Bandari inauzwa kwa waarabu, Gesi LNG inauzwa kwa uingereza, Mbowe, Lissu, Zitto mko wapi kupaza sauti?

Mikataba imeandikwa kwa kiingereza, watakaoisemea bungeni ni Kibajaji, Jah People na Dr. Musukuma
 
Wamekurupuka kutumia helcopter kufanya mikutano ya hadhara walidhani Bilioni mbili nyingi Sasa zimekata wamerudi ufipa kimyaa😂😂😂
 
Zitto, MBowe na Lissu wako kimya kupaza sauti kuhusu ishu hizi.
Yaani Watanzania zaidi ya million sitini hawa tu uliowataja ndiyo wanaweza kupaza sauti kutushinda? Kweli? Weka hoja inayojitosheleza uone kama sauti hazitoki!
 
Kwani Mbowe na Lissu ni wabunge? lazima kila mtu akipate cha moto
 
Si tulishangilia .!!
 
Watanzania hatua waliyofikia sasa hawahitaji tena mwanasiasa wa upinzani kuwatetea wanajitetea wenyewe
 
Hata sijakuelewa. Yaani unakataa kuwa bunge hili halikuwekwa pale na Ngosha!
Miaka yote wabunge wa ccm ndio huwa wengi pale bungeni na wakitaka kupitisha lao hakuna wa kuzuia.
 
Sema ww Kwan lazima wapaza sauti wawe hao uliowataja? Ukikosa percent ndo unaleta kelele
Hao wamejipa kazi ya kuwasea wananchi kuna wengine tunawasifia kwa kukataa kununuliwa kwa sababu ya kuwatetea wananchi, hivyo hiyo ni kazi yao.
 
acha uongo wewe
 
Walishasema sana mpaka na kuwekwa gerezani. Mlichukua maamuzi Gani. Ndio maana sikuhizi naona Mbowe na Zito wanaakili kuungana nao kulamba asali baada ya misoto mingi
 
Ukipaza sauti wewe inatosha
 
Walishasema sana mpaka na kuwekwa gerezani. Mlichukua maamuzi Gani. Ndio maana sikuhizi naona Mbowe na Zito wanaakili kuungana nao kulamba asali baada ya misoto mingi
Wao kuwekwa gerezani ndio kipimo cha kuwa walisema sana?
 
Mkataba Kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya DPW ya Emirates Dubai umeacha maswali mengi na kuamsha hisia za kudai Katiba mpya kwa nguvu zote.

Ni mkataba ambao ulisainiwa kwa mwendokasi bila kuchukua tahadhari juu ya madhara yake yaliyo dhahiri. Mkataba huu haukubaliki kwa sababu nyingi Sana.

Moja , ni mkataba wa milele kwa sababu hauna ukomo. Najua wapo waliosema ni wa miaka 100 na wapo waliosema ni wa miezi 12.

Hawa wote sijui wametoa wapi huo muda wa mkataba. Ibara ya 23 ya mkataba na randama zake (appendixes) zake hakuna popote zinaonyesha mkataba huu ni wa muda gani. Hii inaweza kutafsiriwa kuwa ni mkataba wa kudumu.

Ni kweli unaweza kuwa miaka mia lakini pia hakuna Cha kuzuia uwe wa miaka 1000.

Pili, mkataba huu unanguvu kuliko Sheria za Tanzania pamoja na Sheria za kimataifa (Takes precedent over national and international law)

Mathalani Ibara 23( 4) hairuhusu kuvunja mkataba huu hata pakiwa na ukiukwaji mkubwa (material breach) au kukitokea hali inayopelekea mkataba usitekelezeke (fundamental change of circumstances) ambalo ni Takwa la mkataba wa kimataifa uitwao Vienna Convention on the Law of Treaties,1969 ambao Tanzania imejifunga nao.

Sasa hii tafsiri yake ni kwamba baada ya kusaini mkataba huu hata Dubai wakikiuka kabisa hatuwezi kujitoa. Hicho ni kitu Cha ajabu mno dunia itatushangaa.


Mbaya zaidi mkataba hausemi je una nafuu ili mbadala ukiachilia mbali kuvunja mkataba.

Kifungu Cha 23( 4) kinaenda mbali zaidi na kusema ikitokea sababu yeyote inayotambulika kwenye Sheria za kimataifa ya kupelekea kuvunja mkataba bado mkataba huu hautavunjwa.Tafsiri yake ni kwamba tumeingia kwenye shimo ambalo halina pa kutokea( coup de sac) .

Tatu, mawanda (scope) ya mkataba pia ni mapana, ni Kama hayana ukomo. Ibara ya 2(1) itaruhusu muwekezaji kujenga na kuendesha miradi ya bandari za Bahari na maziwa yote.

Mkataba unakwenda mbali zaidi hata kwenye kile kinachoitwa (logistic parks na trade corridors) ambazo bahati mbaya hazijatafisiriwa kwenye mkataba.

