Barua ya Julius Nyerere ya kujiuzulu ualimu St. Francis College Pugu 1955

Barua ya Julius Nyerere ya kujiuzulu ualimu St. Francis College Pugu 1955

Mzee nimekuelewa ila kama kuna kitu kipya hapa tena nimekiona
Ngoja kidoogo nikafanye marejeo mahala flani
Kisha nipitie na link ulizoweka hapa ili nipate kujua zaidi
itakua vema sana
B...
Umekosea kumtaja Sheikh Hassan bin Ameir.
Sheikh Hassan hakuwa ameshika nafasi yoyote katika chama.

Wala Sheikh Hassan hakuwa na mwenzie katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
Mwenzie kama alikuwepo ni Nyerere.

Sheikh Hassan alikuwa kiongozi bila ya kushika nafasi ya uongozi.

Wengi wenu hamjui nafasi ya Sheikh Hassan bin Ameir katika siasa za Tanganyika hadi Tanzania.

Sheikh Hassan bin Ameir alikuwapo katika mpango wa kuunda TANU toka mwaka wa 1950 akiwa mjumbe wa TAA Political Subcommitee.

Nakuwekea hapo chini mada niliyotoa Zanzibar University kuhusu Sheikh Hassan bin Ameir mpate kumjua.

Swali la pili kuwa Mwalimu awape nini waasisi wa TANU sijui kwa nini unauliza swali hili sidhani kama waasisi walikuwa wanataka kupewa kitu.

Hapa nawasemea waasisi ambao mimi nawajua vyema toka wako hai hadi walipofariki.
Sikupata kuwasikia wakisema kuwa hawakupewa kitu.

Nilichokisikia mara nyingi wakisema ni kuwa historia ya TANU inavurugwa na kupotoshwa.
Nakumbuka maneno ya Mzee Germano Pacha aliyoniambia katika mahojiano yetu wakati wa utafiti wa kitabu.

Mzee Pacha alisema kama si kuwapo ile picha ya waasisi wa TANU kungekuwa na waasisi wengi hivi sasa.

 
Mzee nimekuelewa ila kama kuna kitu kipya hapa tena nimekiona
Ngoja kidoogo nikafanye marejeo mahala flani
Kisha nipitie na link ulizoweka hapa ili nipate kujua zaidi
itakua vema sana
B...
Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ina mambo mengi sana wala sishangai unaposema umekutana na mapya.

Hamkupatapo kusoma haya popote pale.
Karibu ndugu yangu.

Nakala ya kwanza ya Kiingereza ilichapwa na Minerva, London 1998.
Picha yake hiyo hapo chini:
 

Attachments

  • SYKES BOOK MINERVA.jpg
    SYKES BOOK MINERVA.jpg
    16 KB · Views: 2

Nimeletewa barua ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kujiuzu kazi ya ualimu, aliyeniletea bila shaka akidhani siijui barua hii.

Nimeamua kumwandikia kumpa fikra zangu na kumweleza historia nzima ya barua hii ambayo inaitwa ''Uamuzi wa Busara.'':

''Hii barua ni maarufu ila kilichopungua ni vipi Mwalimu Nyerere alifikia katika uamuzi mgumu kama huu wa kuacha kazi na kuamua kuwa mtumishi wa TANU chama kichanga cha siasa kilichoasisiwa miezi minane tu iliyopita.

Chama ambacho kilikuwa kikiendeshwa kutoka fedha za wafadhili wake wanne: John Rupia, Waziri Dossa Aziz na ndugu wawili Abdulwahid na Ally Sykes.

Bahati mbaya barua aliyoandikiwa Mwalimu na mwajiri wake hapa haipo lakini nayo pia ni barua maarufu.

Toka alipochaguliwa kuwa Rais wa TAA tarehe 17 April 1953 mkakati uliokuwa umepangwa na Hamza Mwapachu na Abdul Sykes ilikuwa ni kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Sasa haikutegemewa kuwa Rais wa TANU atadai uhuru wa Tanganyika akiwa mfanyakazi wa Kanisa.

Huu ulikuwa muhali mkubwa na hili viongozi wa TANU wakilijua na Abdul na Nyerere walishalizungumza kabla na ukweli ni kuwa kabla ya safari ya kwanza ya UNO Februari 1955, Nyerere alitaabika sana na fikra ya kuacha kazi.

Ujasiri wa kuacha kazi Mwalimu hakuupata kwa kule kuzingirwa na watu wenye uwezo hawa viongozi na wahisani wakubwa wa TANU.

Ujasiri wa kuacha kazi aliupata siku aliporudi UNO na akapokewa na umma ambao ulikuwa haujapatapo kuonekana Dar es Salaam.

