba ikabadiliswa hadi ijulikane mstakabali wa afya za walengwa wa marehemu.

Ajabu nyingine ni kuwa; taharuki ilibeba mawazo ya watu kiasi hakuna aliekumbuka kufuatilia gari lile linaelekea hospitali gani.

Watu waliendelea na malumbano yasioyo na tija.

Lakini wangejua yanayoenda kuwapata ndugu zao, hakika wasingebishania ratiba ya mazishi ya maiti bandia.

***

Gari ile ya wagonjwa iliishia kwenye nyumba ya kifahari na kisha wakashuka watu wawili waliojifanya kuwa ni wauguzi na baada ya kushuka mmoja akaelekea ndani na punde akarudi akiwa na jamaa wengine wawili waliokuwa wameshiba miili yao na maumbo makubwa yalionasibisha wingi wa mlo wao.

Watu wale wakawashusha na kuwaingiza ndani kisha wakawekwa kwenye chumba cha pamoja na punde mtu mmoja akachukua sindano na kumchoma Jay na kisha alimchoma na Mama Msangu.

Hazikupita dakika tano wote wawili walizinduka na kushangaa wakiwa kwenye chumba kimoja na wamesimamiwa na watu wengine watano ambao walikuwa kimya muda wote.

“Juma mwanangu kwani imekuwaje tena!?” Mama Msangu alihoji kwa woga baada ya kuonekana hayaelewi mazingira waliopo.

Juma akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha akamjibu.

“Sina la kusema ila nadhani tupo kwenye mikono mibaya”.

Akivyokwisha kusema hivyo haikuchukua hata sekunde akajikuta akinyayuliwa kwa nguvu na kupigwa kichwa matata na kisha akaonywa asirudie kusema hovyo kabla hajaruhusiwa.

Akiwa bado anaugulia maumivu akabebwa kwa nguvu na kutolewa kwenye chumba kile na hata Mama Msangu alipojaribu kutetea aliishia kupigwa makofi mazito yaliomwacha akiwa hajui cha kufanya.

Baada ya kutolewa kwenye kile chumba; Jay alipelekwa kwenye gari ambalo lilikuwa nje ya uzio wa nyumba ile waliokuwamo.

Alikutana na Gomba akiwa na mwanamke ndani ya gari.

“Panda tukurejeshe nyumbani kwako!!” Gomba alisema huku akimtizama Jay.

Jay alipanda na gari ikaondolewa.

“Yani sikuwahi kudhani kama kuna mtu mjinga kama wewe aisee!!” Gomba alifoka huku akiwa makini na usukani wa gari.

Jay alikaa kimya.

“Huna kifua kabisa bwana mdogo na utakuwa tatizo badae” Gomba alizidi kufoka.

Wakati Gomba akiendelea kufoka kwenye gari; ni wakati huo ambao Mama Msangu alikuwa ameshikwa kwa nguvu na hakujua wale vijana waliokuwa wamemzunguka walitaka kumfanya nini.

Walimbana vizuri na hakuweza kufurukuta kabisa na ndipo kijana mmoja alichukua kamera na kuiwasha kisha mmoja wa vijana wale akavua nguo zake zote na kusalia na mtupu, kijana mwingine nae alivua nguo zake zote na kisha wakaenda kumvamia Mama Msangu na kumvua nguo zake zote nae akabaki mtupu kama alivyozaliwa.

Mama Msangu alijionea aibu kuwa vile mbele ya vijana wadogo rika sawa na wanae, alilia kwa uchungu mana akili yake ilimwambia ni kitu gani hasa kilikuwa kinafuata kwake wakati huo.

Kwa uchungu na mapigo ya moyo yakaenda mbio kuliko kawaida na taratibu akalegea na kupoteza fahamu.

“Ooh shit!! Hatuwezi kupiga picha akiwa hivi labda tungoje azinduke” Alisema kijana aliekuwa na kamera na wale vijana waliokuwa wamevua nguo wakavaa nguo zao na kisha mwenye kamera alianza kupiga picha mwili wa Mama Msangu uliolala chini bila fahamu.

Aliporidhika akaomba avalishwe nguo zake na kisha wakamchoma sindano nyingine tena kisha wakakubaliana apelekwe Muhimbili kwenye wodi za watu wenye matatizo ya akili, mana waliamini kabisa akiamka hataweza kuwa kwenye utimamu wake tena kulingana na dawa aliochomwa.

Alikuwa ni kichaa mtarajiwa huku picha zake za uchi alizopigwa akiwa amelala zikihifadhiwa kwa kazi waliojua vijana wale.


Vedi alifika hadi kwenye mkahawa wa Hard Rock na kutafuta sehemu nzuri na kukaa kisha akaagiza maji ya baridi na kunywa huku akingojea dakika chache ili kufika saa moja ya usiku, muda ambao walikubaliana na Mamu kukutana hapo.

Akiwa ametulia mara simu yake ikaita.

Namba zilikuwa ni za Mamu.

Akapokea.

“Upo wapi wewe” Mamu aliuliza kwa mashaka kidogo.

“Nipo mashariki mwa mgahawa huu” Vedi alijibu.

Simu ikakatwa.

Akiwa bado anashangaa kukatwa kwa simu, mara mbele yake alisimama mwanamke mzuri wa sura na umbo la kuvutia, ila hakuonekana kuwa na furaha na kila mara alikuwa akiangaza huku na huko kama anaehofia jambo.

“Wewe ndie binti Mashimo?” Mamu alihoji huku akimakinika kumtazama Vedi.

