Barrick vs Tanzania: Tukubali tu kwamba tumezidiwa ujanja na Wazungu

Barrick vs Tanzania: Tukubali tu kwamba tumezidiwa ujanja na Wazungu

Kweli wewe ni vuvuzela huchelewi kubadirisha gia angani!!

Ni kipi cha kunifanya nibadilishe gia angani? Ww kilichokufanya uone huo mkataba ni mnono sana ni hiyo sanaa ya utiaji saini kwakuwa ilifanyika mbele ya TV, lakini hujui chochote kilichopo kwenye huo mkataba, ni sawa tu na ile mikataba ya mwanzo iliyosainiwa huko nje. Kama ni maelezo ya huo mkataba hayana tofauti na ile mikataba ya zamani ambayo walioisaini ndio waliosema sifa ya hiyo mikataba na hakuna hata mmoja tuliuona kwa macho kama huu. Hebu nipe ufafanuzi wa shares 16% kisha faida 50/50, hizo sifa ziko ukurasa wa ngapi na ngapi? Kwa bahati mbaya ama nzuri mimi sio mwepesi wa hivyo.
 
Asilimia hizo ni share holding, ie 16% ya shares zote za Barrick na wao Barick wanamiliki 84%.(In actual fact hizo 84% wanaweza wasizimiliki wao Barrick kwa sababu kila mtu ana uhuru wa kununua shares kwenye stock exchange worldwide ie From Hong Kong, Tokyo, Melbourne, London, Paris, New York au Toronto etc. Kampuni huwa na shares 100 percent ambazo zinajulikana, sifahamu Barrick wana kiasi gani cha shares, usichanganye number of shares na percentage. (FYI shares za Barrick ni worldwide wana chimba Gold kila mahali ulimwenguni na makadirio yao kipato kinachopatikana Tanzania ni kama 16% ya value ya Barrick worldwide, that is why Twinga wapo 50-50 percentagewise. Natumaini unaweza kuwa umeambulia kitu.

1. Unaongele 16% out of 100% Tanzania capital investment Au

2. Unataka kutuambia 16% of 100% Worldwide capital investment?

Hebu rudia kusoma halafu niambie kwa usahihi unamanisha A au B
 
Sasa in actual fact hizo share 84 ni lazima watazinunua na kuzimiliki wao Barick.
Sasa tusidanganyane kwamba mtu mwenye share 16 % atapata mapato sawa na mtu anayemiliki 84 %
kwahiyo kipi bora hapo, hii 16% tutakayopata sasa au 0% ya zamani?
 
Hapa vipi? "...kinachopatikana Tanzania ni kama 16% ya value ya Barrick worldwide, that is why Twinga wapo 50-50 percentagewise. Natumaini unaweza kuwa umeambulia kitu."

Are you sure?
 
Naomba kuuliza na kufahamishwa yafuatayo mkuu..

84% Barrick na 16% TZG mwisho wa siku wanatengeneza kampuni inaitwa Twiga. Twiga ikisajiliwa DSE hisa zitakazouzwa ni 84% za Barrick? au hizi 16% za TZG.

Kule LSE au NYSE na masoko mengine ya hisa duniani itasajiliwa TWIGA au Barrick na shares zipi zitauzwa 84% au 16% ?

Moja ya Asset za Barrick kwa sasa ni 84% shares za Kwenye kampuni ya Twiga, Kampuni ya Twiga itakuwa inamiliki migodi mitatu ambayo Barrick anamiliki 84%, Nani atakuwa na sauti ya maamuzi?, nani atakuwa anaendesha daily operations na daily spares and other requirements purchase??

Tumeambiwa Twiga itakuwa ikitoa ajira kwa Wazawa sawa, Je ni ajira zipi ambazo Twiga itazitoa na hapo zamani Barrick na Acacia walikuwa hawazitoi??.

Kilio kikubwa cha Wazawa waliokuwa wakifanya kazi kwenye hii migodi ilikuwa ni malipo madogo waliyolipwa kulinganisha na waliyokuwa wakilipwa Wazungu na foreigners wengine, JE TWIGA ITAWALIPA WAZAWA HAWA MALIPO KAMA WANAYOLIPWA WAZUNGU NA STAHIKI NYINGINE?

Twiga sasa itakuwa ikishiriki kwenye kusaidia jamii, Ni nani atakuwa na jukumu hili kati ya mwenye 84% na 16% na ni huduma zipi na kwa kiwango kipi kuliko zilizotolewa mwanzo?..
Hayo maswali hatuwezi kukujibia tafuta muda wako tafuta mkataba upo wazi online ujifungue chumbani usome ujijibu mwenyew hatuwezi kukutafunia wakatu kila kitu kipo wazi
 
Ujuaji umekuzidi mpaka Umli
Unapotosha Vibendera na wapuuzi wenzie unajiona mjanja kumbe mpuuzi tu.
Kupata kidogo nibora zaidi kuliko kukosa
Watu wenye kujitambua hili watalipongeza

Acha kupanick, kama mlitarajia kupata sifa za kisiasa kuweni wapole, maana sio kila mtu anasifia tu. Kwani hiyo mikataba ya zamani kilio ilikuwa ni kukosa kabisa au ilikuwa ni kupata kiduchu? Je hii mikataba ya sasa iko wazi au ni ya kificho kama ile ya zamani?
 
Hayo maswali hatuwezi kukujibia tafuta muda wako tafuta mkataba upo wazi online ujifungue chumbani usome ujijibu mwenyew hatuwezi kukutafunia wakatu kila kitu kipo wazi

Huo mkataba uko wazi kwenye link ipi? Iweke hapa.
 
1. Hakuna kubadili sheria ya madini mpaka Barrick waondoke nchini.

2. Hakuna kuishtaki Barrick mahakama za ndani.

3. Barrick haitajisajili ndani ya DSE.

4. Hakuna Mtanzania atakayeweza kununua hisa kwenye kampuni.

5. Serikali itapata share ya net profit na net loss kwa 50%.

Kwa mkataba huu tumepakatwa na hatuna pa kutokea uzalendo kweli ndio huu?

Kabudi Mungu anakuona
simba jike na ukali wake lakini bado anapakatwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikiri kwanza, kwamba mimi sio mwanasheria. Halafu swali langu ni kuhusu ufafanuzi wa jumla wa sheria zetu.
Swali: Hivi kama kisheria ardhi ya Tanzania ni mali ya Serikali, madini yaliyomo ardhini pamoja na gesi, mafuta nk ni mali ya Serikali pia au sivyo?
Kama ni mali yetu mbona sijasikia yakitajwa kuwa mtaji wetu katika mikataba ya ubia na wawekezaji?
Pili; Nini kinafanyika mwekezaji mpya anapopewa eneo la kutafuta na kuchimba madini anamilikishwa ardhi tu au na madini yaliyomo?

Nauliza hivi kwasababu kwa sheria za nchi Mtanzania anaruhusiwa kumiliki ardhi tu lakini sio madini yaliyomo ardhini kwake. Serikali nayo haisemi wazi kama inamiliki ardhi na madini! Lakini tunaambiwa sisi ni matajiri!
Utajiri wetu ni upi kama haturuhusiwi kumiliki ardhi na madini yaliyomo ardhini?
Halafu Serikali nayo inapompa mwekezaji mpya eneo la kutafuta na kuchimba madini, inasarenda ardhi na hayo madini jumla jumla kwa mwekezaji au vipi?

Maoni yangu:
Sera yetu ya umiliki wa ardhi kwa sisi wananchi inatunyima fursa za kuitumia ardhi kikamilifu kama mtaji.
Tumpe mwananchi 'free hold' ili itambulike kwamba ardhi na kilichomo ni mali yake.
Vinginevyo Mtanzania atabaki masikini milele wakati nchi yake ni "TAJIRI" masikini.

Unaweza "kumiliki ardhi" na majumba ya kifahari Tanzania lakini siku yoyote unaweza kupokonywa na Serikali kwa kisingizio cha 'eminent domain' na kuishia kupewa fidia ya majengo au mazao yako tu, sio ardhi!
Tafsiri yake ni kama vile ardhi haina thamani, ambayo sio kweli.
Ardhi ina thamani, iwe mjini au kijijini, iwe na madini au haina.

