Barua ya wazi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu hali ya haki jinai nchini

Barua ya wazi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu hali ya haki jinai nchini

Mkuu haya mambo yanakemewa sana,Fuatilia hotuba ya raisi wa TLS ya mwaka jana kwenye siku ya sheria utaona ina mambo mengi tu yalizungumzwa mle ila watawala hawajali,nadhani labda wabadili mbinu ya kuyafikisha
Kweli kabisa CCM wanawadharau sana wataalam wetu, lakini mambo haya yakisemwa na mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu watajifikiria mara mbili tatu.
 
Tito Magoti, Pole sana kwa yaliyokupata Ila huwezi jua kwanini Mungu akaacha ukapata majanga haya.

Kwa akili yangu, Mungu alitaka uende ukaone jinsi raia wanavyoteseka na mfumo mbovu wa Sheria na haki nchini. Wewe ndiyo sauti yao.

Hata Kama Rais SSH hataliona hili, Mimi ninaliona ni zaidi ya Thesis ya Masters/ PhD.

Nakushauri ulisimamie kwa kutafuta wahisani watakao ku-support uwasemee wasio na sauti kupitia Asasi za Kiraia.

Mungu akubariki sana
 
Naomba kwa ruhusa yako niandike kwa kifupi mambo muhimu kutoka kwenye waraka wako kwa manufaa ya Watanzania wote,kama nimekosea mtanirekebisha;

[emoji637]Mahakama kurudishiwa mamlaka yake
[emoji818]Hapa kama ulikuwa na kesi na huridhishwi na mwenendo wake,ukifungua kesi kukosoa mwenendo wa shauri,kesi itafutwa na utakamatwa upya na kushtakiwa kwa kesi hiyohiyo,maana yake kama ulikaa miaka minne jela,kesi itaanza upya kwakuwa shauri ni jipya.

[emoji638]Makosa yasiyo na dhamana yapitiwe upya
[emoji818]Hali ilivyo , watu hukaa gerazani hata miaka 10 baadae huonekana hawana makosa,hapa tutumie mfumo wa "peleleza-kamata-shtaki"

[emoji639]Kuweka kikomo cha muda kwenye upelelezi
[emoji818]Hapa hata kama makosa yana ukomo wa muda wa upelelezi,mtuhumiwa atakamatwa na kushtakiwa upya,na hukaa gerezani au mahabusu wakisubiri upelelezi ukamilike

[emoji640]Watuhumiwa kushikiliwa vituo vya polisi zaidi ya muda wa kisheria
[emoji818]Wapo ambao hukaa hata mwezi mmoja lakini hawaadikwi kwenye taarifa za mahabusu(occurance book)

[emoji641]Kesi za kubambika na mashtaka ya hila
[emoji818]Hapa vita vya kiuchumi,madawa ya kulevya ,wakosoaji wa serikali ndio hutumika kama sababu ya kubambika kesi
[emoji818]Wanaotuhumiwa hapa ni ofisi ya mashtaka ya taifa (NPS)na Jeshi la polisi(task force)

[emoji642]Mateso katika vituo vya polisi
[emoji818]Hapa watu hulazimishwa kukiri makosa kwa mateso kama kuingiziwa spoku kwenye uume nk

[emoji643] Makubaliano ya kukiri kosa( Plea bargain)
[emoji818]Hii imegeuka mbadala wa upelelezi katika makosa ya uhujumu uchumi.Ili umalize kesi lipa uendelee na shughuli zako.(hapa hakuna majadiliano).Zoezi hili lifanyike kwa uwazi.

[emoji644]Mahakam kutoa huduma kwa mfumo wa TEHAMA
[emoji818]Hapa shabaha ilikuwa kurahisisha ila kutojiandaa vema kumesababisha uahirishaji wa kesi kwa sababu ndogondogo kama mtandao kufeli,umeme nk.

[emoji645]Watoto,wenye ulemavu na wageni
Pamoja na kuwepo mahabusu na mahakama za Watoto bado unakuta Watoto katika magereza ya watu wazima(hatari ya kuathirika na ulawiti)
[emoji818]Mahabusu wenye matatizo ya akili kuendelea kushikiliwa gerezani badala ya kupatiwa matibabu hospitalini.
[emoji818]Wakimbizi na wageni wasio na hatia kuendelea kushikiliwa magerezani

[emoji647]Marufuku ya Taulo za kike Magerezani
[emoji818]Huu ni ukatili dhidi ya utu wa mwanamke
[emoji818]Wenye ulemavu,wajawazito wapo hatarini kupata magonjwa kutokana na mazingira.

