Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,252
- 36,513
DRC wakishaondoka bandari ya Dar tutapata majibu yake kwa ongezeko la wigo wa kodi ili kufidia pengo la makusanyo ya bandari.Nawasalimu kwa jina la JMT,bila shaka mnaendelea kuchapa Kazi..
Kama inavyosomeka kwenye kichwa cha habari,Bandari ya Mombasa imetoa Ofa kabambe na kedekede Kwa Mizigo ya Congo DRC kupitia kwao, Kifurishi cha Ofa kinahusisha mambo yafuatayo;
1.Kupunguza gharama za kuhifadhi mizigo.
2.Kufuta gharama na vikwazo visivyo vya kikodi barabarani.
3.Kuwapa eneo Ili wajenge Dryport yao Ili wawe wanahifadhia mizigo yao hapo.
4.Ofa zingine za ki institutions.
Naomba ikumbukwe kwamba Bandari ya Dar inategemea zaidi mizigo ya Congo DRC kwa mapato sasa kwa Ofa hizi ni wazi bandari ya Dar inaenda kuwa tembo mweupe.
Ni vyema serikali kupitia TPA nao wakaja na counter offensive za kukabili ushindani wa kibiashara na kuongeza competitiveness yetu kwenye biashara ya logistics.
Tanzania inaongoza kwa kuwa na utitiri wa Kodi na tozo kwenye biashara bila kusahau utitiri wa vikwazo visivyo vya Kodi NTBs kama mamizani kila sehemu,traffic kila sehemu,sijui parking za malori za Halmashauri na blaa blaa zingine kama hizo.
Tukiendelea hivi bandari yetu itakuwa tembo mweupe na ikumbukwe kwamba hakuna kosa Wakenya Wamefanya ila ni mbinu za kukuza biashara.
Source> Uchumi Forum👇
View attachment 2357571View attachment 2357576View attachment 2357577
Namshauri Rutto apunguze kodi ya mapato kufikia hata 49% off ataona namna makamouni makubwa yatakavhoenda kuwekeza pale Kenya.
Sisi tuendelee na upumbavu wetu wa kuwakamua wananchi bila huruma hadi tukome