Balozi wa Israel ashusha nondo Mkutano wa UN; akata ngebe zote

Kabla ya kufikiria hvyo ww uliwahi kufanya unyama wa wazi kwa hao watu tena wa makusudi.
Je wao wakiapa kulipiza kisasi kwako kuna makosa?
Hitler alipowaua wayahudi alikuwa analipiza unyama gani waliofanya
 
Hitler alipowaua wayahudi alikuwa analipiza unyama gani waliofanya
Mauaji ya Hitler kwa wayahudi isiwe justification ya kuhalalisha mauaji ya wayahudi kwa wapalestina.
Wayahudi wamefanya unyama sio tu kwa wapalestina bali Middle east nzima kimakusudi.
Je unatarajia watu wa mashariki ya kati watakosa kuweka kisasi?
Au unataka mauaji yake yahalalishwe kupitia kujificha nyuma ya mauaji ya Hitler?
 
Si halalishi wala sina ushbiki wake. Wanawathamini wapalestina na wayahudi kama wanadamu wenye Haki sawa mbele za Mungu na ulimwengu.
Kibinadamu kile kilifanywa Mauaji ya halaiki yenye lengo la kuwafuta ktk dunia, ujumlishe na Maneno ya Hamasi pia ya kuwafuta , inatosha wao kujihami zaidi.
Ni bora kujihami kwa gharama kuliko kuuawa kijinga.

Yote kwa yote wote ni waovu mbele za Mungu. Sema wengine wamezidiwa nguvu na maarifa na kuuawa zaidi kwa sasa
 
Ndugu sipingi unachoongea ila kma kweli unafuatilia siasa za mashariki ya kati utagundua unakosea sana kusema Israel ana haki ya kujilinda na utakosea sana kusema wote ni wadhambi mbele za Mungu.
Israel ilipoitwaa ardhi ya palestina haikuridhika ilijaribu kuchukua na maeneo mengine ikwemo Lebanon,Jordan na Syria kinguvu.
Haijatosha kuna maeneo Palestine wameamua kuufyata km Westbank lakini Israel bado akaeneza ubabe kwa kuwakataza Gaza kutumia ukanda wa bahari kwa namna yeyote ile.
Haijatosha kila siku wanawalazimisha Wapalestina waondoke ktk makazi yao walioishi miaka na miaka tena kimabavu na wanawatimua kwa marungu bila kujali wanampiga mzee au mama.
Kaka unatarajia watu watakaa kimya wakuangalie?
Mm najijua ni muislam ila hili suala silitizami kidini bali nalitizama kidiplomasia km wengine je hii ni haki!!?
Hamas anastahili kusema asemayo maana hawa watu hawafai kuonelewa huruma.
Ungeona zile picha za IDF wakifukia vichwa watoto wadogo wa kipalestina miaka ya 2006 kaka usingesema usemalo sasa.
 
Ni kweli. Tatizo hapa lililo kubwa ni hizi jumuiya ta kimataifa ambazo sijawahi kuzikubali maana zina egemea upande na kuwa na sura ya ukandamizaji.
Kama maeneo ya nchi moja yanakaliwa na nchi nyingine kwa nguvu eti kwa kuwa ina nguvu za kijeshi ni kosa la kimataifa.
Na ndipo unapijiuliza iweje UN ikiite kikundi cha wapigania uhuru wa watu wake MAGAIDI?(Hamas).
Huwa mjadala wa Mashariki sipendi utumike kidini kwa kuwa najua Mungu Muumbaji ni Mungu wa dunia yote, ni Mungu wa Mayahudi na Ni Mungu wa Wapalestina ni Mungu wa Kabila zote.
Ushabiki wa eti biblia inasema au msahafu hauna ukweli kwa maana Mungu anauita wote
 
Sina hakika lakini but nahisi kama unamshambulia mleta UZI wakati yeye kanukuu matamshi ya balozi wa Israel, ingawa pia nahisi mleta UZI kaongeza chumvi kwenye tafsiri yake (though sijasoma ya Kingereza but namna ya uletaji wake UZI kaongeza ongeza kidogo kachumbali ) so wa kulaumiwa hapa is either balozi na nchi yake ya Israel au HAMAS na wafuasi wao but sio mleta UZI, mleta UZI ni mjumbe na wote tunajua, mjumbe hauawi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…