Barua ya Julius Nyerere ya kujiuzulu ualimu St. Francis College Pugu 1955

Barua ya Julius Nyerere ya kujiuzulu ualimu St. Francis College Pugu 1955

UNO walimtaka Mkristo ndio akabidhiwe nchi kulikuwa na wasomi kama Said Fundikira aliehitimu Makerere kabla ya Mwl lakini hakufit
Huu ndio uongo wa kulaaniwa, ingawa Mleta uzi hasemi hivyo moja kwa moja ila ni dhahiri kuwa haya ndio anayopigania Watu waone ndivyo ilivyokuwa.

Hivi ni nchi ngapi zilizokuwa zinatawaliwa zikiwa ni nchi za kiislamu na zilipata uhuru chini ya huo huo Uislamu? sasa hao UNO kwa nini waweke kigezo hicho kwa Tanganyika?

Kuna sehemu mnasema UNO walimtaka Mkristo na sehemu mnasema Mwalimu aliachana na kazi ya kanisa ili afanye harakati za kupigania uhuru...hilo kanisa lilishindwa vipi kumuunga Mwalimu mkono ili aje kuwa Kiongozi?

Huu ndio tunaouita utapeli wa historia.
 
UNO walimtaka Mkristo ndio akabidhiwe nchi kulikuwa na wasomi kama Said Fundikira aliehitimu Makerere kabla ya Mwl lakini hakufit
Gas...
Umekosea kumleta Chief Abdallah Said Fundikira.

Yeye hakuwapo kabisa katika orodha ya 1950 ya viongozi waliofikiriwa kujiunga na TAA kisha wachaguliwe nafasi ya urais iundwe TANU na kisha udaiwe uhuru wa Tanganyika.

Ukipitia kumbukumbu za Sykes utamkuta aliyekuwa akifikiriwa na mazungumzo yalifanyika kati ya 1950 hadi 1952 ni Chief David Kidaha Makwaia wa Siha.

Wakati huo Chief Kidaha ni memba wa Legislative Council.

Wala Nyerere hakuwapo katika orodha hiyo hadi 1952 alipokutana na Abdul Sykes.

Taarifa za Special Branch zinaeleza kuwa Chief Kidaha alikuwa akienda nyumbani kwa Abdul Sykes.

Haya ndiyo katika yale mengi ambayo hayakupata kujulikana hadi nilipoandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes 1998.
 
Mohamed Said,

..inasemekana kuna barua ya Mwalimu Nyerere kwenda kwa Kanisa Katoliki akiwashutumu kujiingiza ktk mambo ya siasa. Nimeambiwa barua hiyo inapatikana ktk moja ya vitabu vinavyozungumzia mahusiano kati ya Kanisa na dola hapa Tz. Sijui kama una kitabu chenye barua hiyo, nitashukuru ukiweza ku-share na sisi. Yuko mkongwe mwenzetu Companero aliahidi kuileta hapa JF lakini naona amepotea siku hizi.
 
Mohamed Said,

..inasemekana kuna barua ya Mwalimu Nyerere kwenda kwa Kanisa Katoliki akiwashutumu kujiingiza ktk mambo ya siasa. Nimeambiwa barua hiyo inapatikana ktk moja ya vitabu vinavyozungumzia mahusiano kati ya Kanisa na dola hapa Tz. Sijui kama una kitabu chenye barua hiyo, nitashukuru ukiweza ku-share na sisi. Yuko mkongwe mwenzetu Companero aliahidi kuileta hapa JF lakini naona amepotea siku hizi.
JK,
Sina taarifa ya kitabu hicho.
 
Ili apotoshe uma mwingi?
May Day,
Kitabu leo kipo miaka 20 kimechapwa mara nne na hajatokea mtu yeyote kusema kuwa mimi ni muongo.

