Barua ya Adam Malima kumpinga Spika!

Barua ya Adam Malima kumpinga Spika!

Status
Not open for further replies.
NUNGWI usisahau kuangalia CELTEL INTERUNIVERSITIES COMP. jumapili ijayo 8/4 ni MZUMBE UNIVERSITY vs MAKERERE UNIVERSITY.....juzi nilisikia aibu wakati watoto wadogo zanzibar univ walipokua wanapelekana na wazee wazima MLIMANI,pamoja na mlimani kushinda walipelekwa pelekwa sana!!!!!
 
Mswahili,

Naona una kaugonjwa fulani kanaitwa MAPENZI. Kweli kama alivyosema Mwanakijiji na mimi najiuliza maswali zaidi ya 100 kuhusu maandishi yako. Kama kuna wazushi basi sidhani kama kuna namba moja zaidi yako. Soma between the lines uelewe na uache ulevi wa kupenda. Cheki mtiririko wa elimu utaona kwenye website ya bunge haikupangwa vizuri au hamna A level. Cheki wakati anaingia BOT alikuwa na elimu gani...

Mimi sina muda wa malumbano yasiyo na kichwa wala miguu, kwani kwangu mimi Mbowe, Mrema, Malima, Mnyika, Kichunguu, Murangira, wewe na JK ni raia wema tu wa nchi hii na ninaheshimu michango yenu na fikira zetu, kwani kila mmoja amechagua njia anayo ONA ni sahihi kusaidia waTanzania.

Asante

FD
 
Au umekuwa kama Nungwi??!!!!!! Naona una Nungwi 2🙂

Nungwi nisalimie Hilary Lubengo hapo IDM Mzumbe.

FD
 
Quote:
Originally Posted by Ogah
Nakumbuka nikisoma Physics kulikuwa kuna kitu kinaitwa SI Unit, Nungwi ni SI Unit ya kuchemsha, siku hizi ukichemsha tu , samahani nitatumia SI Unit Nungwi kupima hoja.

Nungwi is too childish and disgusting

Then Quoting Kichunguu:

1 Nungwi (Ngw) is the quantity of stupidity in 1000 mature people who have lost 63.3% or (1-exp(-1)) of their reasoning power. The level of stupidity in a normal person is between 2 to 10 microNungwis and it is normally unnoticeable. People start showing abnormal behavior when their stupidity level reaches abot 100 microNungwis and it becames alarming when it reaches 1 milliNungwi. It is advised to stay away from whoever records stupidity level of above 1 milliNungwi. Sporadically people with stupidity levels of up to 1 full Nungwi have been observed but they are very rare, appearing once in about 100 years per continent.
__________________
Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo
 
Mzeee MMJ,

Heshima mbele mkuu, nimekusikia kuwa wewe sio Kichuguuuu.

Ahsante kwa kuniweka sawa kwa hilo, na tuendelee na ishu!
 
Mzee ES,

Shukran kwa maelezo yako murua.

Paragraph ya kwanza ya maelezo yako unathibitisha nilichokuambia mapema kuwa ndani kesi mama, Mh Ndesamburo ameibua kesi nyingine ya madai ya rushwa. Nafurahi kuwa umekubaliana na hilo.

Napingana na wewe unaposema kesi YOTE ( kwa maana kesi mama Malima Vs Mengi na Mengi Vs Malima) kuwa imepelekwa PCB. Uhitaji kufikiri sana kwenye hili kabla hujagundua kuwa unachosema si sahihi kwa sababu kama kesi mama imepelekwa PCB then kwanini Spika aseme kuwa wataijadili tena bungeni?

Nadhani unafahamu kuwa mjadala ukiwa bungeni hauwezi tena kuwa unajadiliwa na chombo kingine pembeni same as kunapokuwa na kesi mahakamani. Hata hivyo nimenukuu hapo chini uamuzi wa spika kukupa mwanga zaidi:

8.10 Tuhuma za “Wabunge kupewa rushwa” ni nzito na ukizingatia kuwa zimetolewa na Mbunge mtu mzima na mzoefu, haziwezi kupuuzwa hata kidogo. Kutokana na sababu hiyo, na kwa kuzingatia ukweli kuwa, kupokea au kutoa rushwa ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria za nchi;

8.11 Na kwa kuwa, kwa kosa la jinai Wabunge hatuna kinga yoyote, na kwa kuwa kuna chombo mahsusi cha kisheria cha kushughulikia uchunguzi wa rushwa, niliamua kumwagiza Katibu wa Bunge awasiliane kwa maandishi, na Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti Rushwa (TAKURU) ili uchunguzi ufanywe kubaini ukweli, na hatimaye kuachia sheria ichukue mkondo wake.

