Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
Mchambuzi,
Hapo juu kuna kitu umekisema check and balance, na hasa ndio msingi wa hoja yangu.
Suala la madaraka ya rais linachukuliwa vibaya. Wale wanaodhani asipunguziwe madaraka wana hofu kuwa Rais anaweza kushindwa kufanya kazi zake kwa vile tu atakuwa amepokwa uwezo.
Kundi hilo linadhani rais ataondolewa kuwa Amir jeshi mkuu wa vyombo vya usalama au atapunguziwa nguvu kama alivyopunguziwa Gobachev na mwisho wa siku atakuwa powerless.
Kundi hili lina fear of unknown kwasababu tu limebaki kuangalia tulikotoka na limefungia macho twendako na dunia tuliyo nayo. Kuna nchi kama Turkey na nyingine nyingi tu uwezo wa rais unakuwa na mipaka hasa katika majeshi na vyombo vingine kama mahakama na haionekani kuwa tatizo zaidi.
Taifa letu linakua na hivyo lazima lipitie katika mabadiliko kulingana na nyakati.
Kuna wakati tuliaminishwa kuwa vyama vingi maana yake ni Rwanda genocide, Bosnia Hezegovina n.k.
Leo ni mwaka wa 20 hakuna tatizo lolote zaidi ya kuimarisha demokrasia kwa kiwango fulani.
Kundi la pili ambalo mimi ni mmoja wao ni lile linalotaka Rais apunguziwe madaraka.
Ukitazama kwa umakini, nchi yetu haina bunge au mahakama kama vyombo huru.
Bunge na mahakama ni matawi au ''jumuiya za serikali''.
Rais anaweza kuvunja bunge lililochaguliwa na wananchi, akamuondoa Jaji mkuu na kuweka ampendaye hata kwa emergency kama alivyofanya Mwai Kibaki.
Kumpunguzi madaraka nina maana ya kumwekea mipaka ya kazi yake na vyombo vya check and balance.
Leo Obama anafanya mabadiliko ya umiliki wa silaha wakati huo huo akiwa ameshapata ushauri wa kutosha kuhusu second ammendment kwasababu kinyume chake ni impeachment.
Kumpunguzi madaraka ni kuwa na serikali inayozingatia katiba, kufanya kazi kwa ushirikiano na vyombo vingine huku kila kimoja kikiwa watch dog ya kingine.Hiyo ndiyo check and balance.
Ni katika hiyo check and balance ndipo rais atakapolazimika kuteua watendaji ambao baada ya kuthibitishwa si wake tena, watawajibika sehemu nyingine. Hii itatoa nafasi za umakini katika kupata viongozi na kumpa rais ''unafuu'' wa kuwaondoa kwani yeye hatahusika tena.
Hebu fikiria yaliyotokea bungeni ambapo PM alilazimika kuondoka na si kuondolewa na Rais
Lakini pia kumpunguzi madaraka kunalenga kuongeza ufanisi kwa Rais kwa kumpunguzi kazi zisizo za lazima na zingine zinazomtia katika kashfa. Kwanini Rais wa linchi likubwa kama Tanzania ahangaike na uteuzi wa wakurugenzi wa miji au bodi za mashirika na vyuo,kwa mfano.
Kwa ufupi kumpunguzia madaraka rais haina maana ya kumyang'anya nguvu za kiutawala bali kumpa nguvu za kiutawala kwa kuzingatia, sheria, taratibu na maadili.Ni kumpa uwezo wa kufanya mambo ya kitaifa zaidi, kumwepusha na migongano isiyo ya lazima na vyombo vingine hata wananchi.
Ni njia ya kumpa nafasi ya kuiangalia nchi kwa ujumla wake bila haya, kusimamia majukumu yake na wenzake kwa kutambua kuwa kuna watch dog. Na muhimu ni kumfanya atambue kuwa yeye ni mtumishi namba moja wa umma na wala si mtumikiwa namba moja.
Kupunguziwa madaraka kutazuia ''office abuse'' na kumfanya afikirie kwa umakini kila jambo linalogusa wananchi, rasilimali na usalama wao kila sekunde na dakika.
Hatuhitaji kiongozi tunahitaji uongozi na uongozi hautengenezwi na jeshi la mtu mmoja bali collective responsibility ya kila mmoja wetu katika nafasi yake.Endapo ni hivyo kwanini tuna woga wa kugawna madaraka ili tuwe na uongozi badala yake tunataka kumlundikia mtu mmoja ili tuwe na jeshi la mtu mmoja.