Kilichofanyika ni kuundwa jopo linaloongozwa na Prof. Issa Shivji akiwa na Prof. Saida Yahya na Dr. Kamatha ambao sasa wanaandika historia ya Mwalimu Nyerere ili angalau wapate kufahamu nafasi yake katika kuasisi harakati za kujikomboa kutoka ukoloni.

Jopo hili wamefanya mazungumzo na mimi nyumbani kwangu mara mbili na nimewapa picha na nakala za nyaraka kutoka Nyaraka za Sykes ambazo baadhi wamepata kuzionyesha katika Kavazi la Mwalimu Nyerere ambalo Prof. Shivji ni Mwenyekiti wake.

Marehemu Prof. Haroub Othman kaonana uso kwa macho na Mwalimu Nyerere kuhusu kitabu cha Ali Muhsin Barwani, ''Conflict and Harmony in Zanzibar,' Dubai (1997) na ''The Life and Times of Abdulwahis Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika,'' London (1998), vitabu viwili ambavyo Mwalimu katajika sana.

Kama ilivyokuwa kwako wewe Prof. Haroub alichomwa sana na historia hii niliyoandika akili yake ilikuwa inakataa kama yale anayosoma ni kweli.

Mimi nilizungumza na Prof. Haroub ambae ni mwalimu wangu na yeye ndiye aliyeniambia kuwa ameonana na Mwalimu na akamuomba na yeye aandike ili yapatikane majibu kwangu na kwa Sheikh Ali Muhsin.

Napenda kukufahamisha kuwa baada ya kuzungumza na mimi hakutosheka Prof. Haroub alikwenda kufanya mazungumzo na Ahmed Rashad Ali mtu aliyekuwa rafiki kipenzi na Abdul Sykes kutaka ukweli wa yale yeye alikuwa na mashaka.

Prof. Haroub aliondoka katika mazungumzo yake na Mzee Rashad akiwa kichwa kainamisha.
Mimi sina sababu ya kuzua uongo.

1570034190612.png

Kulia: Prof. Haroub Othman, Ahmed Rashad Ali na Ahmed Islam 1997

1570034399049.png

Kulia: Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Othman na Dr. Kamatha siku walipokuja kufanya mazungumzo na Mwandishi kuhusu kitabu cha Abdul Sykes 2013

May Day,
Unaweza kutaka kumjua Ahmed Rashad Ali ni nani katika historia ya Tanzania.
Tafadhali ingia hapo chini:

 
May Day,
Kitabu leo kipo miaka 20 kimechapwa mara nne na hajatokea mtu yeyote kusema kuwa mimi ni muongo.

Kilichofanyika ni kuundwa jopo linaloongozwa na Prof. Issa Shivji akiwa na Prof. Saida Yahya na Dr. Kamatha ambao sasa wanaandika historia ya Mwalimu Nyerere ili angalau wapate kufahamu nafasi yake katika kuasisi harakati za kujikomboa kutoka ukoloni.

Jopo hili wamefanya mazungumzo na mimi nyumbani kwangu mara mbili na nimewapa picha na nakala za nyaraka kutoka Nyaraka za Sykes ambazo baadhi wamepata kuzionyesha katika Kavazi la Mwalimu Nyerere ambalo Prof. Shivji ni Mwenyekiti wake.

Marehemu Prof. Haroub Othman kaonana uso kwa macho na Mwalimu Nyerere kuhusu kitabu cha Ali Muhsin Barwani, ''Conflict and Harmony in Zanzibar,' Dubai (1997) na ''The Life and Times of Abdulwahis Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika, London (1998), vitabu viwili ambavyo Mwalimu katajika sana.

Kama ilivyokuwa kwako wewe Prof. Haroub alichomwa sana na historia hii niliyoandika akili yake ilikuwa inakataa kama yale anayosoma ni kweli.

Mimi nilizungumza na Prof. Haroub ambae ni mwalimu wangu na yeye ndiye aliyeniambia kuwa ameonana na Mwalimu na akamuomba na yeye aandike ili yapatikane majibu kwangu na kwa Sheikh Ali Muhsin.