8.12 Katibu wa Bunge aliandika barua tarehe 26 Januari, 2007 kukabidhi suala hili kwa TAKURU. Aidha, kwa nakala ya barua hiyo, Mhe. Ndesamburo amehimizwa kutoa ushirikiano kwa TAKURU, ili ukweli kamili ufahamike.

8.13 Aidha, nimemwagiza Katibu wa Bunge anipatie ushauri kamili wa uhalali au vinginevyo, wa Mhe. Ndesamburo akiwa mjumbe wa Kamati ya Bunge, kufanya mawasiliano yasiyo rasmi na mmoja wa wanaochunguzwa wakati uchunguzi unaendelea.

8.14 Ingewezekana kuiagiza Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kufuatilia jambo hili, lakini nimeona si hekima kufanya hivyo kwa sasa. Nachelea kuchukua hatua zozote ambazo zitaonekana kumwekea vipingamizi Mhe. Ndesamburo, hasa kwa sababau tuhuma za rushwa anazielekeza kwa Waheshimiwa Wabunge wenzake.

Ndugu yangu ES nadhani hapo nadhani tume elewana.

Naungana na wachangiaji wengine kuwa Spika ama kwa makusudi au kwa kupitiwa amevurunda kwenye suala hili. Tumejikuta sasa tunazunguka ktk circle bunge, kamati, bunge kwa gharama za walala hoi.


Mungu Ibariki Tanzania
 
Jamani mimi naomba msaada kuhusiana na suala hili.

Tunaambiwa kuwa bunge litajadili tena suala hili tena maswali yangu ni;

1. Je wanarudi kujadili ripoti ya kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge ya Mh Juma N'hunga? au

2. Wanarudi kujadili ripoti ya rulling ya Mh Sitta? au

3. Wanarudi kujadili ripoti ya Dissenting views ya Mh Anne Kilango? au

4. Au wanarudi kujadili ripoti ya Dissenting views ya Mh Ole Sendeka?


Bila ya kusahau kiporo cha mzee Ndesa! mbona kazi mwaka huu!
 
ITV sasa kurusha vikao vya Bunge

Mbali na kuonyesha vipindi vya Bunge, pia ITV na Radio One, imeruhusiwa kuonyeshwa nchi nzima kutokana na serikali kuridhishwa na utendaji wake.

Naye Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Joe Bendera, aliipongeza ITV kuwepo Tanzania kutokana na vipindi vyake kuwa bora zaidi na hali hiyo inatokana na wafanyakazi wako kujituma,Vyombo vyako na wewe mwenyewe umechangia kwa kiasi kikubwa kuelimisha jamii kuhusu mageuzi wakati yanaanza kuingia nchini.

Hali hiyo imesaidia Taifa na Watanzania kwa ujumla kutoingia katika kipindi kigumu ambacho kingesababishwa na mageuzi hayo,� alisema Kapteni John Komba.


Unatoa ajira nyingi sana kwa Watanzania... Ni jinsi gani ulivyokuwa na uchungu na nchi yako na Watanzania wenzako. Nilitegemea wakati tunatembelea kwenye ofisi zote tukute Wazungu, lakini ni Watanzania wenzetu tupu,� alisema Amina Chifupa.
 
Hii ina maana gani? why now? au ndio ku- water-down mambo?

Kama awali walikuwa na wasiwasi nae kurusha matangazo ya moja kwa moja, wasiwasi huo ulitokana na nini?. Mbona Star Tv ni kituo kigeni lakini kimeaminiwa kurusha matangazo moja kwa moja? au ndio Diallo?

Kuna kitu kinapikwa hapa...
 
katika ako kakipande ulichoweka mimi napongeza kauli ya mhe chifupa ni kweli itv na radio one imejitahidi kutoa ajira kwa watanzania wengi,nawapa hongera
 
something is very wrong kwenye Bunge letu, I mean very wrong!!

