Barua ya Julius Nyerere ya kujiuzulu ualimu St. Francis College Pugu 1955

Barua ya Julius Nyerere ya kujiuzulu ualimu St. Francis College Pugu 1955

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074

1569989576877.png

Nimeletewa barua ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kujiuzu kazi ya ualimu, aliyeniletea bila shaka akidhani siijui barua hii.

Nimeamua kumwandikia kumpa fikra zangu na kumweleza historia nzima ya barua hii ambayo inaitwa ''Uamuzi wa Busara.'':

''Hii barua ni maarufu ila kilichopungua ni vipi Mwalimu Nyerere alifikia katika uamuzi mgumu kama huu wa kuacha kazi na kuamua kuwa mtumishi wa TANU chama kichanga cha siasa kilichoasisiwa miezi minane tu iliyopita.

Chama ambacho kilikuwa kikiendeshwa kutoka fedha za wafadhili wake wanne: John Rupia, Waziri Dossa Aziz na ndugu wawili Abdulwahid na Ally Sykes.

Bahati mbaya barua aliyoandikiwa Mwalimu na mwajiri wake hapa haipo lakini nayo pia ni barua maarufu.

Toka alipochaguliwa kuwa Rais wa TAA tarehe 17 April 1953 mkakati uliokuwa umepangwa na Hamza Mwapachu na Abdul Sykes ilikuwa ni kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Sasa haikutegemewa kuwa Rais wa TANU atadai uhuru wa Tanganyika akiwa mfanyakazi wa Kanisa.

Huu ulikuwa muhali mkubwa na hili viongozi wa TANU wakilijua na Abdul na Nyerere walishalizungumza kabla na ukweli ni kuwa kabla ya safari ya kwanza ya UNO Februari 1955, Nyerere alitaabika sana na fikra ya kuacha kazi.

Ujasiri wa kuacha kazi Mwalimu hakuupata kwa kule kuzingirwa na watu wenye uwezo hawa viongozi na wahisani wakubwa wa TANU.

Ujasiri wa kuacha kazi aliupata siku aliporudi UNO na akapokewa na umma ambao ulikuwa haujapatapo kuonekana Dar es Salaam.

Siku ile ndiyo Nyerere alitambua kuwa ana watu wanaomuunga mkono na wana mapenzi ya kweli na yeye na TANU na wanataka kuwa huru na wamemkubali yeye kama kiongozi wao.

Kwa upande wa serikali ya Gavana Edward Francis Twining walitanabai ule ukweli kuwa sasa siku zao Tanganyika zilikuwa zinahesabika.

Kwa upande wa mwajiri wa Mwalimu Nyerere, yaani Kanisa iliwadhihirikia kuwa mtumishi wao alikuwa amewasababishia mgongano mkubwa sana wa maslahi kwani Kanisa na Serikali walikuwa na ushirikiano mkubwa katika kuitawala Tanganyika.

Kubwa zaidi lililowashangaza ni kuwa ni ile jamii waliyokuwa wameinyima elimu kwa hila za ukoloni za wagawe uwatawale.

Waislam wameunda chama na kumweka kiongozi Mkatoliki aongoze mapambano ya kuikomboa Tanganyika.

Mkakati huu ulikuwa na maana gani?

Mwalimu alikuwa alama ya umoja na alama ya kuwaita walio mfano wa yeye kuingia TANU na kuunga mkono juhudi za kudai uhuru wa Waafrika wa Tanganyika.

Barua ile aliyoandikiwa Nyerere na mwajiri wake ilisomwa na Abdul Sykes mtu aliyekuwa karibu sana na Nyerere na Abdul alisisitiza kuwa Nyerere aache kazi lakini barua ile akapendekeza ijadiliwe na Halmashauri Kuu ya TANU chini ya Mwenyekiti Clement Mohamed Mtamila na ilikuwa nyumbani kwake Mtamila ndipo barua ile ilipojadiliwa na uamuzi ukawa Nyerere aandike barua ya kujiuzulu kazi.

Nyerere aliandika barua ya kujiuzulu na akaja mjini Dar es Salaam sio mwalimu wa shule tena na kwa muda akaishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuu.