Napenda kukufahamisha kuwa baada ya kuzungumza na mimi hakutosheka Prof. Haroub alikwenda kufanya mazungumzo na Ahmed Rashad Ali mtu aliyekuwa rafiki kipenzi na Abdul Sykes kutaka ukweli wa yale yeye alikuwa na mashaka.

Prof. Haroub aliondoka katika mazungumzo yake akiwa kichwa kainamisha.
Mimi sina sababu ya kuzua uongo.

View attachment 1221898
Kulia: Prof. Haroub Othman, Ahmed Rashad Ali na Ahmed Islam 1997

View attachment 1221902
Kulia: Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Othman na Dr. Kamatha siku walipokuja kufanya mazungumzo na Mwandishi kuhusu kitabu cha Abdul Sykes
Mimi si Mtaalamu sana wa Kiswahili, na sijatumia neno 'muongo'.....nadhani kuna tofauti ya uongo na kupotosha, kwa maoni yangu muongo huweza kusema kisicho ukweli 100%, na anayepotosha huweza kusema yaliyo na ukweli ila akaongeza 'chumvi' au kupunguza kwa lengo la kufikia malengo yake. Ndio maana sikutaja moja kwa moja kama Muongo.

Kama lengo la Makala zako ni kuwapamba/kuwatambulisha wale unaodhani wana ushiriki wao kwenye harakati za kupigania Uhuru, basi huna sababu ya kumuingiza/kumtaja Mwalimu ki hila hila na kumuonyesha kama Mtu 'aliyedandia' tu harakati zile.

Kufanya hivyo sio haki kabisa, kama huna taarifa za kutosha kumuhusu Mwalimu na chimbuko lake kwenye harakati ni bora ungebaki kuwaelezea hawa ambao una taarifa zao za kutosha na kusubiri watakaotafuta taarifa za Mwalimu ndio wamuelezee Mwalimu.

Sioni tatizo kwa yeyote kama Prof Haroub kushangazwa na baadhi ya mambo kwani huenda kweli hawakuyajua kabla, nadhani kitakachowasikitisha Wasomaji ni namna unavyotumia kupasha taarifa hizo kwa lengo la kupindisha mambo.
 
Jamani tujifunze kwa kusoma na kudadisi maandishi ya wenzetu na tuache Kuwa 'biased'.

Binafsi napenda sana stori za Mzee Mohamed Saidi japo sikubaliani nae kwa baadhi.
 
Naam hili ni darasa jipa na elimu mpya. Nadhani kuna mengine ya ziada
 
Mimi si Mtaalamu sana wa Kiswahili, na sijatumia neno 'muongo'.....nadhani kuna tofauti ya uongo na kupotosha, kwa maoni yangu muongo huweza kusema kisicho ukweli 100%, na anayepotosha huweza kusema yaliyo na ukweli ila akaongeza 'chumvi' au kupunguza kwa lengo la kufikia malengo yake. Ndio maana sikutaja moja kwa moja kama Muongo.

Kama lengo la Makala zako ni kuwapamba/kuwatambulisha wale unaodhani wana ushiriki wao kwenye harakati za kupigania Uhuru, basi huna sababu ya kumuingiza/kumtaja Mwalimu ki hila hila na kumuonyesha kama Mtu 'aliyedandia' tu harakati zile.

Kufanya hivyo sio haki kabisa, kama huna taarifa za kutosha kumuhusu Mwalimu na chimbuko lake kwenye harakati ni bora ungebaki kuwaelezea hawa ambao una taarifa zao za kutosha na kusubiri watakaotafuta taarifa za Mwalimu ndio wamuelezee Mwalimu.