- Wakati watu wanalalamika na Richmond na matatizo ya umeme, waheshimiwa wetu walikaa kimya na kufyata mkia hata kujadili hawakutaka! Sasa umeme umeshaanza kupatikana na watu wameanza kusahau ati wao wanataka kujadili Richmond!! What the f!!!!

- Wakati mikataba ya madini inaingiwa na watu wakapiga kelele na kuhoji waheshimiwa wetu walikaa kimya, leo hii ati na wenyewe wako kwenye bandwagon la kuhoji ilikuwaje? Miongoni mwa wabunge ambao wataonesha kushangazwa na mikataba hiyo ni Andrew Chenge! what the f...!

- Suala la Malima limegeuka kuwa kubwa na la Kikatiba kwa sababu Spika hakufanya kile ambacho alipaswa kufanya na baadaye akaamua kutumia mitishamba ya "busara" zake ili kunyamazisha jambo hili. Watu waliposema ripoti ijadiliwe Bungeni aligoma na kusema yeye ndiye Spika!! Leo hii maji yamefika shingoni ati sasa watalizungumza suala hili Bungeni, what the f...!

- Hivi hawa wabunge wetu wanakunywaga ulanzi kwenye vikao? Haiwezekani watu walioapishwa kulinda Katiba ya Nchi wanasita sita kutekeleza jukumu lao!!
 
ebu wana-jf nisaidieni kuondoa mashaka yangu,kwa wale walioko london nasikia manji ana bonge la hekalu na kama siyo hekalu basi ni villa hapo katika jiji la londoni,ingawa jiji ni kubwa lakini mnaweza kufahamu ukweli wa hoja hii na nasikia wakuu karibu wote ndani ya serikali walikuwa ama wanafikia kwenye hilo jumba je ni kweli ? baada ya hapo nitaingia katika kuchangia
 
Mwanakijiji

Unjaua niliposema kuwa you can do better than that ni kutokana na heshima yako na chombo chako cha habari ambacho kina umaarufu mkubwa tuu.

Lakini tatizo ni pale unapotegemewa kuwa impartial na kuweza kujenga arguments ambazo zinaangalia both sides of the issue lakini of recently umekuwa huji na hoja bali umekuwa overwhelmingly biased hoja zako mwanzoni wakati hii thread ilipoanza ulisema kuwa MALIMA KAAJIRIWA NA MANJI. I mean how do you expect watu wakuchukulie serious na chombo chako cha Habari kama na wewe unarukia bandwagon ya kusema jambo bila ya kuwa na uhakika nalo?

Dont get me wrong inawezekana ni kutokana na frustrations lakini kila mtu yuko frustrated lakini kwa status yako katika jamiii we expected more of you instead of coming up with unsubstantiated claim ambazo zimepelekea wewe kuonekana kuwa umekuja na narrow range of debate

That said, ningependa ku clarify kuwa SIJAKULAUMU KUWEKA HII BARUA humu bali hiyo bandwagoning yako inanitisha
 
Mwanakijiji umenikuna na posting yako kuhusu wabunge.

Hawa wazee wanatupeleka mperampera sasa. Hivi suala la Malima na Mengi linapewa nafasi kubwa ktk bunge letu ambalo halina meno ya kujadili Richmond.

Hivi kweli mjadala kama huu kama ungekuwa kwenye Richmond au rada tungeshajua mbivu na mbichi! Inavyo elekea kuna cover up hapa ktk ku - divert attention. Na kwa CCM wao ndio mabingwa wa hizo.

Haya na sisi ktk Forum tumekuwa bandwagon busy na Malima V Mengi badala mambo ya maana kwa taifa.

I think we can do better than this...

Mimi najiondoa rasmi kwenye upuuzi huu hamtaniona kwenye hili tena. Dhamira yangu inanisuta, kuna mengi yanayo husu taifa kama RVF, Umeme, nk tutaonana huko nyie kaeni na kanyaboya mliyowekewa na CCM hii kuficha madhambi yao
 
Kama haijawa shared. Sina interest ni kupashana taarifa tu. Lakini kama kuna maswali ya kikanuni nitajaribu kujibu.




na Mwandishi Wetu




UAMUZI wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta kujaribu kumaliza mzozo kati ya Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima (CCM) na mfanyabiashara maarufu, Reginald Mengi, sasa umeingia hatua mpya inayoweza kukigharimu Chama Cha Mapinduzi.


Hali hiyo kwa kiwango kikubwa imesababishwa na uamuzi wa Malima ambaye ndiye aliyeanzisha mzozo huo, kumshitaki Sitta kwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, hatua ambayo tayari wachunguzi wa mambo wanaiona kuwa ni jitihada za kujaribu kumdhibiti Spika huyo wa Bunge.


Hatua hiyo ya Malima kuamua kuwakwepa Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Edward Lowassa ambaye ni Waziri Mkuu na Katibu wa Wabunge wa CCM, Ali Ameir Mohammed, imeanza kutafsiriwa kuwa na lengo lililojificha la kumhujumu Sitta, ambaye mwenendo wake unaonekana dhahiri kuwakera baadhi ya vigogo ndani ya chama hicho tawala.


Aidha, uamuzi wa Malima kuamua kumshitaki Sitta nje ya utaratibu na kanuni za Bunge, nao umesababisha kuibuka kwa maswali mengi miongoni mwa wabunge, ambao baadhi yao wameshaanza kukiona kitendo hicho kuwa ni cha kulidhalilisha Bunge kimamlaka (Contempt of Parliament).


Wabunge kadhaa wa CCM na wale wa upinzani, waliozungumza na gazeti hili kwa wiki nzima sasa, wamekuwa wakieleza kushangazwa kwao na hatua hiyo ya Malima, ambayo wengi wao wanasema inatiwa nguvu ya kuwapo kwa shinikizo kutoka kwa kiongozi mmoja wa juu serikalini.


“Tumeshangazwa na hatua hiyo ya Malima, ambayo kimsingi ni ‘Contempt of Parliament’ na tunachokitarajia sasa ni kuona mbunge huyo akiitwa mbele ya Kamati ya Haki Maadili na Madaraka ya Bunge ili ahojiwe sababu za kufanya hivyo,” alisema mmoja wa wabunge hao.


Wakati wabunge hao wakieleza kushangazwa na hatua hiyo, wanasema wamekuwa wakifuatilia kwa karibu maamuzi ya viongozi wakuu wawili, ambao ni sehemu ya Bunge, Rais Jakaya Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Taifa wa CCM na Lowassa kwa mamlaka yake ya uenyekiti wa wabunge wa CCM.


Baadhi ya wabunge waliozungumza na Tanzania Daima wamesema kwamba, kati ya viongozi hao wakuu wawili, Lowassa ndiye atakayetakiwa kuwa mwangalifu zaidi katika kulishughulikia suala hili, kutokana na jina lake kuwa miongoni mwa watu wanaotajwa kuwa sehemu ya jambo lililomfikisha Malima kuchukua hatua hiyo.


Kumbukumbu zinaonyesha kwamba, katikati ya mzozo kati ya Mengi na Malima, jina la Lowassa liliwahi kutajwa na Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA).


Kutajwa kwa jina la Lowassa, kulikuja wakati shauri kati ya watu hao wawili lilipokuwa likishughulikiwa na Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.


Ndesamburo ambaye alikuwa mmoja wa wajumbe katika kamati hiyo, alitangaza kujitoa baada ya kudai kupata taarifa kutoka kwa Mengi zilizokuwa zikieleza kuwa, wajumbe takriban wote wa kamati hiyo ya Bunge walikuwa wamehongwa.


Mbunge huyo wa Moshi Mjini, ambaye alizungumza hayo mbele ya waandishi wa habari, alikaririwa akisema Mengi alikuwa amemweleza kuwa, taarifa za wana-kamati hao kuhongwa alikuwa amezipata kutoka kwa Lowassa.


Habari nyingine ambazo Tanzania Daima imezipata hivi karibuni kabisa kutoka miongoni mwa wabunge wengine zinaeleza kuwa, hatua ya sasa ya Malima imezusha mijadala mikali ya chini kwa chini kwa siku kadhaa sasa, ambayo baadhi ya mijadala hiyo inayataja majina ya viongozi wengine kadhaa kuhusika.


Mbunge mmoja kijana wa CCM aliyezungumza na Tanzania Daima kwa sharti la jina lake kutoandikwa gazetini, alisema tayari kundi la wabunge wengine wa chama hicho, wameshaanza kujiandaa kumlinda spika ambaye wanamwelezea kuwa mwanasiasa asiyewabagua wabunge.


“Sisi tunajua kabisa kuwa kile ambacho Sitta alikieleza mapema kabisa kuwa atakuwa ‘Spika wa Speed and Standard’ (Kasi na Viwango) kimekuwa ni kero kwa baadhi ya wana CCM ambao wanaiona hatua hiyo kuwa ni ya kujitafutia umaarufu na kwa kweli huo ndiyo msingi wa chuki dhidi yake,” alisema mbunge huyo.


Mbunge huyo alisema tangu habari zilipoanza kusambazwa kuwa Malima alikuwa amewasilisha barua ya malalamiko kwa Makamba kuhusu mzozo wake na Mengi, wabunge kadhaa wa chama hicho wamekuwa wakikutana ili kuweka msimamo wa pamoja kuhusu jambo hilo.


Kwa mujibu wa mbunge huyo, miongoni mwa maazimio waliyoyafikia ni kuhakikisha kuwa wanafanya kila linalowezekana kuhakikisha Bunge linaheshimiwa, na Spika anapata fursa ya kutimiza wajibu wake pasipo kutishwa na mtu yeyote.


“Sisi tumeshawishika kuamini kuwa Sitta anaonewa na watu wenye malengo binafsi ya kumharibia kazi na wanaotaka apoteze uhuru wake wa kimamlaka wa kuliendesha Bunge pasipo kuingiliwa. Tumejipanga kumlinda kwa hali yoyote na kuwa tayari kuwaangusha wale wenye nia mbaya naye,” alisema mbunge mwingine wa CCM anayetoka Kanda ya Ziwa.


Kundi la wabunge wa CCM linalojenga hoja za kuiua hoja hiyo ya Malima, limeorodhesha vifungu vya Katiba ya Jamhuri na kanuni za Bunge ambazo wanaamini kuwa wakizitumia, wataweza kuikwamisha ajenda ya siri ya Malima ya kummaliza Sitta kisiasa.


Habari kutoka ndani ya duru za wabunge wa CCM zinaeleza kuwa, moja ya vifungu walivyotumia ni sheria namba 3 ya mwaka 1988, iliyo katika Ibara ya 24 (D) ambayo inapinga kuhojiwa kwa mamlaka ya Spika na chombo kingine chochote nje ya Bunge.


Aidha wabunge hao wamepanga pia kutumia kanuni namba 60 ya Bunge iliyo katika toleo la mwaka 2004 ambayo pia inatoa mamlaka kwa maamuzi ya Bunge kutohojiwa na chombo kingine cha nje.


Walipoulizwa sababu hasa za kufikia hatua hiyo, wabunge hao walisema taarifa walizonazo zilikuwa zikionyesha kuundwa kwa mtandao mpya ndani ya mtandao wa wana CCM wenye lengo la kuhakikisha Sitta anawekwa katika mazingira magumu kabisa kikazi.


Wabunge hao ambao walifikia hatua ya kuwataja kwa majina baadhi ya viongozi wa CCM na serikali walio nyuma ya sakata zima la Mengi na Malima, walisema kumekuwa na mahusiano mabaya kikazi kati ya Sitta na baadhi ya viongozi serikalini.


Katika mazingira ya kutatanisha, tangu Ndesamburo atoe tuhuma nzito za rushwa ambazo sasa zimewasilishwa katika Taasisi ya Kupambana na Rushwa (Takuru) si Lowassa wala Mengi waliowahi kujitokeza hadharani kutoa kauli.


Hatua hiyo wakati fulani ilisababisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilazimike kumwandikia barua Waziri Mkuu, Lowassa kikimtaka atoe tamko kuhusu kuhusishwa kwenye tuhuma za rushwa kwa wajumbe wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge zilizotolewa na Ndesamburo.


Barua ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Wilbroad Slaa ya Januari 15, 2007, ilieleza kushangazwa na ukimya wa Lowassa pamoja na tuhuma hizo nzito zilizotolewa na Ndesamburo.


Jitihada za gazeti hili kuwasiliana ama na Lowassa mwenyewe au mwandishi wake wa habari, Said Nguba wakati huo ili kupata maoni yake kuhusu suala hili ziligonga ukuta.


Hata hivyo, ofisa mmoja wa juu serikalini, aliyezungumza na Tanzania Daima kwa sharti la kutotajwa jina, alisema Waziri Mkuu alikaririwa (wakati huo) akiyaelezea maneno hayo ya Ndesamburo kuwa yasiyo na ukweli wowote.


Alipotakiwa na Tanzania Daima aeleze hatua ambazo Lowassa amepanga kuzichukua dhidi ya suala hilo ambalo kauli yake inahusishwa, ofisa huyo alisema, vyombo vinavyohusika vitalishughulikia.


“Sisi tunajua ni kwa nini Ndesamburo kasema maneno hayo. Tunajua kila kitu kinachoendelea kuhusu jambo hili. Ni vyema tukanyamaza. Waziri Mkuu anajua anachofanya, hawezi akasema maneno ya namna hiyo. Ipo siku ukweli utabainika,” alisema ofisa huyo wa serikali alipotafutwa na Tanzania Daima.


Badala yake, ofisa huyo wa serikali alieleza pia kushangazwa kwake na ukimya wa Mengi ambaye ndiye aliyetajwa na Ndesamburo kumwambia maneno hayo, kuendelea kukaa kimya pasipo kutamka hadharani iwapo ni kweli alifikisha maneno hayo au la.


“Ninyi mnamtafuta Waziri Mkuu atoe tamko, mbona hatujasikia Mengi akisema hadharani ni kweli kuwa alimwambia Ndesamburo maneno haya? Si yuko na anapatikana, mbona amekaa kimya,” alihoji ofisa huyo.


Hata hivyo wakati wa kikao cha Bunge cha mwanzoni mwa mwaka huu, Sitta aliamua kulitolea uamuzi suala hilo kwa kufanya kile ambacho gazeti hili lilikielezea kuwa ni kushindwa kwake kumaliza mzozo kati ya Mengi na Malima.


Sitta akitumia falsafa yake ya siku zote; ‘Hekima za Spika’, alitangaza rasmi kuwaita ofisini kwake Dar es Salaam katika siku itakayopangwa, lengo likiwa ni kutafuta suluhu ya kudumu.


“Na kwa kuwa, busara zangu zinanituma kwamba, njia nzuri na iliyo bora ya kuyashughulikia na kuyamaliza malalamiko ya watu hawa wawili, ni kwa usuluhishi (reconciliation) kati yao,” alisema Sitta wakati akisoma maamuzi yake.


Sitta alisema, alikuwa amelazimika kufikia uamuzi huo, baada ya kubaini kuwa, watu hao wawili, kila mmoja alikuwa ametenda kosa la aina fulani, tangu sakata hilo liibuliwe na Malima mwezi Agosti mwaka jana.


Maamuzi hayo yalitokana na malalamiko ya Mengi, aliyowasilisha kwake (Spika) Agosti 6, mwaka jana, akilalamika kwamba, Agosti 2, 2006, wakati akichangia hoja ya Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Bungeni, Malima pamoja na mambo mengine, alishutumu matumizi mabaya ya Kituo cha Televisheni cha ITV pamoja na mmiliki wake ambaye ni Mengi.


Katika matamshi yake, Malima alikishutumu kituo hicho kwa kutumia muda mwingi kutangaza habari zinazomhusu mmiliki wake wakati kikitoa muda mchache kutangaza masuala ya kitaifa yanayowahusu Rais na Waziri Mkuu.


Kwa maneno yake, Malima alisema: “Nimewahi kushuhudia Rais wa Jamhuri ya Muungano ana habari nzito kwenye Taarifa ya Habari ya saa 2:00, anapewa dakika moja na nusu, Waziri Mkuu anataka kuzungumzia njaa anapewa dakika moja na nusu. Watoto wa ‘Primary’ wanakuja kutoka Zanzibar kutembelea Kiwanda cha Coca-Cola wanapewa dakika 10. Mmiliki wa TV anakwenda kuongea na watoto wa madrasa Msasani kwa ajili ya kugombana na sheikh mmoja anapewa dakika 10.”


Mengi aliyachukulia matamshi hayo kuwa shutuma dhidi yake zilizotolewa katika eneo ambalo hawezi kujitetea, na kwamba shutuma hizo dhidi yake na ITV hazikuwa na ukweli wala msingi wowote.


Baada ya matamshi hayo ya Mengi yaliyotolewa na ITV na Radio One, Malima aliomba muongozo wa Spika kuhusu hatua stahili anazopaswa kuchukua yeye binafsi kama mbunge kuhusu matangazo ya IPP Media dhidi yake au hatua zinazoweza kuchukuliwa na Bunge, kwa niaba yake.