Katika Halmashauri Kuu ya TANU mmoja kati ya wajumbe wale alikuwa Tatu bint Mzee.

Yapo mengi sana katika historia ya TANU na historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo wengi hawayajui.

Picha ya kwanza juu ni barua ya Mwalimu Nyerere na picha ya pili hapo chini ni wa kwanza kulia ni Bi. Tatu bint Mzee akifuatiwa na Bi. Titi Mohamed na wa kwanza kushoto ni Bi. Chiku bint Said Kisusa wakimsindikiza Julius Nyerere Uwanja wa Ndege safari ya kwanza UNO.

1569989664206.png
 
Nyerere alijitahidi mno kutimiza wajibu wake kama kiongozi wa taifa hili. Hawa viongozi wa sasa mmhh!!
 
Sidhani kama aliyekutumia barua hii anadhani kwamba huijui, bali anajaribu tu kukumbusha yale yasiyokuvutia sana kwenye makala zako.

Nimeamua kumwandikia kumpa fikra zangu na kumweleza historia nzima ya barua hii ambayo inaitwa ''Uamuzi wa Busara.'': HAKIKA HIZI NI FIKRA ZAKO NA SI HALI HALISI.

Waislam wameunda chama na kumweka kiongozi Mkatoliki aongoze mapambano ya kuikomboa Tanganyika.

Na sijui wamaanisha nini hapo..kwa hiyo utakubaliana na wale tunaoona kwamba Waasisi wa chama hiki TAA na baadae TANU hawakuwa haswa na dhamira ya kutafuta uhuru wa Tanganyika, bali walikuwa na mambo yao..ambayo baada ya kufeli ndio wakabadili muelekeo? ingawa kwa Mtu yeyote mwenye kujipa muda wa kufikiri hili ataliona wazi.

Kupitia hizi stori zako/zenu ni wazi Waasisi 'wako' hawa hawakuwa na uwezo wowote wa kupigania uhuru hata miaka mingine 50 mbele.

Kiufupi stori za Mzee Said zimejaa hila kuliko uhalisia.
 
Sidhani kama aliyekutumia barua hii anadhani kwamba huijui, bali anajaribu tu kukumbusha tu yale yasiyokuvutia sana kwenye makala zako.

Nimeamua kumwandikia kumpa fikra zangu na kumweleza historia nzima ya barua hii ambayo inaitwa ''Uamuzi wa Busara.'': HAKIKA HIZI NI FIKRA ZAKO NA SI HALI HALISI.

Waislam wameunda chama na kumweka kiongozi Mkatoliki aongoze mapambano ya kuikomboa Tanganyika.

Na sijui wamaanisha nini hapo..kwa hiyo utakubaliana na wale tunaoona kwamba Waasisi wa chama hiki TAA na baadae TANU hawakuwa haswa na dhamira ya kutafuta uhuru wa Tanganyika, bali walikuwa na mambo yao..ambayo baada ya kufeli ndio wakabadili muelekeo? ingawa kwa Mtu yeyote mwenye kujipa muda wa kufikiri hili ataliona wazi.

Kupitia hizi stori zako/zenu ni wazi Waasisi 'wako' hawa hawakuwa na uwezo wowote wa kupigania uhuru hata miaka mingine 50 mbele.

Kiufupi stori za Mzee Said zimejaa hila kuliko uhalisia.
Mbona hata waasisi wa TAA Zanzibar nao walikuwa wakatoliki, na baadae wakawatafuta Waislamu ili waunde ASP na kutafuta Uhuru wa Zazibar?
1570005124618.png

IT'S A STRANGE ATTITUDE OF EAST AFRICA POLITICS ENGINEERED BY BRITISH.
 
Asante kwa kumbukumbu hii. Ombi iscan tena barua vizuri maana nimeshindwa kuisoma. Natanguliza shukrani.
 
Wazee wetu kama nyinyi mlitakiwa kuwepo kwenye ya idara serikalini kwa kumbukumbu kama hizi ili zisiweze kupotea kirahisi, upate umri mrefu sana Mzee wetu Mohamed Said.
 
