Barua ya wazi kwa maaskofu wa TEC: Baba zetu tuokoeni, nchi yetu inauzwa Uhuru wetu unamong'onyolewa

Barua ya wazi kwa maaskofu wa TEC: Baba zetu tuokoeni, nchi yetu inauzwa Uhuru wetu unamong'onyolewa

Wataalam wapi, akina Hamza?
Utakuwa unafanya utani mkubwa.
Haya maswala ya bandari hayana ugumu wa kuyaelewa, hata bila kuwa msomi juu yake.
Na isitoshe, unachokomalia hapa siyo maswala ya utaalam na uendeshaji wa bandari kwa ufanisi. Wewe unakomalia DP World na IGA yake.
Huu ndio uhjuha mkubwa sana unaokusumbua wewe.
Juha ni wewe na wote wa aina yako, msioweza kuunganisha uwepo wa IGA na hii mikataba iliyopitishwa na kusainiwa ambayo inatoa kibali kwa mradi wa uwkezaji kuanza.

Tafuta mtaalam akupe shule. Hamza Johari yupo juu sana nchi hii kwa kipindi cha hayati JPM na kipindi hiki cha SSH.
 
Bila ya ile IGA hizi commercial agreements zisingeweza kuandaliwa. Tatizo una kiburi cha kipuuzi ukidhani unajua sana kila kitu.
Kwa ujinga wako unadhani shughuli pale Bandarini zilikuwa haziendelei kabla ya hiyo IGA? Mbona TICTS na wengine wengi tu walisha kuwepo pale!
 
Tafuta mtaalam akupe shule. Hamza Johari yupo juu sana nchi hii kwa kipindi cha hayati JPM na kipindi hiki cha SSH
Kwa mtu kama wewe asiye kuwa na upeo juu ya lolote, huyo Hamza Johari utamwona mtaalam; kwa sababu huna chochote unachojua. Kwa vile ndiye lilikuwa tegemeo lenu, kama kipeperushi cha kutimiza ufisadi wenu, mkamuweka mbele ili kuhadaa watu. Hamza hana lolote.
 
Kwa mtu kama wewe asiye kuwa na upeo juu ya lolote, huyo Hamza Johari utamwona mtaalam; kwa sababu huna chochote unachojua. Kwa vile ndiye lilikuwa tegemeo lenu, kama kipeperushi cha kutimiza ufisadi wenu, mkamuweka mbele ili kuhadaa watu. Hamza hana lolote.
Hamza ndiye aliyeandika hiyo IGA inayokuchanganya wewe na wote wenye viwango vyako vya kufikiri. Ndiye aliyeandaa Commercial Agreements zilizosainiwa pale Ikulu Dodoma.

Wewe ndiye huna lolote usiyeweza kuelewa kuwa IGA imetengeneza mazingira ya documents zilizowezesha mradi kati ya Serikali na DPW kuweza kuanza.
 
Unaona sasa ujuha zaidi toka kwako? Kwa hiyo maana ya hiyo IGA ilikuwa ndiyo itawale na kutuamrisha tufanye nini juu ya mali yetu wenyewe?
Huna hata aibu ya kuyaandika haya humu?
Aibu yako na ya waliokufundisha huko shuleni. IGA ni kanuni za mwanzo zilizopitishwa na bunge ambazo zimewezesha kuandikwa kwa mikataba ya kibiashara.

Kuamini kwamba IGA ilitufunga kiasi cha sisi kushindwa kufanya lolote ndio ujuha wenyewe huo.

Kuamini kwamba IGA ilituzuia kufanya lolote wakati huo huo kuna tender zinatangazwa za kuendesha bandari hiyo hiyo ambayo inadaiwa kuwa hatuwezi kufanya kitu tukiwa tumebanwa na mkataba ni tatizo la uelewa wa wengi wanaojadili hili suala.
 
