Bakwata uislaam huo mmeutoa wapi? Kumbukeni moto ni mkali sana mtaenda chomwa

Bakwata uislaam huo mmeutoa wapi? Kumbukeni moto ni mkali sana mtaenda chomwa

Wewe ndiye unaona hana sehemu nyingine ya kulalamikia ila hapa.

Je unauhakika kuwa hao wahusika wapo humu? na kama unauhakika kwa nini asiwa PM ili ujumbe uwafikie.

Nauliza tena kunafaida gani ya yeye kutuambia haya aliyosema, zaidi ya kutufanya kuzidi kuwaona wapigaji?

Hebu soma comments za wadau ujionee.
Mkuu,,,hivi watu wote waliopo humu unawajuwa kwa majina halisi na shughuli zao? pamoja na hayo ,,wapo watu sio members na wana uwezo wa kusoma,,,kinacholetwa humu,, pia kama hujuwi fuatilia nyuzi nyingi za kero zinazoletwa humu,,baadae ya muda zinafanyiwa kazi na wahusika ,,na watu wanaleta marejesho,,,,,hivi mkuu unajuwa kwann members wengi wa humu wapo nyuma ya keyboard?na kuficha I'd zao?ni sababu mtandao huu unasomwa na known na unknown people,,,, je unajuwa Mimi nine chat na wewe ni nani?na nashughulika na nn? wewe. Usihangaike na hizo comments za member kum dis huyo jamaa mleta Uzi,, kuna watu wapo kazini,,,wata mdis lakini vitafanyiwa kazi,,amini maneno yangu,,,,
 
Mkuu umejinasibisha kwamba huna mihemko wala huendeshwi kwa mihemko ila hoja yako haishabihiani na Hilo.

Inaonekana kulalamikia ada ya kupokelewa shauri. Umewahi kujiuliza BAKWATA KATA wanaendesha ofisi kwa fungu lipi? Je kuna hesabu gani nyuma ya hiyo ada (deligation, mwendo wa kutoka ofisi za kata nk.,).

Kadhi anaendesha ofisi kwa mfuko upi? Analipwa mshahara na nani? Deligation inayoamua kesi hiyo Ina watu wangapi? Nk.

Hatuhalalishi wala kutete tozo, bali kila jambo huamuliwa kulingana na wakati na nyakati husika na kwa vigezo vile vile.

Mwanamke;
Anatoa wapi shilingi elfu 15,000 au 30,000? Nikidhani unazungumzia kwamba ananyanyaswa kingono katika HARAKATI za kuipata haki yake au anazungushwa kwa uamuzi usiosahihi na nk.

Hivi huyu mwanamke ambaye unadhani anahitaji talaka 45,000 inaweza kuwa kikwazo cha kutimiza ombi lake?

Unajua shauri likifika kule gharama ambazo mwanamke anatakiwa aziingie kisheria kuipata hiyo talaka (anatakiwa kurudisha mahari), je Kama aliolewa kwa 200,000/- unadhani atakuwa na uwezo wa kutafuta 200,000/ alafu akose 45,000/?

Usikubali kuwa mjinga kwa hiari.
 
Nauliza hivyo ni kwa sababu Uislam unatutaka tujiepushe na baadhi ya dhana, kwani baadhi ya dhana ni dhambi.

Kwa sababu dhana ikiwa ni si ya kweli ni kuwa umemzushia mhusika uongo. Ni hatari vilevile kwa kuwa itakuwa imejengeka kwenye matamanio ya nafsi.

Waislam tunaifahamu Bakwata jinsi ilivyo! Lakini yanayosemwa haya ni ya kweli kuhusu Bakwata? Au ni utaratibu wa waliyomo ndani ya Bakwata?


Hilo swali ungemuuliza mleta mada kwamba anao ushahidi wa hicho alichokisema??, baada ya majibu yake ndipo tutaenda mbele zaidi kujua je sheria za kiislamu zinaruhusu jambo hilo nk.
 