Siku ile ndiyo Nyerere alitambua kuwa ana watu wanaomuunga mkono na wana mapenzi ya kweli na yeye na TANU na wanataka kuwa huru na wamemkubali yeye kama kiongozi wao.

Kwa upande wa serikali ya Gavana Edward Francis Twining walitanabai ule ukweli kuwa sasa siku zao Tanganyika zilikuwa zinahesabika.

Kwa upande wa mwajiri wa Mwalimu Nyerere, yaani Kanisa iliwadhihirikia kuwa mtumishi wao alikuwa amewasababishia mgongano mkubwa sana wa maslahi kwani Kanisa na Serikali walikuwa na ushirikiano mkubwa katika kuitawala Tanganyika.

Kubwa zaidi lililowashangaza ni kuwa ni ile jamii waliyokuwa wameinyima elimu kwa hila za ukoloni za wagawe uwatawale.

Waislam wameunda chama na kumweka kiongozi Mkatoliki aongoze mapambano ya kuikomboa Tanganyika.

Mkakati huu ulikuwa na maana gani?

Mwalimu alikuwa alama ya umoja na alama ya kuwaita walio mfano wa yeye kuingia TANU na kuunga mkono juhudi za kudai uhuru wa Waafrika wa Tanganyika.

Barua ile aliyoandikiwa Nyerere na mwajiri wake ilisomwa na Abdul Sykes mtu aliyekuwa karibu sana na Nyerere na Abdul alisisitiza kuwa Nyerere aache kazi lakini barua ile akapendekeza ijadiliwe na Halmashauri Kuu ya TANU chini ya Mwenyekiti Clement Mohamed Mtamila na ilikuwa nyumbani kwake Mtamila ndipo barua ile ilipojadiliwa na uamuzi ukawa Nyerere aandike barua ya kujiuzulu kazi.

Nyerere aliandika barua ya kujiuzulu na akaja mjini Dar es Salaam sio mwalimu wa shule tena na kwa muda akaishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Aggrey na Sikukuu.

Katika Halmashauri Kuu ya TANU mmoja kati ya wajumbe wale alikuwa Tatu bint Mzee.

Yapo mengi sana katika historia ya TANU na historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo wengi hawayajui.

Picha ya kwanza juu ni barua ya Mwalimu Nyerere na picha ya pili hapo chini ni wa kwanza kulia ni Bi. Tatu bint Mzee akifuatiwa na Bi. Titi Mohamed na wa kwanza kushoto ni Bi. Chiku bint Said Kisusa wakimsindikiza Julius Nyerere Uwanja wa Ndege safari ya kwanza UNO.

Dah
 
Sikuwahi kusema Mwalimu ndiye alipeleka TANU kwa kina Sykes.

Mwalimu mwenyewe alikiri kwamba jina TANU lililetwa na kina Sykes, na walikuwa nalo tangu wakiwa Burma...na nimeshawahi kusema hili...na kikubwa kilichofanyika pale ni kupitisha jina mbadala wa TAA, na hao waliokuja na TANU wakashinda, sioni kwa nini hilo mnalifanya ni 'big deal' kuliko hata maarifa ya harakati zenyewe.

Mwalimu alikwenda pale na 'road map' ambayo ndiyo muhimu kuliko hata kutunga jina la chama.

Mzee Said unaongozwa sana na dhana binafsi kiasi unamuondolea kabisa msomaji wako picha halisi ya Wazee walivyoendesha hizo harakati.

Haihitaji akili ya ziada sana kuelewa kuwa hao kina Syskes na wenzake walishanyoosha mikono juu, na Mwalimu kwao alikuwa ndiye mkombozi...na namna walivyoishi (m treat) inajieleza vizuri kuliko wewe unavyojaribu kuficha ficha...unaokoteza yale yanayowapamba Wazee wako zaidi.

Ingawa wewe unaonekana kuegemea zaidi kwa hawa 'Wazee wako' lakini Mwalimu amekuwa anawataja kundi la Wazee wa Dar es Salaam ambao walimuamini, kumuelewa na kumuunga mkono ndani ya muda mfupi tu....naona hujali sana michango ya wengine hao zaidi umeegemea kwa hawa 'Wazee wako' wachache.

"...walikuwa nalo tangu wakiwa Burma..." Hilo Nyerere alilisema wapi? Nyerere aliyesema ya kabla la Hilo uliyoyaandika lakini kipande hicho cha "Burma", rejea kumbukumbu zako ukumbuke umelitoa wapi.

Nnakuhakikishia hicho kimetoka kwa Allama Mohamed Said.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
 
Devor,
Ikiwa unataka kushangaa zaidi sikiliza historia hii ya TANU kuasisiwa Tosamaganga:
 
Back
Top Bottom