Kwa ujinga wako unadhani shughuli pale Bandarini zilikuwa haziendelei kabla ya hiyo IGA? Mbona TICTS na wengine wengi tu walisha kuwepo pale!
TICTS waliondolewa kwa ufisadi wao kwa upigaji wao. DP World wanakuja na tija iliyo kubwa kuliko ile ya TICTS kwa makubaliano yenye tija kwa uendeshaji mzima wa bandari.
 
TICTS waliondolewa kwa ufisadi wao kwa upigaji wao. DP World wanakuja na tija iliyo kubwa kuliko ile ya TICTS kwa makubaliano yenye tija kwa uendeshaji mzima wa bandari.
Kwa hiyo mafisadi mkaona ni bora zaidi kubeba bandari nzima kwa manufaa yenu wenyewe au siyo? Mmegonga mwamba.
 
Aibu yako na ya waliokufundisha huko shuleni. IGA ni kanuni za mwanzo zilizopitishwa na bunge ambazo zimewezesha kuandikwa kwa mikataba ya kibiashara.

Kuamini kwamba IGA ilitufunga kiasi cha sisi kushindwa kufanya lolote ndio ujuha wenyewe huo.

Kuamini kwamba IGA ilituzuia kufanya lolote wakati huo huo kuna tender zinatangazwa za kuendesha bandari hiyo hiyo ambayo inadaiwa kuwa hatuwezi kufanya kitu tukiwa tumebanwa na mkataba ni tatizo la uelewa wa wengi wanaojadili hili suala.
IGA haipo, na kazi za waTanzania zitaendelea kila mahali kama ilivyokuwa mwanzo bila ya upumbavu wa hiyo IGA.
Na bado huelewi kitu chochote, wewe ni sawa na msukule tu.
 
Kwa hiyo mafisadi mkaona ni bora zaidi kubeba bandari nzima kwa manufaa yenu wenyewe au siyo? Mmegonga mwamba.
Bandari ina magati namba sifuri mpaka namba tatu yanamilikiwa na TPA, namba nne mpaka namba saba yanamilikiwa na DP World, namba nane mpaka kumi na moja yatamilikiwa na mwendeshaji anayetafutwa kwa sasa.

Kuna baadhi ya shughuli za uendeshaji zitafanywa kwa ushirikiano kati ya DPW na TPA huko mbeleni, lengo ni tija kuongezeka hapo bandarini.

Miaka ile ya Kikwete akiwa ikulu Paul Kagame alimkejeli akimwambia kwamba anao uwezo wa kuiendesha Tanzania nzima kwa kutegemea bandari yetu pekee, Samia anazifanyia kazi hizo kejeli kivitendo kwa kuamua kuhakikisha nchi inapata pato kubwa iwekezanavyo kupitia bandari pekee.
 
IGA haipo, na kazi za waTanzania zitaendelea kila mahali kama ilivyokuwa mwanzo bila ya upumbavu wa hiyo IGA.
Na bado huelewi kitu chochote, wewe ni sawa na msukule tu.
Wewe unayesema IGA haipo ndio huelewi chochote, huko shuleni waalimu walikuwa na kazi nzito sana kukielewesha kichwa kigumu kama cha Kalamu.

IGA ilipitishwa bungeni na imekuja kuzaa commercial agreements zilizosainiwa na watu wanne pale ikulu wiki tatu zilizopita.

Mmiliki wa DP World na mwanasheria wake, na wawakilishi wa serikali ya JMT wawili.
 
Hamza ndiye aliyeandika hiyo IGA inayokuchanganya wewe na wote wenye viwango vyako vya kufikiri. Ndiye aliyeandaa Commercial Agreements zilizosainiwa pale Ikulu Dodoma.

