Fortilo
JF-Expert Member
- Apr 10, 2012
- 5,807
- 17,416
CDM sio ya kufa leo wala kesho mkuu...Siasa za kidemokrasia katika nchi za Demokrasia ni dhahiri wananchi wanajigawa katika pande mbili .Upande wa giza na upande wa nuru yaani Wema na ubaya .
Kwa sasa wetu wanamtaka Lisu ili siasa za Tanzania zihame kutoka kwenye siasa za upande wa wapigaji tu na anayeonekana kinyume na ufisadi anauawa au kushughulikiwa kisasa. Hii imejenga taifa la watu waovu na uovu unaonekana ndio dili. Rushwa imekua ni kama fasheni kwenye nchi hii. Watu wanaofanya biashara halali wanadharaulika ,watu wanaosema na kukemea ufisadi wanaitwa wabangaizaji . Yaani tumerudi zama za giza za kutukuza mali na kudharau haki na hekima . Mtu mwenye pesa hata akitema pumba kama Mbowe anaonekana ana busara .
Mbowe amesababisha mauaji na ulemavu wa watu wengi sana hapa Tanzania lakini hajawahi kusemwa serikali wala kukamatwa kwa tuhuma za kusababisha mauaji isipokuwa ni wakati wa JPM tu ndio alihukumiwa na kupigwa faini kwa kusababisha mauaji ya Akwiline . Familia ya Akwelini ilitakiwa ufungue Kesi ya madai dhidi ya Mbowe baada ya hukumu kuonyesha kuwa Mbowe na wenzake walisababisha kifo cha Akwiline.
Mbowe kama anafikiria kuwa damu za wenzake ndio mtaji wake basi akimlazimisha ushindi wa Rushwa ndio mwisho na anguko la Chama chake na SACCOs yake .kwani Atakua alepoteza watu wengi na hivyo kupoteza Ruzuku kubwa .
Hizi hoja za Rushwa na Ubaridi kwenye Vyama vya upinzani lazima tujiulize tunefikajd hapa?
Magufuli alisababisha kwa kias kikubwa sana huu ubaridi wa Upinzani, lazima tukubali muda ni element muhimu sana kwenye kuchambua mambo