Barbershop girls pose a new threat to marriage

Kuna ukweli ktk hili!!

Wakati wa scrubbing (uso) huwa balaa ila unakuwa mvumilivu tu.

Swala hili hata kina mama linawakumba maana wanasema "wanaume wa kikongo wataalam sana" kwenye kuosha nywele (wana massage kichwa hadi raha), pedicure na manicure.

Mitego ipo kila mahali kinachotakiwa kwa men and women ni kujiheshimu na kumheshimu kama uko kwenye mahusiano!

Tafuta saloon ambayo wanatoa huduma bora lakini wanaheshimu kazi (as profession) yao na wateja wao pia.
 
Kwa walio Dar hebu jaribuni Hash barbershop Sinza opp. na Corner Bar utajua kinadada wa scrub ndio wanaoibeba biashara.
 

sa si ungemaliza tu, mtu anakulegezea kabisa?

 
Vipi kuhusu maradhi hamjafikiria na hizo scrub zenu? maana vitaulo tunachangia na mikono ya wadada pia?

I suggest this should be intervened!
 

Natafuta investors wa kuja kuanzisha HOOTERS!
Itakuwa the first HOOTERS in Africa. Sasa sijui itakuwaje hapo mjini?
 
Mimi nikisha nyolewa sitaki mbembwe naondoka, hao akina dada nikitaka kwa huruma nawapa hela ya soda( ni kawaida yangu hata kutoa kwa omba omba). Sana sana siendi saloon hizo zenye mbembwe, I am very conservetive/yaani enzi ya ujima, mpaka mke wangu wakati fulani anashangaa tofauti na elimu na kazi yangu.
 

penye nyekundu pamekaa vizuri
 
kama mtu ni mhuni ni mhuni tu na mwungwana ni mwungwana.siku hizi madem wanajirahisisha kwa wanaume sijui maisha magumu au ni laana.mtu mstarabu hata akienda salon si lazima atoke na mhudumu tatizo nadhani ni tabia za mtu tu

this is well said, nakubaliana na wewe mkuu
 


hii imenifanya nicheke!!!
 
Seto huyu Mkuu Kituko alimaliza ila kaamua kuminya details nyingine.


Mkuu BAK,
Nilikemea mkuu, unajua hivi vitu vipo kabisa yaani unakuwa tempted kabisa, kwa sasa nipo mwangalifu sana na hivi vitu, yaani hawa na Bar maid ni kundi moja, mora Bar Maid unaanza kutamanika kwa mbali, lakini hawa wanakugusa kabisa ni balaa kubwa
 


Hahahahahahaha sema kweli Mkuu Kituko LOL! mtoto kaumbwa kaumbika mikono yake laini kama vile ana ngozi ya mtoto...hukumalizana naye kweli? au ulikufa na tai yako shingoni?

 
Vipi kuhusu maradhi hamjafikiria na hizo scrub zenu? maana vitaulo tunachangia na mikono ya wadada pia?

I suggest this should be intervened!

Mpasuajipu there is more than this haya unayoyaangalia hata kwenye mazingira mengine unakutana nayo
 

Mimi naenda huko kukata nywele tu, hayo mengine siyajui na nikiambiwa kuwa nahitaji huwa nakataa haata wanaponiambia bei haiongezeki. Siku ya kwanza baada ya mwanaume kunikata nywele akaondoka bila kuondoa kile kitambaa wala nywele, kazi hiyo ikafanywa na mdada ambaye baadae aliniambia twende akanioshe kichwa (sasa sijui ni kilichokatwa nywele au kile kingine!) - nilimwambia nitaoshea nyumbani - hii inataka commitment kwenye ndoa yako tu. Mbona salon za wanawake kuna midume na vitanda vya kupumzikia?
 
Hili suala la sehemu za kujikwatua na kutanashitika zina athari siyo tu kwa ndoa bali hata kiafya.

Kuhusu athari katika ndoa, binafsi nadhani kila mahali kuna athari kama tutaangalia kwa undani.Ni mtu binafsi kujihadhari na mitego.Mara nyingi mchezo mchezo mtu hujikuta kwenye hatari.Kuanzia majumbani kuna wale wadada wasaidizi tumesikia nao huhatarisha ndoa, ukienda maofisini nako usiseme, kwenye sehemu za starehe nako si haba. Hata mitandaoni nako hivyo hivyo .Kwa hiyo hakuna palipo salama.Usalama utapatikana ahera peke yake.

Tukija kwenye suala la usafi, kwanza kitu ambacho nimekiona kwenye hizo barber shops - hao wanaofanya " facial scrub" hawana hata moja walijualo kwenye ufanyaji facial scrub.Ukitaka "facial" yauhakika nenda kwenye saloon zenye specialisation hii na huwa ni ghali siyo bei chee kam humo kwenye barber shops maana hii ni taaluma inayokaribiana na tiba kama siyo tiba.Inatakiwa isomewe ili mtu ajue hasa anafanya nini na kuzingatia taratibu za afya ya ngozi na mambo mengine kama mzio nk.kitu cha kusikitisha sana utaona hata mataulo wanayotumia wanayarudia na hata kufua hayafuliwi. Ukizingatia kuwa wanaume hunyolewa ndevu na wengine wana mapele na huenda mikwaruzo, mtu haoni anajihatarishia afya yake.Yuko radhi aka enjoy hizo huduma za kushikwa masikioni nk.

Kingine ni handling ya products za scrub.Kitaalamu au kiafya, haipaswi kuingiza vidole kuchota ile scrub bali inatakiwa ichotwe ama na spatula au kijiko maana ni kama uji fulani ambao huweza kuzalisha bacteria.Sasa mtu anapoingiza vidole tena ambavyo siyo sterile humo, bacteria wanajizalisha kwa wingi na matokeo yake huweza kuambukiza magonjwa. Yako mengi sana kwenye hii ishu lakini kwa leo naishia hapo.

Tip:
Ushauri kwa wale wasiokuwa na agenda tofauti zaidi ya kutaka usafi wa ngozi ya uso, nenda supermarket au duka la vipodozi, nunua products za ku scrub na ziko za kila aina - bei huanzia 3500/- hadi 30,000/= kutegemeana na unataka nini. Unapooga au kunawa uso, tumia . Au mwambie mkeo/ mpenzi wako akutengenezee home-made - changanya unga wa ulezi au hata oats na maziwa , sugua uso wako na kisha osha kwa maji ya uvuguvugu.Waweza pia kutumia limao au ndimu kutakatisha uso wako.
 

Haya uliyoyasema WOS kwangu mimi kuna saloon moja tu Bongo ambayo ndiyo inayoyazingatia
 
WoS.. nimepata wazo.. inabidi upatiwe kajukwaa kakutoa elimu hii ya maisha (life skills) maana nadhani hapa kuna wengi tunaweza kufaidika katika weledi wako. Kumbe ndio maana unaitwa "wa Substance".. halafu ulikuwaga na ile signature yako moja hivi ya mwanzoni.. naikumbuka kumbuka hivi..
 

Mzee halafu sijui kwanini mtu ukimaliza kunyoa ukawaambia sifanyi hizo scrub wala usinioshe nitaenda nyumbani kuoga wanakuwa wanakasirika kweli huwa sielewi ni kwanini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…