Wewe ndiye huna lolote usiyeweza kuelewa kuwa IGA imetengeneza mazingira ya documents zilizowezesha mradi kati ya Serikali na DPW kuweza kuanza.
Toka mwanzo ulimshudu Hamza Johari. Akajitokeza kueleza anayo juwa yeye, ikaonekana kuwa kioja, lakini kwa mtu kama wewe uliyeweka matumaini yako yote kwake, bado huamini na huelewi ufinyu wa uwezo wake.
IGA ilipitishwa bungeni na imekuja kuzaa commercial agreements zilizosainiwa na watu wanne pale ikulu wiki tatu zilizopita.
Kwa hiyo, wewe unachojua pekee, ni kwamba kila mradi unaofanyika huko bandarini na yote iliyokuwa imezungumziwa kwenye hiyo takataka yenu ya IGA, inatekelezwa kwa misingi ya hiyo IGA? Mbona unajitoa akili namna hii.

Huko "kupelekwa bungeni" unakokung'ang'ania wewe, njama mliyokuwa mkidhani ikitimia kila kitu kinawanyookea, hiyo haikuwa hatua ya mwisho kuipitisha hiyo IGA yako. Hilo bunge halikumaliza kazi yake lililotakiwa kuikamilisha. Bila ya kubadili sheria zilizotakiwa zibadilishwe, ili IGA itimize mahitaji yake, kazi hiyo ilizimwa baada ya wazalendo wa nchi hii kusimama kulinda maslahi ya nchi yao.

Sitakujibu tena katika hili, kwa sababu unazungusha upumbavu tu humu. Ukiendelea kulileta hivyo hivyo, nitakuwekea upumbavu unaozidi huo utakaoweka wewe.

Hopeless Kabisa watu wa aina yako.
 
Bandari ina magati namba sifuri mpaka namba tatu yanamilikiwa na TPA, namba nne mpaka namba saba yanamilikiwa na DP World, namba nane mpaka kumi na moja yatamilikiwa na mwendeshaji anayetafutwa kwa sasa.

Kuna baadhi ya shughuli za uendeshaji zitafanywa kwa ushirikiano kati ya DPW na TPA huko mbeleni, lengo ni tija kuongezeka hapo bandarini.

Miaka ile ya Kikwete akiwa ikulu Paul Kagame alimkejeli akimwambia kwamba anao uwezo wa kuiendesha Tanzania nzima kwa kutegemea bandari yetu pekee, Samia anazifanyia kazi hizo kejeli kivitendo kwa kuamua kuhakikisha nchi inapata pato kubwa iwekezanavyo kupitia bandari pekee.
Sikiliza wewe mpumbavu. Hakuna asiyejua haya unayoweka hapa. Wote tunayajua.
Tunakataa uwepo wa hiyo IGA ya kipumbavu mliyotaka kutuingizia hapa kwa maslahi yenu na wajomba zenu. Haya mengine yooote unayozunguka nayo tunayaelewa wote, na umuhimu wake tunaujua.
 
Bandari ina magati namba sifuri mpaka namba tatu yanamilikiwa na TPA, namba nne mpaka namba saba yanamilikiwa na DP World, namba nane mpaka kumi na moja yatamilikiwa na mwendeshaji anayetafutwa kwa sasa.
Na unaelewa kweli maana ya neno "kumiriki"?
Inaonekana unajipigia tu maneno bila hata ya kujua unalo andika wewe ni lipi!
namba nane mpaka kumi na moja yatamilikiwa na mwendeshaji anayetafutwa kwa sasa.
Na kwa jinsi akili yako isivyoweza kazi, unafikiri huyo mwekezaji anatafutwa kwa masharti na maelekezo ya IGA ya waarabu milyoileta nyinyi!
Huo ndio ujuha ninao kueleza na bado huwezi kuelewa.
 
Miaka ile ya Kikwete akiwa ikulu Paul Kagame alimkejeli akimwambia kwamba anao uwezo wa kuiendesha Tanzania nzima kwa kutegemea bandari yetu pekee, Samia anazifanyia kazi hizo kejeli kivitendo kwa kuamua kuhakikisha nchi inapata pato kubwa iwekezanavyo kupitia bandari pekee.
Kwa kuigawa bandari kwa waarabu kufuatanana yale matakwa ya IGA, Tanzania itafaidika na kitu gani hapo?

