Bajeti 2021/22: Wadau tunakataa kodi ya Majengo kulipwa kwa LUKU

Bajeti 2021/22: Wadau tunakataa kodi ya Majengo kulipwa kwa LUKU

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Kitendo cha Waziri wa Fedha kupendekeza kodi ya majengo ikatwe kwenye manunuzi ya umeme kinapaswa kufafanuliwa vizuri ili wananchi waelewe vizuri.

Hii ni kwa sababu nyumba nyingi zina wapangaji na ambao ndio walipaji wa bili ya umeme kwa vile wao ndio wanaoutumia, ziko nyumba ambazo wenye nyumba hawamo kabisa, wanaokaa humo ni wapangaji tu, wanawezaje kulipishwa kodi ya jengo kupitia ununuzi wa umeme huku wakiwa si wenye nyumba?

Hata kama hela hiyo itakatwa kidogo kwa mtindo wa kudunduliza, lakini haipaswi kulipwa na wapangaji .

Hili lifafanuliwe au lifutwe tuweke utaratibu mwingine utakaowalipisha kodi ya majengo wahusika tu.
 
Kuna wakati unajiuliza hivi hawa tunaita wasomi wa uchumi wanajua uchumi wa wananchi wao kweli au wanajua kuwa wote wamejenga na wana uhakika wa kula Milo mitatu kama wao...
Nadhani Mwigulu anaamini kila Mtanzania anaishi kwenye nyumba yake kutokana na porojo za uchumi wa kati
 
Nadhani Mwigulu anaamini kila Mtanzania anaishi kwenye nyumba yake kutokana na porojo za uchumi wa kati
Yaani naona kabisa bajeti alizo kuja nazo ni mzigo kwa wanachi kuanzia Hili LA kodi ya jengo ukija LA. Laini za simu unaona kabisa huyu ni mzigo kwa watanzania ambao ni walala hoi.

Jiulize mtu amesaidiwa umeme wa LEA na wajukuu huko kijijini Leo unampa mzigo wa kulipi nyumba ambayo hata hadhi ya kuwekewa umeme ilikuwa haina.

Mungu atupe uvumilivu na hili maana naona mpango alifanya vitu ambayo vilikuwa haviendani na watanzania ila huyu kafanya ambavyo havipo kabisa Tanzania.
 
Katika madudu ya hii Bajeti sidhani kama hili ni tatizo, wapangaji wana mkataba kwahio katika mkataba wao watadeduct hilo ongezeko katika mkataba wao....

Issue ni hizi kodi zisiongezeke maradufu au wasinogewe kila kitu wakaweka kwenye luku....
 
Katika madudu ya hii Bajeti sidhani kama hili ni tatizo, wapangaji wana mkataba kwahio katika mkataba wao watadeduct hilo ongezeko katika mkataba wao....

Issue ni hizi kodi zisiongezeke maradufu au wasinogewe kila kitu wakaweka kwenye luku....
hivi unazijua nyumba za kupanga linapofika suala la kununua umeme ?
 
hivi unazijua nyumba za kupanga linapofika suala la kununua umeme ?
Let's say kodi ya jengo ni 10,000/= kwahio ni around 833 /= kwa mwezi (itakuwa bora ipigwe kwa mwezi since mtu anaweza kuhama wakati wowote)... hivyo basi kama kuna wapangaji kumi hio ni around 83.3/= inaweza ikaongeleka baina ya mpangaji na mwenye nyumba ikafanyika hio deduction kwenye rent.

Pia lazima ujue Serikali hizi za Bin Adamu lengo lao ni kukusanya tu na wamekusanyaje hayo ni matokeo... (binafsi naona kwenye mafuta, vocha na miamala ndio wamefanya madudu).
 
... siku zote mlipa kodi ni mlaji wa mwisho! Mwenye nyumba mzigo wa kodi mwisho wa siku ataushusha kwa wapangaji tu! Kwangu, hili la kulipia kodi ya pango kupitia Luku angalau lina ubunifu badala ya kuweka "task force" zikimbizane na wenye nyumba vichochoroni angalau automatically watu watalipa kodi za majengo.
 
Sasa itakuaje kwa nyumba zisizo na umeme ama choose zenye umeme
... hizo ni chache. Hata hivyo lengo la serikali kupeleka umeme hadi vijijini (REA) tena kwa bei nafuu (27,000/=) sio bure; n ili jitihada hizo zitumike kwa faida kama hivi kuongeza wigo wa kodi. Faida ya kutumia njia hii kukusanya kodi za majengo ni kubwa kuliko kutumia njia nyingine.
 
Bajeti iko poa sana. Vitu vingi vimeshuka kodi au kusamehewa kabisa. Ilikuwa ngumu na gharama kubwa kukusanya kodi za majengo (TRA WANAJUA HILO) Mtu atoke sinza aende KINONDONI KULIPA ELFU KUMI AU 50000 KWA MWAKA? bora waingize huko ambapo hakutakuwa na ukwepaji wa hiyo KODI.
TUWE WAZALENDO, SISI KILA KITU TUNALALAMIKA KAMA WAPUMBAVU HIVI.
 
Back
Top Bottom