Napenda sana Habari za Mkatoliki Mwaminifu, Mwenyeheri Julius K Nyerere. Mungu amtukuze!
Kirchhoff,
Siku nilipokabidhiwa Nyaraka za Sykes na kumkuta Julius Nyerere ndani ya nyaraka hizi nilikuwa kama mtu aliyepagawa.

Nilitamani kusoma majalada yote kwa usiku mmoja jambo lisilowezekana.

Hakika Mwalimu Nyerere alikuwa mtu hodari sana.
Mimi ndiye mtafiti pekee ukitoa John Iliffe ambae amebahatika kuziona nyaraza hizi.
 
Nyerere alijitahidi mno kutimiza wajibu wake kama kiongozi wa taifa hili. Hawa viongozi wa sasa mmhh!!
Hua nasema Mungu alitupendelea sana kutupa Mwl Nyerere kama baba wa Taifa,kuna viongozi flani flani hua nawaza kama wao ndio wangekua waasisi wa Taifa sijui tungekua na hali gani kwa kweli.
 
Mbona hata waasisi wa TAA Zanzibar nao walikuwa wakatoliki, na baadae wakawatafuta Waislamu ili waunde ASP na kutafuta Uhuru wa Zazibar?
View attachment 1221456
IT'S A STRANGE ATTITUDE OF EAST AFRICA POLITICS ENGINEERED BY BRITISH.
Battawi,
Ahsante kwa mchango wako.

Zanzibar haikuwa TAA ilikuwa AA yaani African Association.
Kujikusanya kwa Wakatoliki Zanzibar na kuunda AA si kitu cha kustaajabisha.

Hao walihitaji chama kwani walikuwa ugenini na wakitofautiana na wenyeji wao kwa kila hali.
 
Sidhani kama aliyekutumia barua hii anadhani kwamba huijui, bali anajaribu tu kukumbusha tu yale yasiyokuvutia sana kwenye makala zako.

Nimeamua kumwandikia kumpa fikra zangu na kumweleza historia nzima ya barua hii ambayo inaitwa ''Uamuzi wa Busara.'': HAKIKA HIZI NI FIKRA ZAKO NA SI HALI HALISI.

Waislam wameunda chama na kumweka kiongozi Mkatoliki aongoze mapambano ya kuikomboa Tanganyika.

Na sijui wamaanisha nini hapo..kwa hiyo utakubaliana na wale tunaoona kwamba Waasisi wa chama hiki TAA na baadae TANU hawakuwa haswa na dhamira ya kutafuta uhuru wa Tanganyika, bali walikuwa na mambo yao..ambayo baada ya kufeli ndio wakabadili muelekeo? ingawa kwa Mtu yeyote mwenye kujipa muda wa kufikiri hili ataliona wazi.

Kupitia hizi stori zako/zenu ni wazi Waasisi 'wako' hawa hawakuwa na uwezo wowote wa kupigania uhuru hata miaka mingine 50 mbele.

Kiufupi stori za Mzee Said zimejaa hila kuliko uhalisia.
May Day,
Ndiyo uzuri wa kuandika na wasomaji wakasoma na kila mtu baada ya kusoma akatoa mchango wake kwa jinsi alivyoelewa hata kama atakushambulia.
 
Mbona hata waasisi wa TAA Zanzibar nao walikuwa wakatoliki, na baadae wakawatafuta Waislamu ili waunde ASP na kutafuta Uhuru wa Zazibar?
View attachment 1221456
IT'S A STRANGE ATTITUDE OF EAST AFRICA POLITICS ENGINEERED BY BRITISH.

Hapo umechemka mkuu. NI kweli Waasisi wa AA Zanzibar walikua ni wakatoliki ila hayo maelezo ulioyaeleza mbele hayana ukweli.
 
Kiliwakuta nini hao waislamu waliounda Chama afu nchi akachukua mkristo?
UNO walimtaka Mkristo ndio akabidhiwe nchi kulikuwa na wasomi kama Said Fundikira aliehitimu Makerere kabla ya Mwl lakini hakufit
 
Back
Top Bottom