Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Yeah japo mnaponda ila aheri kufanya vitu vinavyoonekana! Hautakuwa na maana leo ila mbeleni utakuja kusaidia watu!

Kwani angetaka hela zile aweke mfukoni au agawane na jamaa zake angeshindwa?
Yaani uwanja wa chato utakuja kuwa na msaada? mko serious kweli? umewauliza wakongo kuhusu uwanja wa Mobutu?

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
 
Hata Marekani wanadaiwa. Hivi mlikuwa wapi kusema wakati Magufuli hajafariki ?Amefariki ndo mnaongea. It's too late. Kwanza serikali ni ile ile far enough aliyekuwa waziri wa fedha ndo makamu wa Rais.
In short wote wameoza.
 
Watu wengine wajinga Sana mkuu anadhani anadanganya watoto tofauti ya Deni hili na Yale anayodhani yalikuwa madogo Ni fedha ilitumika kufanyia Nini, Kuna wakati tulifika mahali tukawa tunakopa ili kulipa mishahara. Kwa ujumla bin adamu Hana shukurani.
Kikwete wanajidai kumkumbuka lakini wawaambia hakuna Rais dhaifu kama kikwete katika nchi hii hata Mama anamzidi! Ni mtu ambaye alikuwa hajui hata anafanya nini?

Ndo maana alipoenda nchi za ulaya wakamuuliza kwa nini nchi yako licha ya kuwa na rasilimali nyingi ni masikini akajibu hata mimi sijui! Huoni huyo alikuwa Rais Mpumbavu sana!
 
Kuna tofauti ya kukopa kwa riba na kutumia fedha zako za mapato yako.

Tofauti ni kwamba mkopo una gharama ya ziada iitwayo riba.

Haikuwa sahihi kuaminisha uma kuwa ni fedha za ndani ilihali ni mikopo. Pale raisi wetu JPM alitupotosha hata tukimtetea kwa nguvu zote ila ukweli ni kuwa katika hili alikosea.

Yeye si Mungu ni binadamu, anafanya makosa. Nadhani Katiba yetu ina udhaifu sana kuruhusu mtu mmoja kuamua mwelekeo wa nchi.
Nakubaliana sana na wewe
 
Tupe na thamani ya miradi iliyotokana na deni, kama uwiano wa deni na uchumi kukua ni 30% huko kutendwa kunatokeaje?

Anzia upanuzi wa bandari, SGR, Upanuzi wa highways, mabarabara ya mitaa, stand za mabasi nchi nzima, New mwendokasi roads, vituo vya afya nchi nzima, Hospitali za wilaya nchi nzima, Mashule, Ndege, upanuzi wa viwanja, ujenzi wa Dodoma plus Ikulu ya Chamino, usambazaji umeme kila kijiji, vivutio vya utalii, Hydropower ya Nyerere na vingine vingi. Ulitegemea hela haitumiki?

Then go back angalia uwiano wa uchumi na ukuaji wa madeni! Njoo kwenye probability means of return. Angalia makusanyo per annual sio kuandika kinafiki.
Mkuu si Kama umemuelewa vizuri ndugu Balile,tatizo siyo miradi mingi ya maendeleo slitoianzisha ndugu MAGUFULI,tatizo ni kutuaminisha kuwa miradi yote inayotekelezwa na awamu ya 5 ni fedha zetu za ndani,hatukopi kwa MABEBERU Tena tutembee kifua mbele sisi Ni Donor cantry,
Hivyo Basi Balile alitaka kujua
Je ndeni la Taifa limefikaje kuwa kubwa kwa kiasi hicho?
 
Lakini ameanika.ukweli
Unafiki mtupu! Kwani wakati JPM yupo hiyo tovuti ya BoT haikuwepo?
Ukweli kwamba yeye peke yake ndiye alikuwa anaijua Katiba na andiko lake ndilo lilifanya katiba ifuatwe? Take my words, anataka kuvizia uteuzi
 
Kwa ulie fikia ukomo wa kufikiri Kama wewe hauna faida, kwa waliofungua akili na kuwa na mawazo chanya unafaida kubwa Sana Ni suala la kuamua tu.
Tuna kikosi Cha anga pale Mwanza vipi kikihamishiwa chato tukaachana na huo uwanja wa kiraia.
Nchi yetu Haina uwanja mkubwa wa kijeshi ndio huo hapo sasa tunashindwa kuutumia.
Tusijiruhusu kuwa Ziro brain kuwa na mawazo hasi na lawama kibao,tuwaze chanya tusonge mbele.
Akili hizi yaani unaanza kujenga halafu unafikiria chakufanyia

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
 
Yaani uwanja wa chato utakuja kuwa na msaada? mko serious kweli? umewauliza wakongo kuhusu uwanja wa Mobutu?

Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app
Wewe hujui hivi wewe unafikiri Chato ni kijiji? Endelea kusikiliza wapuuzi hapa! Chato ina miji kama Katoro kuna watu wanahela ya kupanda ndege na wanafata bidhaa China!
 
