Barua ya wazi kwa Alikiba

Barua ya wazi kwa Alikiba

AdvocateFi

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
11,492
Reaction score
5,047
Wasalaam wakuu!
Sio siri uzalendo umenishinda haswaa! Yote ni juu ya Alikiba "Kingkiba" Maana mpaka sasa nashindwa kuelewa ni Nani aliyekuroga hadi unaendesha mziki wako kizaman sana.

Uliporudi na "Mwana" ilikuwa ni nyota njema na tumain jipya kwa sisi mashabiki wako dunian kote, Kweli hakuna anayebisha kwamba kuanzia "Mwana, Chekecha Cheketua, Nagharamia mpaka sasa "Aje" umefanikiwa kweli kweli kuzitingisha kuta za mabaazazi na mahafidhina wa Mziki wa Bongflava waliotaka kujimilikisha mziki kwa kujifanya miungu watu, Kwa hilo nakupa pongezi.

Ni ukweli uliowazi kuwa umerudi na Kasi ya "4G" ila ubaya ni 4G inayosoma "H", Alikiba sisi fans wako umeendelea kututesa kwa muda mrefu sana hasa kwa mambo yako unayofanya sisi hayatupendezi kabisa, Nilitaka waraka huu uwe wa siri ila mbinu zote hizo zimeshindikana. Na haya yafuatayo ni miongoni mwa mambo yanayotutesa sisi washabiki zako.

1. UKOSEFU WA COLLABO ZA KIMATAIFA, maana tangu ujinasibu kuwa una collabo na fally pupa na wasanii wengine wakubwa ni miaka imepita, Kweli Alikiba wewe ni wa kutupa collabo za wakina Nuh mziwanda, Abbyskilz, Dayna nyange, ommy dimpoz, Hapa najiuliza target yako hapo ni market ipi? Ali mbona unatutesa kiasi hiki?For How long we gonna wait?

2. PAGE ZAKO KWENYE SOCIAL MEDIA ZINABOA SANA, Mi nachofahamu social media ni sehemu adhimu na muhimu sana ya mafans kuwasiliana na msanii wao, kwa kupata updates mbalimbali, ila kwako hili suala limekuwa kinyume, Acc zako mfano Instagram 70% ya posts zako ni birthday za watu, kazi zako hatuon kabisa ukipost, Pia msanii gani muda mwingine unakaa week nzima bila kupost kitu kabisa, Unataka fans wako wafanyaje?

3.MSIMAMO WAKO KUHUSU TUZO, hapa napo tunashindwa kukuelewa je unataka tuzo au hautaki? Tangu mwaka umeanza tumeshuhudia ukipata nominations za tuzo mbalimbali Africa( Afrimma, UEA awards, Afrima Nigeria, AEUSA,AYCA Awards, African Oscar awards etc) lakin hata siku moja hatujawah kuona ukiripost au kuapreciate hicho kitu, mfano mwezi August ulishinda tuzo 2 za [HASHTAG]#AfricanOscarChoiceAwards[/HASHTAG] lakini cha ajabu umekausha hadi leo kurepost hicho kitu, hapa sasa tunabaki njia panda, je unadharau waandaaji wa tuzo au sisi fans wako tuliokesha tukikupigia kura? Hapa tunaomba majibu au tupotezee kukusuport kwenye tuzo.

4: UCHELEWESHAJI WA PROJECT ZAKO, Hapa napo Alikiba umekuwa jipu sugu, tunashindwa kuelewa je tatizo ni wewe au management yako? Porojo na ahadi zimekuwa nyingi bila vitendo, Tunahitaji majibu ya kutosha zaidi tunataka tuone tofauti ya msanii wa Sony global music na wasanii wa mchangani

5. USIRI KATIKA MIKATABA NA MALI ZAKO, Hapa napo ndio kumekuwa na jipu sugu lenye ukungu kabisa, Sababu mara nyingi umekuwa ukiulizwa maswala adhimu kuhusu profit unazopata kutokana na mikataba yako ya Sony music na endorsement unazopata kama ubalozi wa Wild aid, ubalozi Jam food nutrition, Mali unazomiliki etc, Lakin umekuwa na kigugumizi kujibu, Mashabiki zako tuna kiu ya kusikia msanii wetu ananufaika vipi na mziki wake, na hili pia ni haki yetu ya msingi. Tuna mengi sana ila kwa leo tuishie hapa.