Sioni tatizo kwa yeyote kama Prof Haroub kushangazwa na baadhi ya mambo kwani huenda kweli hawakuyajua kabla, nadhani kitakachowasikitisha Wasomaji ni namna unavyotumia kupasha taarifa hizo kwa lengo la kupindisha mambo.
May Day,
Laiti ningeandika kwa nia ya kupindisha mambo ningelikiua hiki kitabu changu zamani sana.

Lakini kwa kuwa kitabu hiki nimekiandika kwa nia ya kusahihisha historia ambayo kwa hakika haikuwa historia ya kweli ya TANU, kitabu hiki leo miaka 20 baada ya kuchapwa tuko hapa tunakijadili na kipo toleo la nne.

Mimi napenda nikutaarifu kuwa nina taarifa za kutosha kuhusu Mwalimu Nyerere na historia yake katika TANU kutoka vyanzo vya kuaminika.

Mwalimu kafika Dar es Salaam 1952 kapokewa na wazee wangu na naweza kukutajia majina yao mmoja baada ya mwingine wake kwa waume na hawa ni watu mimi wameniona toka utoto wangu pale Mtaa wa Kipata, Gerezani na kwengineko na watoto wao ni wenzangu katika makuzi.

Acha haya mimi nina taarifa za kutosha za Mwalimu Nyerere na TANU niilizosoma ndani ya Nyaraza za Sykes.

Nchi nzima hii hakuna mtu ana nyaraza kama hizi hata Tanzania National Archives (TNA).

Nyaraza hizi zinaanza toka 1929 wakati African Association inaundwa nyumbani kwa Cecil Matola, Mtaa wa Masasi Mission Quarter, Kleist Sykes akiwa mmoja wa waasisi hao na akaja kuandika historia hii na sasa ni sura katika kitabu, ''Modern Tanzanians, ' (1973) kilichohaririwa na John Iliffe.

Nyumba hii ilipoasisiwa AA ipo hadi leo kwa hiyo usizungumze habari ya kuwa ati mimi simjui Nyerere au siijua historia ya TANU.

Nawajua waasisi hadi nyumba walizoishi.

Hakuna hila yoyote katika historia niliyoandika.
La una ushahidi kuwa kuna hila tuwekee hapa hizo hila.

Wala hakuna popote niliposema Nyerere, chembelecho ''kadandia.''

Lakini ukweli utabakia kuwa Mwalimu aliikuta mipango ya TANU nyumbani kwa Abdul Sykes la kama una ushahidi kuwa yeye ndiye aliipeleka TANU kwa Abdul Sykes lete huo ushahidi.

Elewa kuwa huwezi kuandika historia ya Nyerere au historia ya TANU usimtaje Abdul Sykes.

Chuo Cha CCM Kivukoni kimejaribu kumtoa Abdul Sykes ktika historia ya TANU, angalia balaa walilochuma hii leo baada ya mimi kuandika historia ya TANU na kumtaja Abdul Sykes.

1570043422513.png

Kulia: Lawi Sijaona, Abdul Sykes, Julius Nyerere na Dossa Aziz
katika hafla ya kumuaga Nyerere Ukumbi wa Arnautoglo safari ya pili UNO 1957

1570043603115.png

Ally Sykes na Julius Nyerere nyumbani kwa Nyerere Magomeni 1958
 
May Day,
Laiti ningeandika kwa nia ya kupindisha mambo ningelikiua hiki kitabu changu zamani sana.
Lakini kwa kuwa kitabu hiki nimekiandika kwa nia ya kusahihisha historia ambayo kwa hakika haikuwa historia ya kweli ya TANU, kitabu hiki leo miaka 20 baada ya kuchapwa tuko hapa tunakijadili na kipo toleo la nne.

Mimi napenda nikutaarifu kuwa nina taarifa za kutosha kuhusu Mwalimu Nyerere na historia yake katika TANU.