[emoji637][emoji637]Kutofuatwa kwa sheria magerezani
[emoji818]Ukaguzi magerezani ni zoezi linalodhalilisha utu(kuvuliwa nguo) bila kuzingatia rika,kupigwa,matusi,kulazimishwa kujisaida na kuleta kinyesi nk

[emoji637][emoji638]Huduma duni za afya na msongamano
[emoji818]Gereza la kuhifadhi wafungwa 800 kuhifadhi zaidi ya 2000
[emoji818]Malazi yasiyoridhisha(godoro la futi 3 kwa sita kulaliwa na mahabusu zaidi ya wawili nk.
Farolito Asante kwa kurahisisha andiko la Tito Magoti, ni rahisi kufollow hata kwa sisi lay men
 
Kwa bahati nzuri Mr. Tito nchi yetu tuna bahati kwamba Waziri wa Sheria, Jaji Mkuu, Katibu Mkuu wizara ya sheria na Mwanasheria Mkuu wa serikali wote ni wasomi wa kiwango cha Professor wa chuo kikuu! Wote pia ni wacha mungu na wazalendo. Ni matumaini yetu kwamba kwa kushirikiana na bunge waheshimiwa hawa wanalo jukumu na uwezo wa ku reform our nation's justice system na hivyo kumsaidia Rais Samia.
Hata hivyo ni vigumu kuamini tukizingatia mwaka jana nchi yetu ilijitoa ktk mahakama ya afrika ya haki za binadamu! Makao makuu yake Ausha. Can you imagine?

Wasomi wengi wa Tanzania wakishangia kwenye madaraka wanakuwa hopeless. Jaribu kuangalia kila Kabudi, Kitila Mkumbo, Bashiru nk, walichokuwa wanaongea kabla ya kupata madaraka na wanachoongea baada ya kupata madaraka.
 
Naomba kwa ruhusa yako niandike kwa kifupi mambo muhimu kutoka kwenye waraka wako kwa manufaa ya Watanzania wote,kama nimekosea mtanirekebisha;

[emoji637]Mahakama kurudishiwa mamlaka yake
[emoji818]Hapa kama ulikuwa na kesi na huridhishwi na mwenendo wake,ukifungua kesi kukosoa mwenendo wa shauri,kesi itafutwa na utakamatwa upya na kushtakiwa kwa kesi hiyohiyo,maana yake kama ulikaa miaka minne jela,kesi itaanza upya kwakuwa shauri ni jipya.

[emoji638]Makosa yasiyo na dhamana yapitiwe upya
[emoji818]Hali ilivyo , watu hukaa gerazani hata miaka 10 baadae huonekana hawana makosa,hapa tutumie mfumo wa "peleleza-kamata-shtaki"

[emoji639]Kuweka kikomo cha muda kwenye upelelezi
[emoji818]Hapa hata kama makosa yana ukomo wa muda wa upelelezi,mtuhumiwa atakamatwa na kushtakiwa upya,na hukaa gerezani au mahabusu wakisubiri upelelezi ukamilike

[emoji640]Watuhumiwa kushikiliwa vituo vya polisi zaidi ya muda wa kisheria
[emoji818]Wapo ambao hukaa hata mwezi mmoja lakini hawaadikwi kwenye taarifa za mahabusu(occurance book)

[emoji641]Kesi za kubambika na mashtaka ya hila
[emoji818]Hapa vita vya kiuchumi,madawa ya kulevya ,wakosoaji wa serikali ndio hutumika kama sababu ya kubambika kesi
[emoji818]Wanaotuhumiwa hapa ni ofisi ya mashtaka ya taifa (NPS)na Jeshi la polisi(task force)

[emoji642]Mateso katika vituo vya polisi
[emoji818]Hapa watu hulazimishwa kukiri makosa kwa mateso kama kuingiziwa spoku kwenye uume nk

[emoji643] Makubaliano ya kukiri kosa( Plea bargain)
[emoji818]Hii imegeuka mbadala wa upelelezi katika makosa ya uhujumu uchumi.Ili umalize kesi lipa uendelee na shughuli zako.(hapa hakuna majadiliano).Zoezi hili lifanyike kwa uwazi.

[emoji644]Mahakam kutoa huduma kwa mfumo wa TEHAMA
[emoji818]Hapa shabaha ilikuwa kurahisisha ila kutojiandaa vema kumesababisha uahirishaji wa kesi kwa sababu ndogondogo kama mtandao kufeli,umeme nk.

[emoji645]Watoto,wenye ulemavu na wageni
Pamoja na kuwepo mahabusu na mahakama za Watoto bado unakuta Watoto katika magereza ya watu wazima(hatari ya kuathirika na ulawiti)
[emoji818]Mahabusu wenye matatizo ya akili kuendelea kushikiliwa gerezani badala ya kupatiwa matibabu hospitalini.
[emoji818]Wakimbizi na wageni wasio na hatia kuendelea kushikiliwa magerezani

[emoji647]Marufuku ya Taulo za kike Magerezani
[emoji818]Huu ni ukatili dhidi ya utu wa mwanamke
[emoji818]Wenye ulemavu,wajawazito wapo hatarini kupata magonjwa kutokana na mazingira.

