Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78

Zipo faida na hasara za kukopa WB na IMF na pia kukopa benk binafsi.
Of course, kila jambo lina faida na hasara zake...

Muhimu ni mizania!!
Mkuu TUJITEGEMEE... hiyo sio hasara bali ni faida!!!

From my experience working in financial sector, moja ya sababu inayofanya wafanyabiashara wengi ku-default ni kuelekeza mikopo "sekta" tofauti na ile uliyokopea...

As a private enterprise, ukienda benki kukopa lazima utawasilisha mchanganuo wako wa kibiashara!! Merits za mkopo uliopewa itatokana na loan appraisal uliyowaisilisha!!

Sasa ni kawaida sana unakuta Mfanyabiashara anapeleka mchanganuo wa biashara ya mahindi, akipata pesa anawekeza kwenye mpunga! Wengi huwa wana-default kwa ujinga huu!!

Tukija at a state level!!

Miradi mingi huwa inakwama kwa sababu ya kukosa close monitoring na mischannelling of loan funds!!! IMF lazima wahakikishe hakuna mischannelling kwa sababu mkopo ukishindwa kufikia malengo, hawana chochote cha kukufanya! Sana sana wataacha tu kukukopesha!!

On the otherhand, at a state level, benki binafsi wala hawana haja ya kukufuatilia unatumia vipi... kwanza hiyo jurisdiction wataitoa wapi! Lakini kubwa zaidi, wao wanachojali ni kurudi kwa pesa zao, na riba juu! Na wapo tayari kutoa hadi rushwa kuhakikisha wanakukopesha kwa saabbu serikali, hususani yenye resources and stability, ni less risk!!

They don't care kama umejenga hayo mashule au hapana kwa sababu it's none of their concerns!! Hawa kazi yao sio "elimu kwa wote" au "afya kwa wote" kama unavyoweza kukutana nayo hayo IMF... they're strictly FOR BUSINESS that turns into PROFIT...
Hasara ya kukopa benki binafsi nikuwa riba yao nikubwa ingawa hatuelezwi ukubwa wa riba hiyo. Mikopo ya hawa jamaa haina masharti zaidi ya kuelekezwa ulipe deni kwa wakati. Mifano ipo
Haina masharti kama you've something to offer kama nilivyosema hapo juu!!

Hawa hawawezi kukupa masharti sijui ya Utawala Bora, mara social liberty n.k lakini watakupa masharti ambayo purely ni commercial... na kubwa zaidi uwezo wa serikali husika kuweza kurejesha!! Kwa nchi yenye raslimali kama hii, wanajua hata usipolipa leo, utalipa kesho au hata mwakani! Kadri unavyochelewa, kwao ni faida kwa sababu riba inaongezeka!!!

Nadhani umeshasikia sana suala la Bandari ya Hambantota... maarufu kama Bandari ya Sri Lanka!!!

Serikali ilifikia uamuzi wa kuuza hisa za ile bandari baada ya kuona deni linaendelea ku-accumulate kila uchao... kutokana na riba!!
Sina hakika mkuu wangu, Chige hauyajui haya.
Nafahamu sanan
Nikipata muda nitapitia lakini nikujuze tu kwamba, kwa yeyote aliyesoma uchumi at university level, anafahamu vema masuala ya Structural Adjustment Program kwa sababu tumesoma sana hayo!!!

Lakini labda nikung'ata sikio...

Structural Adjustment Programs sio mbaya kihivyo kama ambavyo watetezi wa serikali za kiafrika wanavyojaribu kuaminisha watu...

Hata hapa tulipofikia, ni matokeo ya Structural Adjustment Program, ingawaje ni kweli pia yapo maeneo ambayo hatukufanya vizuri!!

Of course, kuna mambo mengine am
 
Huyu mnafiki sana na wataibuka wanafiki wengi sana kama huyu, masikitiko tuliyonayo wakati yupo hai walikuwa wanajifanya wanampamba sana, sasa hayupo hai wanajikweza ili waonekane wanaenda sawa na Mama, watu wa hivi ni wa kuogopwa sana,bora mchawi kuliko mnafiki
 
Sasa inahusiana nini na nilichosema?!

Narudia, Acha Mbwembwe na tambo....

Kufuchua uongo wako ndo kukupotezea muda?!

Unaleta mbwembwe za kuwa mtalaamu wa Public Finance baada ya kuweka bayana uongo wako?
 
Upo sahihi kwa 900%... Balile mnafiki sana!!

Kuna siku nilishawahi kumwelezea hapa...
 
Mleta mada kaandika ukweli mtupu. Awamu ya tano imeacha mzigo wa madeni. Mama anapambana kwa ubunifu alionao ili yaweze kulipwa.
Mama Samia anaubunifu? Yeye alishasema kazi yake ni kuangali graph! Sasa hapo ujiongeze nini kitatokea? Mama samia tumwache apambane kivyake msije hapa kumtetea wakati mwenzake JPM alikopa na akafanya vitu vya kuonekana!
 
Sasa inahusiana nini na nilichosema?!

Narudia, Acha Mbwembwe na tambo....

Kufuchua uongo wako ndo kukupotezea muda?!

Unaleta mbwembwe za kuwa mtalaamu wa Public Finance baada ya kuweka bayana uongo wako?
Hivi wewe unaowaamini ni wale wenye makaratasi pee kuwa wanajua mambo ya fedha? Hebu niomeshe Supermarket yeyote ya maana dar,arusha au mwanza ianyomilikiwa na mtu wa degree uchwara za finance hapa?

Watu wakawaida wanaweza kuwa na mchango bora sana kuliko hao wenye makaratasi! Kwanza nyinyi mnaojidai mnamakaratasi mlikuwepo tokea uhuru lakini mnatufanyia upumbavu tu kila siku! Matokeo sifuri licha ya maneno mengi!
 
Heshima yako Bw. Chige

Huwa naenjoy sana nikiona mabandiko yako kwangu ni darasa tosha. Mengine huwa naya-print nayaweka kwa mfumo wa documents (kimasijala zaidi). Sababu kuu ni kuwa: Chochote utakachokiandika kinachohusu mjadala huwa unaweka fact!

Mwishoni huwa unaweka ushauri kwa mwenendo kadhaa cha kufanyika ni kipi! Upo tofauti na wengi, wengi wao wanajibu kifikra. Mathalani kwenye huu Uzi umewekwa kidata. Kuupinga ama kukubaliana nao kunahitajika kwa data pia. Kingine wewe ni mkweli.

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwako.
 
Hivi ulikuwa unajaribu kusema nini hasa?!

Au umeamua kuonesha kwa mifano linapokuja suala la kujieleza na kujenga hoja kati ya hao uliowaita wana makaratasi na wale wasio na makaratasi?
 
Tupe na thamani ya miradi iliyotokana na deni, kama uwiano wa deni na uchumi kukua ni 30% huko kutendwa kunatokeaje?

Anzia upanuzi wa bandari, SGR, Upanuzi wa highways, mabarabara ya mitaa, stand za mabasi nchi
Una AKILI sana.

Jina lako limeafiki ulichonacho kwamba mwanga wako kweli ni mkali
 
Watanzania hawasomi na Wala hawana maarifa ya kutafuta taarifa kwenye internet. Ilikuwa Magufuli akiwadanganya ndiyo imetoka hivyo
 
Kheee situliambiwa hatugemei kuombaomba wala kukopa tunajenga wenyewe na mapipa yetu tumenunua cash kwa kodi zetu wenyewe bahati mbaya sana wakubwa hawadanganyi ila tu wanakua hawasemi ukweli
 
kweli nchi sasa inapumua yaani kipindi cha mwendazake Jamaa wange Mlissu fasta , weeeee umseme mungu wa Chattle heheheeeeeee kina utapata tabu sana wanaweza wakakuua hadharani kabisa na cheo wangeongezewa
 
Hata hivyo, wataalamu wa uchumi wanasema deni hili si tishio kwa uchumi wa taifa.

Unaleta myth kwamba nchi yetu inapata maendeleo,you are pointing to the flyovers. Lakini wanafunzi wengi wanavuka mito mingi na mifereji mingi kwenda shule kila siku. Siyo bora kujenga vijidaraja vingi kuliko kujenga flyover moja?

Huyu Balele ataumia kusema kuwa yeye ndiye ametuletea rais huyu. Wataalamu wa uchumi wamesema hilo deni siyo kubwa. Hiyo ndiyo modus operandis ya IMF. Wataalamu hao wanapangiwa jambo la kusema.

Hata hivyo, wataalamu wa uchumi wanasema deni hili si tishio kwa uchumi wa taifa.
Kama hakuna tatizo,why are we discussing it?
 
Lakini ukweli unabaki palepale, acha siasa
 
Sawa ila kwa maana angetaka ausitishe kama ile Bandari ya Bagamoyo angeshindwa?
Asingeshindwa ila angeonekana kiroja cha karne...

Dar Metropolitain Project iliyojenga barabara za Dar, kwa mfano... JPM anaingia madarakani tayari mkopo ulishaidhinishwa...

Sasa hapo angesitisha kwa grounds zipi?

Ubungo Interchange... ule ni mradi wa BRT! Plan ya mwanzo haikuhusisha kujenga interchange lakini wakati ujenzi wa Phase I ukielekea kukamilika, ikaonekana design ya awali ingesababisha jam ya kufa mtu kwa magari yanayotoka N. Mandela na kuingia S. Nujoma.

TANROAD wakaandaa proposal, na kuiwasilisha kwa Mzee wa Msoga, nae bila hiyana akaona waende kwa wale wale World Bank waliotoa mkopo wa BRT, Kama ilivyotarajiwa, WB wakakubali ku-finance ujenzi wa interchange!

Sasa hapo tena angesitisha kwa kutumia grounds zipi?

Kwahiyo again, angetaka angeweza kusitisha, na uzuri wa Waafrika, Wafuasi wake wale wale wanaoshangilia leo hii interchanges na barabara Dar es salaam, ndio hao hao ambao wangeshangilia endapo angesitisha miradi hiyo!!
 
Sasa inahusiana nini na nilichosema?!

Narudia, Acha Mbwembwe na tambo....

Kufuchua uongo wako ndo kukupotezea muda?!

Unaleta mbwembwe za kuwa mtalaamu wa Public Finance baada ya kuweka bayana uongo wako?
Uongo kwa kuniwekea maneno yako. Unakuja na story ambazo unataka nizijibu vitu ambavyo sijaongea.

Issue ya Credit Suisse ni kukopesha taasisi ya serikali bila ya idhini ya serikali kuu huku deni likiwa na guarantee ya serikali.

Na kwa kanuni ya madeni ya serikali ni lazima yafanyiwe stress taste na frameworks wanazotumia ni za IMF na WD ata kama unaenda kukopa private bank kuona kama una uwezo wa kulipa.

Sasa kuelezea hizo stress taste zinahusu ni mlolongo mrefu ndio maana kila nchi ina DMO ya kufanya hiyo kazi. Hiki ndio nilichosema mimi.

Sasa wewe unataka ni entertain mawazo yako na maswali yasiyo na msingi sijui ina maana private lending ni rahisi kukopa kushinda IMF na WB ndio nilichoandika hiko.

Besides if you do not know ata hela wanazotoa IMF na WD asilimia kubwa ni za private banks; sema zinakuwa channeled through them ili ku control mikopo ya nchi na kuminimise risk za default.



Na ndio maana IMF walipobaini kwa mara ya kwanza kuna mkopo wa siri walisitisha mkopo wao 2016 na donors wengine walifuata; hizo stress test zipo kwa sababu zake.

Nakuletea sasa link ya ruling kukuonyesha sababu ya hizo fines za Credit Suisse ni kutotoa taarifa IMF na WB (hayo mengine ya rushwa na nini ni sehemu ndogo tu) nchi maskini mikopo yao ipo regulated.


 
Mama Samia anaubunifu? Yeye alishasema kazi yake ni kuangali graph! Sasa hapo ujiongeze nini kitatokea? Mama samia tumwache apambane kivyake msije hapa kumtetea wakati mwenzake JPM alikopa na akafanya vitu vya kuonekana!
Una ushahidi gani kama yeye hakopi?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…