Vedi alitikisa kichwa kukubali.

Mamu alikaa kwenye kiti kilichokuwa kwenye meza aliokuwa anatumia Vedi.

“Wewe ulipata wapi namba yangu” Mamu alihoji huku akimtizama Vedi usoni.

“Samahani kama nitakuwa nimekukwaza ila nimeipata sehemu ambayo ilinishawishi nikupigie” Vedi alijibu huku akikwepa kujibu mahali alikoipata hiyo namba.

“Sawa! Na ulijuaje inanihusu mimi na Banzi” Aliuliza Mamu kwa sauti ya chini kidogo.

“Niliipata kwenye vitu vya Banzi na pale nilikuwa nabahatisha tu baada ya kuona kuna ujumbe unakuhusu” Vedi alijibu.

“Vitu gani! Begi lake ama simu zake?” Mamu alihoji kwa papara.

“Hapana,sio vyote hivyo” Alijibu Vedi.

“Sasa vitu gani labda!?”

“Kitabu!!” Vedi alijibu.

“Ooh shit!! Hilo ni kosa litakalokugarimu binti” Mamu alisema kwa wasi wasi huku akitizama pande zote kwa makini.

Vedi alitumbua macho kwa kutokuelewa ni vipi hicho kitabu kiwe kina matatizo upande wake.

“Hicho kitabu kidogo kimepeleka wengi kuzimu na yawezekana hata mume wangu nae ameshafariki kwa sababu ya hicho kitu!” Mamu alisema kwa huzuni huku dhahiri akionekana chozi linamtoka.

Eh makubwa,inamaana hajui kama mume wake ameshafariki? Na hicho kitabu kina shida gani hadi kichukue uhai wa watu kiasi hicho hadi Mamu aogope na Mamu anajua nini kuhusu mkasa wa mumewe?

Yalikuwa ni maswali yaliopita kwa kasi ndani ya kichwa cha Vedi.

“Kwani kuna nini katika mambo haya? Alihoji Vedi.

“Trust me kama wanajua una hiko kitabu, watakuhangaisha sana watu wale na kama uliwahi kuonana na Banzi; basi wewe ni sawa na maiti inayotembea.”

Vedi alitumbua macho kwa maneno yale.

“Banzi nilimuonya hakusikia, ona sasa…..anyway hakikisha unaubeba msalaba wa roho zote zilizotoka kwa ajili ya mambo yaliomo humo na pia pigana kwa ajili yetu sote na aamini utavuka majaribu yaliotushinda sisi” Mamu alisema na kusimama ili aondoke; Vedi alimshika mkono.

“Dada unaniachia mafumbo bila utatuzi na peke yangu siwezi, pigana juu ya mumeo tafadhali. Mumeo ameuwawa” Vedi alisema kwa hisia.

Mamu akigeuka na kujibweteka kwenye kiti kama mgonjwa, ilikuwa ni ngumu kukubaliana na hiyo hali ya kusikia kifo cha mumewe kwenye masikio yake, alifuta machozi yalioanza kumtiririka kwa fujo.

“Hapa si pahali salama na wamejaa Jezebeli wenye masikio ya popo,tafadhali fanya niliokwambia, nilipambana kuokoa uhai wake ila nimeshindwa, nawe tumia njia zako kutafuta uhuru wako” Mamu alisema huku akijifuta machozi.

Vedi kuna kitu alikitilia maanani kwenye maelezo ya Mamu.

Neno Jezebeli!

Akajiuliza; Jezebeli ni nini na kama ni watu ni kina nani na kwenye kile kitabu cha kumbukumbu alichonacho Jezebeli alitajwa na alitajwa kupatikana kwenye hilo eneo la Hard Rock Café.

“Jezebeli ni kina nani au ni nani?” Vedi alihoji.

Mamu aliangaza tu kisha akaelekeza macho yake upande wa pili kulikokuwa na wahudumu wa mgahawa ule; Vedi nae alitazama kule ila aliishia kuona wahudumu wakipishana huku na huko.

Hakujua iliashiria nini na zaidi alichogundua ni kuwa miongoni mwa wahudumu wale baadhi hawakuwa wanaume wa kawaida kwa kuwaona tu, walikuwa ni wanaume waliozidiwa na homoni nyingi za kike na kujikuta wakifanya matendo kama ya wanawake.

Wanaume jina tu.

Vedi akarudisha macho kwa Mamu.

“Sijaelewa lolote!!” Vedi alisisitiza

Mamu hakumjibu, akasimama na kuchukua mkoba wake na kuondoka na kumwacha Vedi akiwa aezubaa na chupa ya maji mkononi.

“Hapa kuna kitu sio bure” Vedi alijisemea huku nae akisimama na kutoka ndani ya mgahawa ule.

Alihitaji kurejea nyumbani kwa Jay ili apumzike na asubiri siku ya kesho itakavyokuwa.


Jay alifikishwa nyumbani na Gomba kisha Gomba yeye akapanda gari na kuondoka bila kusema jambo lingine lolote.

Jay alipiga hatua chache na kufikia lango la nyumba yake, akafungua na kuingia ndani.

Nyumba nzima ilikuwa ni kiza kizito na hakuhofia mana alijua ni yeye anaepaswa kuwasha taa ili nuru ipate kutamalaki ndani.

Akavua viatu vyake kuvitupia karibu na sofa kisha akaenda ukutani na kuwasha taa.

Nusura apige mweleka kwa alichokiona.

