Duh! Kama ulikuwa unaamini kuwa lile bifu la wakali
wawili wa Bongo Fleva , Nasibu Abdul Diamond
Platnumz na Ali Saleh Kiba , limekwisha, basi umenoa
baada ya jamaa hao kukutana ukumbini na kuchuniana .
Baadhi ya wasanii wa Bongo fleva wakiwa kwenye
mkutano .
Ishu hiyo ilijiri kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Double Tree
Hilton jijini Dar , juzikati ambapo wasanii mbalimbali
walikutanishwa na kampuni moja ya huduma ya simu
za mkononi ili kuzungumza na wanahabari juu ya
maandalizi ya tamasha .
Waandishi wetu, wakiwa wameingiwa na roho ya
kutaka ubuyu , hatimaye muda wa kuingia Kiba
ukawadia ambapo alitinga na timu yake ya watu
wanne .
Alipofika , Kiba alikaa sehemu ya viti vya kushoto akiwa
bize na mrembo mmoja wakichati kabla ya Diamond
kutimba na timu yake kubwa .
Kama ilivyo ada, macho ya waandishi wetu
yakaelekezwa kwa Diamond huku mapichapicha
yakiendelea kwa ajili ya kutupia kwenye mitandao ya
kijamii .
Kila msanii aliyefika kwenye ukumbi huo alianza kutoa
salamu kwa mtu anayeona anafaa kwake , lakini cha
kushangaza mastaa wawili Kiba na Diamond
walishindwa kupeana hata mikono huku kila mmoja
akiwa ameuchuna na kampani yake .
Hata hivyo , wakati ulipofika wa wasanii kujitambulisha
mbele ya wadau, mastaa hao walitahadharishwa
kwamba atakayeanza au atakayekuwa wa mwisho
kujitambulisha haina maana kwamba yeye ndiye
mkubwa zaidi kistaa .
Katika kujitambusha , Kiba ndiye aliyeanza huku kila
mtu akitamba kufanya vizuri kwenye kila shoo
zitakazofanyika mwaka huu.
Hakuna aliyekuwa tayari kumzungumzia mwenzake .