Baada ya kupitia hoja hizo kwa kulinganisha na sheria, taratibu na kanuni zilizopo, Sitta alibainisha kuwa, wote wawili walikuwa wametenda makosa.


Kwa upande wa Malima, Spika alisema kuwa, mbunge huyo alikuwa amelidanganya Bunge, kwani takwimu alizozitoa kuhusu taarifa za habari za ITV hazikuwa sahihi.


Maamuzi hayo ya Sitta, ndiyo yaliyosababisha Malima afikie hatua ya kuandika barua kwa Makamba akiyapinga.
 
Nilikwishasema hapo awali kuwa nina wasiwasi na Uwezo wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano.Bunge limekuwa Butu mno!!,kuna mambo mengi ya maana kwa ajili ya maendeleo ya wananchi ya kujadiliwa huko lakini hatuyasikii,sijui kwamba Wabunge wanaogopa kuhoji au kwamba Bunge lina wenyewe, kwa maana kwamba wanaamua nini kizungumzwe humo!!.
Sasa leo Bunge linazizima kwa Ugomvi huu wa Malima na Mengi ambao umegeuka na kuwa Ugomvi wa Malima na Sita.Huyu Mzee Sita ana matatizo!,hata kama Kijana Malima anataka attention na aeleweke kama ni muakilishi wa watu (Mbunge wa kuchaguliwa),lakini pia tumuangalie Sita na maamuzi yake huko nyuma.Sita amekuwa mbabe na kuamua mambo anavyotaka yeye,alimvuruga na hatimaye kumtisha Kabwe,alimtisha na kumlaumu Ndesamburo kwa madai yake dhidi ya Kamati ya Bunge.Sasa wanadai madai ya Malima ya kwamba haki haikutendeka kwenye maamuzi ya kesi yake dhidi ya Mengi ni ukiukwaji wa sheria za Bunge!,Malima amempinga Spika na sio Bunge!.
Malima kuwa ngangari ama sivyo utaombwa uombe msamaha,kwa sababu kesi umeipeleka CCM kwa Bwana Makamba, huyo Mh. ni bure kabisa,hawezi kuzungumza lolote na Sita,kwanza hajui chochote na pili ni muoga.Ni mtu ambaye ana ujanja wa kwenda kuzungumza na WanaCCM Mlalo na sio kujadili issue na watu wenye upeo wa uelewa.
Imefika wakati sasa Spika aelezwe UKWELI na sio kuogopwa,kwani Nchi yetu ni Nchi ya Kidemokrasia na sio Nchi inaoogozwa na viongozi wa kiimla,ambao Kauli yao ni ya Mwisho na hakuna anayeweza kuijadili!.
 
Mwanakijiji

Unjaua niliposema kuwa you can do better than that ni kutokana na heshima yako na chombo chako cha habari ambacho kina umaarufu mkubwa tuu.

I'll take that as a compliment.. thank you!

Lakini tatizo ni pale unapotegemewa kuwa impartial na kuweza kujenga arguments ambazo zinaangalia both sides of the issue lakini of recently umekuwa huji na hoja bali umekuwa overwhelmingly biased hoja zako mwanzoni wakati hii thread ilipoanza ulisema kuwa MALIMA KAAJIRIWA NA MANJI. I mean how do you expect watu wakuchukulie serious na chombo chako cha Habari kama na wewe unarukia bandwagon ya kusema jambo bila ya kuwa na uhakika nalo?

DrWho, naona bado unanichanganya na kunihusisha na jambo ambalo sijalifanya. Umesema "mwanzoni wakati hii thread ilipoanza"... hivyo nimeamua kwenda na kuangalia nisijie kuwa nimesema kitu "nisichomaanisha".. sasa "mwanzoni".. ilikuwa hivi:

a. Nimepost barua... watu wakaanza kuchangia...
b. Sikuchangia mimi zaidi ya kuelezea "tetesi" na sikumhusisha Manji na Malima. Aliyefanya hivyo ni Mzee ES kwa maneno haya:

Mwanakijji,

Adam Malima, ni mfanyakazi wa Manji licha ya ubunge wake hiyo ni fact, ina maana asipokuwepo bungeni ni mkurugezni katika ofisi za Manji, hakuna la ajabu,

Mzee Ogah,

Maneno mazito hayo bro, keep it up!