Jinsi akili yako isivyokuwa na kumbukumbu, leo tena unamkumbuka Kagame yule yule uliye kwisha mweleza kuwa hana uwezo hata wa kusimamia "ICD" pale kwake hadi akawatafute hao hao DP World!

Wewe utakuwa ni mwarabu mwenyewe, huna uTanzania wowote.
 
Kwenu baba zetu maaskofu.

Nawaandikieni nikiwa na hisia nzito iliyojaa huzuni kubwa juu ya mustakbali wangu na Taifa langu na vizazi vijavyo.

Baba zetu, siku zote Taifa letu linapokuwa katika mtanzuko mzito, hamjawahi kusita kusimama thabiti na kutoa muelekeo wenye kuponya ili kuwasaidia kondoo zenu.

Wakati, Utawala ulipokana Uwepo wa ugonjwa wa maangamizi wa Covid mlisimama kidete kuuambia wazi utawala kuwa Haiwezekani useme ugonjwa haupo, wakati watawa wenu wanafariki kwa ugonjwa huo.

Wakati utawala uliopita ulipominya Demokrasia, mlitoa waraka wa Kwaresma kukemea uminywahi huo wa haki.

Sasa leo mababa askofu, Bandari yetu, lango letu kuu la uchumi linapewa watu wa nje kwa mkataba ambao ni dhahiri siyo mzuri. Mkataba huu una mapungufu mengi sana ikiwemo:

1. Hauna ukomo.

2. Scope yake ni kubwa hadi kugusa bandari za kwenye maziwa yetu.

3. Mkataba hauelezei Share zetu zisipungue ngapi.

4. Mkataba hauelezi tunaweza kujitoaje pindi mwekezaji asipokidhi masilahi yetu.

5. Mkataba huu unavunja sheria ya bandari ya mwaka 2004 na ya rasilimali ya mwaka 2017 na hata katiba ya nchi kwenye suala la bandari maana bandari ni jambo la muungano.

6. Mkataba unatishia suala la muungano wetu maana ni bandari za upande mmoja tu wa muungano ndo zinaguswa ila za upande mwingine haziguswi. Hii inaibua hisia mbaya dhidi ya muungano.

7. Mkataba hauelezei chochote juu ya matakwa ya mwekezaji kulinda haki za binadamu.

8. Mkataba Unampa veto mwekezaji juu ya masuala yetu ya uwekezaji kwenye mambo ya bandari, maana yake Sovereignity yetu remote tumempa mgeni

Kwa hoja hizo hapo juu mababa askofu, mimi binafsi sina amani, nina wasiwasi na uhuru wangu na watoto wangu na watoto wa nchi hii. Kwa hivyo nakuombeni mababa zetu maaskofu.

1. Tusaidieni kuwaambia watawala kwa waraka mzito kuwa mnakataa vipengele vibaya katika mkataba huu na kwamba watawala wakae na mwekezaji wavirekebishe.

2. Nyie kama wachungaji wema Tunawaomba mfikishe ujumbe wa tahadhari kwa waumini wenu wote nchi hii ili wajue hatari ya mkataba huu.

3. Tunawaomba ikibidi muandae hata matembezi na makongamano ya amani ili kujenga awareness ya umma juu ya suala hili.

Asanteni sana.
HGA imesawazisha yote ?
 
Kwa kuigawa bandari kwa waarabu kufuatanana yale matakwa ya IGA, Tanzania itafaidika na kitu gani hapo?

Jinsi akili yako isivyokuwa na kumbukumbu, leo tena unamkumbuka Kagame yule yule uliye kwisha mweleza kuwa hana uwezo hata wa kusimamia "ICD" pale kwake hadi akawatafute hao hao DP World!

Wewe utakuwa ni mwarabu mwenyewe, huna uTanzania wowote.
Kagame alijenga ICD ili afaidike na deal ya DP World, hana kosa lolote tatizo ni uelewa wetu nadhani.

