KERO Barabara za Pemba ni nyembamba, vyombo vya usafiri vimeongezeka, imekuwa kero na hatari pia

KERO Barabara za Pemba ni nyembamba, vyombo vya usafiri vimeongezeka, imekuwa kero na hatari pia

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

MeVSMe

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2024
Posts
270
Reaction score
425
IMG_20241106_161337_809.jpg
Kuna ajali ilitokea jana maeneo ya Kanambe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazi Pemba, gari la fuso ambalo lilikuwa limebeba mchanga liliachia njia na kuanguka.

Kuna mtu mmoja alipoteza maisha kati ya 10 ambao walikuwa vibarua waliokuwa wamebebwa ndani ya Fuso hilo, wengine wakipata majeraha mbalimbali.

Dereva naye ni mmoja alibanwa miguu ilibidi jitahada za ziada zifanyike kutolewa kwani alikuwa amebanwa kwenye Skani.

Nimeanza na mfano huo kwa kuwa hiyo ni mara ya pili gari kama hilo la kupata ajali ndani ya mwezi mmoja.

Pamoja na vyanzo kudaiwa kuwa ni kupasuka kwa mipira lakini kuna haja ya Serikali kuboresha barabara za Pemba kwa kuzitanua.
WhatsApp Image 2024-11-06 at 14.30.23_140f2363.jpg

WhatsApp Image 2024-11-06 at 14.30.24_6360e00a.jpg
Wananchi wa Pemba tumekuwa tukiishi kwa hofu kutokana na ongezeko la Vyombo vya moto hasa magari, madereva pia wamekuwa hawaendeshi kistaarabu.

Hatari zaidi ni magari makubwa, yakiendeshwa ovyo inakuwa hatari zaidi kwa kuwa shida ni wembamba wa Barabara

Ukiachana na vyombo vya moto, pia kuna Wanyama na Watu wanaopita kando ya Barabara, hali hiyo inafanya mazingira kuwa magumu zaidi.
 
Kuna ajali ilitokea jana maeneo ya Kanambe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazi Pemba, gari la fuso ambalo lilikuwa limebeba mchanga liliachia njia na kuanguka.

Kuna mtu mmoja alipoteza maisha kati ya 10 ambao walikuwa vibarua waliokuwa wamebebwa ndani ya Fuso hilo, wengine wakipata majeraha mbalimbali.

Dereva naye ni mmoja alibanwa miguu ilibidi jitahada za ziada zifanyike kutolewa kwani alikuwa amebanwa kwenye Skani.

Nimeanza na mfano huo kwa kuwa hiyo ni mara ya pili gari kama hilo la kupata ajali ndani ya mwezi mmoja, yote yakiwa ya kampuni moja ya “Irisi”.

Pamoja na vyanzo kudaiwa kuwa ni kupasuka kwa mipira lakini kuna haja ya Serikali kuboresha barabara za Pemba kwa kuzitanua.
Wananchi wa Pemba tumekuwa tukiishi kwa hofu kutokana na ongezeko la Vyombo vya moto hasa magari, madereva pia wamekuwa hawaendeshi kistaarabu.

Hatari zaidi ni magari makubwa, yakiendeshwa ovyo inakuwa hatari zaidi kwa kuwa shida ni wembamba wa Barabara

Ukiachana na vyombo vya moto, pia kuna Wanyama na Watu wanaopita kando ya Barabara, hali hiyo inafanya mazingira kuwa magumu zaidi.
Tembeleeni kwenye maji, halafu mambo ya zenjiberi sisi watanganyika yanatuhusu nini? ninyi si mnasemaga sisi vyogo hamtupendi. au ndio gia kutaka kuchota mihela ya Tanganyika mjengee hiyo wilaya yenu kwa sababu rais ni mtu wenu.
 
Kwa sasa mmekamata kote bara na visiwani. Mnashindwa nini kuzifanya ziwe za njia sita kama China?
 
Hivi Pemba mtu unaishije nilienda kikazi miezi mitatu aisee kama miaka 3..
 
Yaaan mnataka ziwe vipi an....
Huko pemba nasikia kila kitu ni chembamba tuu

Au ngoja aongee huyu mvuna asali DIVISHENI FOO
 
Tembeleeni kwenye maji, halafu mambo ya zenjiberi sisi watanganyika yanatuhusu nini? ninyi si mnasemaga sisi vyogo hamtupendi. au ndio gia kutaka kuchota mihela ya Tanganyika mjengee hiyo wilaya yenu kwa sababu rais ni mtu wenu.
Heee, Sasa mbona ubguzi huo
 
Back
Top Bottom