Kuna wakati Ushabiki wa jambo ukizidi huleta upofu wa kufikiri na kudadavua mambo. Hao Wachezaji wa Yanga wangekua na Uwezo Uwanjani Yanga ingekua inacheza Champions League lkn kwakuwa ni Magarasa yanayobebwa na Mipango ya Nje ya Uwanja yapo Loosers Cup.
Tumia akili ya Mpira kufikiri, huwez Mlinganisha Inonga na Job au Mwamnyeto kwa kifupi pale Yanga hakuna beki wa kumweka Inonga kwenye mbao ndefu. Baleke na Mayele ni 50/50 time will tell
Punguza ushabiki akili zinakupungua!
Inonga Hana namba Yanga, Utopolo tuko kikazi zaidi tunahesabu pointi hatuchezi kufurahisha jukwaani kama Inonga kakalia masifa timu yake wanaitoboa tu ukuta mbovu !
Mayele hakuna straika wa kumlinganisha nae angalia jinsi ana kipaji mwaka Jana kakiwasha sana na mwaka huu moto wake ni WA gesi Mpole kakata pumzi! Hao ndondo kina Baleke si level ya Mayele rudisha akili yako kichwani! Mchezaji anastahili kukaa nyuma ya Mayele ni Abdul Sopu wa Azam dogo anajua kutafuta goli na ana kipaji halisi ana mbio ana chenga anapasua ukuta Sasa Eng Hersi sijui hamuoni au? Abdul Sopu ndie mbadala wa Feisal sio Mudathir maana Mudathir ni kiungo mkabaji namba kumi Yanga Iko wazi baada ya Feitoto kutimka na nafasi ni ya Sopu kwa akili zangu za utopoloni! Sipati picha combination ya Mayele, Musonda na Sopu hatoki mtu hata Barcelona wanakaa!!
Yanga Si timu ya kubeza meza hiyo dawa japo ni chungu!
Chukua clip za mechi za Yanga vs Al Hilal Kisha hesabu ni mara ngapi Al Hilal walijiangusha kisha hesabu dakika ngapi zilipotea halafu angalia kujiangusha kwao kuliharibu ladha ya mpira kiasi Gani na kuliwasumbua wachezaji wa Yanga kwa kiasi Gani ule haukuwa mpira be smart.
Yanga haikutolewa na Al Hilal kwa kuzidiwa mpira Bali Al Hilal kucheza mchezo wa kuanguka na Si mchezo wa soka na ndo Maana wametolewa pia na wao! Tulijua kwa dizaini Ile hawafiki popote.
Mwakani tutawafunga midomo Maana Winner Takes All Yani Yanga ni mabingwa Kila kitu ni chetu , mtanyamaza tu Yanga Iko na action tu nyie makelele tu timu hamna! Kombe hamna, Kocha hamna, pesa hamna!!
Tunahitaji kuripoti CAF kuwa kombe la klabu bingwa kuanzia Sasa zicheze timu bingwa tu nchini mwao tuone kama Simba itacheza Maana Simba si bingwa Tanzania , kwani Simba ni bingwa wa nchi Gani? ifikie mahali Makolo fc muone aibu kujitapa sana mko klabu bingwa wakati hata harufu ya kombe la ubingwa Tanzania bara hamuijui!! Kweli mikia wote mbumbumbu!!
Yanga tunakiwasha home and away hata ulete Real Madrid, Brazil , Nigeria, Bulgaria, sijui Denmark au Bayern wakicheza fair , open football kwa Mkapa wanakaa!
Siku hizi "tatu mzuka fc" mmekoma Raja kawakomesha hamsemi Tena kwa Mkapa hatoki mtu!
Acha kubeza timu ambayo huwezi kuifunga tangu Nabi atue Jangwani!