Barrick na Tanzania waunda Kampuni ya ubia iitwayo Twiga Minerals na Serikali itamiliki asilimia 16

Umejuaje kama tumeuziwa mbuzi kwenye gunia?
Nilitegemea utatoa ufafanuzi kivipi hiyo 84/16 na 50/50 haiko sawa.

Kwani Hesabu zina hitaji Siasa ?.Ni vigumu kugawana Faida sawa kwa sawa halafu Hisa zisiwe sawa kwa sawa.Mimi nitoe Millioni 100 kwenye Mtaji na wewe uchanhie Millioni 20 halafu kwenye Faida itakayo patikana tugawane sawa kwa sawa kweli ?

Kiasi cha Hisa za Mtu ndio huwa zinaamua wingi/uchahe wa gawio.
 
Mkuu soma post ya 23 ya uzi huu usipoelewa unalako jambo.

Nimeshasoma hiyo ' post ' yako #23 ila mbona nimeona umeandika tu Upuuzi kama si Utumbo mtupu? Una Elimu gani Kwanza kwani hata Hoja zako zote ulizoziweka hapo naona ni za ' Kitoto ' mno huku Wewe mwenyewe ukijiona ni kama vile umeshusha Nondo za maana wakati si kweli. Ningekuelewa kama ungesema kuwa kote kote huko kungekuwa na 50 / 50 na si vinginevyo na hapa kataa kubali kuna Kitu Watanzania ' tunafichwa ' au tumeshaingizwa ' Chaka ' vile vile.
 
Hapo kuna mtego unaweza ukaambiwa ili faida ianze kupatikana ni after 20 yrs
 
Tumeambiwa kuwa serikali inamiliki hisa 16 na mabeberu watamiliki hisa 84 lakini wakasema faida itakuwa 50/50! Kama ni hivyo kwa nini na hisa zisiwe 50/50? Nahisi kuna kitu hakiko wazi naomba kama kuna mtu mwenye ufafanuzi wa hili anisaidie

Utawezaje kujua mambo yako sawa au si sawa iwapo Rais Magufuli ameshindwa kufanya mikataba ya maliasili hii kuwa wazi?

Si bado inasainiwa gizani?

Hebu tujiulize, Mzee wa "HAPA KAZI TU" (Pombe) anasifiwa katika eneo hili kwa kufanya kitu gani hasa kipya ambacho hakikuwepo tangu enzi za mzee wa "UBINAFISISHAJI" (Mkapa) na kupokelewa na mwenzake mzee wa "ARI MPYA, KASI MPYA na NGUVU MPYA" (Kikwete) walichosahau kukifanya kama mkakati wao kuiba na kuiuza nchi kwa mikataba ya kisheria ya kimataifa??

Hizi awamu za CCM chini ya MKAPA (1995 - 2005) na KIKWETE (2005 - 2015) ndizo zilizosaini mikataba za kuiuza nchi hii rasmi......!!

Na tusidanganywe na mtu awaye yeyote kwa sababu mikataba hii masharti yake ni IRREVERSIBLE in anyway.....!!

Mikataba hii ina masharti ya mbele kwa mbele mpaka ukomo wake and not otherwise......

Labda kinachoweza kufanyika si kuivunja ama kuitengua bali kuyaomba majamaa kukaa nayo tena chini na ili ingalau wakubali kulegeza baadhi ya "clause" ili ingalau na sisi kama nchi tuambulie kitu kidogo....

Hakuna wa kubadilisha haya mambo, si Magufuli na hata akiingia ZITO KABWE na ACT yake ama TUNDU LISSU na CHADEMA yake.....

Absolutely, they all can't reverse anything.....!!

However, there is way forward to get through these problem by minimizing its consequences.....

MOSI; kilicho ndani ya uwezo wetu kama nchi ni kuwachukulia HATUA KALI wote kuanzia Mkapa & Co, Kikwete & Co na sasa Magufuli & Co ambao kwa TAMAA ZAO MBAYA waliiuza nchi yetu kwa vipande vya fedha.....

MBILI; Tusiingie mikataba mingine tena kwa mtindo waliotumia hawa wenzetu wasio WAZALENDO wa KWELI wa nchi hii mpaka kwa pamoja tukae chini na kurekebisha makosa haya.....

Hii ifanyike baada ya wale waliofanya makosa haya kwa makusudi kuwa Magerezani kwanza....

TATU; michakato yote ya mikataba ihusuyo uvunaji wa maliasili zetu iwe wazi (ingalau ipitie bungeni) kuanzia hatua ya negotiation hadi utiaji saini na implementation yake hatua kwa hatua......

NNE; Kufanyike mabadiliko makubwa ya KIKATIBA na KISHERIA kwa kuhakikisha kwamba mamlaka ya usimamizi wa rasrimali za nchi yanakuwa mikononi mwa wananchi wenyewe kupitia vyombo vyao vya uwakilishi na kamwe asiachiwe mtu mmoja aitwaye "Rais" ama "Waziri mwenye dhamana" bila ya kuwa na "checks" ili kuamua kwa niaba yetu....