Hakuna mtu mwenye uwezo wala kiburi cha kuweza kuigawa bandari ni akili za kitumwa kuamini hivyo.

Tanzania inakwenda kufaidika kwa maana ya ongezeko la mzigo utakaoshushwa pale TPA linakwenda kuongeza kile kinachokusanywa na TRA, kikiongezeka hicho kinachokusanywa maana yake miradi mingi ya ndani inakwenda kutegemea pesa zetu wenyewe.

Hii ni biashara kubwa sana tofauti na wenye hulka za kijamaa wanavyoiangalia na kuishia kuja na mawazo tofauti kabisa na lengo la uwekezaji pale bandarini.
 
Na unaelewa kweli maana ya neno "kumiriki"?
Inaonekana unajipigia tu maneno bila hata ya kujua unalo andika wewe ni lipi!
Na kwa jinsi akili yako isivyoweza kazi, unafikiri huyo mwekezaji anatafutwa kwa masharti na maelekezo ya IGA ya waarabu milyoileta nyinyi!
Huo ndio ujuha ninao kueleza na bado huwezi kuelewa.
Bandari inakwenda kupangishwa hilo ndilo la muhimu zaidi. Ufanisi unakwenda kuongezeka na mitambo ya kisasa itakayofungwa inakwenda kukomesha uingizaji wa madawa ya kulevya, magendo na biashara zote haramu.
 
Sikiliza wewe mpumbavu. Hakuna asiyejua haya unayoweka hapa. Wote tunayajua.
Tunakataa uwepo wa hiyo IGA ya kipumbavu mliyotaka kutuingizia hapa kwa maslahi yenu na wajomba zenu. Haya mengine yooote unayozunguka nayo tunayaelewa wote, na umuhimu wake tunaujua.
Mpumbavu ni wewe unayetoa mapovu bila ya kuelewa hata unaandika kitu gani. IGA ile ndio imesababisha biashara ya Tanzania na Dubai iweze kufanyika.

Mpimbavu ni wewe unayeelezwa mara milioni kitu kile kile na bado huelewi.
 
Toka mwanzo ulimshudu Hamza Johari. Akajitokeza kueleza anayo juwa yeye, ikaonekana kuwa kioja, lakini kwa mtu kama wewe uliyeweka matumaini yako yote kwake, bado huamini na huelewi ufinyu wa uwezo wake.
Kwa hiyo, wewe unachojua pekee, ni kwamba kila mradi unaofanyika huko bandarini na yote iliyokuwa imezungumziwa kwenye hiyo takataka yenu ya IGA, inatekelezwa kwa misingi ya hiyo IGA? Mbona unajitoa akili namna hii.

Huko "kupelekwa bungeni" unakokung'ang'ania wewe, njama mliyokuwa mkidhani ikitimia kila kitu kinawanyookea, hiyo haikuwa hatua ya mwisho kuipitisha hiyo IGA yako. Hilo bunge halikumaliza kazi yake lililotakiwa kuikamilisha. Bila ya kubadili sheria zilizotakiwa zibadilishwe, ili IGA itimize mahitaji yake, kazi hiyo ilizimwa baada ya wazalendo wa nchi hii kusimama kulinda maslahi ya nchi yao.

Sitakujibu tena katika hili, kwa sababu unazungusha upumbavu tu humu. Ukiendelea kulileta hivyo hivyo, nitakuwekea upumbavu unaozidi huo utakaoweka wewe.

Hopeless Kabisa watu wa aina yako.
Hamza Johari ni mwanasheria jembe sana hapa Tanzania, uelewa wake ni mkubwa kiasi cha fitina za Kalamu kugonga ukuta.

Unapoongelea kubadilisha sheria ni kuendelea kuanika uelewa wako mdogo wa suala hili kwa ujumla wake. Hakuna sheria iliyobadilishwa naona wanasheria magumashi kina Madeleka wamewaingiza mkenge na mkaingia mazima.
 
Back
Top Bottom