Hapo juu kuna kitu umekisema check and balance, na hasa ndio msingi wa hoja yangu.
Suala la madaraka ya rais linachukuliwa vibaya. Wale wanaodhani asipunguziwe madaraka wana hofu kuwa Rais anaweza kushindwa kufanya kazi zake kwa vile tu atakuwa amepokwa uwezo.
Kundi hilo linadhani rais ataondolewa kuwa Amir jeshi mkuu wa vyombo vya usalama au atapunguziwa nguvu kama alivyopunguziwa Gobachev na mwisho wa siku atakuwa powerless.
Kundi hili lina fear of unknown kwasababu tu limebaki kuangalia tulikotoka na limefungia macho twendako na dunia tuliyo nayo. Kuna nchi kama Turkey na nyingine nyingi tu uwezo wa rais unakuwa na mipaka hasa katika majeshi na vyombo vingine kama mahakama na haionekani kuwa tatizo zaidi.
Taifa letu linakua na hivyo lazima lipitie katika mabadiliko kulingana na nyakati.
Kuna wakati tuliaminishwa kuwa vyama vingi maana yake ni Rwanda genocide, Bosnia Hezegovina n.k.
Leo ni mwaka wa 20 hakuna tatizo lolote zaidi ya kuimarisha demokrasia kwa kiwango fulani.
Kundi la pili ambalo mimi ni mmoja wao ni lile linalotaka Rais apunguziwe madaraka.
Ukitazama kwa umakini, nchi yetu haina bunge au mahakama kama vyombo huru.
Bunge na mahakama ni matawi au ''jumuiya za serikali''.
Rais anaweza kuvunja bunge lililochaguliwa na wananchi, akamuondoa Jaji mkuu na kuweka ampendaye hata kwa emergency kama alivyofanya Mwai Kibaki.
Kumpunguzi madaraka nina maana ya kumwekea mipaka ya kazi yake na vyombo vya check and balance.
Leo Obama anafanya mabadiliko ya umiliki wa silaha wakati huo huo akiwa ameshapata ushauri wa kutosha kuhusu second ammendment kwasababu kinyume chake ni impeachment.
Kumpunguzi madaraka ni kuwa na serikali inayozingatia katiba, kufanya kazi kwa ushirikiano na vyombo vingine huku kila kimoja kikiwa watch dog ya kingine.Hiyo ndiyo check and balance.
Ni katika hiyo check and balance ndipo rais atakapolazimika kuteua watendaji ambao baada ya kuthibitishwa si wake tena, watawajibika sehemu nyingine. Hii itatoa nafasi za umakini katika kupata viongozi na kumpa rais ''unafuu'' wa kuwaondoa kwani yeye hatahusika tena.
Hebu fikiria yaliyotokea bungeni ambapo PM alilazimika kuondoka na si kuondolewa na Rais
Lakini pia kumpunguzi madaraka kunalenga kuongeza ufanisi kwa Rais kwa kumpunguzi kazi zisizo za lazima na zingine zinazomtia katika kashfa. Kwanini Rais wa linchi likubwa kama Tanzania ahangaike na uteuzi wa wakurugenzi wa miji au bodi za mashirika na vyuo,kwa mfano.
Kwa ufupi kumpunguzia madaraka rais haina maana ya kumyang'anya nguvu za kiutawala bali kumpa nguvu za kiutawala kwa kuzingatia, sheria, taratibu na maadili.Ni kumpa uwezo wa kufanya mambo ya kitaifa zaidi, kumwepusha na migongano isiyo ya lazima na vyombo vingine hata wananchi.
Ni njia ya kumpa nafasi ya kuiangalia nchi kwa ujumla wake bila haya, kusimamia majukumu yake na wenzake kwa kutambua kuwa kuna watch dog. Na muhimu ni kumfanya atambue kuwa yeye ni mtumishi namba moja wa umma na wala si mtumikiwa namba moja.
Kupunguziwa madaraka kutazuia ''office abuse'' na kumfanya afikirie kwa umakini kila jambo linalogusa wananchi, rasilimali na usalama wao kila sekunde na dakika.
Hatuhitaji kiongozi tunahitaji uongozi na uongozi hautengenezwi na jeshi la mtu mmoja bali collective responsibility ya kila mmoja wetu katika nafasi yake.Endapo ni hivyo kwanini tuna woga wa kugawna madaraka ili tuwe na uongozi badala yake tunataka kumlundikia mtu mmoja ili tuwe na jeshi la mtu mmoja.