[emoji637][emoji637]Kutofuatwa kwa sheria magerezani
[emoji818]Ukaguzi magerezani ni zoezi linalodhalilisha utu(kuvuliwa nguo) bila kuzingatia rika,kupigwa,matusi,kulazimishwa kujisaida na kuleta kinyesi nk

[emoji637][emoji638]Huduma duni za afya na msongamano
[emoji818]Gereza la kuhifadhi wafungwa 800 kuhifadhi zaidi ya 2000
[emoji818]Malazi yasiyoridhisha(godoro la futi 3 kwa sita kulaliwa na mahabusu zaidi ya wawili nk.
Correct.
 
Nje ya mada, Tito umejiunga hapa JF mwaka 2014 lakini una post chini ya 10! Naona umeona wapi unaweza weka gazeti lako ukaona ni hapa JF, kisha unaenda kushinda Twitter.

Huu mchezo anao Zitto, naye huleta post zake ndefu kisha anakuwa kama karushia mbwa, halafu anaenda zake kushinda Twitter bila kujibu lolote kwenye bandiko lake.

Tito jirekebishe kwa hilo.
 
Mkuu haya mambo yanakemewa sana,Fuatilia hotuba ya raisi wa TLS ya mwaka jana kwenye siku ya sheria utaona ina mambo mengi tu yalizungumzwa mle ila watawala hawajali,nadhani labda wabadili mbinu ya kuyafikisha

Viongozi wa kiafrika huwa hawajali malalamiko yanayotolewa kwa njia ya amani/kistaarabu, njia wanayoilewa viongozi wengi wa kiafrika ni ya maandamano, migomo au machafuko.

Haya madai ya Tito haijalishi yana ukweli kiasi gani, ili mradi yametolewa kwa njia ya kistaarabu, kwao hayana uzito wowote.

Kwa njia hii ya maelezo ya kistaarabu bila maandamano ama mgomo, yataandikwa hata miaka 100 bila kufanyiwa kazi.
 
Nje ya mada, Tito umejiunga hapa jf mwaka 2014 lakini una post chini ya 10! Naona umeona wapi unaweza weka gazeti lako ukaona ni hapa jf, kisha unaenda kushinda Twitter. Huu mchezo anao Zito, naye huleta post zake ndefu kisha anakuwa kama karushia mbwa, halafu anaenda zake kushinda Twitter bila kujibu lolote kwenye bandiko lake. Tito jirekebishe kwa hilo.
tindo, yawezekana anayo ID nyingine kama ya kwako na Mimi hapa anayoitumia. Mara nyingine ID ya NIDA haikupi uhuru wa kujiachia kama mimi na wewe tunavyojiachia. Just thinking aloud
 
Umeeleza vizuri, ninachoona DPP ndo chanzo cha matatizo yote, kuanzia mlundikano wa mahabusu magerezani, hadi ukosefu wa dhamana kwa watuhumiwa, DPP apunguziwe mamlaka zaidi, mahakama iwe ndo mwamuzi wa mwisho kuhusu dhamana za washtakiwa
 
tindo, yawezekana anayo ID nyingine kama ya kwako na Mimi hapa anayoitumia. Mara nyingine ID ya NIDA haikupi uhuru wa kujiachia kama mimi na wewe tunavyojiachia. Just thinking aloud

Sikatai usemacho, lakini mimi nimetolea angalizo hii Id yake verified. 2014 ilikuwa dhalimu hajaingia madarakani, mbona nayo michango ni michache mpaka 2015?
 
Hili andiko ni bora sana. Yanahitajika mageuzi makubwa mno. Ikibidi kiwepo chombo huru cha kufatilia haki za mahabusu. Bora zitungwe sheria kali kwa wataobainika kuvunja hayo wasiyopenda lakini si kuumiza watu. Pole sana Tito
haya ndiiyo mambo yamefanya hasira ya mungu kuwaka na kumwondoa mfalme
 
Duuh...! Asante kwa barua nzuri,na yenye mafunzo na masuruhisho. Mpaka mwili umesisimka. Unaweza ukadhani tuko huru tunatamba mitaani kumbe ukiingia kwenye 18 za watu fulani fulani,bora ya jehanum
 
Hili andiko ni bora sana. Yanahitajika mageuzi makubwa mno. Ikibidi kiwepo chombo huru cha kufatilia haki za mahabusu. Bora zitungwe sheria kali kwa wataobainika kuvunja hayo wasiyopenda lakini si kuumiza watu. Pole sana Tito
Moyo umeniuma sana kusoma hili andika
 
Viongozi wa kiafrika huwa hawajali malalamiko yanayotolewa kwa njia ya amani/kistaarabu, njia wanayoilewa viongozi wengi wa kiafrika ni ya maandamano, migomo au machafuko. Haya madai ya Tito haijalishi yana ukweli kiasi gani, ili mradi yametolewa kwa njia ya kistaarabu, kwao hayana uzito wowote. Kwa njia hii ya maelezo ya kistaarabu bila maandamano ama mgomo, yataandikwa hata miaka 100 bila kufanyiwa kazi.
Uko sahihi nadhani mbinu ibadilike
 
Back
Top Bottom