Itaendelea
 
Mwisho wa siku ally kiba atabaki kuwa ally kiba.... ana management yake kubwa tu huko Sony ambayo mliisifia itampeleka kimataifa..

Itakuwa ni vigumu sana kumtaka ally kiba awe kama mtu fulani maana kuna sababu nyingi sana zinamfanya aliyepo namba moja awe namba moja..
 
Ally Kiba ni sawa na machungwa ya kilwa...
sijaona machungwa matamu kama ya kilwa....
lakini wengi hata hawajui kilwa kuna machungwa

wengine wanakula machungwa ya kilwa wakifikiri ni machungwa ya Tanga...

Machungwa ya Tanga yamebeba soko na umaarufu mkubwa
wakati hata robo hayaingii kwa machungwa ya kilwa....

Hata huko Kilwa hao wakulima hawajui machungwa yao ndo the best in East Africa...
na umasikini bado uko vilevile
 
5. USIRI KATIKA MIKATABA NA MALI ZAKO, Hapa napo ndio kumekuwa na jipu sugu lenye ukungu kabisa, Sababu mara nyingi umekuwa ukiulizwa maswala adhimu kuhusu profit unazopata kutokana na mikataba yako ya Sony music na endorsement unazopata kama ubalozi wa Wild aid, ubalozi Jam food nutrition, Mali unazomiliki etc, Lakin umekuwa na kigugumizi kujibu, Mashabiki zako tuna kiu ya kusikia msanii wetu ananufaika vipi na mziki wake, na hili pia ni haki yetu ya msingi. Tuna mengi sana ila kwa leo tuishie hapa.

Washabiki inawahusu nini kuhusu mali zake?

Hilo ni lake yeye mwenyewe na familia yake.

Muziki anaowapa unatosha. Mengine mwachieni mwenyewe.
 
Washabiki inawahusu nini kuhusu mali zake?

Hilo ni lake yeye mwenyewe na familia yake.

Muziki anaowapa unatosha. Mengine mwachieni mwenyewe.
wanataka wajue ili waanze kumpambanisha na yuleee anayewanyima Usingizi
 
Mnategemea mambo makubwa sana kutoka kwake kitu ambache yeye mwenyewe amethibitisha kuwa hawezi!
 
Nashukuru, mimi ni alikiba die-hard fan, blood fan Yaani magroup yote yamuhusuyo alikiba Mimi nimewafollow huko insta!! Ulichosema ni kweli, ananiboaga mbaya yani,,kwenye interview zake sasa,,Hee! Utachoka, ana majivuno design, hajibu anachoulizwa Mpaka anawakwaza interviewer nahisi,,anaulizwa hili hajibu,mara anajifanya Naye kumuuliza anaemuhoji,, pathetic!! Napenda mziki wake pamoja na changamoto hizi zote!!
Kuna siku Niliwahi kucomment kuhusu alikiba kuwa Mvivu kupost vitu kne page yake,,pia kujitia spesheli,hajamfollow hata jokate!! Sipendi hii mambo,, metoa kero yangu
 
Usiumize sana kichwa amia kwa domo kama ulivyo ji-nasibu
Hivyo hivyo sisi tumeridhika nae
 
Ally Kiba ni sawa na machungwa ya kilwa...
sijaona machungwa matamu kama ya kilwa....
lakini wengi hata hawajui kilwa kuna machungwa

wengine wanakula machungwa ya kilwa wakifikiri ni machungwa ya Tanga...

Machungwa ya Tanga yamebeba soko na umaarufu mkubwa
wakati hata robo hayaingii kwa machungwa ya kilwa....

Hata huko Kilwa hao wakulima hawajui machungwa yao ndo the best in East Africa...
na umasikini bado uko vilevile
Asanterr[emoji122] [emoji122] [emoji122] umemaliza
 
Nyege mshindo za vijana wa boarding wakirudi makwao mwezi wa 6 ndio sawa na ujumbe wako.
 
Teh wewe sio shabiki wa Kiba, collaboration za kimataifa ndo nini sasa, nampenda kiba sababu anafanya mambo yake anavyotaka, wakati huo aje inaniburudisha
 
Naomba Diamond apite apa ayachukue yote uliyoyaandika kisha ayafanyie kazi uone within minutes
 
Back
Top Bottom