Barua ya wazi kwa maaskofu wa TEC: Baba zetu tuokoeni, nchi yetu inauzwa Uhuru wetu unamong'onyolewa

Unanilinganisha mimi na Dude kubwa lenye mtandao mpana sana la TEC?

Nipo ground napambana pia
Vema kama unafanya push back pia, TEC nao wana battles zao,achana nao wewe ukiona haki yako inaminywa ingia kwenye battle kuipigania, never ever utegemee watu wengine,Soweto Uprising in 1976 ilianzishwa na mwanafunzi mdogo sana kiumri, Tunisia 🇹🇳 Arab springs ilianzishwa na mmachinga
 
Zenji imejibu kupitia kiongozi muhimu Zanzibar. Sikiliza dakika ya 9.15 hadi ya 12.
 
 
Unanilinganisha mimi na Dude kubwa lenye mtandao mpana sana la TEC?

Nipo ground napambana pia

Hawana ukubwa huo mkuu, hilo unaloliita dude sijui ni kikundi cha maslahi kwa baadhi ya watu na si kwa wa Tanzania wote , sasa mimi linipiganie kwa lipi? Acha kuvipa ukubwa vitu ambavyo vikilazimisha sana itatokea machafuko yasiyo hata na sababu mkuu
 
Mkumbuke mwarabu huyu huyu ameshapewa Uwanja wa ndege wa Kia, misitu yetu yote, shirika la posta, loliondo.

Sultani anarudishwa kidogo kidogo.
 
Hainaga haja ya kuweka ukomo kwenye nchi maana ni makubaliano ya nchi in general
Lakini hayavunjiki hata kama kuna matatizo ya kidiplomasia wala vita? Sasa haina haja ya ukomo hivi vifungu vya nini? Wanalinda nini ambacho sisi hatuna haja ya kulinda?
 
Mkumbuke mwarabu huyu huyu ameshapewa Uwanja wa ndege wa Kia, misitu yetu yote, shirika la posta, loliondo.

Sultani anarudishwa kidogo kidogo.
Unampa mtu misitu ambaye kwao kuna Jangwa?

Ni sawa na kuingia mkataba na Samaki wa kusaidiana kuangua nazi
 
Nchi inauzwa kwa kasi kubwa!
 
Muda utawekwa kwenye mikataba inayohusu specific projects. Inaitwa Host Government Agreements ( HGA). Una swali lingine?
Moja ya faida zinazojadiliwa ni kuwa DP World wakipewa bandari watapunguza mda wa meli kuwa nangani ambapo mda huu meli zinakaa kusubiri mpaka siku 5, hawaishii hapo wanataja na bandari shindani ikiwwepo ya Mombasa (Kenya) kuwa kule meli inasubiri nangani kwa mda wa siku 1½ pekee

Swali Mombasa kuupata huo ufanisi wao pia waliipa mkataba DP World au wana-operate wenyewe? Kama wanafanya wenyewe why sisi tushindwe,,,
 
Pia bunge la CCM liache kujitoa ufahamu kudhani wana akili kuliko watanzania wote wakumbuke wanapokuwa bungeni wanatumia pesa zetu tunazo lipa kodi, wakumbushwe pia DPWORLD wanaingia mkata wa matumizi ya rasilimali za nchin ya Tanzania na siyo mkataba wa biashara ya familia
 
Ombi lako leo limetimia; wameshauri! Utekelezaji wa ushauri ni suala jingine.
 
Yaani ulitaka viongozi wa Kikristo waone watu wanapotezwa, wakae kimya? Ukiristo haujawahi na hautawahi kuwa hivyo. Ukweli na ukweli utatuweka huru. Magufuli alipokengeuka TEC walitoa nyaraka 2. Waraka wa Covid na Waraka wa uminyaji demokrasia. TEC haijawahi kuwekwa mfukoni mwa Mtu kisa ni Mkristo.
Miongoni mwa waliompinga Nyerere kuhusu utaifishaji Mali ni Askofu Msakila wa Jimbo Katoliki Rukwa.
 
Kiongozi TEC wamekusikia
Nalishukru baraza la maasikofu catoliki ni chombo imara na wamekuwa walezi bora na ndivyo inavyotakiwa. Tangu zamani manabii na waonaji moja ya kazi zao ilikuwa kuliongoza taifa kiroho na kuwaelekeza,kuwaonya na kuwakemea watawala
 
Wamekusikia na wamejibu.

Hoja 8 muhimu za TEC

14. Ibara zifuatazo za Mkataba huu zina matatizo yatakayosababisha nchi kutofikia uhuru wa kiuchumi (economic independence):

14.1. Ibara ya 2 (1): inayohusu lengo la Mkataba huu ambalo ni kuweka utaratibu unaoibana Tanzania kisheria katika kuendeleza, kuboresha na kuendesha bandari zote za bahari na maziwa, maeneo maalum ya uwekezaji, maeneo ya usafirishaji wa mizigo, na maeneo mengine ya kiuchumi.

14.2. Ibaraya 4: inayohusu wigo wa Mahusiano na Utekelezaji unaoitaka Serikali ya Tanzania kuwajibika kuijulisha Dubai kila fursa ya uwekezaji inapojitokeza.Hiiinakinzana na baadhi ya sheria za nchi yetu, kwa mfanosheria ya ushindani na ile ya manunuzi.

14.3. Ibaraya 5: ambapo DPWorldimepewa haki ya kuendeleza, kusimamia na kuendesha miradi pekee yake, wakati Tanzania inabaki na wajibu wa kumwezesha kufurahia haki hiyo.

14.4. Ibaraya 6:inayoitaka Tanzania kuwajibika kuipatia DP World vibali na vivutio vya kutekeleza miradi yake kama Serikali. Hii inapingana na baadhi ya sheria za kiutaratibu.

14.5. Ibaraya 7: inayoitaka Serikali kuwajibika kutoa mamlaka yanayotakiwa na mwekezaji bila ucheleweshaji.

14.6. Ibaraya 8: Haki ya kutumia ardhi ambapo Mkataba unasababisha uvunjifu wa sheria za ardhi na sheria zinazohusu masuala ya ardhi.

14.7. Ibaraya 10: Usiri wa Mkataba ambapo Mkataba unazuia mamlaka nyingine kama TAKUKURU /BUNGE kufuatilia mikataba.

14.8. Ibara za 23 na 24: zenye ugumu wa kujitoa kwenye Mkataba
 
Nawashukuru mababa askofu kwa kutuitikia barua yetu.

Tamko lenu, limetupa matumaini mapya kuwa nchi yetu kuna watu wenye hekima, watetea haki na wakindao mustkabli mwema kwa kizazi cha sasa na vijavyo.

Asanteni sana mababa askofu.
 
UTanzania wa huyu kiongozi ni wa 'maslahi' tu; nafsi yake inamweka nje ya nchi hii. Huyu ni Mwarabu, hana uTanzania wowote.
Wakati Salim Ahmed anazongwa na akina Kikwete, tena mtu aliyekuwa kalitumikia taifa lake kwa heshima kubwa sana, hao hao akina Kikwete wakaenda kumwokota Mwarabu halisi na kumweka atawale taifa letu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…