Mwalimu kafika Dar es Salaam 1952 kapokewa na wazee wangu na naweza kukutajia majina yao mmoja baada ya mwingine wake kwa waume na hawa ni watu mimi wameniona toka utoto wangu pale Mtaa wa Kipata, Gerezani.

Acha haya mimi nina taarifa za kutosha za Mwalimu Nyerere na TANU niilizosoma ndani ya Nyaraza za Sykes.

Nchi nzima hii hakuna mtu ana nyaraza kama hizi.

Nyaraza hizi zinaanza toka 1929 wakati African Association inaundwa nyumbani kwa Cecil Matola, Mtaa wa Masasi Mission Quarter.

Nyumba hii ipo hadi leo kwa hiyo usizungumze habari ya kuwa ati mimi simjui Nyerere au siijua historia ya TANU.

Hakuna hila yoyote katika historia niliyoandika.
La una ushahidi kuwa kuna hila tuwekee hapa hizo hila.

Wala hakuna popote niliposema Nyerere, chembelecho ''kadandia.''

Lakini ukweli utabakia kuwa Mwalimu aliikuta mipango ya TANU nyumbani kwa Abdul Sykes la kama una ushahidi kuwa yeye ndiye aliipeleka TANU kwa Abdul Sykes lete huo ushahidi.

Elewa kuwa huwezi kuandika historia ya Nyerere na TANU usimtaje Abdul Sykes.

Chuo Cha CCM Kivukoni kimejaribu na angalia balaa walilochuma hii leo baada ya mimi kuandikia historia ya TANU na kumtaja Abdul Sykes.
Sikuwahi kusema Mwalimu ndiye alipeleka TANU kwa kina Sykes.

Mwalimu mwenyewe alikiri kwamba jina TANU lililetwa na kina Sykes, na walikuwa nalo tangu wakiwa Burma...na nimeshawahi kusema hili...na kikubwa kilichofanyika pale ni kupitisha jina mbadala wa TAA, na hao waliokuja na TANU wakashinda, sioni kwa nini hilo mnalifanya ni 'big deal' kuliko hata maarifa ya harakati zenyewe.

Mwalimu alikwenda pale na 'road map' ambayo ndiyo muhimu kuliko hata kutunga jina la chama.

Mzee Said unaongozwa sana na dhana binafsi kiasi unamuondolea kabisa msomaji wako picha halisi ya Wazee walivyoendesha hizo harakati.

Haihitaji akili ya ziada sana kuelewa kuwa hao kina Syskes na wenzake walishanyoosha mikono juu, na Mwalimu kwao alikuwa ndiye mkombozi...na namna walivyoishi (m treat) inajieleza vizuri kuliko wewe unavyojaribu kuficha ficha...unaokoteza yale yanayowapamba Wazee wako zaidi.

Ingawa wewe unaonekana kuegemea zaidi kwa hawa 'Wazee wako' lakini Mwalimu amekuwa anawataja kundi la Wazee wa Dar es Salaam ambao walimuamini, kumuelewa na kumuunga mkono ndani ya muda mfupi tu....naona hujali sana michango ya wengine hao zaidi umeegemea kwa hawa 'Wazee wako' wachache.
 
Sikuwahi kusema Mwalimu ndiye alipeleka TANU kwa kina Sykes.

Mwalimu mwenyewe alikiri kwamba jina TANU lililetwa na kina Sykes, na walikuwa nalo tangu wakiwa Burma...na nimeshawahi kusema hili...na kikubwa kilichofanyika pale ni kupitisha jina mbadala wa TAA, na hao waliokuja na TANU wakashinda, sioni kwa nini hilo mnalifanya ni 'big deal' kuliko hata maarifa ya harakati zenyewe.

Mwalimu alikwenda pale na 'road map' ambayo ndiyo muhimu kuliko hata kutunga jina la chama.

Mzee Said unaongozwa sana na dhana binafsi kiasi unamuondolea kabisa msomaji wako picha halisi ya Wazee walivyoendesha hizo harakati.