Wewe ndiye unaona hana sehemu nyingine ya kulalamikia ila hapa.

Je unauhakika kuwa hao wahusika wapo humu? na kama unauhakika kwa nini asiwa PM ili ujumbe uwafikie.

Nauliza tena kunafaida gani ya yeye kutuambia haya aliyosema, zaidi ya kutufanya kuzidi kuwaona wapigaji?

Hebu soma comments za wadau ujionee.

Wewe ni mgeni wa JF inaonekana hujui nguvu ya JF au yawezekana wewe ni muhusika mmoja wapo huko Bakwata, wewe unafkiri yeye ataenda kusemea wapi?vyombo kibao vinasemwa kupitia JF na vinajirekebisha.
 
Naunga mkono aliyo yaandika mtoa mada, na hapa ngoja niseme machache kuhusu suala la "Kadhi". Katika soma soma yangu na kufatilia mambo ya dini, katika Uislamu hakuna sampuli ya majukumu ya kadhi kama yalivyo katika hizi mahakama za kadhi na sisi tulishawahi kuwashauri hata hizo mahakama za kadhi zisiwepo sababu kuwepo kwake tu kunaenda kinyume na Uislamu.

Na haya tunayo yaona ni matokeo ya wahusika kuuacha Uislamu.
 
Wewe ni mgeni wa JF inaonekana hujui nguvu ya JF au yawezekana wewe ni muhusika mmoja wapo huko Bakwata, wewe unafkiri yeye ataenda kusemea wapi?vyombo kibao vinasemwa kupitia JF na vinajirekebisha.
Kwa mfano wewe ukiwa ni kiongozi, utakapokuwa umekosea ungependa raia wako wakukosoe kwa namna gani.

Wasimame tu barabarani na kuanza kupayuka, kwa kuwa wanajua utasikia ilhali wanakuvunjia heshima, au wakufuate faragha na kukueleza makosa yako?

Tatizo sio kuwasema tatizo pahali gani anapowasemea.
 
TANBIHI: Mods naomba uzi huu msiufute na mkiuhamisha basi nifahamisheni mmehamishia wapi?

Nayaandika haya nikiwa na uchungu mkubwa rohoni mwangu. .. Nikiangalia wale walio pewa mamlaka ya usimamizi wa sheria ya Allah wanafanya mambo mazito ya kumuasi Allah na kudhulumu watu...

Kwanza nibainishe MIMI SIO MTU WA KUENDESHWA NA MIHEMKO YA KIHARAKATI... SINA CHUKI JUU YA BAKWATA NA NAWAHESHIMU SANA KWA SABABU NDIO CHOMBO TEGEMEWA CHA KUWASEMEA WAISLAAM NCHINI NA KUISIMAMISHA SHERIA YA ALLAH. .. LAZIMA TUKITII NA TUKIHESHIMU BILA SHAKA. .. NA NAKITII NA KUKIHESHIMU CHOMBO HIKI. ..

Bakwata Mashaa Allah, Allah amejaalia lwa serikali hii kuruhusu WAISLAAM kujihukumia mambo yao msingi ya kijamii yenyewe na MIFUMO YA KIDOLA ikazitambua na kuzirasimisha sheria hizo(NDOA, TALAKA NA MIRATHI). . . NA HUKUMU ITAKAYOTOLEWA NA BAKWATA KWENYE MASUALA HAYO MAHAKAMA ZA NCHI HAZIWEZI INGILIA.. .

TUMSHUKURU ALLAH KWA HILO.. . Ni jambo mlilolipigania kwa muda mrefu kupata mahakama ya Qadhi, ili waislaam tujihukumie mambo yetu wenyewe bila kuingiliwa kwenye ibada hizo. ..

Kumbe bhanaa wenzetu BAKWATA na BAADHI viongozi Wake waliliangalia kwa jicho la kimaslahi(LA KIUPIGAJI) . .. MCHENI ALLAH NYIE WATU.. . ADHABU YA ALLAH NI CHUNGU. ..HAMTOOKOKA NA VIREMBA VYENU WALA VYETI VYENU VYA THANAWY MLIVYOVIPATIA TANGA...