TANO; mwekezaji yeyote ambaye atashindwa kukubaliana na utaratibu wetu juu ya mali yetu wenyewe, atupishe na maliasili yetu kama ni madini, wanyama, ardhi itabaki vivyo hivyo huku sisi wenyewe tukijenga uwezo wa kuivuna.....!!

SASA SWALI NI HILI;

Rais Magufuli Pombe amefanya hata moja tu kati ya hayo hapo juu??

Kwangu mimi sioni mwanga wowote, sioni na kwa kweli hakuna mabadiliko yoyote......!

Still mambo bado ni "business as usual??"

Ni kwa sababu CCM ni ileile yenye watu (kina John Pombe Magufuli, Change Andrew & Co) wenye vichwa na akili zilezile zilizotengeneza matatizo haya....!

Kwa hiyo ni ngumu sana ama haiwezekani kabisa mtu aliyetengeneza tatizo, akalilea kwa karibu miaka 69 umtegemee huyohuyo atatue tatizo hilo...

IMPOSSIBLE....!!!
 
usanii mtupu. the good thing kwao ni kuwa wewe mdanganyika you have no access to those contracts.
 
Unapoandika tumeuziwa mbuzi kwenye gunia maana yake una uhakika... Wenzako hua wanaandika "tetesi" hujachelewa unaweza kubadili kichwa cha habari.
Vijana wa Zitto mnafundishwa kutukana tu
na wewe haujachelewa kutengeneza fake ID maana hiyo verified account inakufanya ushindwe kujiamini unaishia kujibaraguza kwa watawala.
 
Hapo kuna mtego unaweza ukaambiwa ili faida ianze kupatikana ni after 20 yrs

Hahahaaa hapo pia kunahitaji maelezo.
Kwa kawaida ya makampuni yakisha breakeven wanaanza kulipa Cooporate tax 30% na kwa Acacia/barrick walishabreakeven na kuanza kulipa hiyo 30%, je kwa kuanzisha kampuni mpya TWIGA ngoma inarudi kuanza upya?
 
Hahahaaa hapo pia kunahitaji maelezo.
Kwa kawaida ya makampuni yakisha breakeven wanaanza kulipa Cooporate tax 30% na kwa Acacia/barrick walishabreakeven na kuanza kulipa hiyo 30%, je kwa kuanzisha kampuni mpya TWIGA ngoma inarudi kuanza upya?
mabeberu hawakuwahi kuwa stupid mbele ya wakoloni weusi. never anywhere.
 
Poa, ila kuwa mstarabu, unajidhalilisha kwa kutumia lugha hiyo.
 
Tumeambiwa kuwa serikali inamiliki hisa 16 na mabeberu watamiliki hisa 84 lakini wakasema faida itakuwa 50/50! Kama ni hivyo kwa nini na hisa zisiwe 50/50? Nahisi kuna kitu hakiko wazi naomba kama kuna mtu mwenye ufafanuzi wa hili anisaidie

16% ni shares ambazo unapata dividend kila mwaka kutokana na kampuni inavyofanya kazi share hizi zitakuwa kwenye stock exchange ya Dar es salaam (DSE) na London (LSE) mtu yeyote ananunua kwa uwezo wake. Kama ikipatikana faida unapata hizo asilimia 16 za hiyo faida, wenzetu wanaita dividends. 50/50 ni asilimia ya faida ya kampuni inayofanya kazi i.e ijiendesha kwa faida, hakuna kampuni inayofanya kazi bila faida. Management yake yote kama kampuni inapata faida wanalipwa mishahara minono. Huko lazima wawepo Watanzania vile vile wafaidi hiyo mishahara na marupurupu mengine then faida ya kutoka huko mnagawana 50/50.
 
Soma post ya 23 ya uzi huu.

Mkuu kwenye hiyo post yako unayowaambia watu wasome hakuna ufafanuzi unaoeleweka tena zipo sehemu ambazo zinaonyesha huna uelewa na historia ya hili jambo..

Kabla ya huu mkataba mpya Tanzania ilikuwa inalipwa mrahaba kiasi gani??? na Kodi nyinginezo zilikuwage?? Tulipokwenda kwenye majadiliano demand zetu zilikuwa ni nini?? na nini tumeachieve??

Unafahamu kuwa Barrick sio kampuni mpya Tanzania na hiyo grace period unayoiongelea ilishaisha siku nyingi na ndio maana mrahaba na mengineyo vililipwa?
 
At least watu wangekuwa wanatoa hoja kama hizi kuliko kumshambulia mtoa post
 
Hizi hoja ndiyo zinatakiwa sasa siyo wale wanaomshambulia mleta post
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…