Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Walishirikiana na
Wewe nawe ni team msoga miradi hiyo aliisaini Kikwete waziri wake wa miundombinu alikuwa nani? Huyo kikwete kwa akili yako alikuwa na mda wa kufatilia ujenzi? Watu wanaangalia aliyetekeleza mradi hapa ni Magufuli! Kikwete wako chini ya REA ya waziri Ngereja walifanya nini cha maana?
seth na rugemalila kugawana 250M kila siku😂
 
Mzee wakati wa Mwendazake hiyo tovuti ya BoT si ilikuwepo, mbona hukuitumia na kuleta taarifa kama hizi? Nakumbuka kuna wakati gazeti lako lilisifiwa hadharani na JPM kwa kuibua uozo sijui bandarini ama wapi lakini hili ambalo unasema linatutoa utumbo hukulisema. Leo ndio umeliona, kweli ya Mungu mengi.
Wewe unaona hatudaiwi
 
Tupe na thamani ya miradi iliyotokana na deni, kama uwiano wa deni na uchumi kukua ni 30% huko kutendwa kunatokeaje?

Anzia upanuzi wa bandari, SGR, Upanuzi wa highways, mabarabara ya mitaa, stand za mabasi nchi nzima, New mwendokasi roads, vituo vya afya nchi nzima, Hospitali za wilaya nchi nzima, Mashule, Ndege, upanuzi wa viwanja, ujenzi wa Dodoma plus Ikulu ya Chamino, usambazaji umeme kila kijiji, vivutio vya utalii, Hydropower ya Nyerere na vingine vingi. Ulitegemea hela haitumiki?

Then go back angalia uwiano wa uchumi na ukuaji wa madeni! Njoo kwenye probability means of return. Angalia makusanyo per annual sio kuandika kinafiki.
Kumbe tulikopa sio fedha zetu za Ndani
 
Wewe unaona hatudaiwi
Tatizo langu ni unafiki wa huyu aliyekuja kutuambia sasa kwamba tunadaiwa na taarifa zimekuwepo muda wote huo lakini hakusema anasubiri mpaka JPM hayupo ndio anaanza kusema kwamba ooo alikopa, mbona wakati anakopa na taarifa zikawekwa kwenye tovuti ya BoT hakusema?
 
Lakini si tungepata fursa ya kumshauri asichukue mikopo ya kibiashara inayoanza kututoa utumbo sasa
Mikopo aliyokopa Marehemu Magufuli inakutoaje wewe utumbo??

Kuna watu mnahangaika na vitu visivyowahusu. Mikopo ya Serikali inakunyima usingizi wewe??

Hata kama deni la taifa litafikia trillion 200 bado mimi siwezi kuugua tumbo au kukosa usingizi sababu hainihusu.

Kuna watu watasema, oooh, sijui wananchi ndiyo watabeba huo mzigo wa madeni kwa kulipa kodi kubwa. Well, well, hata kama itakuwa hivyo lakini bado ukweli unabakia pale pale, deni la taifa halituhusu sisi wananchi wa kawaida.
 
Tatizo langu ni unafiki wa huyu aliyekuja kutuambia sasa kwamba tunadaiwa na taarifa zimekuwepo muda wote huo lakini hakusema anasubiri mpaka JPM hayupo ndio anaanza kusema kwamba ooo alikopa, mbona wakati anakopa na taarifa zikawekwa kwenye tovuti ya BoT hakusema?
Wewe ulikua unajua mbona hukusema pia?
 
Shida ya Magufuli alipenda pesa ya wazungu lakini masharti alikuwa hayapendi, ndio maana akaangukia kwenye mikopo umiza. Serikali inakopaje mikopo ya muda mfupi hivyo tena kwa riba ya 8%??

Huko alikoenda kama kuna kufa tena, afe tu again.
 
Kwa taarifa yako hizo unazoambiwa ni fedha za kujenga madarasa kutokana na tozo ndio rejesho la vaccine ya Uviko19 na usitegemee eti ipo siku serikali itakuwa na transparency kwa kila jambo. Bora hata JPM alisema fedha zetu za ndani na kimantiki alikuwa sahihi kama unakopa kujenga then unalipa from inner source hizo fedha ni zako baada ya kukamilisha mkopo (na ndio maana deni huwa lako) hizo ni tofauti na msaada wa mashimo ya vyoo. Kinadharia anaweza kuwa hakuwa sahihi na hilo ni swala binafsi na pia ki protocol... Kitu ambacho unakishangilia sasa ni mama kukopa fedha za Uviko then hakwambii nani atazilipa na kutoka chanzo gani?.

Angalia kupanda kwa bidhaa za petrol angalia Chuma angalia ushuru wa imported products kuanzia mafuta ya kula mpaka utaelewa tu.
Hii lugha ya mkopo kutoka nje kuitwa fedha za ndani ndipo alipotulaghai kwa kutuingiza chaka, hapa tuwe wakweli na si kuupaka rangi uongo mkubwa kiasi hiki. Hapa tuliaminishwa wananchi kuwa tunajitegemea.
 
Hivi unadhani mabeberu ata kwa kupitia private banks yanakopesha nchi maskini bila ya IMF na WB kufanya stress test kama unaweza kulipa madeni yako huko mbele based on your tax collections.
Hivi hoja ni kuweza kulipa deni au kukopa kwenye private commercial banks ambazo riba zake zinakuwa juu?!
Embu fuatilia sakata la ‘Credit Suisse’ linaloendelea wamelimwa fine ya $475 million na kulazimishwa kufuta deni $200 million walilokopesha taasisi ya serikali msumbiji; yote kwa sababu huo mkopo ulitolewa kwa swirl bila ya kuwaambia IMF na WD.
Ni kweli wamelimwa hicho kiwango,lakini SIO KWELI kwamba eti wamepigwa faini kwa sababu walitoa mkopo bila kuwaambia IMF na WB... SIO KWELI!!!

Na wala hawakuwa punished na IMF/WB kama unavyodai hapa bali wamekuwa punished na regulators wa US, UK, na Uswisi!! Yaani ni kama uchunguzi ambao hatima yake BAE walitakiwa kurejesha change ya radar...

Kwa maelezo yako hayo inaonesha wazi kwambahata wewe HUJAFUATILIA hilo unalowaambia wengine hawajafuatilia!

Na lau kama ungefuatilia, usingeleta ushabiki kwa sababu tu unaona kuna wmtu ameguswa! Badala yake, ulitakiwa kuwa na hofu kwa taifa lako kukopa kwenye private banks!! Makosa ya Credit Suisse ni yale yale yalizoeleka unapoamua kukopa kwenye benki za biashara!

Pamoja na mambo mengine, CS na benki nyingine ya Russia wanatuhumiwa ku-violate missing ya money laundering control na rushwa! Millions of dollars zilishia kwenye mifuko ya watumishi wa benki waliofanikisha kupatikana kwa mkopo!!

Na hayo ndo matatizo ya hizi benki binafsi!!! Hata wakati wa JK, serikali yake iliwahi kukopa Stanbic, na baadae ikagundulika kampuni ya Growth Market Advisors waliingiziwa zaidi ya Sh 10 Billion na Stanbic!

Ni hawa Growth Market Advisors ndio waliwezesha serikali kupata mkopo kutoka Stanbic!

So, pamoja na possible higher interest rates, matatizo mengine ya benki binafsi ndo hayo!!
Mozambique wameshindwa kulipa madeni yao mengine jamaa donors wamewaka watalipa wao ‘Credit Suisse’ waliotengeneza madeni ya nyongeza nchi maskini bila ya ridhaa yao.
Donors gani?! Ina maana financial regulators ni donors?
Unadhani mzungu mjinga, JK na Mkapa sio kwamba walikua awataki kukopa, sema walikuwa awakopesheki na hela ilikuwa aifanyi kazi iliyokopewa.
Ushabiki mwingine mbaya sana!!!
Wenye akili timamu walijua IMF na WD watatia nanga soon, ‘mama’ kujifanya anaenda na utaratibu wake; ameshaonywa na watu wengi sana kaa mbali na JK, rudi njia ya Magufuli hataki na bado.
Yaani we jamaa bhana!!

Yaani ili mradi uweze kutetea ujinga, unafikia kushangilia mikopo from private banks na kuponda kukopa IMF?! Hivi unafahamu kwanini Mkapa aliacha deni dogo?!

Ingawaje Mwandishi kasema Mkapa" Alipambana nayo, akaiingiza nchi katika Mpango wa Kusamehe Madeni Nchi Maskini (HIPC) " lakini uhalisia HIPC Initiative ulikuwa ni mpango wa IMF, WB na Paris Club. Mpango huu uliasisiwa kabla Mkapa hajawa Rais, na ni huo Mpango ndio uliingiza Tanzania.

Mkapa alipambana kutekeleza matakwa ya HIPC ili hatimae nchi ifutiwe madeni, na kweli, kwa ujasiri mkubwa, Mkapa alifanikiwa katika hilo na hatimae kupunguziwa mzigo wa madeni!!

Hizo ndo faida za kukopa kwa IMF, WB na Paris Club!!
 
Tupe na thamani ya miradi iliyotokana na deni, kama uwiano wa deni na uchumi kukua ni 30% huko kutendwa kunatokeaje?

Anzia upanuzi wa bandari, SGR, Upanuzi wa highways, mabarabara ya mitaa, stand za mabasi nchi nzima, New mwendokasi roads, vituo vya afya nchi nzima, Hospitali za wilaya nchi nzima, Mashule, Ndege, upanuzi wa viwanja, ujenzi wa Dodoma plus Ikulu ya Chamino, usambazaji umeme kila kijiji, vivutio vya utalii, Hydropower ya Nyerere na vingine vingi. Ulitegemea hela haitumiki?

Then go back angalia uwiano wa uchumi na ukuaji wa madeni! Njoo kwenye probability means of return. Angalia makusanyo per annual sio kuandika kinafiki.
Thumb up Bro!!
Hata Nyerere alituambia kukopa sio shida -shida umekopa kufanyia nini?
 
Toa mfano acha projo Huyo mama yenu hakopesheki ndo maana hela za UVICO zimekuwa za kudanganyia wananchi miradi uchwara!

Kwa kuona kwamba hakopesheki ameanzisha tozo ovyo ovyo! Unafikiri hao IMF&WB huwa hawajui kuwa Rais fulani ni mtendaji sio wa maneno! Hapa wanajua Mama ni Maneno sio vitendo! Ila JPM walijua ni vitendo sio maneno!
Hakika wewe ni genius.
 
Hivi hoja ni kuweza kulipa deni au kukopa kwenye private commercial banks ambazo riba zake zinakuwa juu?!

Ni kweli wamelimwa hicho kiwango,lakini SIO KWELI kwamba eti wamepigwa faini kwa sababu walitoa mkopo bila kuwaambia IMF na WB... SIO KWELI!!!

Na wala hawakuwa punished na IMF/WB kama unavyodai hapa bali wamekuwa punished na regulators wa US, UK, na Uswisi!! Yaani ni kama uchunguzi ambao hatima yake BAE walitakiwa kurejesha change ya radar...

Kwa maelezo yako hayo inaonesha wazi kwambahata wewe HUJAFUATILIA hilo unalowaambia wengine hawajafuatilia!

Na lau kama ungefuatilia, usingeleta ushabiki kwa sababu tu unaona kuna wmtu ameguswa! Badala yake, ulitakiwa kuwa na hofu kwa taifa lako kukopa kwenye private banks!! Makosa ya Credit Suisse ni yale yale yalizoeleka unapoamua kukopa kwenye benki za biashara!

Pamoja na mambo mengine, CS na benki nyingine ya Russia wanatuhumiwa ku-violate missing ya money laundering control na rushwa! Millions of dollars zilishia kwenye mifuko ya watumishi wa benki waliofanikisha kupatikana kwa mkopo!!

Na hayo ndo matatizo ya hizi benki binafsi!!! Hata wakati wa JK, serikali yake iliwahi kukopa Stanbic, na baadae ikagundulika kampuni ya Growth Market Advisors waliingiziwa zaidi ya Sh 10 Billion na Stanbic!

Ni hawa Growth Market Advisors ndio waliwezesha serikali kupata mkopo kutoka Stanbic!

So, pamoja na possible higher interest rates, matatizo mengine ya benki binafsi ndo hayo!!

Donors gani?! Ina maana financial regulators ni donors?

Ushabiki mwingine mbaya sana!!!

Yaani we jamaa bhana!!

Yaani ili mradi uweze kutetea ujinga, unafikia kushangilia mikopo from private banks na kuponda kukopa IMF?! Hivi unafahamu kwanini Mkapa aliacha deni dogo?!

Ingawaje Mwandishi kasema Mkapa" Alipambana nayo, akaiingiza nchi katika Mpango wa Kusamehe Madeni Nchi Maskini (HIPC) " lakini uhalisia HIPC Initiative ulikuwa ni mpango wa IMF, WB na Paris Club. Mpango huu uliasisiwa kabla Mkapa hajawa Rais, na ni huo Mpango ndio uliingiza Tanzania.

Mkapa alipambana kutekeleza matakwa ya HIPC ili hatimae nchi ifutiwe madeni, na kweli, kwa ujasiri mkubwa, Mkapa alifanikiwa katika hilo na hatimae kupunguziwa mzigo wa madeni!!

Hizo ndo faida za kukopa kwa IMF, WB na Paris Club!! Hayo madeni yangekuwa ya private banks, unadhani yangefutwa?!
Mikopo yooote ya JPM tunajua ilifanya nini nakila mtanzania anaiona na iliyokamilika anaifaidi. Tunasubiri isiyokamilika kama JKN Hydro dam ikamilike mwezi ujao. (ingawa kwa huyu mama na akina January wake-nina mashaka!)
 
Mkuu unasema ati Trilion 78 tunadaiwa ok, sasa kwa sababu tupo million 60 sasa nagawanya kila mtu afe na deni lake bana.

78,000,000,000,000 / 60,000,000 = 7,800,000.

Wakuu kila mmoja anadaiwa Mil 7 na laki nane. Deni ulipe kabla ya Dec 31st 2021.
 
Toa mfano acha projo Huyo mama yenu hakopesheki ndo maana hela za UVICO zimekuwa za kudanganyia wananchi miradi uchwara!
Hivi nyie watu mmerogwa, au?!

Yaani unaonea fahari kukopa sekta binafsi... are you serious?!

FYI, ukiona taifa linakopa kwenye private bank basi hiyo ni last resort!! Private Banks wanafurahia hii mikopo ya kuwakopesha serikali, na ndo maana mingini inahusishwa na rushwa!!

Na watoaji wa rushwa hizi sio wengine, bali mabenki wenyewe!! Kuna mwenzako mmoja hapo juu katolea mfano wa Credit Suisse na mkopo wa Msumbiji, lakini inaelekea ama issue yenyewe haifahamu vizuri au ameamua tu kudanganya!!!

Credit Suisse wametoa mkopo Msumbiji huku mabilioni ya pesa yakiwa yameishia mifukoni mwa waliofanikisha deal la Msumbiji kukopa Credit Suisse!! Ni kama ambavyo ilitokea back in 2013 pale tulipochukua mkopo Stanbic!!

Kwenye mkopo ule ikaja kugundulika Enterprise Growth Market Advisors, kampuni ambayo iliiunganisha Stanbic na serikali, wao wakaingiziwa zaidi ya Sh 10 Billion na Stanbic!!

Ukishakuwa na collateral, Benki Binafsi watakupa tu pesa... kwahiyo wala sio issue ya kukopesheka!!

Hata Msumbiji walikopeshwa USD 1 Billion na Credit Suisse wakati ambao taifa hilo lilipogundua gas ya kutosha!!!

With huge gas discovery in Tanzania, hakuna private bank inayoweza kuacha kuikopesha! And FYI, hizo benki binafsi zinaweza kuwa comfrtable zaidi kumkopesha Samia kuliko JPM ambae alikuwa branded kwamba hatabiriki!!

Kitu kinachoogopwa zaidi na private banks ni unpredictability of the government policy!! That having been said, kama hizo benki ziliweza kumkopesha JPM, basi kwa Samia wanaweza kufanya mara 10...

hapa naongelea financial risk assessments... sio ushabiki wa kisiasa!

Kwahiyo acheni huu ushabiki wenu!!! Kukopeshwa na benki binafsi wala sio jambo la kujivunia kwamba eti "tunakopesheka"!!
Kwa kuona kwamba hakopesheki ameanzisha tozo ovyo ovyo! Unafikiri hao IMF&WB huwa hawajui kuwa Rais fulani ni mtendaji sio wa maneno! Hapa wanajua Mama ni Maneno sio vitendo! Ila JPM walijua ni vitendo sio maneno!
Sasa kama hao IMF & WB walifahamu kwamba JPM ni matendo na sio maneno, na Samia ni maneno na sio vitendo; kwanini basi wakaamua kumkopesha mtu wa maneno bila vitendo na kuacha kumkopesha mtu wa vitendo badala ya maneno?!

Ukiangalia mikopo mingi ya IMF na WB iliyotolewa enzi za JPM ni ile ambayo ni mwendelezo wa awamu zilizopita!!