Mathalani. .. KWENYE MASUALA YA NDOA. .. SIKU ZOTE UKIONA SUALA HILO LIMEFIKA KWA QADHI UJUE MLETAJI NI MWANAMKE(MKE). ..

Kwa sababu Kisheria MWANAUME hapati shida amepewa Mamlaka, YAKIMKERA ANAACHA TU(TALAKA). ..

Ila mwanamke hana uwezo wa kutoa Talaka, Suluhisho lake ni kwa Qadhi...

Na kwa mfumo wenu wa uendeshaji QADHI MMEMUWEKA KUANZIA WILAYA kisha MKOA kisha TAIFA. ..

LAKINI wa kumpata huyo QADHI sasa ndio unaleta ukakasi. ..

Binti akiwa na tatizo kwenye ndoa yake na Mumewe anabidi aanzie shauri lake BAKWATA KATA ili lifike kwa QADHI WA WILAYA. ..

Huko KATA sasa ETI BINTI MASKINI ANATOZWA KUANZIA SH. 15,000/- Ili tu shauri lake lifunguliwe na lisikilizwe. ..

Tujue kabisa OFISI YA BAKWATA KATA HAINA MAMLAKA YA KUSIKILIZA NA KUIAMUA KESI ILI WATAPOTEZA TU MUDA WAKO ILA MWISHO WA SIKU UTAPEWA BARUA UENDE BAKWATA WILAYANI. ..

Ukifika BAKWATA WILAYA kabla hawajakusikiliza lolote... NENDA KADEPOSIT SH. 30,000/-...

ILA KUMBUKA MWENYE MAMLAKA YA KUSIKILIZA NA KUAMUA NI QADHI NA SI BAKWATA(Si sheikh wa wilaya wala katibu wake). . . Ila hela yako wanaitaka...

Kwahiyo mwisho wa siku lazima upelekwe kwa Qadhi. ..

Sijajua na hadi kufika huko kwa Qadhi nako inabidi utoe kiasi gani!

KINACHONIUMA ROHO SIO HELA WANAYOIPIGA. ..

Ila ni HUYU MWANAMKE aliyepeleka Kesi huko. .. KUMBUKA KISHERIA YA KIISLAAM MWANAMKE ANATAKIWA AKAE NYUMBANI NA WATOTO ALEE FAMILIA NA AMTII MUMEWE TU. .. Suala ya kufanya kazi limeruhusiwa kwa mwanamke ila INATILIWA NGUVU ZAIDI ASIFANYE KAZI. ..

ANAYEMHUDUMIA MWANAMKE NI MUMEWE. ..

SASA FIKIRIA Mwanamke amegombana na Mumewe anayemhudumia. .. Ikafikia hatua anahitaji msaada kutoka kwenu BAKWATA. .. LAKINI NINYI MNAMCHAJI OVER SHS. 45,000/- ILI APATE HUDUMA NA MSAADA WENU ILI APATE HAKI YAKE. ..

Sasa hiyo hela anaitoa wapi MDHAIFU HUYU. ..? BADALA YA KUMSAIDIA KUMPA HAKI YAKE MNAMUONGEZEA MATATIZO?

UISLAAM WENU MMEUTOA KWA SHEITWAANI GANI?

MBONA HATA HAMUMUOGOPI ALLAH... HIVI HATA MTUME ANGEKUWA ANAFANYA HUU UPUMBAVU WENU. .. HUU UISLAAM USINGEFIKA HAPA ULIPO. ..

MTUME AMESEMA "ZICHENGUENI HAKI ZA MADHAIFU WAWILI HAWA, NAO NI WANAWAKE NA MAYATIMA".

Lakini ninyi mnashiriki kuwakandamiza. ..

Mcheni Allah ndugu zangu. ..

