Bahati yetu ni Jua, Unyevunyevu (humidity) na Joto - Corona hatambi

Bahati yetu ni Jua, Unyevunyevu (humidity) na Joto - Corona hatambi

Ipe muda muda tu, itathibitisha uhalisia wake, hamna anayeijua mpaka sasa zaidi ya kupiga ramli.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo pa kupiga amri ndipo panapofanyiwa kazi mkuu na tafiti mbalimbali zinazoendelea, mojawapo ikiwa uthibitisho wa kimaabara kuwa coronavirus anaathiriwa na joto, mionzi na unyevunyevu, kwa pamoja. Hii sio ramli tena, bali ni jambo lililothibitishwa kwa utafiti.

Sasa basi, hii haina maana kwamba mazingira hayo ndio yatakuwa tegemeo la moja kwa moja kuiondoa coronavirus; hapana. Hakuna utafiti uliofikia hitimisho hilo, ila itaeleweka sasa kwamba, hali ya joto/unevunyevu/mwanga ni sehemu mhimu katika kupunguza nguvu ya coronavirus kusambaa na kufanya maambukizi.
Maana ya hili ni kwamba ni lazima njia nyingine za kinga zitumike sambamba ili kuongeza kinga zaidi, ikiwa ni pamoja na kunawa mikono, kutumia barakoa na hata kupata chanjo yenyewe.
 
Naam, tatizo lipo kwenye takwimu zinazo tolewa na serekali za ukanda huo wa kijiografia, siyo reliable, haziaminiki kabisa. Yapo mataifa machache yanayo weza kukupa taarifa za kutegemewa japo Tz si miongoni mwayo. Kwenye mataifa yetu haya fukara case nyingi zinapita bila kutambuliwa, taarifa kama za akina ummy mwalimu haziwezi kutumika kufanya hitimisho sahihi.
Ninakubaliana nawe juu ya hili. Baadhi ya nchi ni swala la kutokuwa na uwezo wa kupima na kutoa takwimu kamilifu. Hawa wangekuwa na uwezo takwimu zao kidogo zingeonyesha uhalisia wa hali iliyopo kwenye nchi hizo.

Baadhi yetu, kama Tanzania, sisi tunasukumwa na kutaka tuonekane hatuathiriki. Namba zetu tunataka zionekane nzuri tu hata kama tunajua kwamba hali sivyo hivyo. Hili ni tatizo.

Lakini pamoja na kutokuwa na uwezo wa kupata takwimu sahihi, kinachozungumziwa kwenye mada hii ni utafiti unaoonyesha pasipo shaka kwamba hali ya joto/unyevunyevu/mwanga, mazingira haya yanapunguza wingi wa coronavirus, kwa hiyo kutoa mwanya zaidi wa kupunguza kasi ya maambukizi. Hali hiyo haizuii moja kwa moja coronavirus kuendelea kuwepo na kusambaa, lakini kasi yake inapunguzwa.
Kwa hiyo, njia za ziada, kama kunawa mikono,kuvaa barakoa na njia zingine mhimu zikitumika sambamba na mazingira hayo, hali ya maambukizi katika nchi hizi kidogo inakuwa si sawa na hali za milipuko iliyokwishaonekana sehemu mbalimbali duniani..

Kwa hiyo juhudi inabidi ziongezwe katika njia za kukinga ili maambukizi yaendelee kupungua zaidi.

Na hapo hapo, kumbuka kwamba watu wengi wamekwishaambukizwa tayari, hata wengine wasioonyesha dalili za ugonjwa kabisa.

Kwa hiyo ugonjwa utaendelea kuwepo, ila tunaweza kuuhimiri zaidi kwa kuongeza umakini katika njia za kinga, huku mazingira yetu ya joto/unyevunyevu/mwanga navyo vikisaidia.
 
Unaelimu yoyote ya mambo ya Geography ndugu.

unajua kitu kiitwacho Tabia ya Nchi na athari zake kwa viumbe.

Huko Saudia na Kuwait unajua Tabia yake ya nchi( Climatic condition).

Unajua tofauti katika ya Tabia ya Nchi( Climatic condition) na Hali ya Hewa (Weather Condition).

