Bajeti 2021/22: Wadau tunakataa kodi ya Majengo kulipwa kwa LUKU

Bajeti 2021/22: Wadau tunakataa kodi ya Majengo kulipwa kwa LUKU

Kitendo cha Waziri wa Fedha kupendekeza kodi ya majengo ikatwe kwenye manunuzi ya umeme kinapaswa kufafanuliwa vizuri ili wananchi waelewe vizuri.

Hii ni kwa sababu nyumba nyingi zina wapangaji na ambao ndio walipaji wa bili ya umeme kwa vile wao ndio wanaoutumia, ziko nyumba ambazo wenye nyumba hawamo kabisa, wanaokaa humo ni wapangaji tu, wanawezaje kulipishwa kodi ya jengo kupitia ununuzi wa umeme huku wakiwa si wenye nyumba?

Hata kama hela hiyo itakatwa kidogo kwa mtindo wa kudunduliza, lakini haipaswi kulipwa na wapangaji .

Hili lifafanuliwe au lifutwe tuweke utaratibu mwingine utakaowalipisha kodi ya majengo wahusika tu.
Kwani mwenye nyumba anapangisha kwa hasara. No wazi hela anayolipwa na mpangaji ndio hiyo hiyo anaenda kulipia hiyo kodi ya nyumba
 
Naamini litafanyiwa kazi. Hata pesa za mabango ziondolewe huko serikali kuu.
Sawa kabisa, na maeneo mengine madogo madogo ya kikodi. Nadhani itakuwa jambo mzuri kama Serikali Kuu ikaheshimu mamlaka ya Serikali za Mitaa. Ile mipaka ya kimamlaka kati yao ziheshimiwe na zifuatwe.
 
Kwani mwenye nyumba anapangisha kwa hasara. No wazi hela anayolipwa na mpangaji ndio hiyo hiyo anaenda kulipia hiyo kodi ya nyumba
basi alipe mwenyewe kama siku zote
 
Kitendo cha Waziri wa Fedha kupendekeza kodi ya majengo ikatwe kwenye manunuzi ya umeme kinapaswa kufafanuliwa vizuri ili wananchi waelewe vizuri.

Hii ni kwa sababu nyumba nyingi zina wapangaji na ambao ndio walipaji wa bili ya umeme kwa vile wao ndio wanaoutumia, ziko nyumba ambazo wenye nyumba hawamo kabisa, wanaokaa humo ni wapangaji tu, wanawezaje kulipishwa kodi ya jengo kupitia ununuzi wa umeme huku wakiwa si wenye nyumba?

Hata kama hela hiyo itakatwa kidogo kwa mtindo wa kudunduliza, lakini haipaswi kulipwa na wapangaji .

Hili lifafanuliwe au lifutwe tuweke utaratibu mwingine utakaowalipisha kodi ya majengo wahusika tu.
Wanaopanga bajeti ndio wale wanaomiliki mijengo zaidi ya ishirini na wanapangisha, wao wameamua kijichomoa kwenye kulipia mijengo yao na kuwabambikizia wapangaji wao wawalipie huku wao wakikusanya kodi! Hawa wanampima mama kwa kutumia matete na watafanikiwa dhidi ya tusiokuwa na nyumba ila tunalipishwa kodi ya nyumba hewa! CCM hoyee, BUNGE la CHAMA KIMOJA hoyeeee, hoyee.
 
Sawa kabisa, na maeneo mengine madogo madogo ya kikodi. Nadhani itakuwa jambo mzuri kama Serikali Kuu ikaheshimu mamlaka ya Serikali za Mitaa. Ile mipaka ya kimamlaka kati yao ziheshimiwe na zifuatwe.
Itaongeza mzunguko wa fedha pia. Kuna tenda si lazima malipo yatoke serikali kuu.
 
basi alipe mwenyewe kama siku zote
Kwani hulipi luku , haufaidiki na hilo jengo , sema mwenye nyumba apunguze kodi ya nyumba, ili hela ya property tax aliokuwa atanipatia kwenye rent aipate sehemu moja ya kwenye luku
 
Mimi nimeipenda hiibya kodi kulipwa kwenye LUKU.

Hapo kama wewe ni mpangaji unarekebishwa mkataba unamkata mwenye nyumba. Shida ni ukivunja mkataba, unakosa kila kitu.
 
Tulipe kodi kwa maendekeo ya nchi letu pendwa aje nani kuijenga donors ? Beberu nooooo tujenge wenyewe
 
Kwa hiyo mpangaji ni Dalali.
Regulation za rent zitajiset automatically accordingly to economy....
Luku moja ni nyumba moja by approximate.
EXELLENT IDEA...!
Yaani nahisi akili hii imetoka kwa mzee baba R.I.P kwani halmashauri walishindwa,TRA walishindwa mnaenda majumbani watu hawapo.,watendaji wa mitaa hawana hata pikipiki za kupita nyumba kwa nyumba kutoa invoice.mwisho wa siku walipaji ni wale wale.
Hao wanaojiita sijui wapangaji wataelewana na mwenye nyumba,kama atalipia huo umeme wa elfu kumi kwa mwaka ,au mtakatana kwenye kodi ni maelewano yenu.sisi tunachotaka fedha zikusanywe na zitumike kuhudumia umma.

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
NAKUPONGEZA MWIGULU LAMEKI NCHEMBA UMEFANYA JAMBO ZURI MNO,SASA PROPERTY TAX ITAPATIKANA VIZURI MNO BY MASS PAYMENTS.
HONGERA SANA.
HILI LINAFANANA NA LILE LA MOTOR VEHICLE.
Kwani motor vehicle imerudishwa?
Natamani irudishwe ili bajaji zipungue barabarani.zimekuwa kero mpaka hiace zinakimbia ruti.

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Kitendo cha Waziri wa Fedha kupendekeza kodi ya majengo ikatwe kwenye manunuzi ya umeme kinapaswa kufafanuliwa vizuri ili wananchi waelewe vizuri.

Hii ni kwa sababu nyumba nyingi zina wapangaji na ambao ndio walipaji wa bili ya umeme kwa vile wao ndio wanaoutumia, ziko nyumba ambazo wenye nyumba hawamo kabisa, wanaokaa humo ni wapangaji tu, wanawezaje kulipishwa kodi ya jengo kupitia ununuzi wa umeme huku wakiwa si wenye nyumba?

Hata kama hela hiyo itakatwa kidogo kwa mtindo wa kudunduliza, lakini haipaswi kulipwa na wapangaji .

Hili lifafanuliwe au lifutwe tuweke utaratibu mwingine utakaowalipisha kodi ya majengo wahusika tu.
Sijui ndio mmesomea kupinga kila kitu.

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Wanaopanga bajeti ndio wale wanaomiliki mijengo zaidi ya ishirini na wanapangisha, wao wameamua kijichomoa kwenye kulipia mijengo yao na kuwabambikizia wapangaji wao wawalipie huku wao wakikusanya kodi! Hawa wanampima mama kwa kutumia matete na watafanikiwa dhidi ya tusiokuwa na nyumba ila tunalipishwa kodi ya nyumba hewa! CCM hoyee, BUNGE la CHAMA KIMOJA hoyeeee, hoyee.
Ishu ya indirect taxation ikishika kasi hata gharama Fulani za serekali zitapungua,hata BAADHI ya matamko hatutayasikia tena.
 
Mbona kodi yenyewe ni ndogo sana...Buku tu kwa mwezi or elfu 12 kwa mwaka hii nayo tutoe mishipa kuijadili humu?
Km nyumba ina wapangaji wa 5 hio ni 200 kwa mpangaji, hii kweli nalo la kujadili kweli...mpangaji analipa kodi ya 50k-150k anashindwaje kuchangia 200 km kodi ya Jengo.
Kuna watu tunakatwa 30% PAYE na kuna watu wanakatwa 8% na kuna watu hawakatwi kabisa, hili ndo tuliongelee ila sio issue ndogo ndogo km hizi unless tumekosa kazi za kufanya.
Na km tuna taka ku protest kuhusu hii kodi then tuanze na ushuru wa magari ulioingizwa kwenye mafuta unaowafanya ht wasio na magari waulipie, mtu unanunua petrol ya jenereta unalipia na ushuru wa magari.

Watanzania tupende kulipa kodi...kuna mchangiaji hapo juu kazungumzia kushuka kwa gharama za kuunganishiwa umeme kutoka 300k mpaka 27k, haya ni mapato yamepungua ila hamlalamiki, ila buku tu kwa mwezi tunatoka mapovu...tunataka maendeleo ila hatutaki kuyachangia, then serikali ikikopa kufidia nakisi napo tunalalamika deni la taifa...kila kitu kwetu ni lawama, hatuna jema.
Hakuna cha 200 hapo, vipi kama wapangaji hao watano kila mmoja anatumia LUKU yake! kama kodi ya jengo inatozwa kwenye kila LUKU vipi yale majengo yanayotumia zaidi ya LUKU moja, naomba jibu ndugu mdadavuzi....
 
Katika madudu ya hii Bajeti sidhani kama hili ni tatizo, wapangaji wana mkataba kwahio katika mkataba wao watadeduct hilo ongezeko katika mkataba wao....

Issue ni hizi kodi zisiongezeke maradufu au wasinogewe kila kitu wakaweka kwenye luku....
au iwe hiv.kama kod laki mbili kwa mwez unampa mwwnye nyumba raki na themanain.180. ile 20 utaifidia kwenye property tax

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kuna kitu kimenifurahisha ni hii namna mpya ya kulipia kodi kupitia Luku. Kuna baadhi ya wapangaji wamechikichia fedha za wenye nyumba waliowatumia ili walipe kodi hiyo. Ubunifu huu ni wa kupongezwa sana. Rejea sheria inasema u
Inatakiwa kulipwa na mwenye nyumba au anaeitumia. Wapangaji kuweni wapole anayeona anaonewa ajenge nyumba yake tuone kama hatailipa .
Umefunga mjadala
 
Hakuna cha 200 hapo, vipi kama wapangaji hao watano kila mmoja anatumia LUKU yake! kama kodi ya jengo inatozwa kwenye kila LUKU vipi yale majengo yanayotumia zaidi ya LUKU moja, naomba jibu ndugu mdadavuzi....
Tanesco hawakubali kuweka mita zaidi ya moja kwenye nyumba moja unless ni apartments zinazojitegemea or umefanya mchongo, na km umeweza kupata pesa ya kuhonga tanesco wakuekee mita ya ziada then sio mbaya kuichangia serikali io buku kwa mwezi.
Kuna watu wanakatwa PAYE 30% zaidi ya milioni na kuna watu wanalipa 8% less than 30k km PAYE na kuna watu hawalipi kabisa PAYE ila wote hawa wanatumia miundo mbinu sawa sawa. Sio issue kuchangia buku kwa mwezi.
 
Tanesco hawakubali kuweka mita zaidi ya moja kwenye nyumba moja unless ni apartments zinazojitegemea or umefanya mchongo, na km umeweza kupata pesa ya kuhonga tanesco wakuekee mita ya ziada then sio mbaya kuichangia serikali io buku kwa mwezi.
Kuna watu wanakatwa PAYE 30% zaidi ya milioni na kuna watu wanalipa 8% less than 30k km PAYE na kuna watu hawalipi kabisa PAYE ila wote hawa wanatumia miundo mbinu sawa sawa. Sio issue kuchangia buku kwa mwezi.
Sina taarifa kwamba kuna watu hawalipi PAYE, unaweza kunifahamisha ni wapi hao....na kwa nini mishahara yao haikatwi kodi? na kwa nini hao wengine walipe 8%...
 
Back
Top Bottom