Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78


Wewe unaekopesheka c ukachukue huo mkopo
 
We ndo utueleezee vizuri unadhan imeenda wap!! Maana transaction zote za serikali n documented!! Kama unadhan kuna upotevu wa hela n sh ngap
Assad alijaribu kusema kuna 1.5 tril hazijulikani zipo wapi kwenye hesabu, unajua kilichompata, kutokana na hilo tunaweza sema hela nyingi kipindi cha awamu pendwa ilikuwa inatolewa kutegemea na Bwana Yule anachosema/kuamua! Hakuna aliyethubutu kumuuliza chochote kuhusu matumizi na documentation! Inachofanya awamu hii ni kujaribu kumsitiri, kufunika kombe! Wakiamua miaka 5 ya jamaa ichunguzwe kwenye matumizi ya fedha itakuwa ni aibu haijapata kutokea nchi hii
 
Huyu ni mwanamtandao hana lolote zaidi ya fitina. Timu JK hawa

Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
 
Ni bora ya Magufuli kuna miradi tunaiona kwa macho ,Mbowe alichangisha bilkion7 za wabunge na akatafuna zote.
Ofisi ya chama pale ufipa ni pagala vilevile hadi leo
 
[emoji106][emoji106]
 
Onyesheni basi hizo 29 Trilioni mlizokopa kimyakimya usiku wa manane mmezitumiaje kwenye hiyo miradi? Maana mlituambia kila kitu ni fedha zetu za ndani...
 
Ukiangalia mikopo mingi ya IMF na WB iliyotolewa enzi za JPM ni ile ambayo ni mwendelezo wa awamu zilizopita!!

Au ndo kwavile unadhani kukopa benki binafsi ni suala la kujivunia?
Zipo faida na hasara za kukopa WB na IMF na pia kukopa benk binafsi.

Hasara ya kukopa WB na IMF nikiwa wakopeshaji hawa wanakupangia fedha walizokukopesha uzitumieje na kuchunguza sana masharti wanayokupa ukiyafuata kama yalivyo huo mradi uliopanga kuutekeleza kwa fedha hizo hautakaa uje kukuletea tija. Kibaya zaidi uambatanisha na masharti ambayo hayahusu financial issues kwa nchi mkopaji. Mifano ipo. Riba inasemwa ni ndogo hatuelezwi udogo wake.

Hasara ya kukopa benki binafsi nikuwa riba yao nikubwa ingawa hatuelezwi ukubwa wa riba hiyo. Mikopo ya hawa jamaa haina masharti zaidi ya kuelekezwa ulipe deni kwa wakati. Mifano ipo
====
Sina hakika mkuu wangu, Chige hauyajui haya.

Pitia peer reviewed article hii inayofafanua vizuri hasara ya kutumia wb na imf hasa kwa nchi za Afrika.

 
Ametuwekea BOT summary report since 2000 to date halafu unasema uwongo? Acha undezi jombaa na kama wewe una ubavu tuwekee na wewe BOT report unayohisi ni ya kweli. Msilete mahaba yenu ya matandu/ukoko wa wali kwenye masuala nyeti ya uchumi wa nchi.
 
Igweeeeee [emoji120][emoji120][emoji106][emoji106]
 
Huyu mwandishi kasomea uchumi au ni mchumua tumbo tu .Mbona aelewi kabisa anachoandika.?Huyu ni mchumia tumbo tu.Amepewa vijisenti na timu Fulani.Tunaijua.Ili amchafue Mzalendo Magu.
 
Balile ile heshima yangu kwako nimeipunguza kaka. Hizo numbers za BOT hazisomwi bila consideration ya mambo mengi. Alafu unaposema alidanganya kuwa miradi tunafanya kwa fedha zetu ni kusema uongo na unfortunately zipo dhambi ni za kuepuka kama kusema uongo makusudi kwa lengo la kuharibu utu wa mtu ambaye hawezi kujitetea!

Saga la SGR, na bwawa la Nyerere inafahamika nini kilitokea hadi JPM akaamua kuanza kibishi kwa funds za ndani! Hakuna aliposema hii miradi itakamilishwa na fedha za ndani tu bali hakutaka kushindwa kupitia masharti ya mikopo ila lengo lake lilikuwa kukopa tangu awali.

Uongo kama huu, kutenga muda kuuandika na jinsi ulivyokuwa unachagua maneno ni dhahiri hili lina dhamira isiyo njema.
 
Balille ameleta hoja muhimu sana sana kwetu waungwana humu tuichambue. Kosa lake lililoshusha credibility yake ni kutaka tuamini kwamba alisababisha Rais Samia aapishwe kama Rais kwa mujibu wa Katiba ya nchi. Kwamba Katiba aliijua yeye tu. Serious? Anyways tusimlaumu timing kwa sababu sote tulijua JPM hakuwa ana entertain mijadala inayokwenda kinyume na malengo yake binafsi. Alisema ni pesa zetu za ndani tu na kutuambia ubaya wa wazungu/mabeberu huku tukijua wazi anakopa kama anatukomoa wanyonge wake na mbaya zaidi kwa hao hao mabeberu. Sote tunajua malengo ya JPM kutaka kumuondoa Govornor mkweli Ndulu na CAG Assad ili aendelee kudanganya umma mambo ya kiuchumi, fedha na ubadhirifu na hapa ndipo tulipo na hoja za Balile. Tusingekuwa Taifa tunu yake kuu ni UNAFIKI, Bwana Rioba CEO wa TBC angeandaa mjadala wa wazi miongoni mwa wasomi, raia na wanasiasa tujadili kwa hoja na facts. Lakini Lissu alinyanyuka kukemea uongo mwingi wa JPM pamoja na viongozi wachache wa dini. Uthubutu wa namna ya pekee! Ukweli ni kwamba JPM alikopa kifichoni mwa walipaji hiyo mikopo na ukweli ni kwamba faida ya hiyo mikopo alipeleka ALIPOKUWA na maslahi binafsi kwa manunguniko kwa wengi na hatuna uhakika kama yote ilitumika kwa maslahi ya Taifa hasa katika mazingira ambayo CAG hakutakiwa kufanya kazi yake. Kwa sasa mwacheni Rais Samia afanye anachoona kitatuokoa na nafurahi anashirikisha viongozi waliopita. Wito wangu Rais aruhusu upinzani, amwachie Mbowe, Lissu, Zitto et all, ili tusifiche mambo ambayo mwisho wa siku yanatufikisha tuliko leo. Hapo ndio umuhimu wa Katiba mpya unaonekana. Kumbukeni Mficha uchi....Mficha Marathi...
 
