Baraza la Sanaa limfungie Bambo kazi zake. Anaharibu sana Kiswahili kwa makusudi

Bambo ni msanii tena mzuri sana ni mbunifu kwa hicho anachofanya hakuna mwingine mwenye ubunifu huo alionao ni wa pekeyake

Katika kizazi chetu ametulea akiwa mchekeshaji mahiri sana

Naomba comment yako kwa wenye shida ya L badala ya r na r badala ya L
Nafikiri ni wazaramo na wakuria
Lakini watu wa mwanza wana matamshi ya aina yao pia
Na hawa ndiyo wako serious achana na huyo Bambo ambaye anaigiza


Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Unaweza kuwa sahihi ila hao basata waanze kwanza na wale wasanii wako unaowasifia sana maana wanaimba matusi tu
 
aonywe au kufungiwa kwa kosa lipi?
huyo muanzisha uzi ni mtoto wa mama jobless promax
Nimeelewa concern yake ya kutumia kiswahili ndivyo sivyo, japo sijui kama ni kosa kisheria, however likiwa kosa adhabu haitakiwi kuwa kufungiwa, akifungiwa sisi kama taifa tunapata nini?
 
Samehe bure, hao ndio wasanii wa kimasikini
Huwa wanatokwa povu mdomoni hata hawafuti

Na kuna mwingine alikuwa mpaka makamasi ila anaona ni usanii
 
Acha kumsagii kunguno!!
 
Halafu ndio huyu MTANASHATI? . Vuruga tu hilo jina hapo. Utanashati ni kipengele mkuu. Kuanzia kuongea,ni mdogo mdogo kwa mpangilio tena point tupu. Tembea yako,sio unavuruga vuruga tu. Usikimbie kimbie. Mavazi pia. Ukiwa serikalini usile rushwa,usifisadi hata kidogo. Wabunge wenzio wanapotaka kujiongezea mishahara,wakati wananchi wana hali ngumu,mbali ya kupangua hiyo hoja,inatakiwa wewe uikatae kwako hiyo nyongeza. Utanashati ni kipengele,sio bure bure kama hivi.
 
Dah yaani mkuu unamuonea wivu mtu kama bambo
 
Tatizo liko kwa wanaofuatilia ujinga wake.
 
Chai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…