Bahati yetu ni Jua, Unyevunyevu (humidity) na Joto - Corona hatambi

Bahati yetu ni Jua, Unyevunyevu (humidity) na Joto - Corona hatambi

KalamuTena

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2018
Posts
13,187
Reaction score
17,167
Namba zetu za maambukizi na vifo hadi sasa vinaelekea kuwa tofauti na zile za wenzetu walioko kwenye nchi za baridi.
Ushahidi unaanza kupatikana sasa kueleza tofauti hizi kati ya nchi zetu na za hawa wengine.

Ingawa pamekuwepo na dhana ya kuhusisha joto, unyevunyevu na mwanga katika kupungua kwa kasi ya maenezi ya coronavirus, dhana hii bado ilikuwa haijapata ushahidi wa kimaabara kuhusisha hali hizo na kupunguza kasi ya kuenea kwa coronavirus.

Sasa uchunguzi huo umefanyika na inabainishwa wazi kwamba corona anadhurika haraka anapokutana na mazingira hayo ya joto, mwanga na unyevunyevu.

Huu utakuwa ni ushahidi wa kujitosheleza kuhusu bahati yetu ya kutokuwa na kasi ya maambukizi kama ile tuliyoiona Italy, Uingereza, USA na kwingineko.

Corona anadhurika haraka, kwa hiyo maambukizi yanapungua. Hii haina maana kwamba maambukizi hayatakuwepo kabisa. Maambukizi yatakuwepo kama haya tuliyokwishayashuhudia, lakini kasi yake haitafikia ile inayoonekana kwenye nchi za baridi.

Maana ya utafiti huo ni kwamba, sisi tukiongeza juhudi ya kuongeza kuzuia maambukizi, kama kunawa mikono, barakoa na kutokaribiana zaidi, nafasi yetu ya kuzuia maambukizi na vifo inaweza kuwa kubwa zaidi.

Hii ina maana, Mungu, alishasikiliza sala zetu kuhusu ugonjwa huu, ndiyo maana katuweka hapa tulipo.
Tuzidi kusali/kuswali.

Najua utataka nikupe source ya utafiti huo. Vuta subira. Kwa sasa nikupe tu kwamba tafiti za aina hii zinaendelea India, USA na kwingineko.

Hata sisi hapa tungeweza kufanya; aaah, acha tupige siasa kwanza. Kwa sababu siasa inalipa!
 
Mheshimiwa rais asitishwe na mtu, hakuna lockdown hapa. Angalia nchi walizoimplement lockdown kama italy na spain maambukizi yalishamiri bado na sasa wanaanza kuruhusu shughuli za kiuchumi ziendelee maana yake performance ya lockdown ni sifuri. Hongera sana JPM the JIWE himself.
 
Mheshimiwa rais asitishwe na mtu, hakuna lockdown hapa. Angalia nchi walizoimplement lock down kama italy na spain maambukizi yalishamiri bado na sasa wanaanza kuruhusu shughuli za kiuchumi ziendelee maana yake performance ya lockdown ni sifuri. Hongera sana JPM the JIWE himself.
Sio suala la kutishwa. Nchi unazozitaja wali implement lockdown ikiwa ni too late.

Ndio sababu yamewakuta ya kuwakuta. Pia wana idad kubwa ya watu wanao.ingia na kutoka.kutoka nchi mbalimbali.
Tofauti na kwetu bado tunao muda, sasa usijifananishe na wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mheshimiwa rais asitishwe na mtu, hakuna lockdown hapa. Angalia nchi walizoimplement lock down kama italy na spain maambukizi yalishamiri bado na sasa wanaanza kuruhusu shughuli za kiuchumi ziendelee maana yake performance ya lockdown ni sifuri. Hongera sana JPM the JIWE himself.
Uelewa wako ni mashaka matupu...hivi unajua nchi hizo robot tatu yake ni miji? Unajua muingiliano yao mikubwa kuliko huku Africa? Wasingeweka lock down kwasasa wangekua wanaongea mengine kwa taarifa yako.
 
Maelezo mazuri sana na yanatia moyo ingawa bado haujaweka ushahidi wa kisayansi.

Jambo lingine nina miezi mitatu tangu nipatiwe uraia na Waziri wa Mambo ya Ndani bahati nzuri hakuna aliyepinga nisipewe uraia Naomba nipatiwe tofauti ya kusali na kuswali bado sijamaliza course ya Kiswahili
 
Sio suala la kutishwa. Nchi unazozitaja wali implement lockdown ikiwa ni too late. Ndio sababu yamewakuta ya kuwakuta. Pia wana idad kubwa ya watu wanao.ingia na kutoka.kutoka nchi mbalimbali. Tofauti na kwetu bado tunao muda, sasa usijifananishe na wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaani nyinyi wapinganji (walalamikaji) mna kila sifa ya kuwa ndugu na hicho kirusi.

Wakati taifa liko silini likijiombea nyinyi mko chimbo mnaomba hali iwe mbaya zaidi,ni kama hamtaki kusikia habari zozote njema.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi unajua nchi hizo robot tatu yake ni miji? Unajua muingiliano yao mikubwa kuliko huku Africa? Wasingeweka lock down kwasasa wangekua wanaongea mengine kwa taarifa yako.
Uelewa wangu hauna mashaka ila TUNATOFAUTIANA PERSPECTIVE, tujifunze kuheshimiana.
 
Maelezo yako yana mashaka makubwa. Kuna nchi kama Ufilipino ambako kuna joto kali kuliko hapa kwetu lakini maambukizi yako juu. Tatizo la msingi ni kwamba hatupimi watu wengi kwa hiyo hatujui ukubwa wa tatizo. Na hii si kwa Tanzania tu, nchi nyingi za Afrika zinapima idadi ndogo sana ya watu, tena wale wanaojipeleka wenyewe hospitalini au wale waliowekwa karantini. Kumbuka asilimia kubwa ya watu wenye maambukizi hawaoneshi dalili yoyote
 
Iran na Saudi Arabia Joto Ni kubwa Sana na Umeona Jinsi Corona Ilivyopiga huko.

The difference ni kuwa wenyewe walikuwa wanafanya testing sisi hatufanyi.

Hakuna Cha Joto Hapa Wala Baridi. Muda si Mrefu Mtaongea Lugha Moja.
 
Ulichoandika siyo kweli.
South Africa kwao ni kiangazi sasa hivi. Wanazika.
Australia kwao ni kiangazi pia wanazika.
Huu ugonjwa ni mpya tabia yake haifahamiki.
Wakifika wagonjwa 250, hesabu siku kumi baadaye kutakuwa na wagonjwa 5000 (late of exponentially growth). Nchi yoyote ambazo zilipunguza mizunguko ya watu kabla ya wagonjwa 50 hawajaumwa ndo aina idadi chache za wagonjwa.
Mafundi seremala huu msimu wenu wa kuvuna.
Tutazika wengi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo hii tukipima watanzania wote,unadhani maambukizi yatakuwa kiasi gani?Acheni ujinga kwenye mambo serious
 
Back
Top Bottom