MTAFANYA WAUKIMBIE UISLAAM NA WAULALAMIKIE UISLAAM KWA TAMAA ZENU ZA MAISHA YA DUNIA YASIYO CHOCHOTE. ..

MNATUPELEKA WAPI NYIE WATU MSIOMUOGOPA ALLAH. ..

MNA TOFAUTI GANI NA WAPIGA DILI WA RICHMOND NA WALA RUSHWA. ..

NYINYI MTACHOMWA KWA KUDHULUMU MALI ZA WATU KWA KUZILA PASIPO HAKI. ..

KAMA MLITAKA KIPATO MNGEKUWA NA SUBRA MKAMSIKILIZA HUYO DHAIFU ALAFU MWISHO MTWANGENI HIZO GHARAMA MWANAUME. .. ILA MWANAMKE MNAMUONEA ANAZIPATA WAPI?

AKIWA HANA MAANA YAKE AKAENDELEE KUMUASI ALLAH KWA ZINAA KWA MLOLONGO WENU KWA KUDHULUMU WATU. ..

mwisho:
NITOE TANBIHI NYINGINE... UISLAAM NA SHERIA ZAKE HAZINA SHIDA KABISA WALA HAZINA KASORO.. .

NA UKIZIFUATA NA ZIKASIMAMISHWA VIZURI KWA UADILIFU UTAUPENDA NA KUUFURAHIA UISLAAM. .. UTA ENJOY NA KUJIVUNIA KUWA MUISLAAM.

ILA HAWA WAPIGA DILI HAWA NDIO WANAOUCHAFUA UISLAAM...

NIMUOMBE MUFTI.. . BARAZA LAKO UNALOJITAHIDI KULISAFISHA NA KULIRUDISHA KWA UMMA... KUNA WATU WA MASLAHI WANAKUANGUSHA.. . WANALICHAFUA BARAZA KWA TAMAA ZAO ZA MATUMBO... MIJITU IMEJAZA VITAMBI NJAA ZIMEWAJAA HAWANA HOFU YA ALLAH... ADHABU YA ALLAH YAWANGOJA WASIPOTUBU. .. ALLAH AWAONGOZE. ..

NB: MODS TAFADHALI UZI HUU USIFUTWE MUHIMU SANA KWA UMMA...
Mleta mada kwani mahakama ya kadhi iliyokua inapiganiwa imeshapitishwa? Lini?
 
Wewe ndiye unaona hana sehemu nyingine ya kulalamikia ila hapa.

Je unauhakika kuwa hao wahusika wapo humu? na kama unauhakika kwa nini asiwa PM ili ujumbe uwafikie.

Nauliza tena kunafaida gani ya yeye kutuambia haya aliyosema, zaidi ya kutufanya kuzidi kuwaona wapigaji?

Hebu soma comments za wadau ujionee.
Vizuri ni vema ukawekwa uovu wazi ili iwe ni serious case waweze kujirekebisha... Baada ya kugundua umma umewafahamu uovu wao.. .
 
SISI KWENYE UISLAAM MWANAMKE ALIYEACHWA KWA MATATIZO YA MUMEWE ILIBIDI NDIO AANGALIWE NA APEWE SWADAQAH... BADALA YAKE WAO NDIO WANAMTOZA PESA YA LAZIMA. .. TABU JUU YA TABU...
 
Wewe ndiye unaona hana sehemu nyingine ya kulalamikia ila hapa.

Je unauhakika kuwa hao wahusika wapo humu? na kama unauhakika kwa nini asiwa PM ili ujumbe uwafikie.

Nauliza tena kunafaida gani ya yeye kutuambia haya aliyosema, zaidi ya kutufanya kuzidi kuwaona wapigaji?

Hebu soma comments za wadau ujionee.
Vizuri hebu nisaidie kulifikisha hili wewe.. .

WAAMBIE KULE JF KUNA MTU KAKUANDIKENI.. .
 
Back
Top Bottom