Balozi Seif Ally Iddi; Leo kutakuwa na tamasha la taarabu kwa wageni waalikwa wa sherehe za mapinduzi.

Kwani taarabu wewe unaichukuliaje!??
 

Hiyo vidole juu ni morden taarabu na iko bara kule Zanzibar kuna taarabu asilia na ndio muziki wao

Ni kama ushangae rais wa Congo kusema kuna muziki wa rhumba kwa wageni
 
Hivi ile Televisheni ya Zanzibar ipo siku hizi?

Nakumbuka miaka ya themanini tulikuwa tunaangalia taarab TVZ.

Ni kitu tofauti kabisa na hii taarab ya mipasho ya siku hizi.

Taarab ya asili Zanzibar ni muziki wa kuheshimika sana. Na ndiyo maana hata sherehe kubwa kama hii watu wanataja taarab.

Huu ni kama muziki wa Zanzibar.

Nakumbuka mahojiano fulani alifanyiwa Dr. Salim Ahmed Salim, katika kumuonesha kuwa ni mtu anayependa asili yake, wakasema, licha ya kuzunguka dunia nzima, lakini muziki alioupenda zaidi ulikuwa taarab.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TVZ bado Hua inaonesha taarab isipokua kipindi kifupi si kama zamani, maana kwa sasa mambo ni mengi sana ya kureport kwa TV.
 
Hakuna burudani nyingine zaidi ya taarabu tena kwenye tukio kubwa la kitaifa Kama hili.
Taarab ndio utamaduni wao visiwani, kabla mimi na wewe hatujazaliwa.

Haya masuala ya kisasa hayana ulazima kuwa ni ya muhimu kwa wenyeji wa visiwa hivyo.
 
Nadhani ni vema ulivotoa huo ufafanuzi hapo.
Kuchambana ndio nini mkuu.?
 
Kwani kuna sehemu nilitaja ccm na cuf hapo mkuu.
 
Hiyo vidole juu ni morden taarabu na iko bara kule Zanzibar kuna taarabu asilia na ndio muziki wao

Ni kama ushangae rais wa Congo kusema kuna muziki wa rhumba kwa wageni
Kwani hiyo modern taarab ilianzia wapi mkuu hadi useme huko Zanzibar haipo.?
 
Nadhani ni vema ulivotoa huo ufafanuzi hapo.
Kuchambana ndio nini mkuu.?
Ahaa ! Kumchamba mtu ni pale wanawake hasa wa pwani kuenda kumsema mwenzao ambaye ni muongo au mfitini ili akome! Tendo hili hufanywa mbele ya halaiki au kadamnasi ya watu. Wakati mwingine wachambaji hupendelea kuvaa nguo aina ya dira sare sare na kibwebwe kiunoni ili kukoleza mambo ! Mchambwaji Hua hapewi hata nafasi ya kujitetea na anaweza kusingwa vile vile. Inasemekana kabila la wazaramo ndio wataalam wa kuchamba maana huweza kumchamba mwenzao mpaka akazimia bila hata kuguswa! 😁 Nadhani nimefafanua vya kutosha.😎
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…