Haihitaji akili ya ziada sana kuelewa kuwa hao kina Syskes na wenzake walishanyoosha mikono juu, na Mwalimu kwao alikuwa ndiye mkombozi...na namna walivyoishi (m treat) inajieleza vizuri kuliko wewe unavyojaribu kuficha ficha...unaokoteza yale yanayowapamba Wazee wako zaidi.

Ingawa wewe unaonekana kuegemea zaidi kwa hawa 'Wazee wako' lakini Mwalimu amekuwa anawataja kundi la Wazee wa Dar es Salaam ambao walimuamini, kumuelewa na kumuunga mkono ndani ya muda mfupi tu....naona hujali sana michango ya wengine hao zaidi umeegemea kwa hawa 'Wazee wako' wachache.
May Day,
Hapana Mwalimu hakuja na Road Map.
Mwenye kuongozwa na dhana ni wewe.

Mimi naongozwa na ''primary sources'' na nitakupa ushahidi.

Siko hapa ndugu yangu kufanya maskhara niko hapa kulinda hadhi na heshima ya wazee wangu.

Kweli Nyerere kawataja wazee wangu lakini si kwa majina yao.
Huko si kuadhimishaa huko kunaitwa kuondoa ngoma juani.

Kweli kamtaja Abdul Sykes lakini hivi kweli Mwalimu anamjua Abdul kwa sifa ya Burma basi, hakuna mengine makubwa kuliko hayo?

Road Map kama unavyoita ilikuwa katika memorandum iliyopelekwa kwa Constitutional na Development Committee ya Gavana Edward Francis Twining ambayo ilitayarishwa na TAA Political Subcommittee na wajumbe wake walikuwa hawa wafuatao: Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Said Chaurembo, Hamza Mwapachu, Abdul Sykes, Dr. Vedasto Kyaruzi, Steven Mhando na John Rupia.

Aliyesaidia sana katika kutayarisha hili document alikua Earle Seaton mwanasheria kutoka Bermuda aliyekuwa akifanya shughuli zake za uwakili Moshi.

Earle Seaton na Abdul Sykes walikuwa marafiki wakubwa na ni Abdul ndiye aliyemtia katika siasa za Tanganyika kwanza kwenye hili la mapendekezo ya katiba 1950 na kisha 1952 kwenye Meru Land Case awasaidie Meru Citizens Union ya Japhet Kirilo kuandika petition kwenda UNO.

Haya yote yamo katika Nyaraka za Sykes na mengine mengi na nimeyaeleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes na nimeweka ''citations,'' zote hapo.

Huu waraka wa TAA Political Subcommittee ulijadiliwa katika mkutano wa TAA wa 1954 uliozaa TANU na ndiyo uliotengeneza hotuba ya Nyerere UNO 1955.

Sasa kama wewe una Road Map ya Nyerere nitafurahi kama utaiweka hapa tuisome.

Sasa ikiwa historia ndiyo hii nani anaeficha ukweli?

Mimi naegemea zaidi kwa wazee wangu kwa kuwa hiyo TANU ndiyo chama chao waliokiunda wao na wametoka na fikra hii toka 1929.

Ikiwa wewe una historia nyingine ya TANU isiyokuwa hii iweke hapa tuisome.
Unaweza kusoma historia hii zaidi hapo chini:


1570050510094.png

Earle Seaton na Julius Nyerere baada ya uhuru wa Tanganyika
 
UNO walimtaka Mkristo ndio akabidhiwe nchi kulikuwa na wasomi kama Said Fundikira aliehitimu Makerere kabla ya Mwl lakini hakufit

Sio sahihi kuwa UNO ndio walimchagua Nyerere ingawa walikuweo wengine kama Said Fundira, Tewa Said Tewa na wakina John Keto. Nyerere alichaguliwa kwasababu ya kukubalika kwake na wale aliokuwa anawaongoza!
 
Back
Top Bottom