Kwenye sofa walikuwa wamekaa watu wawili bila wasiwasi; Jay akatazama mlango na kuhakikisha ni yeye alieufungua na si mwingine. Imekuwaje watu hawa wapo ndani tena?

Hakukuwa na wa kumjibu.

Walikuwa ni Panga na Cholo.

“Aisee ninyi mmeingiaje humu?” Jay alihoji kwa wasiwasi.

“Kwa hiyo unahisi sisi ni majini au?” Panga aliuliza kwa kebehi.

“Inabidi mniheshimu hata kama mnaniongoza tafadhali, hapa sio pa kuingia kila mnapotaka aisee!!” Jay alifoka akiwa bado amesimama kwa wasiwasi.

“Shida yetu alikuwa ni mkeo ila kwa kuwa umetangulia wewe, basi haina shida mana hata wewe tunashida na wewe” Cholo alijibu huku akijipapasa kwenye paji la uso bila wasiwasi.

“Unajua dogo leo umetuudhi sana kwa kile ulichoonesha pale msibani, yani kama si ujanja ungeharibu kila kitu aisee!” Panga alilalama.

“Sasa mimi nimefanya nini labda.” Jay alihoji.

“Hujui?” Cholo alishangaa kisha akajichekesha kidogo.

“Kwa hiyo ulivyomkwida Gomba si kuharibu mambo kule? Au unadhani kungekuwa na askari kanzu si angefuatilia kujua kinachoendelea?” Cholo alihoji huku dhahiri sauti yake ikiwa imetawaliwa na jaziba kubwa.

“Lakini alipaswa kunishirikisha kabla hajafanya lolote jamani, akili yangu haipo sawa kabisa mjue!” Jay alilalama.

“mh! Eti akili haipo sawa” Panga alisema huku akimgeukia Cholo.

“Si unaona? Nilikwambia huyu sio njia ya kutufikisha tunakokutaka, ila ni janga hili, sasa akikutana na mwela(polisi) itakuwaje? Panga aliendelea kufoka huku akimlaumu Cholo.

“Sasa tumfanyeje labda,kumuua sasa ni tatizo jipya na kubwa zaidi” Cholo alisema kama vile wanaemeongelea hayupo pale.

Jay aliyasikiliza vyema maongezi yao na hapo aliona kabisa kinachofuata kwake ni kifo bila huruma. Hakutaka hilo limtokeaa.

Haraka akaundea mlango ili atoke nje na awakimbie wale jamaa, ila wakati anafungua mlango alikutana na sura ambayo hakuitarajia kuikuta pale mlangoni na ni kama walijua atafanya hicho kitendo.

Wakati anafungua, alikutana na Gomba akiwa amesimama na kisu mkononi bila wasiwasi.

Jay alistuka kwa sababu aliachana na Gomba akigeuza gari na yule mwanamke ambae hakuwa muongeaji kabisa, sasa vije tena yupo mlangoni kwake? Jay alipagawa na jasho likamtoka mfululizo.

“Dogo; Hivi unadhani unaakili kutuzidi?” Cholo alisema huku akisimama kumfuata Jay ambae alikuwa ameganda kama sanamu asijue cha kufanya.

“Yaani bwana mdogo, tumekuzidi kila kitu, Pesa; mademu; umri; akili na hata dhambi tumekuzidi aisee!” Cholo aliendelea kusisitiza kwa hasira.

Jay aligonganisha viganja vyake ishara ya kuomba radhi kwa wale jamaa watatu ambao aliamini kabisa sio watu wazuri kabisa katika maisha yake wakati huo. Alijiuta kumfahamu Vedi ambae ni dhahiri ndie aliemuingiza kwenye mauzauza yale. Jay aliangusha chozi la uchungu kwa kuona uhai wake unaenda kupotea hivi hivi; Jay hakutegemea kusamehewa na baradhuli wale.

Jay alipiga magoti na kusihi aachiwe huku kimoyo moyo akiomba Mungu wake amuokoe na dhahama inayomfuata.


**

Maoni yako tafadhali
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA

SIMU; 0758573660

SEHEMU YA TISA



Mazishi yaliingiliwa na taharuki, ratiba ikabadiliswa hadi ijulikane mstakabali wa afya za walengwa wa marehemu.

Ajabu nyingine ni kuwa; taharuki ilibeba mawazo ya watu kiasi hakuna aliekumbuka kufuatilia gari lile linaelekea hospitali gani.

Watu waliendelea na malumbano yasioyo na tija.

Lakini wangejua yanayoenda kuwapata ndugu zao, hakika wasingebishania ratiba ya mazishi ya maiti bandia.

***

Gari ile ya wagonjwa iliishia kwenye nyumba ya kifahari na kisha wakashuka watu wawili waliojifanya kuwa ni wauguzi na baada ya kushuka mmoja akaelekea ndani na punde akarudi akiwa na jamaa wengine wawili waliokuwa wameshiba miili yao na maumbo makubwa yalionasibisha wingi wa mlo wao.

Watu wale wakawashusha na kuwaingiza ndani kisha wakawekwa kwenye chumba cha pamoja na punde mtu mmoja akachukua sindano na kumchoma Jay na kisha alimchoma na Mama Msangu.

Hazikupita dakika tano wote wawili walizinduka na kushangaa wakiwa kwenye chumba kimoja na wamesimamiwa na watu wengine watano ambao walikuwa kimya muda wote.

“Juma mwanangu kwani imekuwaje tena!?” Mama Msangu alihoji kwa woga baada ya kuonekana hayaelewi mazingira waliopo.

Juma akavuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha akamjibu.