Ukijua kutofautisha hapo utaelewa ni kwa nini Saudia na Kuwait Hali ya hewa yake ni joto ingawaje Tabia ya Nchi yake ni yakimediterania na huku kwetu Tabia ya Nchi ni Kitropic japo kuna maeneo baadhi hali ya hewa yake ni baridi
Mpuuzi wewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maelezo yako yana mashaka makubwa. Kuna nchi kama Ufilipino ambako kuna joto kali kuliko hapa kwetu lakini maambukizi yako juu. Tatizo la msingi ni kwamba hatupimi watu wengi kwa hiyo hatujui ukubwa wa tatizo. Na hii si kwa Tanzania tu, nchi nyingi za Afrika zinapima idadi ndogo sana ya watu, tena wale wanaojipeleka wenyewe hospitalini au wale waliowekwa karantini. Kumbuka asilimia kubwa ya watu wenye maambukizi hawaoneshi dalili yoyote
Acha uongo Philippine ni kiangaza kwa sasa man's take ni kipindi cha baridi
 
Ulichoandika siyo kweli.
South Africa kwao ni kiangazi sasa hivi. Wanazika.
Australia kwao ni kiangazi pia wanazika.
Huu ugonjwa ni mpya tabia yake haifahamiki.
Wakifika wagonjwa 250, hesabu siku kumi baadaye kutakuwa na wagonjwa 5000 (late of exponentially growth). Nchi yoyote ambazo zilipunguza mizunguko ya watu kabla ya wagonjwa 50 hawajaumwa ndo aina idadi chache za wagonjwa.
Mafundi seremala huu msimu wenu wa kuvuna.
Tutazika wengi.


Sent using Jamii Forums mobile app
South Africa IPO kwenye tropic ya cancer kama Tanzania but eneo lake limeathiriwa na makutano ya bahari na kutengeneza baridi Kali pale port Elizabeth ,unajifanya mjanja kumbe hujui chochote
 
South Africa IPO kwenye tropic ya cancer kama Tanzania but eneo lake limeathiriwa na makutano ya bahari na kutengeneza baridi Kali pale port Elizabeth ,unajifanya mjanja kumbe hujui chochote
kwa Hiyo korona inapiga Port Elizabeth huko kwingine mambo shwari?
 
Namba zetu za maambukizi na vifo hadi sasa vinaelekea kuwa tofauti na zile za wenzetu walioko kwenye nchi za baridi.
Ushahidi unaanza kupatikana sasa kueleza tofauti hizi kati ya nchi zetu na za hawa wengine.

Ingawa pamekuwepo na dhana ya kuhusisha joto, unyevunyevu na mwanga katika kupungua kwa kasi ya maenezi ya coronavirus, dhana hii bado ilikuwa haijapata ushahidi wa kimaabara kuhusisha hali hizo na kupunguza kasi ya kuenea kwa coronavirus.

Sasa uchunguzi huo umefanyika na inabainishwa wazi kwamba corona anadhurika haraka anapokutana na mazingira hayo ya joto, mwanga na unyevunyevu.

Huu utakuwa ni ushahidi wa kujitosheleza kuhusu bahati yetu ya kutokuwa na kasi ya maambukizi kama ile tuliyoiona Italy, Uingereza, USA na kwingineko.

Corona anadhurika haraka, kwa hiyo maambukizi yanapungua. Hii haina maana kwamba maambukizi hayatakuwepo kabisa. Maambukizi yatakuwepo kama haya tuliyokwishayashuhudia, lakini kasi yake haitafikia ile inayoonekana kwenye nchi za baridi.

Maana ya utafiti huo ni kwamba, sisi tukiongeza juhudi ya kuongeza kuzuia maambukizi, kama kunawa mikono, barakoa na kutokaribiana zaidi, nafasi yetu ya kuzuia maambukizi na vifo inaweza kuwa kubwa zaidi.

Hii ina maana, Mungu, alishasikiliza sala zetu kuhusu ugonjwa huu, ndiyo maana katuweka hapa tulipo.
Tuzidi kusali/kuswali.

Najua utataka nikupe source ya utafiti huo. Vuta subira. Kwa sasa nikupe tu kwamba tafiti za aina hii zinaendelea India, USA na kwingineko.

Hata sisi hapa tungeweza kufanya; aaah, acha tupige siasa kwanza. Kwa sababu siasa inalipa!
Weka source basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maelezo yako yana mashaka makubwa. Kuna nchi kama Ufilipino ambako kuna joto kali kuliko hapa kwetu lakini maambukizi yako juu. Tatizo la msingi ni kwamba hatupimi watu wengi kwa hiyo hatujui ukubwa wa tatizo. Na hii si kwa Tanzania tu, nchi nyingi za Afrika zinapima idadi ndogo sana ya watu, tena wale wanaojipeleka wenyewe hospitalini au wale waliowekwa karantini. Kumbuka asilimia kubwa ya watu wenye maambukizi hawaoneshi dalili yoyote
Kuna suala la watu weupe kuathiriwa pakubwa na magonjwa ya mafua, tangu enzi za ukoloni na utumwa watu weuoe walidondoshwa kwa wingi sana na mafua aina ya Influenza, wacha watafiti watupe majibu.
 