Umeeleza meeengiii lakini hujajibu Trilioni 29 zimetumikaje? Kulikuwa na shida gani kuweka wazi in public matumizi ya hizo fedha kama aliyofanya juzi SSH? Hiyo si ni pesa ya umma unaficha matumizi yake kwa nini? Pili kujenga majengo makuubwaa kama hayo mahospitali unayosema lakini hayana vifaa tiba, watumishi wa kutosha, madawa etc kuna faida gani? Unajenga masoko (Mtwara na Dodoma) kwa billions of money but mwisho wa siku hakuna wafanyabiashara wanataka kwenda huko really?? Unajenga mahakama sawa halafu mahakama unazikandamiza hazitoi haki what's that?? Pale penye kutoa haki hata mahakama ikiwa chini ya Mwembe watu wataisifia kwa kutoa haki!!
 
Masharti ya mikopo ya IMF ni nafuu zaidi kuliko ya private commercial banks. This is a fact!
Concessional loans inayoambatana masharti ya kutiliwa mashaka.
=====

"Whilist the World Bank and IMF require budget cuts in the public sectors of the African
countries, the Structural Adjustment Programme permitted public sector spending on arms and the overall military sector. As a direct result, African government spending on arms import increased leading to the proliferation of arms in the continent thereby increasing the occurrence of conflicts and the violation of human rights on a wider scale.

The United States (one of the architects of the IMF) is the world’s biggest arms exporter. In 1999, the United States exported well over $11.8 billion arms and armaments, out of which about $7.6 billion worth were sold in Africa at the peak of SAP.

Sad, isn’t it?" Written by Kingston (2011).
 



Ungesoma post hii na mwenye uelewa wa ‘public finance’ na historia yake vizuri.

Ungefahamu DMO stands for ‘Debt Management Office’ na hizo department zinatakiwa kuwa wizara fedha zote duniani, hasa nchi maskini kama sehemu ya kuangalia mikopo ya nchi na kufanya stress ambazo IMF na WD wanazipitia kwa kufuata frameworks zako.

Sasa maana yake nini ili ukope kuna frameworks zao moja wapo ni hiyo DSA, by know you should public finance sio uwanja so tusipotezeane muda.
 
Kuanzia 2016-2020 kumbe ulikuwa unatania eti?

Kupewa tu Uenyekiti wa Jukwaa 2021 na baada ya Mh.Magufuri kufariki Dunia ndio unasema "utanii" si ndio au?

Siku zote hizo 2016-2020 nyinyi kama Jukwaa lenye taarifa kwanini hamkuyasema haya (Takwimu za nyuma).?


Ifike mahala watu wazima tuwe tunaheshimiana walau kidogo,kuna siku tutakuja kuchekwa na wahisani huku kizazi kijacho kikituzomea.

Mikopo iliyokopwa wengi tumeona matunda yake,kumlaumu Hayati Mh.Magufuri huko ni kutengeneza mazingira ya kuhujumu miradi inayotegemea mikopo hiyo.

Ndugu Balile kipi bora kuendelea kukopa tumalizie miradi tuanze tufanye return au tuache kukopa miradi isitekelezeke tupunguze madeni?

Hata hivyo nini sababu ya kusema haya kwa sasa?
Na labda unategemea nini kifanyike?

Hujuma na njama sio kuiba au kufanya jambo lolote la kivitendo,kalamu/ulimi ina/unaweza kuwa
na silaha nzito ya kuhujumu/kula njama za kuhujumu.

Siku zote mtu mzalendo sio muoga wala mnafiki,mzalendo wa kweli husema ukweli pasipo kuangalia anayemsema atamfanya nini ,ungelisema hayo kipindi unayemsema yupo hai ungeliliokoa Taifa/kupata ufafanuzi kwa kina,kwa sasa ni kama vile unajichoresha na kujihaibisha na kuhaibisha taaluma ya Uhandishi wa habari.

Tunaomba utupe takwimu za riba ya mikopo hiyo kwa awamu zilizopita (Mh.Mkapa na Mh.JK) kwa kuwa riba zake usituambia hazijaiva hadi leo (Mikopo yake bado hiko fixed au?).....elewa ya kuwa riba za mikopo mara nyingi ni Geometrically na sio Arthmetrically unless otherwise...?
 
Mleta mada kaandika ukweli mtupu. Awamu ya tano imeacha mzigo wa madeni. Mama anapambana kwa ubunifu alionao ili yaweze kulipwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…