“Sina la kusema ila nadhani tupo kwenye mikono mibaya”.

Akivyokwisha kusema hivyo haikuchukua hata sekunde akajikuta akinyayuliwa kwa nguvu na kupigwa kichwa matata na kisha akaonywa asirudie kusema hovyo kabla hajaruhusiwa.

Akiwa bado anaugulia maumivu akabebwa kwa nguvu na kutolewa kwenye chumba kile na hata Mama Msangu alipojaribu kutetea aliishia kupigwa makofi mazito yaliomwacha akiwa hajui cha kufanya.

Baada ya kutolewa kwenye kile chumba; Jay alipelekwa kwenye gari ambalo lilikuwa nje ya uzio wa nyumba ile waliokuwamo.

Alikutana na Gomba akiwa na mwanamke ndani ya gari.

“Panda tukurejeshe nyumbani kwako!!” Gomba alisema huku akimtizama Jay.

Jay alipanda na gari ikaondolewa.

“Yani sikuwahi kudhani kama kuna mtu mjinga kama wewe aisee!!” Gomba alifoka huku akiwa makini na usukani wa gari.

Jay alikaa kimya.

“Huna kifua kabisa bwana mdogo na utakuwa tatizo badae” Gomba alizidi kufoka.

Wakati Gomba akiendelea kufoka kwenye gari; ni wakati huo ambao Mama Msangu alikuwa ameshikwa kwa nguvu na hakujua wale vijana waliokuwa wamemzunguka walitaka kumfanya nini.

Walimbana vizuri na hakuweza kufurukuta kabisa na ndipo kijana mmoja alichukua kamera na kuiwasha kisha mmoja wa vijana wale akavua nguo zake zote na kusalia na mtupu, kijana mwingine nae alivua nguo zake zote na kisha wakaenda kumvamia Mama Msangu na kumvua nguo zake zote nae akabaki mtupu kama alivyozaliwa.

Mama Msangu alijionea aibu kuwa vile mbele ya vijana wadogo rika sawa na wanae, alilia kwa uchungu mana akili yake ilimwambia ni kitu gani hasa kilikuwa kinafuata kwake wakati huo.

Kwa uchungu na mapigo ya moyo yakaenda mbio kuliko kawaida na taratibu akalegea na kupoteza fahamu.

“Ooh shit!! Hatuwezi kupiga picha akiwa hivi labda tungoje azinduke” Alisema kijana aliekuwa na kamera na wale vijana waliokuwa wamevua nguo wakavaa nguo zao na kisha mwenye kamera alianza kupiga picha mwili wa Mama Msangu uliolala chini bila fahamu.

Aliporidhika akaomba avalishwe nguo zake na kisha wakamchoma sindano nyingine tena kisha wakakubaliana apelekwe Muhimbili kwenye wodi za watu wenye matatizo ya akili, mana waliamini kabisa akiamka hataweza kuwa kwenye utimamu wake tena kulingana na dawa aliochomwa.

Alikuwa ni kichaa mtarajiwa huku picha zake za uchi alizopigwa akiwa amelala zikihifadhiwa kwa kazi waliojua vijana wale.


Vedi alifika hadi kwenye mkahawa wa Hard Rock na kutafuta sehemu nzuri na kukaa kisha akaagiza maji ya baridi na kunywa huku akingojea dakika chache ili kufika saa moja ya usiku, muda ambao walikubaliana na Mamu kukutana hapo.

Akiwa ametulia mara simu yake ikaita.

Namba zilikuwa ni za Mamu.

Akapokea.

“Upo wapi wewe” Mamu aliuliza kwa mashaka kidogo.

“Nipo mashariki mwa mgahawa huu” Vedi alijibu.

Simu ikakatwa.

Akiwa bado anashangaa kukatwa kwa simu, mara mbele yake alisimama mwanamke mzuri wa sura na umbo la kuvutia, ila hakuonekana kuwa na furaha na kila mara alikuwa akiangaza huku na huko kama anaehofia jambo.

“Wewe ndie binti Mashimo?” Mamu alihoji huku akimakinika kumtazama Vedi.

Vedi alitikisa kichwa kukubali.

Mamu alikaa kwenye kiti kilichokuwa kwenye meza aliokuwa anatumia Vedi.

“Wewe ulipata wapi namba yangu” Mamu alihoji huku akimtizama Vedi usoni.

“Samahani kama nitakuwa nimekukwaza ila nimeipata sehemu ambayo ilinishawishi nikupigie” Vedi alijibu huku akikwepa kujibu mahali alikoipata hiyo namba.

“Sawa! Na ulijuaje inanihusu mimi na Banzi” Aliuliza Mamu kwa sauti ya chini kidogo.

“Niliipata kwenye vitu vya Banzi na pale nilikuwa nabahatisha tu baada ya kuona kuna ujumbe unakuhusu” Vedi alijibu.

“Vitu gani! Begi lake ama simu zake?” Mamu alihoji kwa papara.

“Hapana,sio vyote hivyo” Alijibu Vedi.

“Sasa vitu gani labda!?”

“Kitabu!!” Vedi alijibu.

“Ooh shit!! Hilo ni kosa litakalokugarimu binti” Mamu alisema kwa wasi wasi huku akitizama pande zote kwa makini.

Vedi alitumbua macho kwa kutokuelewa ni vipi hicho kitabu kiwe kina matatizo upande wake.

“Hicho kitabu kidogo kimepeleka wengi kuzimu na yawezekana hata mume wangu nae ameshafariki kwa sababu ya hicho kitu!” Mamu alisema kwa huzuni huku dhahiri akionekana chozi linamtoka.

Eh makubwa,inamaana hajui kama mume wake ameshafariki? Na hicho kitabu kina shida gani hadi kichukue uhai wa watu kiasi hicho hadi Mamu aogope na Mamu anajua nini kuhusu mkasa wa mumewe?

Yalikuwa ni maswali yaliopita kwa kasi ndani ya kichwa cha Vedi.

“Kwani kuna nini katika mambo haya? Alihoji Vedi.

“Trust me kama wanajua una hiko kitabu, watakuhangaisha sana watu wale na kama uliwahi kuonana na Banzi; basi wewe ni sawa na maiti inayotembea.”

Vedi alitumbua macho kwa maneno yale.

“Banzi nilimuonya hakusikia, ona sasa…..anyway hakikisha unaubeba msalaba wa roho zote zilizotoka kwa ajili ya mambo yaliomo humo na pia pigana kwa ajili yetu sote na aamini utavuka majaribu yaliotushinda sisi” Mamu alisema na kusimama ili aondoke; Vedi alimshika mkono.

“Dada unaniachia mafumbo bila utatuzi na peke yangu siwezi, pigana juu ya mumeo tafadhali. Mumeo ameuwawa” Vedi alisema kwa hisia.

Mamu akigeuka na kujibweteka kwenye kiti kama mgonjwa, ilikuwa ni ngumu kukubaliana na hiyo hali ya kusikia kifo cha mumewe kwenye masikio yake, alifuta machozi yalioanza kumtiririka kwa fujo.

“Hapa si pahali salama na wamejaa Jezebeli wenye masikio ya popo,tafadhali fanya niliokwambia, nilipambana kuokoa uhai wake ila nimeshindwa, nawe tumia njia zako kutafuta uhuru wako” Mamu alisema huku akijifuta machozi.

Vedi kuna kitu alikitilia maanani kwenye maelezo ya Mamu.

Neno Jezebeli!

Akajiuliza; Jezebeli ni nini na kama ni watu ni kina nani na kwenye kile kitabu cha kumbukumbu alichonacho Jezebeli alitajwa na alitajwa kupatikana kwenye hilo eneo la Hard Rock Café.

“Jezebeli ni kina nani au ni nani?” Vedi alihoji.

Mamu aliangaza tu kisha akaelekeza macho yake upande wa pili kulikokuwa na wahudumu wa mgahawa ule; Vedi nae alitazama kule ila aliishia kuona wahudumu wakipishana huku na huko.

Hakujua iliashiria nini na zaidi alichogundua ni kuwa miongoni mwa wahudumu wale baadhi hawakuwa wanaume wa kawaida kwa kuwaona tu, walikuwa ni wanaume waliozidiwa na homoni nyingi za kike na kujikuta wakifanya matendo kama ya wanawake.

Wanaume jina tu.

Vedi akarudisha macho kwa Mamu.

“Sijaelewa lolote!!” Vedi alisisitiza

Mamu hakumjibu, akasimama na kuchukua mkoba wake na kuondoka na kumwacha Vedi akiwa aezubaa na chupa ya maji mkononi.

“Hapa kuna kitu sio bure” Vedi alijisemea huku nae akisimama na kutoka ndani ya mgahawa ule.

Alihitaji kurejea nyumbani kwa Jay ili apumzike na asubiri siku ya kesho itakavyokuwa.


Jay alifikishwa nyumbani na Gomba kisha Gomba yeye akapanda gari na kuondoka bila kusema jambo lingine lolote.

Jay alipiga hatua chache na kufikia lango la nyumba yake, akafungua na kuingia ndani.

Nyumba nzima ilikuwa ni kiza kizito na hakuhofia mana alijua ni yeye anaepaswa kuwasha taa ili nuru ipate kutamalaki ndani.

Akavua viatu vyake kuvitupia karibu na sofa kisha akaenda ukutani na kuwasha taa.

Nusura apige mweleka kwa alichokiona.

Kwenye sofa walikuwa wamekaa watu wawili bila wasiwasi; Jay akatazama mlango na kuhakikisha ni yeye alieufungua na si mwingine. Imekuwaje watu hawa wapo ndani tena?

Hakukuwa na wa kumjibu.

Walikuwa ni Panga na Cholo.

“Aisee ninyi mmeingiaje humu?” Jay alihoji kwa wasiwasi.

“Kwa hiyo unahisi sisi ni majini au?” Panga aliuliza kwa kebehi.

“Inabidi mniheshimu hata kama mnaniongoza tafadhali, hapa sio pa kuingia kila mnapotaka aisee!!” Jay alifoka akiwa bado amesimama kwa wasiwasi.

“Shida yetu alikuwa ni mkeo ila kwa kuwa umetangulia wewe, basi haina shida mana hata wewe tunashida na wewe” Cholo alijibu huku akijipapasa kwenye paji la uso bila wasiwasi.

“Unajua dogo leo umetuudhi sana kwa kile ulichoonesha pale msibani, yani kama si ujanja ungeharibu kila kitu aisee!” Panga alilalama.

“Sasa mimi nimefanya nini labda.” Jay alihoji.

“Hujui?” Cholo alishangaa kisha akajichekesha kidogo.

“Kwa hiyo ulivyomkwida Gomba si kuharibu mambo kule? Au unadhani kungekuwa na askari kanzu si angefuatilia kujua kinachoendelea?” Cholo alihoji huku dhahiri sauti yake ikiwa imetawaliwa na jaziba kubwa.

“Lakini alipaswa kunishirikisha kabla hajafanya lolote jamani, akili yangu haipo sawa kabisa mjue!” Jay alilalama.

“mh! Eti akili haipo sawa” Panga alisema huku akimgeukia Cholo.

“Si unaona? Nilikwambia huyu sio njia ya kutufikisha tunakokutaka, ila ni janga hili, sasa akikutana na mwela(polisi) itakuwaje? Panga aliendelea kufoka huku akimlaumu Cholo.

“Sasa tumfanyeje labda,kumuua sasa ni tatizo jipya na kubwa zaidi” Cholo alisema kama vile wanaemeongelea hayupo pale.

Jay aliyasikiliza vyema maongezi yao na hapo aliona kabisa kinachofuata kwake ni kifo bila huruma. Hakutaka hilo limtokeaa.

Haraka akaundea mlango ili atoke nje na awakimbie wale jamaa, ila wakati anafungua mlango alikutana na sura ambayo hakuitarajia kuikuta pale mlangoni na ni kama walijua atafanya hicho kitendo.

Wakati anafungua, alikutana na Gomba akiwa amesimama na kisu mkononi bila wasiwasi.

Jay alistuka kwa sababu aliachana na Gomba akigeuza gari na yule mwanamke ambae hakuwa muongeaji kabisa, sasa vije tena yupo mlangoni kwake? Jay alipagawa na jasho likamtoka mfululizo.

“Dogo; Hivi unadhani unaakili kutuzidi?” Cholo alisema huku akisimama kumfuata Jay ambae alikuwa ameganda kama sanamu asijue cha kufanya.

“Yaani bwana mdogo, tumekuzidi kila kitu, Pesa; mademu; umri; akili na hata dhambi tumekuzidi aisee!” Cholo aliendelea kusisitiza kwa hasira.

Jay aligonganisha viganja vyake ishara ya kuomba radhi kwa wale jamaa watatu ambao aliamini kabisa sio watu wazuri kabisa katika maisha yake wakati huo. Alijiuta kumfahamu Vedi ambae ni dhahiri ndie aliemuingiza kwenye mauzauza yale. Jay aliangusha chozi la uchungu kwa kuona uhai wake unaenda kupotea hivi hivi; Jay hakutegemea kusamehewa na baradhuli wale.

Jay alipiga magoti na kusihi aachiwe huku kimoyo moyo akiomba Mungu wake amuokoe na dhahama inayomfuata.


**

Maoni yako tafadhali
Nimelipia Mpesa boss
 
RIWAYA; BAHARIA

NA; BAHATI MWAMBA


SIMU; 0758573660


SEHEMU YA KUMI



Mamu aliangaza tu kisha akaelekeza macho yake upande wa pili kulikokuwa na wahudumu wa mgahawa ule; Vedi nae alitazama kule ila aliishia kuona wahudumu wakipishana huku na huko.

Hakujua iliashiria nini na zaidi alichogundua ni kuwa miongoni mwa wahudumu wale baadhi hawakuwa wanaume wa kawaida kwa kuwaona tu, walikuwa ni wanaume waliozidiwa na homoni nyingi za kike na kujikuta wakifanya matendo kama ya wanawake.

Wanaume jina tu.

Vedi akarudisha macho kwa Mamu.

“Sijaelewa lolote!!” Vedi alisisitiza

Mamu hakumjibu, akasimama na kuchukua mkoba wake na kuondoka na kumwacha Vedi akiwa aezubaa na chupa ya maji mkononi.

“Hapa kuna kitu sio bure” Vedi alijisemea huku nae akisimama na kutoka ndani ya mgahawa ule.

Alihitaji kurejea nyumbani kwa Jay ili apumzike na asubiri siku ya kesho itakavyokuwa.


Jay alifikishwa nyumbani na Gomba kisha Gomba yeye akapanda gari na kuondoka bila kusema jambo lingine lolote.

Jay alipiga hatua chache na kufikia lango la nyumba yake, akafungua na kuingia ndani.

Nyumba nzima ilikuwa ni kiza kizito na hakuhofia mana alijua ni yeye anaepaswa kuwasha taa ili nuru ipate kutamalaki ndani.

Akavua viatu vyake kuvitupia karibu na sofa kisha akaenda ukutani na kuwasha taa.

Nusura apige mweleka kwa alichokiona.

Kwenye sofa walikuwa wamekaa watu wawili bila wasiwasi; Jay akatazama mlango na kuhakikisha ni yeye alieufungua na si mwingine. Imekuwaje watu hawa wapo ndani tena?

Hakukuwa na wa kumjibu.

Walikuwa ni Panga na Cholo.

“Aisee ninyi mmeingiaje humu?” Jay alihoji kwa wasiwasi.

“Kwa hiyo unahisi sisi ni majini au?” Panga aliuliza kwa kebehi.

“Inabidi mniheshimu hata kama mnaniongoza tafadhali, hapa sio pa kuingia kila mnapotaka aisee!!” Jay alifoka akiwa bado amesimama kwa wasiwasi.

“Shida yetu alikuwa ni mkeo ila kwa kuwa umetangulia wewe, basi haina shida mana hata wewe tunashida na wewe” Cholo alijibu huku akijipapasa kwenye paji la uso bila wasiwasi.

“Unajua dogo leo umetuudhi sana kwa kile ulichoonesha pale msibani, yani kama si ujanja ungeharibu kila kitu aisee!” Panga alilalama.

“Sasa mimi nimefanya nini labda.” Jay alihoji.

“Hujui?” Cholo alishangaa kisha akajichekesha kidogo.

“Kwa hiyo ulivyomkwida Gomba si kuharibu mambo kule? Au unadhani kungekuwa na askari kanzu si angefuatilia kujua kinachoendelea?” Cholo alihoji huku dhahiri sauti yake ikiwa imetawaliwa na jaziba kubwa.

“Lakini alipaswa kunishirikisha kabla hajafanya lolote jamani, akili yangu haipo sawa kabisa mjue!” Jay alilalama.

“mh! Eti akili haipo sawa” Panga alisema huku akimgeukia Cholo.

“Si unaona? Nilikwambia huyu sio njia ya kutufikisha tunakokutaka, ila ni janga hili, sasa akikutana na mwela(polisi) itakuwaje? Panga aliendelea kufoka huku akimlaumu Cholo.

“Sasa tumfanyeje labda,kumuua sasa ni tatizo jipya na kubwa zaidi” Cholo alisema kama vile wanaemeongelea hayupo pale.

Jay aliyasikiliza vyema maongezi yao na hapo aliona kabisa kinachofuata kwake ni kifo bila huruma. Hakutaka hilo limtokeaa.

Haraka akaundea mlango ili atoke nje na awakimbie wale jamaa, ila wakati anafungua mlango alikutana na sura ambayo hakuitarajia kuikuta pale mlangoni na ni kama walijua atafanya hicho kitendo.

Wakati anafungua, alikutana na Gomba akiwa amesimama na kisu mkononi bila wasiwasi.

Jay alistuka kwa sababu aliachana na Gomba akigeuza gari na yule mwanamke ambae hakuwa muongeaji kabisa, sasa vije tena yupo mlangoni kwake? Jay alipagawa na jasho likamtoka mfululizo.

“Dogo; Hivi unadhani unaakili kutuzidi?” Cholo alisema huku akisimama kumfuata Jay ambae alikuwa ameganda kama sanamu asijue cha kufanya.

“Yaani bwana mdogo, tumekuzidi kila kitu, Pesa; mademu; umri; akili na hata dhambi tumekuzidi aisee!” Cholo aliendelea kusisitiza kwa hasira.

Jay aligonganisha viganja vyake ishara ya kuomba radhi kwa wale jamaa watatu ambao aliamini kabisa sio watu wazuri kabisa katika maisha yake wakati huo. Alijiuta kumfahamu Vedi ambae ni dhahiri ndie aliemuingiza kwenye mauzauza yale. Jay aliangusha chozi la uchungu kwa kuona uhai wake unaenda kupotea hivi hivi; Jay hakutegemea kusamehewa na baradhuli wale.

Jay alipiga magoti na kusihi aachiwe huku kimoyo moyo akiomba Mungu wake amuokoe na dhahama inayomfuata.

“Tunamfanya nini huyu pimbi!” Panga alihoji huku akisimama pale alipokuwa amekaa mwanzo.

“Plan b nadhani inaweza kutuweka salama zaidi kuliko hii plan A.” Gomba alisema huku akichezea kisu chake kwa vidole vyake na akimtizama Jay kwa macho fulani yenye ujumbe usio tafsirika.

Jay aliona akakufa kizembe akiendelea kuzubaa ni lazima afanye jambo litakaloweza kumsaidia aponyoke kwenye mikono ya watu wale wabaya.

Akiwa amepiga magoti chini, aliona namna ambavyo Panga na Cholo walivyokuwa wanamfuata kwa hatua za taratibu huku wakibwabwaja.

Pale alipokuwa aliona pembe ya zulia ipo karibu na magoti yake,akaona huo ndio mwanya wa kufanya kile alichofikiria ili ajinasue kwenye janga linalomkabili.

Akafanya kitendo ambacho hakuna ambae alikitegemea.

Akaishika pembe ya zulia kisha akalinyanyua juu kwa kasi na kusababisha liteleze kwenye marumaru na kisha akalivutia kwake kwa kasi na kufanya Cholo na Panga wapige mweleka mkubwa chini bila kutarajia huku kila mmoja akianguka kwa namna yake na kilio cha hamaniko.

Jay hakutaka kuzubaa, haraka akataka kuruka na kuuendea mlango, ila hesabu zake zilikuwa nyuma ya muda na hii ni kwa sababu hakuwa mzoefu wa mapigano la sivyo hesabu zake angemjumlisha na Gomba.

Kushindwa kupiga hesabu vyema kukapelekea kujutia kosa lake.

Akakutana na ngumi nzito iliomrudisha nyuma bila kupenda,akampatazama tena Gomba ambae alikuwa amesimama bila wasiwasi wowote.

Akajaribu tena bahati yake na akajifyatua mzima mzima ili amkumbe Gomba ila napo hakujua Gomba ni mtu wa aina gani, akajikuta akidakwa kama mchezo hivi na kusukumwa chini kwa nguvu na alipotaka kusimama alikutana na teke zito kutoka kwa Panga ambae alikuwa ameshasimama na gadhabu kubwa.

Jay akataka kujinyanyua tena ila aliishia mikononi mwa Panga na kujikuta akichezea makonde mengi ya uso na kuanza kuvuja damu.

“Punguza jaziba bwana Panga” Cholo alimshika mkono Panga huku akimsihi.

“Pimbi wewe, yani unataka kuweka mchapo na sisi!! Yani wa kutuotea sisi kweli! Ebo!” Panga aling’aka kwa gadhabu huku akijishika makalio ambayo dhahiri yalionekana kupata shuruba wakati anayaangukia.