Hayati alijisifu Tanzania ni tajiri mno, tulichezewa mno, tunatekeleza miradi kwa fedha za ndani.

Bhaghosha! Inakuaje deni la taifa liongezeke wakati pesa ya walipa kodi ndio ilitumika kugharamia miradi ! [emoji848][emoji848]
 
Ishu ni kuifanya mikopo ni siri, hatujui hata ilitumikaje!! Hii trl 1.3 imewekwa wazi na ina mchanganuo wote wa matumizi, tusipoona hayo waliyosema watayafanya lazima tutahoji! And pia why kuwatukana kila siku watu wanaokukopesha majukwaani kwa kuwapa kila aina ya majina wakati ukitoka hapo unapita mlango wa nyuma kuwaomba mpunga?
Tatizo lako hujui maana ya pesa za ndani. Nyumbani kwako ukikopa benki ukajenga nyumba na kulipa deni kwa mshahara wako utasema benk ilikujengea??????????????????????????????????????????????? hebu ujisumbue kidogo kufikiri bhana
 
Wewe hujui hivi wewe unafikiri Chato ni kijiji? Endelea kusikiliza wapuuzi hapa! Chato ina miji kama Katoro kuna watu wanahela ya kupanda ndege na wanafata bidhaa China!
Wewe kufuata bidhaa China unaona ni ishu sana hadi mletewe uwanja wa ndege?? kuwa serious wewe jamaa
 
Wewe kufuata bidhaa China unaona ni ishu sana hadi mletewe uwanja wa ndege?? kuwa serious wewe jamaa
Unaona kama anataka kwenda China si lazima apande ndege kwenda dar ndo achukue fulaiti ya China! Mkuu sisi tumezunguka nchi hii! Watu wa mikoa hiyo ya Geita na mikoa jirani watautumia uwanja maana wako vizuri! Ukitaka kujua nenda huko geita ukaone watu walivyo na pesa! Usifikiri kupanda mwendo kasi ndo ujanja!
 
Kwani deni linalipwa na pesa za nje?

Ni msaada tu ndio huwa za nje, borrowed zote ni za ndani. Unachanga unalipa... ukikamilisha mradi ni wako.

We ukikopa ukajenga nyumba then ukikamilisha mkopo ni bank imekujengea au we mwenyewe?
Sidhani Kama Swali Lako Litajibika, Kwa mtazamo wangu ni irrelevant ktk context ya development financing.

Jambo lingine Mortgage financing ina kanuni zake zipo wazi na nyingi sana ni kama development financing.

Mkopo wa kibiashara ukitolewa kujenga barabara hata kama barabara imekamilika na mkopo haujalipwa ile barabara haiwezi kuuzwa lkn tayari imekamilika na inatumika.

Lakini ukitaka kujua kwanini mkopo huu ni kitanzi basi kwa uchache tu fuatilia kwanini ATCL hairuki kwenda South Africa licha ya kwamba ni sehemu yenye soko zuri kwa biashara ya utalii....au bado Xenophobia inaendelea ndiyo maana ndege zetu haziendi huko zinaishia Zimbabwe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa wa hovyo ni yule anae pewa taarifa za hovyo nakuzipokea kama zilivyo Kama wewe..
Naweza kusema wewe na mleta mada ni watu wa hovyo sana kuwahi kutokea jf.View attachment 1987985

ndo mwisho wako wa kufikili mkuu? ivi mtu kama mwigulu tangu lini akaamika? unataka niamini taarifa iliyotolewa na BOT, au mwigulu, acha ushabiki maandazi
 
Magufuli katutenda deni la taifa, trilioni 78 Samia msalabani

Jamhuri October 26, 2021

Na Deodatus Balile

Kazi hii ya uandishi wa habari moja ya majukumu yake ni kuanika ukweli minong’ono inapotawala katika jamii.
Nimesikitika sana kusikia mikopo ilikopwa kwa masharti ya kibiashara na ya mda mfupi kiasi hicho huku huku Aliyekuwa Rais anadanganya.

Kiukweli Rais wa sasa alifaa awafute Kazi wapuuzi wote wa serikali iliyopita.

Mwisho kwa kuwa ndio yuko Ofisini kwa sasa lazima atafute ufumbuzi na hakuna namna.Ndio maana serikali kwa sasa iko tayari kuchukua mikopo ya masharti nafuu na bei rahisi kwa ajili ya kugharamia miradi na kulipa sehemu ya madeni hayo yaliyoiva.

Kwa hali hii naungana na Serikali ya mama waongeze tozo kadiri inavyowezekana na pia nampongeza kwa kuwa muwazi kwenye mikopo mipya.

Magu akiharibu Sana hii nchi na bila shaka hasira za kuita mabeberu zilitokana na kunyimwa misaada na mikopo ya masharti nafuu kwa sababu mikopo ya aina hiyo inakwenda na uwazi na kuweka wazi matumizi ya serikali.

Nakumbuka serikali ya Mwendazake ilijitoa kwenye mfumo wa kutathmini uwazi.
 
Back
Top Bottom