Hawa hawa wanaosema tunahitaji lockdown ndio watakaokuja kusema “kama mataifa makubwa lockdown imewashinda sisi ni nani Tanzania tuiweze, lockdown inaua watu wengi kuliko Corona”.

Na wale wale wasioihitaji, ipo siku watabadilika na kusema “kipindi cha nyuma Rais alikua na nafasi nzuri ya kuweka lockdown na ikaleta manufaa ona sasa watu wanavyo angamia”.

SOMO: Binadamu.

Mimi naona lockdown ni bora kwa kupunguza maambukizi lakini wengine walioiona lockdowns wameanza kukasirika na kuvunja utaratibu
Njaa kitu kingine Mkuu
USA na kila kitu wameanza kutoka kwa maelfu nje tena wamebeba na bunduki kabisa kujihami na jeshi
Adjustments.jpg



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
kwanza hongera kwa kujiunga ktk nchi ya kusadikika, pili japo liko nje y mada husika ila ningependa nikujibu kwa uelewa wangu tofauti ya kusali na kuswali, (kwa uelewa wangu) KUSALI na KUSWALI ni maneno mawili tofauti hila yana maana moja, yani yote yanamaanisha KUABUDU MUNGU na tofauti yake ni spellings na jamii ya wanayoyatumia yani KUSALI ni neno linalotumiwa na Wakristo likimaanisha kuabudu (kumuomba mungu) na KUSWALI ni neno linalotumiwa na Waislam pia likimaanisha kuabudu. hivyo ndivyo nijuavyo mimi. mwisho hongera na pole sana kwa uku ulipokuja na usisahau kuchuku tafadhali ya corona

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwahiyo hapa walengwa ni waKristo [kusali] na waIslam [kuwali] . Je sisi tunaoabudu miti na mawe makubwa makubwa hata yale Mheshimiwa fulani aliandika yeye ndio Rais mbona tumetengwa ?.Bora niurejee uraia wangu wa zamani kama huku kwenu mnadharau dini zetu za mabab tangu enzi na enzi.
 
South Africa IPO kwenye tropic ya cancer kama Tanzania but eneo lake limeathiriwa na makutano ya bahari na kutengeneza baridi Kali pale port Elizabeth ,unajifanya mjanja kumbe hujui chochote

Rudia ‘geography’ yako vizuri.South Africa ipo kwenye Tropic ya Capricorn na siyo cancer
 
Ulichoandika siyo kweli.
South Africa kwao ni kiangazi sasa hivi. Wanazika.
Australia kwao ni kiangazi pia wanazika.
Huu ugonjwa ni mpya tabia yake haifahamiki.
Wakifika wagonjwa 250, hesabu siku kumi baadaye kutakuwa na wagonjwa 5000 (late of exponentially growth). Nchi yoyote ambazo zilipunguza mizunguko ya watu kabla ya wagonjwa 50 hawajaumwa ndo aina idadi chache za wagonjwa.
Mafundi seremala huu msimu wenu wa kuvuna.
Tutazika wengi.


Sent using Jamii Forums mobile app
South Africa wanazika??.wamezika wangapi out of 2000 ambao wako positive?
 
Ulichoandika siyo kweli.
South Africa kwao ni kiangazi sasa hivi. Wanazika.
Australia kwao ni kiangazi pia wanazika.
Huu ugonjwa ni mpya tabia yake haifahamiki.
Wakifika wagonjwa 250, hesabu siku kumi baadaye kutakuwa na wagonjwa 5000 (late of exponentially growth). Nchi yoyote ambazo zilipunguza mizunguko ya watu kabla ya wagonjwa 50 hawajaumwa ndo aina idadi chache za wagonjwa.
Mafundi seremala huu msimu wenu wa kuvuna.
Tutazika wengi.


Sent using Jamii Forums mobile app
Naamini tz wagonjwa wa Corona Ni wengi Sana hata 500 wanafika.

Sema hatupimi na tunazidi kuambukizana. Na lockdown imechelewa tumeshaambukizana vya kutosha.
 
Back
Top Bottom