Au ndo kwavile unadhani kukopa benki binafsi ni suala la kujivunia?
 
Hivi hoja ni kuweza kulipa deni au kukopa kwenye private commercial banks ambazo riba zake zinakuwa juu?!

Ni kweli wamelimwa hicho kiwango,lakini SIO KWELI kwamba eti wamepigwa faini kwa sababu walitoa mkopo bila kuwaambia IMF na WB... SIO KWELI!!!

Na wala hawakuwa punished na IMF/WB kama unavyodai hapa bali wamekuwa punished na regulators wa US, UK, na Uswisi!! Yaani ni kama uchunguzi ambao hatima yake BAE walitakiwa kurejesha change ya radar...

Kwa maelezo yako hayo inaonesha wazi kwambahata wewe HUJAFUATILIA hilo unalowaambia wengine hawajafuatilia!

Na lau kama ungefuatilia, usingeleta ushabiki kwa sababu tu unaona kuna wmtu ameguswa! Badala yake, ulitakiwa kuwa na hofu kwa taifa lako kukopa kwenye private banks!! Makosa ya Credit Suisse ni yale yale yalizoeleka unapoamua kukopa kwenye benki za biashara!

Pamoja na mambo mengine, CS na benki nyingine ya Russia wanatuhumiwa ku-violate missing ya money laundering control na rushwa! Millions of dollars zilishia kwenye mifuko ya watumishi wa benki waliofanikisha kupatikana kwa mkopo!!

Na hayo ndo matatizo ya hizi benki binafsi!!! Hata wakati wa JK, serikali yake iliwahi kukopa Stanbic, na baadae ikagundulika kampuni ya Growth Market Advisors waliingiziwa zaidi ya Sh 10 Billion na Stanbic!

Ni hawa Growth Market Advisors ndio waliwezesha serikali kupata mkopo kutoka Stanbic!

So, pamoja na possible higher interest rates, matatizo mengine ya benki binafsi ndo hayo!!

Donors gani?! Ina maana financial regulators ni donors?

Ushabiki mwingine mbaya sana!!!

Yaani we jamaa bhana!!

Yaani ili mradi uweze kutetea ujinga, unafikia kushangilia mikopo from private banks na kuponda kukopa IMF?! Hivi unafahamu kwanini Mkapa aliacha deni dogo?!

Ingawaje Mwandishi kasema Mkapa" Alipambana nayo, akaiingiza nchi katika Mpango wa Kusamehe Madeni Nchi Maskini (HIPC) " lakini uhalisia HIPC Initiative ulikuwa ni mpango wa IMF, WB na Paris Club. Mpango huu uliasisiwa kabla Mkapa hajawa Rais, na ni huo Mpango ndio uliingiza Tanzania.

Mkapa alipambana kutekeleza matakwa ya HIPC ili hatimae nchi ifutiwe madeni, na kweli, kwa ujasiri mkubwa, Mkapa alifanikiwa katika hilo na hatimae kupunguziwa mzigo wa madeni!!

Hizo ndo faida za kukopa kwa IMF, WB na Paris Club!! Hayo madeni yangekuwa ya private banks, unadhani yangefutwa?!
In case you don’t know ni serikali ya Mozambique ndio waliomba London waingilie kati sakata lote, taasisi yao kuchukua government guarantee loan bila ya serikali kujua.


82234082-7672-418A-9FC0-BBDD11F56551.jpeg



Unasoma article moja halafu unasema ulifanya research on the matter na kesi ilifunguliwa UK kwa maombi ya serikali ya Mozambique kwa sababu waliotoa mkopo ni subsidiary ya CS iliyopo UK.

Sasa tafuta na articles zingine uone badala ya kutumia Investors wametaja hao investor wenyewe ni IMF na WB.

Hayo mengine ya Mkapa kila mtu anajua historia ya madeni ya third world na mzozo ulipoanzia late 70’s baada ya baadhi ya nchi kuanza kushindwa kulipa madeni kwa sababu petrol money ilitumika cheaply kukopesha nchi maskini kupitia IMF na WD mpaka solution za kufuatiana madeni nchi maskini, Paris Club and so forth.

Issue niliyozungumzia mimi ni ugumu wa kupata mikopo kwa uraisi wa Mkapa na J.K, hiyo historia yako ya kufutiwa madeni kila mtu anajua and more.

Off for two hours.
 
Back
Top Bottom