Tukiendelea na sera ya kinafiki kwamba ardhi haina thamani tunaitangazia dunia umasikini wa Watanzania.

Haya ni MAONI yangu tu. Kuna watu ukitoa maoni wanasema umewapinga kwahiyo ni adui yao! Binadamu gani asiye na maoni?
Maendeleo yatakujaje kama hamtaki kusikiliza MAONI ya wenzenu?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi huwa ninapinga matendo mengi ya huyu Mtawala wa Awamu ya Tano.

Lakini katika Hili la Barick kwa kiasi flani tumefanikiwa kama nchi ukilinganisha na ilivyokua huko kabla.

Hata Kuanzishwa kwa Hiyo Kampuni ya Pamoja (Twiga) ni hatua muhimu ambapo Serikali imepewa offer ya hisa 16%.


Na hili la 50/50% profit and loss sharing si baya tukidhibiti usimamizi kuna nyakati tutapata faida nzuri tu lakini zipo nyakati tutakosa endapo BARICK hatazalisha faida which is normal katika biashara yoyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hayo maswali hatuwezi kukujibia tafuta muda wako tafuta mkataba upo wazi online ujifungue chumbani usome ujijibu mwenyew hatuwezi kukutafunia wakatu kila kitu kipo wazi

Mkuu samahani naomba link ulipo huwa mkataba nikausome, pia bila shaka utakuwa umeandikwa kiswahili ili na sisi tusiojua kiEnglish tukausome..
 
Ili mradi maccm ndo yanaendelea kua madarakani tuendelee kusubiri maumivu zaidiiii......NI USANII TU SASA MIAKA MINNE YA RAIS MZALENDO YEYE ANAJENGA CHATTEL TUUUU
 
Ninakushukuru sana kwa kutoa elimu nzuri kwa mleta mada lakini naomba uelewe kuwa tatizo la wengi hapa Jamiiforums wanadhani wanajua wakati hawajui. Wengine wanadhani mambo ya siasa ni sawa na ushabiki wa vyama vya michezo kama simba na yanga!

Mtu anayedhani anajua wakati hajui ni vigumu sana kuelimishwa na kuelimika!
Kwani hiyo mikataba ya zamani nayo ilisainiwa na watu wenye elimu ya ngumbaro??

Nadhani ilikuwa ni serikali ya ccm awamu ya 3, leo anakuja ccm awamu ya 5 anasema kulikuwa na mikataba ya hovyo, wala hatuoni Mkapa na watu wake wakipelekwa mahakamani kwa mikataba ya hovyo...mnatuchanganya mjue ninyi ma ccm!!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi unakuwaje na ubia wa usawa wakati unamiliki asilimia 16 na mwenzako 84
Afu eti faida mgawane 50%by 50%..??logically sioni uhalisia,labda huyu mwenye. Share 16 kuna misamaha au favor flan atatoa kwa mwenye share 84.
 
Kwani ndg, kabudi aliwahi kukuchukulia mkeo, mbona unamuandama kwa hoja Dhaifu kabisaa... Mkuu siku hizi Threads zako unayumba Sana. Kalekebishe hizo antena zilizoyumba Kama inawezekana.
Waliosaini mkataba wa 3% ni viongozi wa chama kipi?
Mwaka 1991 Lisu aliwekwa ndani na serikali ya CCM akiwa anapinga hiyo 3%. Alikuwa anataka mapato ya madini yagawanywe 50 kwa 50. Alipigwa sana na akasekwa ndani.
Acheni ufala wenu
CCM wana akili ndogo kama za kuku.

Hawana kumbukumbu hata za miaka miwili nyuma.

Tuchukue mfano wa miezi kadhaa nyuma, kwamba mwenyekiti wao aliutangazia uma kwamba hakuna mtu atakayekosa mawasiliano kwa kukosa kusajili laini yake kwa alama za vidole, baadae waziri wa mambo ya ndani akarejea msimamo wa mwenyekiti wake.

Leo watu hawajakosa mawasiliano kwa msimamo ulio kinyume na maneno ya mwenyekiti wao?

Ukiwasikiliza hawa watu ni lazima uchanganyikiwe, kwa sababu ccm hawajitbui, wako kama jamii ya kambale, kila limoja linasifiwa kwa kumiliki misharubu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom