Banda wa Simba SC nimemuona akicheza AFCON ya Cameroon, ila Diara wa Yanga SC namuona 'anaozea' Benchi tu. Kulikoni?

Banda wa Simba SC nimemuona akicheza AFCON ya Cameroon, ila Diara wa Yanga SC namuona 'anaozea' Benchi tu. Kulikoni?

Sasa kama Kipa Djigui Diara ( Yanga SC ) ni mdaka Mishale na kila Siku Magazeti ya Kinafiki ya Mwanaspoti na Championi yanajipendekeza Kumpamba ( Kumsifia ) mbona tokea aitwe na Mali huko AFCON ya Cameroon anaozea tu Benchi / Mkekani?

Cha Kushangaza yule Mchezaji Bora na asiyeimbwa na Magazeti ya Kinafiki Championi na Mwanaspoti Peter Banda ( Simba SC ) ndiyo ameweza Kucheza huko AFCON ya Cameroon na kuingarisha vyema Simba SC kwani kila alipokuwa na Mpira Watangazaji walikuwa wakisema anachezea Simba SC ya Tanzania.

Nina Rafiki yangu Mmoja wa Kikongo ( kutoka Congo DR ) huwa anatushangaa sana Watanzania kwa Kuwasifia na Kuwapamba Kutwa akina Mayele, Moloko, Makambo, Bangala, Djuma, Mukoko na huyu Mbovu wa Juzi Ushindi wakati Wote hawa huko Kwao Congo DR ni 'Makapi' tupu na hata tukisikia wanaitwa Timu ya Taifa ni kujaza tu Idadi ila huishia Mkekani ( Benchini ) tu Kuchoma Mahindi.

Hata hivyo Mchezaji pekee huko Kwao Congo DR anaimbwa sana, ameshapata mpaka Tuzo kadhaa katika Ligi Kuu ya Congo DR na kwamba hata hapa Simba SC alipo saaa anapita zake njia kwani muda wowote anaelekea zake Ulaya ( hasa Ufaransa, Uhispania na Ubelgiji ) ni Beki Henock Inonga peke yake na ndiyo Mkongo anayejua Mpira kati ya Wachezaji wote wa Kikongo walioko hapa Kwetu Tanzania.
Kamusoko wa Yanga hukumuona? Hata hivyo screen protector yupo reserved kucheza mechi ya final ambako huyo joyce banda hawezi kufika
 
Leta fact zako na sio porojo na hadithi za abunwasi apa muwe mnawaadaa na kuwadanganya wasiopenda kujishughulisha kutafuta details, jibu hoja izo moja baada ya nyingine kama kweli unachokiongea kina mashiko!
umeumia sana 😂
 
Mchezaji wao wa kuitwa Kanoute ni Mali ila hata kuitwa haitwi ila makolo hayasemi. Au huyu Sakho kama ni bora kwa Nini haitwi huko senegal
mada inazungumzia diarra tuliedanganywa atatitangaza ligi yetu kule AFCON na sio hao maan hawakuitwa
 
Djigui Diarra wa Yanga ni chaguo la Tatu ktk safu ya makipa timu ya taifa ya Mali

1. Ibrahim Mounkoro ( Tp Mazembe)
2. Diawarra ( FF Malmo- Sweden)
3. Diarra

Mounkoro amedaka mechi zote tatu afcon na ana clean sheet mechi mbili

Mechi alizocheza Diarra kwa mwaka jana 2021 ( full time goal keeping)

Algeria vs Mali (1-0) 06.06.2021
Guinea vs Mali (1-0) 24.03.2021
Mali vs Morocco ( 0-2) 07.02.2021
Mali vs Guinea (1-0) 03.02.2021

Hivyo kwa mechi hizo Diarra mechi ya mwisho kucheza ilikuwa tar 06.06.2021 dhidi ya Algeria ambapo ilikuwa kabla hajasajiliwa kuja Yanga

Kwa maana hio kitendo cha yeye kuja Yanga ambayo haishiriki michuano yoyote mikubwa barani África na wala haina mafanikio yoyote ktk ngazi ya kimataifa ni kama imeshusha CV yake kwa kiasi kikubwa ndio maana amedrop kutoka chaguo la kwanza mpaka la tatu

Na kwa mwenendo huo basi inawezekana akajikuta siku za mbeleni hata kuitwa timu ya Taifa ikawa baba Jeni bye bye
OKAY
 
[emoji94].... Djigui Diara aliondoka akiacha Simba ina point 24

Anarudi anakuta Simba ina point 25

Anajiuliza Ligi ilisimama au???!![emoji848][emoji848][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Back
Top Bottom