Huo ulikuwa ukurasa wa kwanza. Kwenye ukurasa wa pili huko "mwanzoni" nilichangia wakati namjibu Kingwele:

Kingwele, miye nimetoa mawazo ya watu wengine kuhusu hili.... vyanzo ambavyo vimenipatia barua hiyo ndio ambavyo vimeleta hoja hiyo ya kuunganisha historia ya Malima na NRA.
Nilionesha kuwa "tetesi" za Malima na NRA hazikuwa mawazo yangu bali "vyanzo" vilivyonipenyezea barua hiyo! Na nikaendelea kusema:

Ila hili la kuwa Malima alikuwa/au bado ni mfanyakazi wa Manji sikulijua.

Na kwa umakini mkubwa nikasema kwa kutumia an obvious qualifier:
Kama ni kweli, basi it makes a lot of sense! He has nothing to lose na mgogoro wake na Mengi then unaonekana kwa kutumia mwanga mkubwa zaidi.

Hivyo utaona kuwa siye mimi niliyesema kuwa Manji ni mfanyakazi wa Mengi. Sijasema hivyo na siwezi kusema hivyo kwani sina ujuzi huo!

Dont get me wrong inawezekana ni kutokana na frustrations lakini kila mtu yuko frustrated lakini kwa status yako katika jamiii we expected more of you instead of coming up with unsubstantiated claim ambazo zimepelekea wewe kuonekana kuwa umekuja na narrow range of debate[q/uote]

Narudia tena.. sijaja na unsubstantiated claim!! mnayetakiwa kumbana hapa ni Mzee ES na wale wanaokubali kuwa Malima ni mfanyakazi wa Manji! Hata katika maswali yangu kwa Bw. Malima utaona nimeuliza kama hoja za watu wengine siyo za kwangu binafsi!

I hope this will help you in understand that I do not arguet emotionally or illogically! All my arguments are well crafted, formulated, and yes reasoned. Whether they can stand in the light of other stronger counter arguments that is for other people to decide

That said, ningependa ku clarify kuwa SIJAKULAUMU KUWEKA HII BARUA humu bali hiyo bandwagoning yako inanitisha

sawa!
 
KNKCU,Mzee ES,Masatu,Mwanakijiji,
Spika alitamka kwamba Malima alishindwa kuthibitisha kauli yake aliyoitoa bungeni. Kwa kanuni za Bunge hilo ni KOSA. Sasa Sijui kwanini Kamati ya Maadili ilimuona hana hatia yoyote, unless ilikuwa inachunguza jambo tofauti.

Hata Malima mwenyewe hazungumzii kabisa kushindwa kwake kuthibitisha matamko aliyoyatoa ndani ya bunge. Anachokisisitiza ni haki ya wabunge kuzungumza kwa "uhuru" wanapokuwa ndani ya bunge.

Mimi nilifikiri "busara za Spika" ni ule uamuzi wa Mzee Sitta kutokumchukulia hatua za sheria za bunge Mh.Malima kwa kutoa madai ya uongo dhidi ya Bw.Mengi na ITV. Mimi nadhani Malima angekubali kukutana na Mengi hata kama yeye binafsi hana ugomvi naye. Hili suala limejadiliwa mpaka na kamati ya bunge, kwa msingi huo there are some issues/differences that need to be sorted/ironed out btn Mh.Malima na Bw.Mengi
 
JokaKuu,

Ripoti ya Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge iliyofanya vikao 60 na kutumia zaidi milioni 100 imemuona Mh Malima hakufanya kosa ( excluding dissenting views)

Counter ripoti aliyoiandaa Spika ndio imemuona Mh Malima ana hatia. Hata kwa mujibu wa ripoti yake mwenyewe mzee Six inayomtia hatiani Mh Malima ameshindwa kumhukumu badala yake "busara" zake zimemtuma awasuluhishe.

Sio siri mzee Six amevurunda katika hili. Kile alichokikwepa mwanzo cha kukataa kujadili ripoti na bunge zima ndio sasa kinafanyika. Ndio maaana wachangiaji wengine wanasema hii ni karata 3 tutakaoliwa ni sisi!

Mungu ibaraki Tanzania
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom