Balozi Mulamula: Marekani sasa wanaamini ni salama kuwekeza Tanzania

Balozi Mulamula: Marekani sasa wanaamini ni salama kuwekeza Tanzania

Kupitia chombo fulani cha habari, nimemsikia Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Liberatha Mulamula akidai kwamba kwa sasa Wamarekani wanaamini kuwa ni salama kuwekeza Tanzania, lakini hasemi ni wakati gani Wamarekani waliona si salama kuwekeza Tanzania.
Hivi unaijua lugha ya mabeberu!! Kwa mabeberu mahali panaponyonyeka hapo ndipo wanapopasifu kuwa ni salama kuwekeza!! Kwa mfano Richmond ilivyotunyonya katika kuiuzia tanesco umeme kwa bei mbaya hapo, kwao ndiyo salama. Wanakuuzia kwa kigezo cha capacity charges!! Richmond ikabadilika jjna ikawa Dowans! Dowans ikabadilika jina ikawa Symbion!! Mitambo ile ile. Kwa kigezo cha capacity charges, uwezo wa mitambo yao kuzalisha umeme ndiyo unayolipia na siyo kiasi cha umeme ulioutumia!! Kwa jamaa hawa capacity charge kwa siku moja ni sh.152,000 000/=, Hata kama haujatumia kabisa umeme wao, lakini bado utalipa kiasi ambacho wana uwezo wa kuzalisha na siyo waliozalisha!! Kwa hiyoTanesco walikuwa wanalipia umeme ambao hawajautumia na hawauhitaji hasa wakati wa masika ambapo mabwawa ya kufua umeme kama mtera, nyumba ya Mungu na kidatu yakiwa yanazalisha umeme wa kutosha !
Mabeberu wakikusifu tayari ujue wameshaona mwanya wa kukunyonya!! Ndiyo maana mabeberu hawampendi mchina maana mchina hanyonyeki!!
 
Alaaaaaa, kumbe wakati wa meko haikuwa salamaaa...

Kwani ni kipi kilichoondoa imani hiyo hapo awali?
Kwani wao serikali wanasemaje?

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
Ukikomaa kwenye kodi tu tayari mabeberu wanasema mazingira ya uwekezaji siyo salama!!
Kama unakumbuka kuna makubaliano yalikuwa yamefanyika huko nyuma kuwa bidhaa za wajasiliamali toka Tanzania hazitatozwa kodi ziingiapo marekani na kadhalika wao pia wakileta bidhaa Tz wasitozwe kodi!!
Sasa kwa hali ya kawaida sisi hatuna bidhaa nyingi za kupaleka marekani lakini wao wataleta bidhaa nyingi zaidi!! Kwa hiyo mpango huu uliinyonya sana Tanzania!!! Maana walitusamehe pesa kidogo na sisi tukawasamehe pesa nyingi!
 
Huyu mama naye atakuja kujipambanua kungali mapema sana kwamba hajui kitu, ni mlamba viatu tu vya wakubwa.

Marekani kawekeza wapi kwingine Afrika, kiasi cha kupapatika na kujitoa ufahamu kiasi hiki.

Badala ya kuhimiza wananchi waweke bidii kuleta maendeleo kwenye nchi hii, na kuwawezesha kwenye shughuli zao, mawazo ya hawa viongozi yametekwa na propaganda.
Bila shaka matamko yake hayo ni kumbukumbu za uwekezaji walioufanya hao wamarekani wakati wa enzi za Kikwete? Atuonyeshe uwekezaji huo basi ni upi.
Ndugu yangu hakuna NCHI yoyote DUNIANI iliweza kuendelea bila FOREIGN INVESTMENT kwani NDIO huleta mitaji katika NCHI husika kwahiyo huyo waziri anayo haki yakusema hivyo ile kuwavutia wawekezaji tatizo kubwa la Kwetu TANZANIA kuwaleta wawekazi hapa linakuwa zito kidogo kutokana na POLICY zetu ni UNPREDICTABLE.

Foreing Investmen ina faida kubwa kwa NCHI huleta mitaji ,Ajira pamoja na taaluma( Elimu) kwa Raia leo hii unaiona CHINA imefika pale walipo kutokana na UWEKEZAJI uliofanywa na USA pamoja na EU wamekuja kushtuka CHINA wapo mbali sn.
 
Kupitia chombo fulani cha habari, nimemsikia Waziri wa Mambo ya Nje, Balozi Liberatha Mulamula akidai kwamba kwa sasa Wamarekani wanaamini kuwa ni salama kuwekeza Tanzania, lakini hasemi ni wakati gani Wamarekani waliona si salama kuwekeza Tanzania.
Nilicheka pale balozi aliposema walinambia "finally Tanzania mmerudi tena".
 
... Mama alishauriwa vibaya ama? Atengue?
Hizo 'hang'over' za siasa na fikra ,na propaganda za Ujamaa kwa karibu miaka 60 zimefail, na sasa afadhali tuangalie popote kule iwe 'east or west' kwa mipango dhabiti makini, madhubuti kwa maendeleo endelevu ya nchi yetu maskini.Kwa nchi yetu iliyojaliwa kila aina ya rasilimali lakini hadi leo, hatuna sababu ya msingi ya kuendelea kuogelea kwenye lindi la umaskini tu.... kazi iendelee.
Hivi unaijua lugha ya mabeberu!! Kwa mabeberu mahali panaponyonyeka hapo ndipo wanapopasifu kuwa ni salama kuwekeza!! Kwa mfano Richmond ilivyotunyonya katika kuiuzia tanesco umeme kwa bei mbaya hapo, kwao ndiyo salama. Wanakuuzia kwa kigezo cha capacity charges!! Richmond ikabadilika jjna ikawa Dowans! Dowans ikabadilika jina ikawa Symbion!! Mitambo ile ile. Kwa kigezo cha capacity charges, uwezo wa mitambo yao kuzalisha umeme ndiyo unayolipia na siyo kiasi cha umeme ulioutumia!! Kwa jamaa hawa capacity charge kwa siku moja ni sh.152,000 000/=, Hata kama haujatumia kabisa umeme wao, lakini bado utalipa kiasi ambacho wana uwezo wa kuzalisha na siyo waliozalisha!! Kwa hiyoTanesco walikuwa wanalipia umeme ambao hawajautumia na hawauhitaji hasa wakati wa masika ambapo mabwawa ya kufua umeme kama mtera, nyumba ya Mungu na kidatu yakiwa yanazalisha umeme wa kutosha !
Mabeberu wakikusifu tayari ujue wameshaona mwanya wa kukunyonya!! Ndiyo maana mabeberu hawampendi mchina maana mchina hanyonyeki!!
Jamani ndugu zangu, tatizo sio 'mabeberu'' wala mbuzi... tatizo ni lenu nyie wenyewe, ambao wawakilishi wenu ambao husaini mikataba wakiwa wamefunga macho. Wala msiwalaumu hao mnaowaita' mabeberu!
 
Back
Top Bottom