Bandari inauzwa kwa waarabu, Gesi LNG inauzwa kwa uingereza, Mbowe, Lissu, Zitto mko wapi kupaza sauti?

Stuka

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
282
Reaction score
906
Tumesikia ishu ya bandari kuuziwa mwarabu, mradi wa LNG nao mkataba wake haueleweki wa namna Tanzania itakavyonufaika, barabara ya kibaha moro dodoma kuendeshwa na mwekezaji na kulipiwa tozo kila ukipita, madudu yote yanaendelea lakini Zitto, MBowe na Lissu wako kimya kupaza sauti kuhusu ishu hizi.

watanzania watetewa na nani? maana bunge la kijani kama mlivyosikia wenyewe yanayoendelea bungeni.
 
Tuanze na wazalendo waliotukuka waliopo pale bungeni je wanasemaje?
 
Mwendo kukimbizwa vifungu kwa kasi za mwendo kasi🏃🏃
 
Ndio tujifunze uzalendo. Hakuna mwekezaji anakuja kwa lengo la kukufaidisha wewe. Kila mtu anaangalia maslahi yake, ukiweza kupata maslahi yako ndani ya maslahi yake siyo mbaya.

Ila hii kwangu inadhihirisha kuwa Afrika ni masikini kwasababu hatuna akili. Tunastahili kutawaliwa na kuibiwa tu. Mabeberu wanatuhadaa na haki za binadamu na haki za mtu mweusi lakini moyoni wanatuona sisi ng'ombe tu.

Yaani hata mwarabu na mchina wameshaanza kuwa 'mabeberu' wapya 🤣🤣. Tutatawaliwa milele.
 
Watanzania ni watu wa hovyo sana, kwahiyo hadi Lissu awasemee?
 
2020 mlipokuwa mnakata mauno kwenye kampeni za magufuli mlikuwa hamjui haya yatatokea?, Mkishatoka kwenye chaguzi ndio lawama zote mnazidondoshea kwa Lissu na Mbowe?. Lissu na Mbowe Kama mnanisoma endeleeni kulamba asali ili watz tujitambue na tuanzishe wenyewe harakati za kudai haki.
 
Stuka,
Ungeandika hivi:

''Bandari inauzwa kwa Waarabu, Gesi LNG inauzwa kwa Waingereza.''

 
Inaonekana ama una IQ below average, auupeo wakoni dunizana kiasi kwamba hata unachosikia huelewi maana yake.

Weka efforts za kujifunza ilo angalao uwe hata na ule uelewa wa kawaida.
 
Wamsema Mh Mnowe na wenzake, na wewe umefanya nini? Ni wajibu wa kila mmoja wetu kupaza sauti sio kumsakizia akina Mbowe peke yake nawe umekaa tu
 
Wewe ni mtu wa ovyo angalia baraza la mawaziri nani ni waziri mpya?watu ni wale wa zamani Magufuli aliwakuta
Hata sijakuelewa. Yaani unakataa kuwa bunge hili halikuwekwa pale na Ngosha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…