“Mchezo wa kuotea ni mbaya sana bwana mdogo” Gomba alisema huku akimwinamia.

Jay alijitahidi kusema ila haikuwezekana, kipigo kilimkolea.

“Tunaweka usiku mjue” Panga alizungumza huku bado akionekana kuwa na gadhabu iliopitiliza kwa kitendo walichofanyiwa.

“Sasa tunakupa dozi bwana mdogo na ili uipate ni lazima ututafute na ukumbuke pia unaumwa Kansa ya mifupa na ili upone lazima ututafute,sasa rudia ujinga wako ufe na auche Cholo akimuoa mkeo, si uliona picha zake wakiwa wote lakini eeh!” Gomba alizungumza akiwa bado amemshika kwa kumwinamia Jay ambae alikuwa nusu amelala na nusu ameinuka. Alikuwa kifudifudi.

Ile kusikia neno mkeo, kukawa kama amesikia kitu cha ajabu kikipita mwilini mwake na kumwachia mamumivu moyoni.

Aliona kama ambae amemkosea sana Vedi kwa kutomsikiliza wakati alipomfikia siku hiyo lakini pia nafsi nyingine ilijuta kukutana na Vedi katika maisha yake japo yajayo hawakuwahi kuyajua kama watafikia hapo.

“Hii inaitwa dope na inaliwa na matajiri tu sasa ni bahati kwako kidampa kuipata eti” Gomba alimwambia Jay huku akisogeza ncha ya kidole kisu kwenye pua za Jay. Jay aliona kwa mbali kitu kama poda kikiwa juu ya ncha ya kisu na akalirudia neno “Dope”…

“Noo;msinifanye hivyo…” Jay alijitahidi kusema bila mafanikio na alipojaribu kujitikisa alijikuta akiwa amedhibitiwa vyema na miguu ya Gomba ambae alikuwa amemyanyua na kumbana usawa wa mbavu na miguu yake huku mkono mmoja ukipita kwenye usawa wa mabega yake na kumfanya ainuke kwa kutazama juu.

Bado aliona kile kisu kikimsogelea taratibu, akataka kuvuta pumzi nyingi ili azihifadhi wakati akipambana asivutishwe ule unga.

Alikuwa amechelewa tena hesabu zake.

Wakati akitaka kuvuta ni wakati huo ncha ya kisu ilikuwa sambamba na tundu moja ya pua hivyo akajikuta akivuta sambamba na unga ule.

Akalia kwa uchungu kwa tukio lile.

Gomba alimwachia na kusimama huku akitabasamu kwa kitendo kile kisicho cha kiuugwana.

Jay alianza kuhisi hali ya tofauti ikimjia kwa kasi, alijihisi ni mwepesi na furaha ya ajabu ikimjia, hata yale maumivu ya kipigo hakuyasikia tena na zaidi aliendelea kuhisi amani ikimtawala na yale mawazo mabaya yakiondoka kwake.

Jay alijichekelesha kama bwege.

“Tayari yupo stoned huyu!” Gomba alisema.

“Muda wa high ukifika ndo atajua utamu wa dope na akikolea basi utumwa utamhusu.” Panga aliongeza.

Jay aliendelea aliendelea kushindana na raha ya ajabu iliomkumba,alijitahidi kupishana nayo ila ilikuwa ni kazi bure na alijikuta akiitamani tena ile raha iendelee kuwa nae.

Akajivuta kutoka chini na kuegemea miguu ya Gomba kisha awa hisia.

“Please I need more dope please”

Nafsi yake ilimuwia uzito kukubali kutendo kile cha kuomba ila alijikuta mwili unamsaliti; mwili ulihitaji tena kupata ile raha ya ajabu.

Cholo alisogea na kumwinamia.

“Sikia bwana mdogo,hii kitu tunakupa kwa garama ndogo tu, nayo ni siri kuhusu yanayoendelea, lakini pia tunataka uhakikishe demu wako hakutani na askari yeyote bila sisi kujua na pia hakikisha kila akitoka hapa unajua anakoenda na sisi kila jioni tutakuletea hii kitu” Cholo alimwambia Jay huku akipunga fundo dogo la karatasi hewani.

“Hiyo uliopata inatosha kwa sasa, ukizidisha tutakupeleka mochwari” Cholo alisema tena huku akisimama na kisha akawapa ishara wenzie na wakaanza kutoka ndani ya ile nyumba na kumwacha Jay akianguka chini kwa mauzauza yanayoukumba mwili wake.

Chozi lilitoka kwa uchungu, ila hakuwa na la kufanya zaidi ya kutulia chini na kuacha mwili usisimke kwa furaha ya kununua.

Jay rasimi alikuwa ameingia kwenye uraibu wa madawa ya kulevya bila kupenda.

Lakini kwa nini hawa jamaa wanayafanya haya yote?

Hakuna aliejua chanzo cha yote ni nini, je ni baharia au ni kitabu cha baharia?

Bado hakuna aliejua na Baharia aliona nini; alijua nini hadi kifo kikamkuta? Bado lilikuwa ni swali bila jibu.

Bado Cholo;Panga na Gomba walikuwa washindi kwenye mchezo ule usio na jina la kueleweka, walitumia nguvu nyingi bila sababu ya msingi kueleweka.


Lakini siku zote waswahili wanasema; “Mwenda kombo kwa hisani, hurudi kwa aibu ya huzuni” mchezo uliingiliwa na wababe wa fitina wakiongozwa na Zedi Wimba.
 
Riwaya kali sana ukizingatia na uandishi wake wa namna yake
 
Back
Top Bottom