Kwa namna mkataba huu ulivyo sisi tutakuwa tumepoteza udhibiti wa bandari zote za bahari na maziwa yote.

Mkataba ungeweka wazi ni bandari zipi hasa kwa sababu kwa namna ya Sasa hata usalama wa nchi unaweza kuwekwa rehani.

Nne, mkataba hausemi sisi tutapata nini( consideration) kwa maana ya faida za mradi. Je sisi tutakusanya Kodi tu? Au tutakuwa wabia?

Tano , mkataba hauonyeshi nafasi ya mamlaka ya bandari( TPA) ni ipi katika uendeshaji wa mkataba. Kumbuka kwa mujibu wa sheria TPA ndo chombo chenye mamlaka ya kuendesha bandari zote. Sasa je mkataba huu umefuta sheria hiyo? Kwa mamlaka gani?

Mkataba hauelezei kuhusu usalama wa mapato yetu bandarini na nafasi ya vyombo vya ulinzi na usalama kwaajiri ya usalama wa nchi yetu hasa kwenye marine.

Nafasi pekee ya TPA kwa mujibu ya randama ya kwanza imeachiwa kuendesha na kusimamia " DHOW AND WHARF TERMINAL" ya bandari ya Dar es Salaam.


Sita, pamoja na kuweka kipengele Cha local content ili kunufaisha wazawa kwenye ajira na manunuzi kwenye ibara 13( 2) ibara hiyo haina maana yoyote Kwanza kwa sababu haiweki wazi kwamba threshold ya wazawa kwenye ajira itakuwaje.

Pili hata procurement( manunuzi) ya vitu au items au huduma zinazopatikana ndani hailindwi na mkataba kwa sababu kwa mujibu wa ibara ya 6(2) ya mkataba huu serikali yetu hauruhusiwi kufanya usumbufu wowote (interference) yoyote hata kwenye manunuzi yanayokiuka Sheria isipokuwa tu Kama yanahatarisha usalama( safety and security).

Sasa je wakiamua kuagiza mbao Dubai wakati hapa nchini zipo utawazuia kwa kigezo Cha usalama?

Saba, mkataba hausemi nani atawajibika kulipa fidia yoyote inayotokana na utekelezaji wa mradi pamoja na watumishi ambao ajira zao zinaweza athiriwa na mradi.

Nane , pamoja na kwamba ibara ya 26 ya mkataba inaelekea kuruhusu reservation utagundua kwa namna ibara ya 24 ilivyo imepoka kwa mkono mwingine haki ya reservation iliyopo kwenye ibara ya 26 hivyo sioni uwezekano wa nchi yetu kufanya reservation kwenye makubaliano bila kukwaza mkataba.

Kwa namna ya mkataba huu tukifanya reservation Sasa ivi inaweza kupelekea nchi iingie kwenye mgogoro wa kukiuka mkataba.

Tisa, hata kuridhiwa kwa mkataba huu na Bunge tayari umefanyika nje ya muda.

Ibara ya 25(2) ilitaka mkataba uridhiwe ndani ya siku 30 tu na leo ni zaidi ya miezi Saba.

Kumi, kwa mujibu wa ibara ya 8(3) (c ) mkataba huu ni kama unatoa umiliki wa ardhi kwa mwekezaji kinyume na Sheria ya ardhi.

Kwa mujibu wa sheria ya Ardhu Sura ya 113 Kampuni ya kigeni hairuhusiwi kumiliki ardhi Tanzania.

Tulitegemea mkataba useme ardhi zitakuwa chini ya TPA au mamlaka nyingine za serikali na wao watapata derivative rights badala ya kuwapa ardhi kwa mgongo wa lease hold.
 
Kama hamjaelewa kaeni kimya. Kama ni mikata ya kinyonyaji walishasema sana no support ya wananchi Sasa mnatakaje.
Unadhani kupata support ya wanananchi ni kwa kusema tu kama wafanyavyo?
 
Unadhani kupata support ya wanananchi ni kwa kusema tu kama wafanyavyo?
Basi tunavichwa vizito. Uzuri mlishawapumbaza wananchi hata wakiambiwa hawasikii. Sawa na mlivyokuwa mnawarubuni eti wananchi hawali Katiba wanachohitaji ni chakula, Shule, Barabara, maji
 
Basi tunavichwa vizito. Uzuri mlishawapumbaza wananchi hata wakiambiwa hawasikii. Sawa na mlivyokuwa mnawarubuni eti wananchi hawali Katiba wanachohitaji ni chakula, Shule, Barabara, maji
Ndio uhalisia huo na ndio maana wanaweza kusema hivyo, wananchi hawana uwelewa hata na katiba iliyopo sasa hivi ndio utasema hao watu wanataka mpya? Hivyo hawarubuniwi, cha msingi inahitajika juhudi ya kuwaelimisha ili waelewe na kuanza kutoa hiyo support.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…